NADHARIA Kuna watu hutoka ndani ya miili yao

Taarifa hii ni nadharia tu, tumeitolea ufafanuzi kwa kadiri ilivyowezekana
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Hivi ni kweli kuwa kuna watu ambao hutoa nafsi zao ndani ya miili yao (Astral Projection)?

1681131145876.png
 
Tunachokijua
Kutoka ndani ya mwili (Astral Projection) ni tukio la kiimani ambapo inaelezwa kuwa mtu anatengana na mwili wake kifikra au kiroho, hali hii humfanya mtu kwenda popote duniani kimawazo. Katika tukio hili inaelezwa kuwa roho ya inakuwa imetengana na mwili wa nyama kiimani/ kifikra.

Kutoka ndani ya mwili (Astral Projection) kumekuwa kukifanywa katika tamaduni na dini kadhaa ulimwenguni, style Caster wanabainisha kwamba jambo hili limeanza tangu jamii za kale za Misri lakini pia lilijitokeza kwenye dini ya Kiislam na pia linaendelea kufanyika katika dini nyingine bara la Asia.

Aidha, kwa upande wa Waislam inaelezwa kuwa katika Quran Mtume Muhammad alisafiri kwa mtindo huu kutoka Makka hadi Yerusalemu, na kisha Yerusalemu kwenda mbinguni tukio ambalo Waislam huliita Isra Wal Miraj. Zaidi ya hayo, inaelezwa kuwa Astral Projection inafanywa kwa kiasi kikubwa katika jamii na dini ya Wahindu na Mabuddha barani Asia.

Je ni kweli mtu anaweza kutoka nje ya mwili wake?
Jamiiforums imepitia machapisho ya tafiti mbalimbali tumebaini kwamba zipo nadharia (Imani) kadhaa zinazoamini kuwa ni kweli mtu anaweza kutoka nje ya mwili wake. Wataalamu wa masuala ya ndoto na imani wanaeleza kwamba kwamba mtu anao uwezo wa kuamua kwa makusudi kutoka nje ya mwili wake, na kusafiri na kwenda mbali, mahali popote anapotaka na kurudi ikiwa atafatuata taratibu maalum.

Wataalamu wa Astral Projection wanasema kitendo hicho ni salama na mtu yeyote anaweza kufanya, kinachohitajika ni kuwapo kwa utulivu wa akili wa hali ya juu na uwezo kuulazimisha ubongo ukae katika hali ya kutowaza kitu chochote kwa muda fulani, na kuhakikisha hakuna wasiwasi au hofu yoyote moyoni.

Ili kutoka nje ya mwili wako wataalamu wanashauri kufuata hatua zifuatazo:
  • Oga Na Vaa Nguo Safi Zisizo Bana na uende sehemu yenye utulivu isiyo na kelele ya aina yoyote
  • Lala Chali Mgongo Ukiwa Umenyooka vema huku umefumba macho.
  • Ukipata vishawishi kujigeuza au kujitingisha usivizingatie wala Usijishike wala kujitingisha.
  • Usitingishe Macho Wala Kuchezesha Mwili Wako.
  • Subiri Na Uconcerntrate Kwenye Pumzi (Hapa unakuwa unaudanganya ubongo kuwa mwili unaota)
  • Ukiweza kujizuia Kujigeuza Geuza Au Kujikuna Ubongo Utajua Umelala na Utaruhusu Mwili kuachia kinga ya Paralysis au Ganzi Salama Ya Mwili Mzima ambayo Huwa Inakinga Miili Yetu Kutokujiumiza Wakati wa Kuota Mfano: sleep walking(unaota huku unatembea)
Ingawa wataalamu wanatofautiana kwenye idadi ya hatua za kufuata ili kutoka nje ya mwili wengi wamesisitiza kuwa sehemu tulivu isiyo na kelele, kuvaa nguo zisizobana, kulala chali na kutazama juu.

Hivyo, japokuwa wataalamu wamefafanua kwamba jambo hili linawezekana katika ulimwengu wa kiimani na kifikra, jamiiforums suala la kutoka nje ya mwili utalichukulia kama nadharia ya kiimani kwa sababu mawazo yote yanayofafanua jambo hili hayawezi kuthibitika kisayansi.
Hii yote ni rahisi kufanyika kupitia meditation, hata nitume na manabii waliitumia meditation kuwasiliana na miungu yao...

Hata biblia inaikubali meditation...ni njia nzuri zaidi ya kupunguza msongo wa mawazo ya maisha ya kilasiku...

Binafsi Huwa na meditate sometimes kukiwa na haja ya kufanya hivyo....but kutoka nje ya mwili(astral projection) ni level ya juu zaidi! Sio kwa beginners....hufanywa hata na wengi tu..,hata mitume na manabii mnaowasikia.
 
Sasa ukishindwa kurudi itakuaje, kama umeenda Tanga na pisi zikakung'ang'ania?
Kuna hatua za kufuata mkuu, zinazohitaji umakini wa hali ya juu mno!.

Ndio maana wengi wanaiogopa sana hii meditation ya kutoka nje ya mwili.

hii pia huwaletea wengi utajiri, nyadhfa kubwakubwa za kuteuliwa.

Ukikosea kidogo tu....kwenye hii meditation kidogo tu! Umekwenda na Maji!. Unapotelea huko mazima mzee, you are dead!

Mf mdogo tu....wengi unaosikia wamekufa ghafla wakiwa usingizini. Huwa ni hii meditation ya kutoka nje ya mwili... astral projection.
 
Ukikosea kidogo tu....kwenye hii meditation kidogo tu! ....umekwenda na Maji!.....unapotelea huko mazima mzee!...you are dead!

Mf mdogo tu....wengi unaosikia wamekufa ghafla wakiwa usingizini.....Huwa ni hii meditation ya kutoka nje ya mwili... astral projection.
Hayo uliyo yaandika hayana ukweli...

Ukiona mtu amekufa wakati wa AP ujue siku ilikuwa imefika.
 
Hivi ni kweli kuwa kuna watu ambao hutoa nafsi zao ndani ya miili yao (Astral Projection)?

Hivi umeshawahi kumsikia mbwa akibweka ama pia akitoa mlio wa ajabu kama vile anaomboleza?

Mbwa akibweka kama ilivyokuwa kawaida yake, ni dhahiri huashiria kuwa anakiona kiumbe kilichopo mbele ya macho yake kwa jinsi ya asili yake, na kikiwa katika maumbile yake halisi, yaani kikiwa katika muonekano wa kimwili yaani "physical state" Katika hali hii huashiria anaweza kukabiliana nacho katika hali ya kimwili.

Lakini wajuzi wa mambo ya kiroho husema pale uonapo mbwa akilia na kutoa mlio wa ajabu kama vile anaomboleza, basi hapo huashiria kuwa anakiona kiumbe mbele ya macho yake katika "astral dimension" yaani kikiwa katika maumbile ya kiroho, yaani kikiwa katika muonekano usiokuwa wa kawaida wa kimwili. Hapo huashiria kuwa mbwa hana uwezo wa kukabiliana na kiumbe akionacho katika hali ya kimwili.
 
Kuna hatua za kufuata mkuu, zinazohitaji umakini wa hali ya juu mno!.

Ndio maana wengi wanaiogopa sana hii meditation ya kutoka nje ya mwili.

hii pia huwaletea wengi utajiri, nyadhfa kubwakubwa za kuteuliwa.

Ukikosea kidogo tu....kwenye hii meditation kidogo tu! Umekwenda na Maji!. Unapotelea huko mazima mzee, you are dead!

Mf mdogo tu....wengi unaosikia wamekufa ghafla wakiwa usingizini. Huwa ni hii meditation ya kutoka nje ya mwili... astral projection.
Pepe kale
 
Hivi ni kweli kuwa kuna watu ambao hutoa nafsi zao ndani ya miili yao (Astral Projection)?


Hili suala la kulala chali wengi linawasumbua kwa kuwasababishia kukoroma na kupatwa na jinamizi la kukabwa koo na kuhisi kuna mtu/kitu kimezuia kifua chako kwa kukikandamiza. Hili limekaaje mkuu na utaratibu mzima wa kutoka nje ya mwili?
 
Kuna hatua za kufuata mkuu, zinazohitaji umakini wa hali ya juu mno!.

Ndio maana wengi wanaiogopa sana hii meditation ya kutoka nje ya mwili.

hii pia huwaletea wengi utajiri, nyadhfa kubwakubwa za kuteuliwa.

Ukikosea kidogo tu....kwenye hii meditation kidogo tu! Umekwenda na Maji!. Unapotelea huko mazima mzee, you are dead!

Mf mdogo tu....wengi unaosikia wamekufa ghafla wakiwa usingizini. Huwa ni hii meditation ya kutoka nje ya mwili... astral projection.
Braza huu ni uchawi unaitwa taamuli mm ni expert
 
Ndoto ni tukio halisi la maisha ya kiroho yanayoendelea, kupitia ndoto nimeshawahi kufika mahali napakumbuka zaidi ya Mara tatu
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom