"KUPANGA NI KUCHAGUA" - !~sasa ndio nimemuelewa Mwalimu~!

Felister, nimependa sana mawazo yako:

Kwenye suala la kilimo Tanzania kabla ya kuchangia mawazo yango randomly nitaanza kwa kusema mambo yafuatayo ambayo niliwahi kuyaandika miaka minne iliyopita lakini sasa hivi naamini yana umuhimu wa pekee.

Kwanza, kama Taifa ni lazima tutambue kipaumbele chetu cha kiuchumi ni nini. Miaka hii minne au mitano iliyopita na ukienda hata kumi utaona kuwa dhana ya kupanga ni kuchagua haijaingia katika fikra za watawala na wanasiasa wetu na tumefikia kujaribu vitu vingi na karibu vyote tukivifanya vibaya. Je uchumi wetu utaendeshwa kwa madini (kama ilivyo Botswana na Namibia), Je uchumi utaendeshwa kwa mchanganyiko wa sekta (kama ilivyo Kenya ambapo kilimo, utalii na viwanda) vinachangia kwa kiasi kikubwa?

Tukiuliza kuhusu Uchumi wa Tanzania utaona kuwa in theory we are an agricultural economy lakini kilimo hicho siyo chenye mchango mkubwa kwenye uchumi which makes this statement a kind oxymoronic. So, la kwanza ni lazima tutambue ni nini kinapaswa kuendesha uchumi wetu.

Pili, ni lazima tutafute sera ya kuendesha injini hiyo ya uchumi wetu. Sasa hivi bado tumeweka mkazo mkubwa sana kwenye foreign capital investment (na hasa direct investments). Katika sera ya namna hiyo utaona kuwa tulichokifanya na ambacho tunajivunia kuwa ni maendeleo ni kile ninachokiita "importation of development". Kwa maana ya kwamba, maendeleo tunayaona hayana asili ya Tanzania bali tumeyaingiza kutoka ng'ambo.

Tunapofikia mahali tunaagiza vitunguu na nyanya kutoka ng'ambo, kandambili na samani toka ng'ambo na hadi kuona fahari ya kuvaa suruali na mashati toka majuu basi kile tunachoona kinapendezesha nchi yetu na mazingira yetu kwa kweli si cha kwetu. Nakumbuka (sijui kama vyote bado vipo, tuliwahi kuwa na kiwanda cha radio za national na hata betri!), sijui tungefika wapi kama tungeendeleza hayo hadi kuwa na assembly plants of other electronics na kuchukua nafasi ya sehemu kama South Korea, Taiwan, Hong Kong n.k

So, sera hapa ninayoiashiria ni kuwa kama tunataka kuinua kilimo we have to get back to agriculture for self-reliance. Katika pendekezo lako bado unaona ulazima wa kuwa na wawekezaji wa nje katika kilimo, I don't. Hata hivyo, hilo linaonekana ni la muhimu kwa sababu sisi wenyewe tumeona kilimo ni fani au ajira duni.

Tatu, chochote tunachotaka kufanya kwenye kilimo ni lazima kiwe kitu ambacho tuna faida nacho zaidi kulinganisha na nchi nyingine au sehemu nyingine duniani. Kiviwanda, hatuna faida kuliko Ujerumani, Marekani, China n.k Hivyo, kufikiria tunaweza kuingia katika viwanda vikubwa (heavy industries) na kutengeneza uchumi wenye nguvu ni gumu kweli. Ukija kwenye viwanda vyenye mwelekeo wa teknolojia ya electronics hatuna faida kubwa (comparative advantage) kulinganisha na China, India, Hong Kong, Taiwan na Japan. So, chochote tutakachofanya kitakumbana na ushindani mkubwa sana kwenye soko la kimataifa. Ninachosema ni kuwa bado tuna maeneo mawili tu au matatu na katika hayo matatu ni eneo moja tu naamini tuna comparative advantage kuliko nchi nyingine yoyote ile duniani (if I may so boldly).


Hivyo, kutoka hayo matatu yatafuata mapendekezo yangu ya kuona kilimo chetu kinavyoweza kuwa chanzo cha utajiri wa kudumu kwa mtu wa kawaida, kuchochea pato la taifa, kuingiza fedha za kigeni na kuinua hali ya maisha ya wananchi wetu. So far, bado hatujaanza hivyo.
 
Mwanakijiji:

Makosa makubwa tunayoyafanya ni kutotambua weakeness na strength zetu. Toka tumepata uhuru, kuna projects nyingi tumezifanya lakini nyingi hazikutumia strength yetu zimetumia weakness zetu katika implementation na matokeo yake tumekwama.

Kwa mfano ukichukua blueprint za vijiji vya ujamaa, utaona kuwa nia ilikuwa ni nzuri tu. Watu wakiwa pamoja wata-share vitu vingi kama huduma za elimu, maji, afya n.k

Matatizo yalikuja pale vijiji vinapoanza, na kukuta kuwa hakuna viongozi wa vijiji waliokuwa na uwezo wa kuongoza. Kuna vijiji vilivyopewa matrekta wakati hakuna mtu aliyekuwa anajua uchumi wa kilimo katika vijiji hivyo.

Kuna mipango mingi ya elimu imepita. Lakini hakuna hata mpango wowote uliokuwa na desirable effects.

Mpaka sasa sijaona mtu anayetambua strength ya watanzania. Siku zote mtu anataka watanzania wawe kama waChina. Lakini je strength yetu inaweza kutufanya tuwe kama waChina au tunaongozwa na matamanio tu ??

Kuna watu wako-politically correct wanafikiri kuwa kutambua weakness zao ni inferiority complexity. Hivyo wanatumia juhudi zao ku-prove point. Ukweli wa mambo weakeness inaweza kutafutiwa ufumbuzi pale watu wanapo-master njia nyingine. Lakini kabla hawaja-master ni lazima strength zao ziwe mkombozi wao na sio vitu vingine.

Kwa mfano watanzania wengi ni watu wa oral traditions kwa sababu kumbukumbu za kuandikwa kwenye makaratasi zimekuja miaka ya karibuni. Hivyo unapotunga sheria kwa watu wa oral traditions na kuziacha vitabu, hakuna atakaye-pay attention. Ukiandika theories za maisha na kuziacha vitabu, hakuna atakaye-pay attention.

Vizazi vya watanzania ambavyo viko BOOK-NATIVE, vilivyozaliwa na baba na mama waliokwenda shule na wao kusoma wao sio oral traditionalists. Hivyo wana-pay much attention katika vitu vilivyokwenya maandishi kuliko wazazi wao.
 
Follow me if you will...

Planning is always the same in one important respect. It involves making decision about the allocation of scarce resources; it means choosing between many desirable activities, because not everything can be done at once. It is vital that this should be clearly understood. There are many things which are urgently needed in Tanzania and which the Plan does not provide for.

.. To a greater or lesser extent every country in the world has a limit to its resources and the more it spends on one thing, the less it can spend on another. This is true even in a rich country like the United Stes of America, where it frequently stated that the plans for tackling the internal problem of poverty were destroyed by the costs of the Vietnamn war to which it gave priority.

This problem of choice is very much greater for Tanzania. .. The less your resources, the greater the number of difficult choices which have to be made.

For just as a poor worker has to decide whether to spend less on food in order to buy himself a new shirt, so a poor nation has to decide whether to provide schools or hospitals; new houses or new water supplies; to make an attack on the ignorance which causes people to suffer from preventable diseases, or to build roads which will enable peasants to market the goods they produce.

Indeed, before it can make any of these choices between alternative investments, a poor nation has to decide what proportion of its wealth it is willing to devote to any kind of investment because every shiilling spent on investment means that one shillilng less is available for current consumption.

That is our position now as it was in 1964. We have to make choices between good things, not between good things and bad things.


DO YOU THINK THIS LINE OF THOUGHT MAKE ANY SENSE AT ALL? (I'm writing a treatise titled "Leadership and Development") I would like your criticism as I go along.
 
Nop not you,you are smarter than that unless CCM washakutumia mtu utueleze tujue kama ndio unatutoka hivyo. Think Twice.


SAHIBA.
Naona wewe ndie unatakiwa kuthink twice... Jaribu kusoma tena swali ambalo M'kijiji ameuliza then you can see whats come first between planning and kuchagua. Soma bila kuweka ushabiki wa vyama.
 
Mzee Mwanakijiji

Hayo unayopendekeza yanaweza kufanyika pale tu unapokuwa na Uongozi wenye maono ya kujiletea kimaendeleo kwa njia za "asili". Njia za asili nikimaanisha maana halisi ya maendeleo "Development is for Man, by Man, and of Man". Maono hayo ndiyo aliyokuwa nayo Baba wa Taifa. Aliamini tukienda taratibu kwa "pamoja" (neno pamoja lina umuhimu hapa) tutafika kwa "pamoja" wote au walio wengi tukiwa na uelewa wa maendeleo uliokaribiana. Uelewa huo ukitumiwa vizuri na Viongozi makini ni rahisi kupanga na kuchagua dira ya Taifa kwa msukumo stahili wa kisiasa.

Pamona na kwamba sipendi kuzungumzia siasa, lakini nakubali kuwa bila siasa safi hatuwezi kuendelea. Hivyo, maamuzi ya nini kifanyike kwenye nchi kwa wakati gani ni lazima kipate baraka za wananchi. Kwa sasa hivi wananchi wengi wana uelewa hafifu wa maendeleo, uelewa unaoangalia "leo" ndio maana yakifanyika maamuzi duni leo wanaona sawa kwa sababu leo ikishapita basi hakuna madhara yatakayotokea. Vivyo hivyo, yakifanyika maamuzi mazuri leo wanashangilia na kuomba Mungu huyo alifanya maamuzi hayo, na "kesho" afanye hivyo hivyo.

Hoja yako ya "kupanga ni kuchagua" inaweza kufanikiwa pale tu wananchi watakuwa na uelewa wa maana halisi ya maendeleo. Bila ya uelewa huo, maamuzi yatakosa msukumo wa kisiasa, kitu ambacho ni muhimu sana.
 
Mzee Mwanakijiji

Hayo unayopendekeza yanaweza kufanyika pale tu unapokuwa na Uongozi wenye maono ya kujiletea kimaendeleo kwa njia
za "asili".


Njia za asili nikimaanisha maana halisi ya maendeleo “Development is for Man, by Man, and of Man". Maono hayo ndiyo aliyokuwa nayo Baba wa Taifa. Aliamini tukienda taratibu kwa "pamoja" (neno pamoja lina umuhimu hapa) tutafika kwa "pamoja" wote au walio wengi tukiwa na uelewa wa maendeleo uliokaribiana. Uelewa huo ukitumiwa vizuri na Viongozi makini ni rahisi kupanga na kuchagua dira ya Taifa kwa msukumo stahili wa kisiasa.

Pamona na kwamba sipendi kuzungumzia siasa, lakini nakubali kuwa bila siasa safi hatuwezi kuendelea. Hivyo, maamuzi ya nini kifanyike kwenye nchi kwa wakati gani ni lazima kipate baraka za wananchi. Kwa sasa hivi wananchi wengi wana uelewa hafifu wa maendeleo, uelewa unaoangalia “leo” ndio maana yakifanyika maamuzi duni leo wanaona sawa kwa sababu leo ikishapita basi hakuna madhara yatakayotokea. Vivyo hivyo, yakifanyika maamuzi mazuri leo wanashangilia na kuomba Mungu huyo alifanya maamuzi hayo, na “kesho” afanye hivyo hivyo.

Hoja yako ya “kupanga ni kuchagua” inaweza kufanikiwa pale tu wananchi watakuwa na uelewa wa maana halisi ya maendeleo. Bila ya uelewa huo, maamuzi yatakosa msukumo wa kisiasa, kitu ambacho ni muhimu sana.

Unachosema ni kweli, tatizo unadhani huyo kiongozi awe nani, if the ones we have are not of the type you like then why are'nt you in the office? One thing you have to admit is they are smater than you if you anticipated and you failed to out compete them. Another thing is if a person is as good as he think if he can not manifest that goodness into what we can physically see there is no how we can justify his good will and ability to do what he claim is good. We can only judge if that person can bring what he claims into existence otherwise sorry you need either to concur or to continue blaiming but you will continue to blame for 5 or more years nothing will change and your situation might be worse than it was before.


Kama watu wetu hawanauelewa unaohitajikathen what is your contribution into making them the way you want them be?
 
Last edited:
Unachosema ni kweli, tatizo unadhani huyo kiongozi awe nani, if the ones we have are not of the type you like then why are'nt you in the office? One thing you have to admit is they are smater than you if you anticipated and you failed to out compete them. Another thing is if a person is as good as he think if he can not manifest that goodness into what we can physically see there is no how we can justify his good will and ability to do what he claim is good. We can only judge if that person can bring what he claims into existence otherwise sorry you need either to concur or to continue blaiming but you will continue to blame for 5 or more years nothing will change and your situation might be worse than it was before.


Kama watu wetu hawanauelewa unaohitajikathen what is your contribution into making them the way you want them be?

Felister, hili ni kosa kubwa sana la mtiririko wa mawazo. Kwamba, kwa vile ninaandika ninavyoandika kikosoaji basi ninataka kuwa kwenye madaraka. Kwamba, kwa vile sitaki kuwa kiongozi basi nisitoe mawazo ambayo ninaamini bora au kuonesha makosa ya wale waliopo.

Hii yote ni kutokujua mchango wa fikra huru katika uongozi. Hivi Plato, Socrates, Kent, C.S Lewis, Einstein, Martin Luther King, na wengine walikuwa viongozi wa nani? Ni lazima uelewe kuwa hakuna mchango mkubwa unaoweza kuleta mabadiliko makubwa sana kama mchango wa mabadiliko ya kifikra.

Wachache wale ambao wametamani kuingia kwenye madaraka mara nyingi imekuwa vigumu mno wa kuwaelewa kwani mawazo yao yako maili 100 mbele ya wale wanaoowangoza.

Ndiyo maana hadi leo hii wenzetu katika nchi za magharibi bado wanasoma na kuwachambua kina Plato na Socrates katika kuelewa masuala ya imani, serikali n.k Usipuuzie hata kidogo nafasi ya mawazo huru katika kuleta mabadiliko ya kiuongozi. Cha kwanza ni kutambua kuwa si wote tunapenda au tuna hamu ya kutawala.

Lakini, kama siku moja tutapata nafasi ya kutawala, we can not be worse than these!
 
Naona wewe ndie unatakiwa kuthink twice... Jaribu kusoma tena swali ambalo M'kijiji ameuliza then you can see whats come first between planning and kuchagua. Soma bila kuweka ushabiki wa vyama.


Yes ndio CCM wenyewe hao wananijia juu nana niombe samahani hapa.

SAHIBA.
 
Felister, hili ni kosa kubwa sana la mtiririko wa mawazo. Kwamba, kwa vile ninaandika ninavyoandika kikosoaji basi ninataka kuwa kwenye madaraka. Kwamba, kwa vile sitaki kuwa kiongozi basi nisitoe mawazo ambayo ninaamini bora au kuonesha makosa ya wale waliopo.

Hii yote ni kutokujua mchango wa fikra huru katika uongozi. Hivi Plato, Socrates, Kent, C.S Lewis, Einstein, Martin Luther King, na wengine walikuwa viongozi wa nani? Ni lazima uelewe kuwa hakuna mchango mkubwa unaoweza kuleta mabadiliko makubwa sana kama mchango wa mabadiliko ya kifikra.

Wachache wale ambao wametamani kuingia kwenye madaraka mara nyingi imekuwa vigumu mno wa kuwaelewa kwani mawazo yao yako maili 100 mbele ya wale wanaoowangoza.

Ndiyo maana hadi leo hii wenzetu katika nchi za magharibi bado wanasoma na kuwachambua kina Plato na Socrates katika kuelewa masuala ya imani, serikali n.k Usipuuzie hata kidogo nafasi ya mawazo huru katika kuleta mabadiliko ya kiuongozi. Cha kwanza ni kutambua kuwa si wote tunapenda au tuna hamu ya kutawala.

Lakini, kama siku moja tutapata nafasi ya kutawala, we can not be worse than these!

Mwanakijiji you r very wise and hunajazba I appreciate you.

Lakini kidogo nijaribu kueleza what I mean...hakuna mtu anaweza kukupa nafasi kufanya what you wish to happen; everybody has his/her objective in life. Sasa to be authority in whatever school of thought depends on how smart you are to penetrate the existing ideas or system and take it to the direction you want...respect is not earned by force. Ndiyo maana kwa njia yako umepata heshima kubwa kwenye JF na mimi hata nitamani vipi kama sinta kuwa na better strategies ya kuheshimika kuwavuta watu nikuondoe wewe kwenye chart I will never get that chance so for this case you are smarter than me. sasa mimi kwa inferiority complex zangu nitaanza kuku attack na kutaka respect by force I will never get the chance to be respected by that kind of style for in jf most of people are very analytical. For that case huwezi ku influence change kwakulalamika but unaweza kwa nguvu ya hoja and thats what I meant.

Sasa kama uongozi unadhani ni mbaya mbona hukuweka wale unaodhani ni wazuri kwako au basi mbona huja gombea ukawashinda? Kama wananchi hawako jinsi utakavyo; toa wazo mbadala jinsi ya kuwafanya wawe utakavyo na usilazimishe tuconivice that is a viable strategies kama utaweza ndipo tutaku appreciate. Vinginevyo ndo maana wenye aibu ya kutongoza wanabaka au wanalewa kwanza ila wanaojua kuimbisha.....sorry for these but I have to, kufanya somo lieleweke.
 
Mwanakijiji you r very wise and hunajazba I appreciate you.

Lakini kidogo nijaribu kueleza what I mean...hakuna mtu anaweza kukupa nafasi kufanya what you wish to happen; everybody has his/her objective in life. Sasa to be authority in whatever school of thought depends on how smart you are to penetrate the existing ideas or system and take it to the direction you want...respect is not earned by force. Ndiyo maana kwa njia yako umepata heshima kubwa kwenye JF na mimi hata nitamani vipi kama sinta kuwa na better strategies ya kuheshimika kuwavuta watu nikuondoe wewe kwenye chart I will never get that chance so for this case you are smarter than me. sasa mimi kwa inferiority complex zangu nitaanza kuku attack na kutaka respect by force I will never get the chance to be respected by that kind of style for in jf most of people are very analytical. For that case huwezi ku influence change kwakulalamika but unaweza kwa nguvu ya hoja and thats what I meant.

Sasa kama uongozi unadhani ni mbaya mbona hukuweka wale unaodhani ni wazuri kwako au basi mbona huja gombea ukawashinda? Kama wananchi hawako jinsi utakavyo; toa wazo mbadala jinsi ya kuwafanya wawe utakavyo na usilazimishe tuconivice that is a viable strategies kama utaweza ndipo tutaku appreciate. Vinginevyo ndo maana wenye aibu ya kutongoza wanabaka au wanalewa kwanza ila wanaojua kuimbisha.....sorry for these but I have to, kufanya somo lieleweke.

Felister, ukisikia wanafalsafa wanaanza kugombea madaraka basi ujue kuwa wale wenye madaraka wameshindwa kifalsafa! Hii paradox ya kwanini watu wenye falsafa nzuri na wenye kuchambua mambo hawagombei kuongoza imekuwepo tangu enzi za kina Socrates na Plato (soma "Republic") na utaona kuwa ni paradox ya mgongano wa mambo mengi sana.

Sasa, uzuri wa falsafa au hoja fulani hauonekani kwa mwanafalsafa kugombea uongozi na hili ndilo kosa ambalo nimeliona mara nyingi pale wasomi wanapochukuliwa kuwa ni viongozi! Afrika kwa ujumla wake imeangushwa siyo na wasio wasomi bali na wasomi waliotaka kuwa viongozi!

Lakini zaidi ni kuwa kama mtu hasomi makala zangu au maandishi yangu vizuri atashindwa kuona mapendekezo ambayo tunayatoa na ambayo kwa kiasi kikubwa mengine yamefanyiwa kazi. Tofauti na waandishi wengine, karibu mara zote ninaandika nikitoa mapendekezo ya fikra mbadala na hiki ndicho kiini cha "mapambano ya kifikra".

Mapambano haya yana lengo la kuonesha udhaifu wa fikra zilizopo (kwa njia ya kukosoa) na kuonesha nguvu ya fikra mbabala (kwa njia ya kuzipendekeza). Sasa uzuri wa fikra bora ni kuwa haijalishi nani yuko madarakani kwani uzuri wake hautegemei mtoaji wake (the truths of such ideas do not depend on the person promulgating them). Naweza kuwa maskini kabisa na nisiye na jina lolote la kisiasa lakini fikra zangu nikizipendeza kwa hoja mtu yeyote anaweza kuzikumbatia au kuzipinga na uzuri wake hautegemei mimi kuja kuzitekeleza.

Kuelewa hili basi utaona kuwa watawala wakikubali uzuri wa hoja na kuzifanyia kazi basi hawatakuwa na wasiwasi kuwa kuna mtu anataka kuwatoa madarakani. Hii ni hofu isiyo na msingi.

Hata hivyo, kuna wakati ambapo mstari unavukwa ambapo wanafalsafa wanataka kuwa watawala. Mara nyingi wakifanya hivi mwisho wao si mzuri sana. NI kwa sababu ni vizuri watawala waendelee kutawala, na wanafalsafa waendelee kukosoa na kuiamsha jamii. Kwani, wote wakiishia kuwa watawala basi falsafa inakuwa imehujumiwa, na mchango wa fikra huru kuharibiwa.
 
"Kuelewa hili basi utaona kuwa watawala wakikubali uzuri wa hoja na kuzifanyia kazi basi hawatakuwa na wasiwasi kuwa kuna mtu anataka kuwatoa madarakani. Hii ni hofu isiyo na msingi."

I concur with you!!!

Thats actually what used to be especially enzi za ...zidumu fikra sahihi za Felister... and sowhat still the main problem of Tanzania's politics. Fortunately huo ushamba unaanza kuondoka taar'tibu. I thank JK for that; for his politics tosome extent zimepunguza ubabe na kuwazia watu vibaya na hii itatoa nafasi kwa watu kuja na phylosophy mbadala so in a long run people would be respected not for who they are but what they can do and also for wababaishaji their days are numbered....
 
Back
Top Bottom