Chakochangu
JF-Expert Member
- Mar 21, 2011
- 2,668
- 2,158
Ukweli ni kwamba hakuna tatizo lolote kiafya litakalomkuta mtoto. hii logic IPO kimila na desturi au kijamii si vizuri kutembea na MTU asiye mumeo wakati inanyonyesha.
Mkuu upo sahihi, Niongeze kidogo tu hapo; Ipo hivi "Kama wewe na Mkeo/Mumeo mna mtoto ananyonya swala la kujamiiana nyinyi kama baba na mama wa mtoto halina tatizo kwa mtoto.
Tatizo linakuja mmoja wenu anapotoka nje yaani kujamiiana na mtu mwingine bila ya kuoga ili kuondoa jasho ,halafu anarudi nyumbani anamshika, anampakata mtoto lile jasho linamuasiri mtoto.
Vilevile kwa mama ambae ametoka nje bila kinga, pekupeku, na yale manii ya mwanamume aliyetoka naye baadhi yanaenda kwenye damu ya mama na kusafirishwa hadi kwenye maziwa yake ambayo mtoto wake hunyonya yakiwa na virutubisho vya manii ya mtu mwingine ambaye si baba yake mzazi humuathiri mtoto .
Wazee wetu husema kubemenda au kumkanyaga mtoto