Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,802
- 71,229
Nimekuta mijadala huko X watu wakimjadili Sabaya kuwa naye anapaswa kupewa kazi ili kuinusuru CCM kama mwenzake Makonda ilivyo tokea.
Ila katika pitapita yangu mitandaoni nimegundua kumbe Sabaya yuko kifungoni hadi sasa baada ya kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja (kifungo cha nje) na masharti mengine baada ya kukiri kosa katika mfumo wa plea bargain.
Kwa maana hiyo kifungo hicho cha mwaka mmoja kwa makosa ya jinai kinamnyima nafasi ya utumishi wa umma sasa na hata baadae kulingana na sheria zetu.
Au kwa vile ni CCM hakuna anayejali?
======
Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Moshi mkoani Kilimanjaro, imemhukumu kifungo cha nje cha mwaka mmoja aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, baada ya kukiri kosa kwa utaratibu wa ‘plea bargaining’ katika kesi namba 32 ya mwaka 2023.
Makosa hayo ni kuvamia madaraka yasiyo yake na kula njama na kuzuia haki kutendeka baada ya kufanya upekuzi kwa mfanyabiashara mmoja aliyeko Hai mkoani Kilimanjaro.
Sabaya alibakia kwenye kesi namba 2 ya mwaka 2022 baada ya wenzake Sylvester Nyegu, Nathan Msuya, John Aweyo na Antero Asey ambao waliachiwa Septemba 7 mwaka 2022 baada ya kufanya ‘plea bargaining’ na Mwendesha Mashatka wa Serikali.
Tangu kesi hiyo kuanza kwake haikuwahi kusikilizwa kutokana na sababu mbalimbali za kisheria, ikiwamo mahakama kukosa uwezo wa kusikiliza, hakimu kuwa na kazi nyingine nje ya kituo chake cha kazi na kutokamilika kwa upelelezi.
Kesi hiyo iliyofunguliwa na DPP ilisikilizwa na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Salome Mshasha, ambayo jana ilikuwa kuweka nyaraka pamoja na kusomewa maelezo ya awali.
Lakini upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Verediana Mlenza akisaidiwa na Sabitina Mcharo, ulidai kuwa wamepokea barua kutoka kwa mshtakiwa akiomba makubaliano nje ya mahakama na DPP.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa huyo alifanya upekuzi kwa mfanyabiashara mmoja wilayani Hai.
Akisomewa maelezo ya kosa, alidai Januari 19 hadi Machi 30, 2021 kwa nyakati tofauti, Sabaya na wenzake (hawakuwapo mahakamani) katika maeneo ya Kilimanjaro na Arusha, alitumia mamlaka yake vibaya akiwa Mkuu wa Wilaya kumvamia mfanyabiashara, Alex Swai.
Alidai alichukua zaidi ya Sh. milioni 15, kishikwambi, saa na mkufu wa dhahabu na kuagiza mkewe (Gema Maro), Oldasipha Massawe (Mama wa Alex) na Upendo Swai (Dada wa Massawe) kuwekwa katika kituo cha polisi Bomang’ombe.
“January 23, 2021, Sabaya alidaiwa kuagiza Godbless Swai (Kaka wa Swai) apelekwe kwenye nyumba ya mkuu wa wilaya na kumtaka atoe Sh. milioni 50 ili kumsaidia nduguye Alex Swai asipelekwe mahakamani kwa kosa la kukwepa kodi huku wenzake wakijifanya maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Usalama wa Taifa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kwamba fedha hizo zililipwa kwa awamu tatu.
Ilidaiwa kuwa fedha hizo zililipwa Januari 23, Februari 3 na 9 na kwamba Februari 24,2021, familia hiyo iliachiwa na kurejea nyumbani na kisha kuripoti TAKUKURU.
Upande wa utetezi ukiongozwa na Moses Mahuna, Helena Mahuna na Faudhia Mustapher, uliomba mahakama hiyo kumwonea huruma mteja wao na kuongeza kuwa ni kosa lake na kwanza na wazazi mtoto wanamtegemea.
Akitoa hukumu, Mshasha alisema mahakama kwa kuzingatia maelezo ya pande zote mbili, imemtia hatiani chini ya kifungu namba 38 cha Sheria ya Makosa ya Adhabu kifungo cha nje cha mwaka mmoja, bila kukutwa na kosa lolote la jinai.
“Umehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja nje bila kufanya makosa yoyote ya kijinai. Unaweza kukata rufaa (rufani) kama haujaridhika na adhabu, ingawa sitegemei kuwa utatenda kosa ikizingatiwa kuwa umekaa muda mrefu gerezani,”alisema.
Sabaya amesota magereza kwa siku takribani 660 bila dhamana akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na utatatishaji wa fedha.
Ila katika pitapita yangu mitandaoni nimegundua kumbe Sabaya yuko kifungoni hadi sasa baada ya kuhukumiwa kifungo cha mwaka mmoja (kifungo cha nje) na masharti mengine baada ya kukiri kosa katika mfumo wa plea bargain.
Kwa maana hiyo kifungo hicho cha mwaka mmoja kwa makosa ya jinai kinamnyima nafasi ya utumishi wa umma sasa na hata baadae kulingana na sheria zetu.
Au kwa vile ni CCM hakuna anayejali?
======
Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Moshi mkoani Kilimanjaro, imemhukumu kifungo cha nje cha mwaka mmoja aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, baada ya kukiri kosa kwa utaratibu wa ‘plea bargaining’ katika kesi namba 32 ya mwaka 2023.
Makosa hayo ni kuvamia madaraka yasiyo yake na kula njama na kuzuia haki kutendeka baada ya kufanya upekuzi kwa mfanyabiashara mmoja aliyeko Hai mkoani Kilimanjaro.
Sabaya alibakia kwenye kesi namba 2 ya mwaka 2022 baada ya wenzake Sylvester Nyegu, Nathan Msuya, John Aweyo na Antero Asey ambao waliachiwa Septemba 7 mwaka 2022 baada ya kufanya ‘plea bargaining’ na Mwendesha Mashatka wa Serikali.
Tangu kesi hiyo kuanza kwake haikuwahi kusikilizwa kutokana na sababu mbalimbali za kisheria, ikiwamo mahakama kukosa uwezo wa kusikiliza, hakimu kuwa na kazi nyingine nje ya kituo chake cha kazi na kutokamilika kwa upelelezi.
Kesi hiyo iliyofunguliwa na DPP ilisikilizwa na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Salome Mshasha, ambayo jana ilikuwa kuweka nyaraka pamoja na kusomewa maelezo ya awali.
Lakini upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Verediana Mlenza akisaidiwa na Sabitina Mcharo, ulidai kuwa wamepokea barua kutoka kwa mshtakiwa akiomba makubaliano nje ya mahakama na DPP.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa huyo alifanya upekuzi kwa mfanyabiashara mmoja wilayani Hai.
Akisomewa maelezo ya kosa, alidai Januari 19 hadi Machi 30, 2021 kwa nyakati tofauti, Sabaya na wenzake (hawakuwapo mahakamani) katika maeneo ya Kilimanjaro na Arusha, alitumia mamlaka yake vibaya akiwa Mkuu wa Wilaya kumvamia mfanyabiashara, Alex Swai.
Alidai alichukua zaidi ya Sh. milioni 15, kishikwambi, saa na mkufu wa dhahabu na kuagiza mkewe (Gema Maro), Oldasipha Massawe (Mama wa Alex) na Upendo Swai (Dada wa Massawe) kuwekwa katika kituo cha polisi Bomang’ombe.
“January 23, 2021, Sabaya alidaiwa kuagiza Godbless Swai (Kaka wa Swai) apelekwe kwenye nyumba ya mkuu wa wilaya na kumtaka atoe Sh. milioni 50 ili kumsaidia nduguye Alex Swai asipelekwe mahakamani kwa kosa la kukwepa kodi huku wenzake wakijifanya maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Usalama wa Taifa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kwamba fedha hizo zililipwa kwa awamu tatu.
Ilidaiwa kuwa fedha hizo zililipwa Januari 23, Februari 3 na 9 na kwamba Februari 24,2021, familia hiyo iliachiwa na kurejea nyumbani na kisha kuripoti TAKUKURU.
Upande wa utetezi ukiongozwa na Moses Mahuna, Helena Mahuna na Faudhia Mustapher, uliomba mahakama hiyo kumwonea huruma mteja wao na kuongeza kuwa ni kosa lake na kwanza na wazazi mtoto wanamtegemea.
Akitoa hukumu, Mshasha alisema mahakama kwa kuzingatia maelezo ya pande zote mbili, imemtia hatiani chini ya kifungu namba 38 cha Sheria ya Makosa ya Adhabu kifungo cha nje cha mwaka mmoja, bila kukutwa na kosa lolote la jinai.
“Umehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja nje bila kufanya makosa yoyote ya kijinai. Unaweza kukata rufaa (rufani) kama haujaridhika na adhabu, ingawa sitegemei kuwa utatenda kosa ikizingatiwa kuwa umekaa muda mrefu gerezani,”alisema.
Sabaya amesota magereza kwa siku takribani 660 bila dhamana akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na utatatishaji wa fedha.