Kuhusu Euro Bond!

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,786
Nilikuwa nasikia tu kuhusu euro bond ktk kwenye vyombo vya habari lkn nilikuwa sijaelewa ni nini hasa!

Sasa nimepata picha kidogo kwamba ni fedha ambayo Serikali ya Kenya ilichukuwa kutoka kwa walipa kodi wa Kenya na kuipeleka kwenye benki za nchi ya Uingereza (Britain) ili waweze kupata riba (interest) na kuitumia riba kwenye mambo ya kimaendelo nchini Kenya (sina uhakika na hili)!

Sasa kabla ya kuanza kuihukumu Serikali ya Kenya ningependa kuelewesha kuhusu hili, Je kwanza ni kiasi gani cha fedha kilichopelekwa huko Uingereza kama hiyo Euro bond (in US dollars), na pili kama swala ni riba ni kwa nini hiyo fedha isingewekezwa kwenye mabenki ya nchini Kenya ambapo kwangu mimi ingekuwa ni win win situation kwa Kenya badala ya kupeleka fedha ya mvuja jasho wa Kenya Uingereza na kuilipia kodi huko fedha itakayotumika kusadia wananchi wa Uingereza, kwa kifupi mfuja jasho wa Kenya analipa kodi Uingereza!

Naomba mwenye uelewa wa hili anielimisha hapo na pia kunisahihisha kama nimekosea!
 
Last edited by a moderator:
Mwisho wa siku if it don't make dollars then it don't make sense....

Cha muhimu hapo ni return on investment kwahio sidhani kama waliopeleka huko ni wajinga (unless kama kuna 10%), watakuwa wamecheki wangewekeza nchini wangepata ngapi na wangewekeza nje wangepata ngapi..., Kama ni Pension Funds ndio kazi yao ni kuwekeza pesa za wateja wao ili zirudishe pesa nyingi iwezekanavyo.., sio Africa tu Pension Funds ulimwengu mzima zinawekeza popote pale kama return ni kubwa zaidi kuliko pengine. Kumbuka hii ni investment first priority sio kukuza uchumi wa nchi
 
Back
Top Bottom