Kuna haja gani kumtazama marehemu ikiwa tunamfahamu na tumeishi naye miaka mingi kabla ya kifo?

Kama kuna ulazima wa kuaga ilitakiwa ifanyike ngazi ya familia tu, kuruhusu kadamnasi nayo iage ni kutoa mwanya hata kwa waliokuwa wanamtmb€@ mkewe kupita na kumsanifu tu.
 
Kuna faida gani labda ya Kimantiki Watu Kulazimisha (Kung'ang'ania) Kumuangalia Marehemu akiwa 'Jenezani' tena ameshalala Usingizi wake wa Milele na kwamba hata ukipita Kumuaga kwa kumsogelea au kumgusa na kulia kila aina ya kilio wala hawezi kukujua sana sana utakuwa ni kama vile unapaka tu Rangi upepo?

Haya Waaga 'Marehemu' hebu nijibuni.
Nilijiuliza sana jambo hilo tangu nikiwa mtoto mdogo. Baadaye niliacha mwenyewe kuangalia maiti baada ya kuona hakuna anayekubali kuacha kukodolea mimacho maiti isiyoona wala kuhisi chochote. Nakuunga mkono, sioni maana yoyote ya kuhangaika na mwili mfu zaidi ya kuuzika

Aidha, kama ni heshima anapaswa kupewa aliyehai ili aone anavyoheshimiwa, si baada ya kufa. Uhai ukikatika, mwili hubaki mavumbi tu. Tusiingie gharama za kumpamba marehemu bali tujikite kumsaidia au kumponya maradhi akingali hai. Auone upendo na faraja yetu kwake.

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Urithi wa mila na desturi kutoka magharibi, kwa wazungu vilitiathiri sana ndio maana waafrika mfumo wetu wa kuzika ilikua mtu akifa tunahama hilo eneo na kwenda mbali maana tuliamini kifo ni laana na jamii nyingine mtu akifa hakuna kuaga walikua wanaufunga mwili na wanachaguliwa wanaume wa shoka wanaubeba na kwenda nao mbali na kuchimba shimo huko na kuufukia kimila na kurudi nyumbani tena haikuepo masanduku haya ya sasa.

Tukirudi kwenye mila zetu waafrika tutaishi muda mrefu sana na tutakua na furaha
Sawa kabisa!

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Kila kitu cha mwafrika kilifanyiwa propaganda kionekane kibaya na kweli walifanikiwa, naona hadi wasomi uwezo wa kujiuliza kua hizi sio tamaduni zetu haupo, ok hoja hutomwona tena sawa nini utakiongeza au utapunguza baada ya kuona ile maiti? Sio kila mila ni ya kupokea na kuiendeleza natamani tupate vizazi vya kuhoji, naamini sasa vizazi hivi vya sasa vingetawaliwa na wakoloni kamwe visingepigania uhuru wa nchi zao kama wazee wetu
 
Huu mnakasha ni mpana kwa kuwaza karibu huwezi kuujadili, inajulikana mwanadamu anazaliwa, anaishi, na atakufa sasa kama ameshazaliwa, ameishi, kwa nini akifa ndio tuseme tunaaga wakati tulijua kufa kupo na akifa hatorudi na hatutomwona tena
 
The act is more emotional than logical.

Nikitumia akili yako naweza hoji "Kuna logic gani mke na mme kulala kitanda kimoja usiku mzima kila siku? au sababu ni uhaba wa vitanda?"

Kuaga miili ni utaratibu wa toka enzi na enzi, tena enzi za machifu, machifu waliagwa kwa kusindikizwa na watu kadhaa (yaani wazima kadhaa waliuliwa na kuzikwa pamoja na chifu).

Unlike robots mwanadamu ana tumia hisia pamoja na logic. Emotional acts can not always be explained logically, ndio maana paka leo wanasayansi wameshindwa kutengeneza complete Artificial Intelligent robots.
 
Huu mnakasha ni mpana kwa kuwaza karibu huwezi kuujadili, inajulikana mwanadamu anazaliwa, anaishi, na atakufa sasa kama ameshazaliwa, ameishi, kwa nini akifa ndio tuseme tunaaga wakati tulijua kufa kupo na akifa hatorudi na hatutomwona tena
Ile ni kusherehesha tu kuaga mwili wa marhemu sio ibada hata neno la kuaga inatokana na kuagiza na unaweza ukamuaga au ukamuagiza mtu alie macho, sio alielala, sasa utaagaje kitu kisicho na uhai?.
Ni kweli KABISA maiti unaweza ukayasindikiza sehemu inayoenda kuhifadhiwa ambaye ni kaburini ndio maana kwa waislam, hakuna kuaga maiti bali kuna kumsindikiza maiti kwenye nyumba yake ya milele tu.
 
Na vipi kuhusu Sendoff
Hii ndio inanikera kabisa. Wanaotakiwa kumuaga binti ni wana ndugu tu, sasa utakuta mtu anachangisha kila atakaekutana nae. Nakumbuka miaka ya nyuma mzazi anafanya shughuli hii nyumbani au kama ni kwenye ukumbi basi wahusika ni wanafamilia tu.
Zamani binti akiolewa kuonana nae tena ni majaliwa sio kama siku hizi. Kama tunaiga umagharibi mbona wao hawachangiani? Nani alianzisha mambo haya. Mpaka mtu anakosa amani kwa kuwa hajamchangia mtu?
 
Limekaa kisaikolojia zaidi, hakuna mtu anaumia kama ambaye hajashuhudia maziko ya mpendwa wake.

Sijui nimeeleweka hapo kwenye 'kushuhudia'.

Ipo hivi pale hatuagi bali tunaenda kushuhudia tu, mwamba ndio kalala hapa kimya na soon tunamzika. Kwaheri.

Tena kwa kuongezea hapa. Ukishashuhudia unapata faraja kwamba mwamba kaenda na unabaki na amani na unamfuta kichwani na maisha yanaendelea bila kuwaza au kufikiri utamuona tena! na unajifunza one day nitaondoka hapa duniani kama wengine... inarudisha na utu wa kuthamini wengine ukijua wewe ni mpitaji tu kama wengine walipita....
 
Kuna faida gani labda ya Kimantiki Watu Kulazimisha (Kung'ang'ania) Kumuangalia Marehemu akiwa 'Jenezani' tena ameshalala Usingizi wake wa Milele na kwamba hata ukipita Kumuaga kwa kumsogelea au kumgusa na kulia kila aina ya kilio wala hawezi kukujua sana sana utakuwa ni kama vile unapaka tu Rangi upepo?

Haya Waaga 'Marehemu' hebu nijibuni.
Binafsi, sionagi ulazima ila ni jambo la hiari sana kuliko ulazima
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom