Kuna nini M-KOBA?

LEARNED BROTHER

JF-Expert Member
Mar 7, 2012
548
735
Wakuu, huduma ya M-KOBA inayotolewa kupitia kampuni ya mawasiliano ya VODACOM imekuwa maarufu miongoni mwa watumiaji wake hasa makundi ya watu wenye malengo mbalimbali kama vile kusaidiana katika masuala mahsusi n.k. Hata hivyo, katika siku za karibuni kupitia makundi sogozi ya "whatsapp" imeonekana kuna shida.

Kumekuwa na uvumi kuwa pesa zilizohifadhiwa ni kama zimeibwa au kumekuwa na shida kwa wahusika kuzitoa au kupata "statement" ya salio la kundi.

Leo, nimesikiliza "voice note" ikieleza changamoto hiyo, na baadaye usiku huu nikaona tena meseji ifuatayo:-

"Jamani habari
Nasikia M-KOBA imeibiwa hela huko Vodacom
Mlio na M koba hebu checking balance zenu
Nasikia wafanyakazi wa Voda ndio wameiba,
Vikundi vinalalamika ukiuliza. Balance hupati,"

Binafsi ni mwanachama wa makundi mawili ambayo tumehifadhi pesa zetu kwenye M-KOBA. Kundi la kwanza tuna salio 15 mil, na jengine tuna salio 9 mil.

Baada ya meseji za "alert", usiku huu nimejaribu kuomba taarifa ya salio la fedha kwa makundi yote lakini sijajibiwa. Hali hiyo imenipa mashaka, na nimewashirikisha wenzangu nilionao kindini.

Aidha, nimeona ni vyema pia jambo hili nililete humu jamvini ili kupata taarifa zaidi ikiwezekana toka kwa wahusika wenyewe, au kutoa hadhari kwa wengine watakaoguswa.
 
Anything can happen lakini pesa kamwe haziwezi kupotea....ila wengine humu watoto kuna Bank inaitwa Meridian Biao...ilishaiba fedha za wateja...Bank kuu ndio "the last resort"...lakini mpaka leo Mungu ndie anayejua.
 
Wakuu, huduma ya M-KOBA inayotolewa kupitia kampuni ya mawasiliano ya VODACOM imekuwa maarufu miongoni mwa watumiaji wake hasa makundi ya watu wenye malengo mbalimbali kama vile kusaidiana katika masuala mahsusi n.k. Hata hivyo, katika siku za karibuni kupitia makundi sogozi ya "whatsapp" imeonekana kuna shida.

Kumekuwa na uvumi kuwa pesa zilizohifadhiwa ni kama zimeibwa au kumekuwa na shida kwa wahusika kuzitoa au kupata "statement" ya salio la kundi.

Leo, nimesikiliza "voice note" ikieleza changamoto hiyo, na baadaye usiku huu nikaona tena meseji ifuatayo:-

"Jamani habari
Nasikia M-KOBA imeibiwa hela huko Vodacom
Mlio na M koba hebu checking balance zenu
Nasikia wafanyakazi wa Voda ndio wameiba,
Vikundi vinalalamika ukiuliza. Balance hupati,"

Binafsi ni mwanachama wa makundi mawili ambayo tumehifadhi pesa zetu kwenye M-KOBA. Kundi la kwanza tuna salio 15 mil, na jengine tuna salio 9 mil.

Baada ya meseji za "alert", usiku huu nimejaribu kuomba taarifa ya salio la fedha kwa makundi yote lakini sijajibiwa. Hali hiyo imenipa mashaka, na nimewashirikisha wenzangu nilionao kindini.

Aidha, nimeona ni vyema pia jambo hili nililete humu jamvini ili kupata taarifa zaidi ikiwezekana toka kwa wahusika wenyewe, au kutoa hadhari kwa wengine watakaoguswa.
Wewe wafanyakazi wao hawakuhusu, pesa zako zipo tu Voda hawakukupa sharti la kuzilinda dhidi ya wafanyakazi wao.
 
Kwa hiyo wafanyakazi wa benki wakiiba pesa za benki na pesa za wateja zitakuwa zimepotea?
Hii itakuwa ni akili za kindezi kwa 100%.
 
M-koba ni salama kabisa.
Kutokupata sms ya salio inawezekana lilikuwa tatizo la mtandao tu. Na hii huwa inatokea.

Uzuri wa M-koba umerahisisha yale mambo ya kuhofia pesa kutumiwa na m/hazina/Viongozi.

Pesa haiwezi kutolewa pasipo utatu wao (M/kiti, Katibu na M/hazina) kuidhinisha. Na hata wakiidhinisha wanachama lazima wapate notifications.
 
Account Za Banks Ndiyo Salama Kuliko M•Koba Viongpzi Wakiungana Wanatoa Mkipata Notification Wao Wamefhamilia Kutenda Hayo
 
Account Za Banks Ndiyo Salama Kuliko M•Koba Viongpzi Wakiungana Wanatoa Mkipata Notification Wao Wamefhamilia Kutenda Hayo
 
Back
Top Bottom