chiembe
JF-Expert Member
- May 16, 2015
- 12,009
- 20,683
Nadhani hali si shwari kati ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera na wanasiasa wa Mkoa huo. Maneno ya Mwijage ni kama vile anatupa vijembe kwa mkuu huyo wa Mkoa.
Itakumbukwa kwamba wakati akiingia kagera, Chalamila alikuwa akitoa kauli kwamba Diwani au mbunge akizingua anamuweka ndani, na alikuwa akiongelea masuala ya stendi na soko. Ikumbukwe mbunge wa Bukoba ni Naibu Waziri, na mbunge wa Karagwe ni Waziri. Haijulikani vitisho hivyo alivielekeza kwao ama laa.
Pia alikuwa akitishia kuweka rumande madiwani, na pia hivi karibuni Kuna story ya Binti kupata ujauzito na kwamba alishindwa kuripoti shule, Chalamila akasema Diwani anatetea hao wanaohusika, akasema na yeye akamatwe.
Nadhani Kuna kutunishiana misuli kati ya RC na wanasiasa wa Mkoa huo. Kisiasa, wenye kura(wabunge na madiwani) watamdondosha Chalamila.
Mwijage ndio senior kwa.wabunge wote wa kagera, na ndiye Mwenyekiti wa umoja wao.
Je Chalamila anakosea wapi? Au Wana kagera ndio wanakosea?
Nimekaa paleeee......kama wasiposuluhishwa, naona mtu akiondoka kagera.
Tasi bota waitu