Kuna sheria kuhusu hili.......?

Dr. Chapa Kiuno

JF-Expert Member
Sep 11, 2009
443
18
Wadau, leo asubuhi wakati natokea nyumbani kuja kazini katika daladala niliyopanda kulikuwa na ugomvi kati ya kondakta na mwanafunzi. Ugomvi huu ulihusu kitendo cha mwanafunzi kugoma kusimama ampishe mtu mkubwa akae n hiyo ilifuatia baada ya mwanafunzi yule kumuahidi akiwa chini kuwa angelipa nauli ya mtu mzima hivyo asimzuie kupanda n mambo yalibadilika mwanafunzi yule wa kike wa Kisutu galz kugoma kunyanyuka kwenye kiti n pia kulipa pesa ya mtu mzima. Ugomvi ukaanza huku konda akimtaka asimame ili ampishe mtu mzima lakini binti yule akagoma.

Je, kuna sheria inayosema mwanafunzi AKAE au ASIMAME?

Nisaidieni kwa hilo.
 
Hakuna sheria ndugu yangu inayosema mwanafunzi akae au asimame kwasababu sheria ya usalama barabarani hairuhusu abiria kusimama, so mwanafunzi anapopanda basi ni abiria.. kusimama kwa mwanafunzi ni heshima tu kwa mtu alie kuzidi umri hii ni kutokana na malezi yetu ya kiafrika.
 
Sheria hiyo haipo kabisa, na sijui ni malegislators wa wapi wangel'weza kutengeneza sheria kama hiyo. ila kwa uzoefu nilionao ni kwamba inaonyesha tu ustaarabu fulani mwanafunzi anaposimama na kumwachia mkubwa aketi kwenye situation kama hiyo.
 
Sheria hairuhusu kabisa gari kutembea akati watu wamesimama ndani ya gari. Sheria inamtaka kila abiria ndani ya gari awe amekaa kitako na kufunga mkanda kabla gari alijaanza kuondoka.

Vile vile sheria imempa nafuu mwanafunzi kulipa pesa pungufu ya nauli a mtu mzima. Hivyo mwanafunzi akiwa ametimiza vigezo vyote vya uanafunzi kama kitambulisho haruhusiwi kulipa nauli ya mtu mzima
 
Sheria Tanzania hatuzifuati kabisa katika mambo mengi kwa kuwa hali halisi inaonyesha ukifuata sheria ndio unajichelewesha mambo yako kufanikiwa.Makondakta wamechukulia udhaifu huu kuwanyanyasa wanafunzi hasa kwa vile nauli wanayolipa ni ndogo.Nakumbuka wanafunzi walikuwa wanalipa shs 50 na nauli ilipopanda kuwa shs 100 waliandamana kupinga ongezeko hilo na ndipo aliyekuwa mkuu wa mkoa Kandoro aliwaahidi kuwa wakubaliane na mabadiliko na watakuwa wanakaa kwenye viti kama abiria wengine.
Kwa desturi zetu za kiafrika ni heshima kumpisha mkubwa wako/mama mjamzito au mama mwenye mtoto kiti.Lakini hii inapotea kabisa Dsm kwa sababu ya shida ya usafiri,na vilevile imewafanya wanafunzi kuwa na kiburi sana na wagomvi kitu ambacho kinawafanya abiriawakati mwingine wasiwatee pale ambapo makonda wanawanyanyasa
 
Lakini hii inapotea kabisa Dsm kwa sababu ya shida ya usafiri,na vilevile imewafanya wanafunzi kuwa na kiburi sana na wagomvi kitu ambacho kinawafanya abiriawakati mwingine wasiwatee pale ambapo makonda wanawanyanyasa

Kuhusu swala la kiburi nakuunga mkono mkuu maana hilo nimeliona leo asubuhi ambapo mwanafunzi wa Kisutu galz aligoma kabisa kunyanyuka kitini na pia akawa anadai chenji kutoka kwa kondacta.
 
Hakuna sheria ndugu yangu inayosema mwanafunzi akae au asimame kwasababu sheria ya usalama barabarani hairuhusu abiria kusimama, so mwanafunzi anapopanda basi ni abiria.. kusimama kwa mwanafunzi ni heshima tu kwa mtu alie kuzidi umri hii ni kutokana na malezi yetu ya kiafrika.

Jibu zuri sana hili. Nadhani sheria inawaruhusu wanafunzi walipe nusu. Akili za konda zina-translate hii sheria kuwa na maana kuwa mwanafunzi anatakiwa kusimama. Kama hii ingekuwa sheria kweli, kungeleta conflict of laws. Ulilosema ni kweli, sheria za barabarani haziruhusu mtu kusimama. Hivyo ungetakiwa umwambie konda twende kituoni....lol
 
Back
Top Bottom