Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Pamoja na ushabiki wangu mkubwa kwa Baba wa Taifa nikiwa mwanafunzi wake nambari moja katika mwamko wa kifikra nimekuwa na matatizo makubwa sana ya kifikra na baadhi ya maamuzi, hatua au mipango aliyochukua au kufanya. Kwamba kwanini kwa mfano, hakuendeleza sekta ya madini kwa kiasi kikubwa na kuamua kusubirri kwa muda mrefu, kwanini aliona ni bora kuwa na chama kimoja mara baada ya uhuru badala ya vyama vingi, kwanini x,y,z
Nimekuwa nikiamini kuwa kuna mambo ambayo tungeweza kufanya au mengi sana tungeweza kufanya wakati ule ambayo leo yangetufikisha "mbali". Tatizo ni kuwa hatukuyafanya.
Nikiwa nimetingwa na fikara namna hiyo nikakumbuka kijitabu (pamphlet) yake moja ambayo aliandika kile kitu ambacho baadaye tukawa tumezoea sana nacho kinaitwa "Kupanga ni kuchagua" yaani "To plan is to choose". Nimekipitia tena na humo anaeleza kwa kirefu kwanini hawakuweza kufanya kila kitu kwa wakati mmoja na kulazimika kuweka kipaumbele kutegemea na malengo ya kitaifa na mambo mengine yakiwa deferred baadaye.
Ninapoangalia jinsi tunavyojaribu kufanya mambo mengi sana kwa wakati mmoja ninajikuta nikishuhudua kuwa kwa wakatimmoja mambo mengi tunajaribu kuyafanya bila tija. Tunabudi kila aina ya mikakati, na miradi lukuki lakini mwisho wa siku tunajikuta kuwa tunafanya kidogo!
Hapa nikakumbuka kanuni ya diminishing returns ambayo naamini ina apply kwa Tanzania sasa.
Hoja yangu kwako na swali ambalo unaweza kusaidia kufikiria katika mwanga wa tunachoona kinaendelea nchini sasa katika ujumla wake, unafikiri tumepanga vizuri au tumechagua vizuri au kimojawapo hatujakifanya vizuri? Is in planning that we went amiss or is it in the choosing? Au ni katika kutekeleza kile tulichochagua ndiko kwenye tatizo?
Lakini sasa nimeelewa kuwa ni lazima tuchague, kwani tukichagua vizuri tutajikuta tumepanga vizuri!
Nimekuwa nikiamini kuwa kuna mambo ambayo tungeweza kufanya au mengi sana tungeweza kufanya wakati ule ambayo leo yangetufikisha "mbali". Tatizo ni kuwa hatukuyafanya.
Nikiwa nimetingwa na fikara namna hiyo nikakumbuka kijitabu (pamphlet) yake moja ambayo aliandika kile kitu ambacho baadaye tukawa tumezoea sana nacho kinaitwa "Kupanga ni kuchagua" yaani "To plan is to choose". Nimekipitia tena na humo anaeleza kwa kirefu kwanini hawakuweza kufanya kila kitu kwa wakati mmoja na kulazimika kuweka kipaumbele kutegemea na malengo ya kitaifa na mambo mengine yakiwa deferred baadaye.
Ninapoangalia jinsi tunavyojaribu kufanya mambo mengi sana kwa wakati mmoja ninajikuta nikishuhudua kuwa kwa wakatimmoja mambo mengi tunajaribu kuyafanya bila tija. Tunabudi kila aina ya mikakati, na miradi lukuki lakini mwisho wa siku tunajikuta kuwa tunafanya kidogo!
Hapa nikakumbuka kanuni ya diminishing returns ambayo naamini ina apply kwa Tanzania sasa.
Hoja yangu kwako na swali ambalo unaweza kusaidia kufikiria katika mwanga wa tunachoona kinaendelea nchini sasa katika ujumla wake, unafikiri tumepanga vizuri au tumechagua vizuri au kimojawapo hatujakifanya vizuri? Is in planning that we went amiss or is it in the choosing? Au ni katika kutekeleza kile tulichochagua ndiko kwenye tatizo?
Lakini sasa nimeelewa kuwa ni lazima tuchague, kwani tukichagua vizuri tutajikuta tumepanga vizuri!
Last edited: