Kumalizika kwa tembo wetu ni vita kamili kati ya askari wa wanyamapori na majangili, nguvu ya ushirikina

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Sep 10, 2017
10,561
19,062
Huko porini wanapokutana katika makabiliano ya silaha kati ya askari wa wanyama pori na majangili wa nyara za serikali hua hakuna mateka. Ama afe/wafe askari au afe/wafe majangili. Hua ni vita kamili, kubwa, kali na yakikatili sana.

Nimefanya mazungumzo na watu mbalimbali ikiwemo wazee wenye uzoefu wa mambo ya porini na uwindaji na wanaeleza hadithi za kusisimua kama sio kutisha za maisha ya wawindaji hasa wawindaji haramu kwa jina maarufu majangili. Watu hawa ndio sababu ya kumalizika kwa wanyama wetu wakubwa kama vile tembo na faru licha ya ulinzi wa kila aina unaowekwa na mamlaka husika.

Kwa maelezo ya wengi ni kwamba majangili huwa ni walozi na washirikina sana na wanapoingia porini kuwinda tembo au faru au hata simba kiongozi wao wa msafara hua ni mtu mwenye utaalamu wa dawa za jadi maarufu kwa jina la "Fundi". Huyu ndio hutoa melekezo, miongozo na miiko ya uindaji kabda, wakati na baada ya safari.

Inasemekana porini kumejaa miujiza na mauzauza ikiwemo wanyama wakubwa wenyewe kama tembo, faru, simba n.k ni kama vile wanavitu sio vya kawaida ambapo bila kugangwa mwindaji hawezi dumu porini hata kwa muda mchache kwani atararuriwa na kuliwa na wanyama wakali.

Wanasema mnyama kama tembo anahisia kali sana za kuweza kumtambua mtu aliyekwenda kwa ajili ya kumdhuru na akikuwahi anakumaliza. Aidha iwapo utamuua mnyama huyo bila kupatiwa zindiko maalum waweza kutwa na mauzauza na mikosi mingi maishani mwako! Kwa maana hiyo hugangwa kuanzia mtu na vifaa vyote vya uwindaji kama mishale na bunduki.

Tena wawindaji baada ya zindiko huingia sehemu yoyote yenye wanyama wanaowawinda na kuwachagua wawatakao bila wanyama kuwaona au majangili kuonekana na askari wa wanyama pori! Kama ni kundi la tembo jangili atekwenda mpaka kwenye kundi la tembo na atakua anamchagua wa kumpiga kwa kumshika na wanyama hao hutulia tu.

Kwa maelezo niliyoyakusanya ni mara chache sana askari wa wanyama pori wakawaona majangili japo wakati mwingine huwa wametenganishwa na umbali mdogo sana wa hata mita ishirini tu! Inasemekana hii ndio sababu kubwa wanyama wetu wanaendelea kupungua kwa kuuwawa licha ya juhudi kubwa na rasilimali nyingi zinazotumika katika ulinzi wao.

Naomba kupewa darasa na uzoefu kutoka wakongwe wa tasnia hii kama Mshana Jr na wengineo kwamba kwa uzoefu wao hili jambo lina asilimia yoyote ya ukweli Na kama ni hivyo askari wetu nao waanze kutafuta "mafundi" wawagange ili waweze kutimiza vyema majukumu yao ya kupambana na majangili na kuokoa tembo wetu wanaotoweka kwa kasi ya ajabu?
 
Jukumu la askari hao ni kupambana kwa njia yoyote kulinda wanyama, watumie weledi na technolojia za kisasa, hatutaki maaskari walio mahiri ktk kupambana na raia wasio na silaha! Waachane na habari za ushirikinana kwani serikali haiamini ushirikina japo wanasiasa ni washirikina.
 
hizo ni hekaya tu, ukienda kwa wavuvi utakutana na hekaya kama hizohizo. na sababu kuu ya kuwepo imani za kishirikina ni ukosefu wa elimu, siwatukani lakini ndio ukweli kuwa wawindaji haramu ni watu wenye upeo mdogo na akili finyu, waliokwenda shule kidogo ni ma boss wao ambao hata porini hawaendi.
Jumla ya maeneo ya nchi kavu ambayo yanalindwa (protected areas) tanzania ni kilomita za mraba 113,838 wakati eneo lote la nchi ambalo ni nchi kavu ni kilomita za mraba 886,676, hivyo utaona maeneo yanayolindwa ni 12.8% ya eneo lote la nchi kavu la nchi, hilo ni eneo kubwa sana kulilinda kwa idadi ya askari wa wanyama pori tuluonao na vifaa tulivyo navyo. ndio maana nchi zilizo endelea zinajitahidi kuunga mkono serikali katika kuyalinda hayo maeneo lakini bado kazi ni ngumu, hivyo majangiri bado wanafanikiwa kuua wanyama sio kwasababu "wana fundi" huo ni upuuzi wanaodanganyana wenyewe kwa wenyewe kutokana na akili zao finyu ila ukweli ni kwamba hatuna rasilimali za kutosha kuyalinda hayo maeneo kwa ufanisi.
 
Sasa hao askàri wananyapori wànazijua hizi taarïfa aina ya wațu wañąopambana nao!!!
Inavoonekana wengine wanazijua hizi taarifa na kibinafsi kila mtu anafnya utaratibu wake

Pale Mikumi National Park niliwahi kukuta wazee kama watatu huwa wanatoka Camp na wanazurura vijiji vya jirani na baadae wanarudi tena

Nilipouliza wafanyakazi wa pale wakasema hao ni askari wastaafu wa wanyama pori wamekua kama vichaa hivi, na hawawezi tena kwenda makwao! Huishia kurudi palepale kambini na marnyingine hutokea bahati mbaya wakaliwa na wanyama wakali

Jamaa wakanambia askari huwa wanakutana na mambo ya ajabu sana maporini na pia wanalazimika mara kadhaa kumwaga damu ya hao majangili kwa kuwauwa inapotokea wamewaona wao kwanza
Wanajua kwamba Majangili yana mambo flani ya kishirikina ambayo wanadhani yana wa haunt hao askari wao mpaka wengine wanakua hawapo sawasawa kiakili
 
Hili la ushirikina kwa majangiri ni kweli na mara nyingi huwa wanakingwa pia wasifuatiliwe na vyombo vya dola.Kuna jamaa anaitwa Lukas Jacob maarufu Mang'era anapatikana Tarime mjini,huyu bwana ni jangili aliyetukuka mbuga ya Serengeti na Mama yake mzazi ni mganga wa kienyeji,kuna kipindi alikuwa anawapa kinga vijana wawili akazuga kuwa eti anawakinga kwasababu wanaenda kuomba kazi ya uaskari wanyama pori.
Pia uyu Lukas Jacob ni mshirika mkubwa wa jambazi nguli Peter Zakaria na ukikutana na uyu jamaa ana makovu usoni na mwilini.Kama TANAPA wapo serious wamtafute uyu bwana atawapa mtandao mzima wa majangiri kanda ya ziwa.
Angalizo:sina chuki nae na nilichoeleza ni ukweli na nilimfahamu kupitia jamaa yangu ambaye ni askari mstaafu wa JWTZ.
 
hizo ni hekaya tu, ukienda kwa wavuvi utakutana na hekaya kama hizohizo. na sababu kuu ya kuwepo imani za kishirikina ni ukosefu wa elimu, siwatukani lakini ndio ukweli kuwa wawindaji haramu ni watu wenye upeo mdogo na akili finyu, waliokwenda shule kidogo ni ma boss wao ambao hata porini hawaendi.
Nakubaliana na wewe mkuu lakini watu wanaotoa taarifa hizi ni watu wenye akili na uzoefu wa miaka mingi kwenye uwindaji

Kwenye uvuvi kuna hadithi za alinacha na nimeziishi nilipokua mdogo, wala hakuna chochote cha kutisha hasa barini ambapo nina kauzoefu kidogo

Lakini kwenye mapori na mbuga zenye wanyama wakubwa na wakali ni hadithi nyingine mkuu. Jambo moja ninalokubaliana nawe ni kua wanofaidika na biashara hii hua hata porini/mbugani hawaendi lakini ndio wanaoongoza kupandishwa kizimbani kwa makosa ya kukutwa na nyara. Ni nadra sana kuona muindaji aliyeenda front kapandishwa kizimbani au kakamatwa akiwa hai maana huwa wanawamaliza hukohuko au hawawakamati!

Jiulize kwanini pamoja na hatua zoote za kulinda wanyama pori takwimu zitolewazo kila wakati zinaonyesha kua wanapungua kwa kasi ya ajabu? Unadhani wanakufa kwa magonjwa mkuu?
 
Hili la ushirikina kwa majangiri ni kweli na mara nyingi huwa wanakingwa pia wasifuatiliwe na vyombo vya dola.Kuna jamaa anaitwa Lukas Jacob maarufu Mang'era anapatikana Tarime mjini,huyu bwana ni jangili aliyetukuka mbuga ya Serengeti na Mama yake mzazi ni mganga wa kienyeji,kuna kipindi alikuwa anawapa kinga vijana wawili akazuga kuwa eti anawakinga kwasababu wanaenda kuomba kazi ya uaskari wanyama pori.
Pia uyu Lukas Jacob ni mshirika mkubwa wa jambazi nguli Peter Zakaria na ukikutana na uyu jamaa ana makovu usoni na mwilini.Kama TANAPA wapo serious wamtafute uyu bwana atawapa mtandao mzima wa majangiri kanda ya ziwa.
Angalizo:sina chuki nae na nilichoeleza ni ukweli na nilimfahamu kupitia jamaa yangu ambaye ni askari mstaafu wa JWTZ.
 
Hili la ushirikina kwa majangiri ni kweli na mara nyingi huwa wanakingwa pia wasifuatiliwe na vyombo vya dola.Kuna jamaa anaitwa Lukas Jacob maarufu Mang'era anapatikana Tarime mjini,huyu bwana ni jangili aliyetukuka mbuga ya Serengeti na Mama yake mzazi ni mganga wa kienyeji,kuna kipindi alikuwa anawapa kinga vijana wawili akazuga kuwa eti anawakinga kwasababu wanaenda kuomba kazi ya uaskari wanyama pori.
Pia uyu Lukas Jacob ni mshirika mkubwa wa jambazi nguli Peter Zakaria na ukikutana na uyu jamaa ana makovu usoni na mwilini.Kama TANAPA wapo serious wamtafute uyu bwana atawapa mtandao mzima wa majangiri kanda ya ziwa.
Angalizo:sina chuki nae na nilichoeleza ni ukweli na nilimfahamu kupitia jamaa yangu ambaye ni askari mstaafu wa JWTZ.
 
Hili la ushirikina kwa majangiri ni kweli na mara nyingi huwa wanakingwa pia wasifuatiliwe na vyombo vya dola.Kuna jamaa anaitwa Lukas Jacob maarufu Mang'era anapatikana Tarime mjini,huyu bwana ni jangili aliyetukuka mbuga ya Serengeti na Mama yake mzazi ni mganga wa kienyeji,kuna kipindi alikuwa anawapa kinga vijana wawili akazuga kuwa eti anawakinga kwasababu wanaenda kuomba kazi ya uaskari wanyama pori.
Pia uyu Lukas Jacob ni mshirika mkubwa wa jambazi nguli Peter Zakaria na ukikutana na uyu jamaa ana makovu usoni na mwilini.Kama TANAPA wapo serious wamtafute uyu bwana atawapa mtandao mzima wa majangiri kanda ya ziwa.
Angalizo:sina chuki nae na nilichoeleza ni ukweli na nilimfahamu kupitia jamaa yangu ambaye ni askari mstaafu wa JWTZ.
Dah! Mkuu hii ni hatari sana
 
Haaa wapi, hizo mambo za ushirikina nazichukulia ni kama excuse tu za kushindwa kwetu kudhiti huo ujangiri unaondelea kwenye mbuga zote za wanyama hapa nchini.

Ukweli ni kwamba kuna mikono ya wengi sana ambao ndio wanufaika wakuu wa huo ujangiri na wengine ndio hao hao wanaojifanya kututungia sheria za kupambambana na ujangiri.

umewahi kujiuliza ni kwanini karibia 80% ya poachers tunaowakamata na vithibitisho ni raia wa kigeni, lakini leo hii ukitembelea keko au jela yoyote huwezi kuwakuta hao majangiri wa kigeni? sababu case zinakuwa solved ndani ya muda mfupi tu na tembo wanaendelea kuuwawa.
 
Inavoonekana wengine wanazijua hizi taarifa na kibinafsi kila mtu anafnya utaratibu wake

Pale Mikumi National Park niliwahi kukuta wazee kama watatu huwa wanatoka Camp na wanazurura vijiji vya jirani na baadae wanarudi tena

Nilipouliza wafanyakazi wa pale wakasema hao ni askari wastaafu wa wanyama pori wamekua kama vichaa hivi, na hawawezi tena kwenda makwao! Huishia kurudi palepale kambini na marnyingine hutokea bahati mbaya wakaliwa na wanyama wakali

Jamaa wakanambia askari huwa wanakutana na mambo ya ajabu sana maporini na pia wanalazimika mara kadhaa kumwaga damu ya hao majangili kwa kuwauwa inapotokea wamewaona wao kwanza
Wanajua kwamba Majangili yana mambo flani ya kishirikina ambayo wanadhani yana wa haunt hao askari wao mpaka wengine wanakua hawapo sawasawa kiakili
Duh! Hizi mambo ndo nimezijua leo hii kutoka ķwako. Kuna jamaa ni askari wànyamapori nikipata muda wa kukutana nae nitamuuliza zaidi
 
Ukweli ni kwamba kuna mikono ya wengi sana ambao ndio wanufaika wakuu wa huo ujangiri na wengine ndio hao hao wanaojifanya kututungia sheria za kupambambana na ujangiri.
Kama ni syndicate basi itakua inawahusu watu sensitive kutoka taasisi sensitive maana kwa rasilimali zinazotumika katika kupanga ulinzi kwenye mbuga zetu sio za kawaida

Hili la ushirikiana ni simulizi za watu wenye uzoefu na hayo mambo wengine ni watu wazima sana
 
Back
Top Bottom