Ni afadhali PHD ya Dr. Slaa kuliko PHD ya Prof. Lipumba kama unataka kujua ukweli nendaserikalini uwaulize ni mwanasiasa gani huwa akiongea wanakosa usingizi au nenda kwa wananchi uwaulize ni mwanasiasa gani akiitisha mikutano watajazana kumsikiliza. Dr. Slaa ni exeptional hata rais anajua
<br />Hapa mkuu umekosea!<br />
Prof Lipumba ni one of the best professors wa Economics. Ni world renown consultant kwenye maswala yanayohusu economics, he does a lot for world bank na IMF. Kati ya wanasiasa wote nchini, yeye ndio mwenye CV iliyoenda shule. Pamoja na Dr Slaa kuwa better politician, he is no where close to Prof Lipumba kwenye maswala ya Academics, no where!!
Barubaru ni Dr (PhD) anayefanya kazi huko Doha na nakumbuka tukio la kumsaidia Mtanzania mmoja aliyepita hapo Doha na pia kutuma Tende/Halua wakati wa Mwezi wa Ramadhani.
Ni Mhasibu wa kampuni kubwa tu (Alishajitambulisha hivyo na si kuwa namwaga habari zake) na alishakuwa Mhasibu hapabongo kabla hajatofautiana na Wanasiasa wa CCM anao walamba miguu.
Kutokana na kuwa na Biashara zake kubwa tu hapa Tanzania, inabidi awatetee CCM kwani Kisasi cha Kikwete kinaweza kuwa kibaya sana kwake. Jamaa anafahamu sana anachokiandika na anafahamiana na Dr. Slaa kwa karibu tu na si kama sisi wengi wetu hapa tunamsoma tu.
Sijui walikosana wapi hadi akaanza kumchukia Dr. Slaa au huyu Barubaru wa sasa, siyo huyo Msomi aliyepo Doha (PhD). Au jamaa ANAPOTEZA tu muda hapa na kama ambavyo aliandika mwanzo, yupo kujifunza Kiswahili na kuhakikisha hasau. Anyway, kama hasomi alama za nyakati na anazidi kumshambulia Dr. Slaa, siku ikifika basi kampuni zake itabidi zimulikwe vizuri ki Sheria.
Kwa muda mrefu sasa, suala kuhusu kisomo cha darasani cha Dr. Slaa na hasa PhD limejitokeza mara nyingi. Kwa namna ya pekee nimeshavutiwa kuanzisha mjadala wa tafakuri ya kina kuhusu PhD ya Dr Slaa ambaye ni rais wa moyoni kwa watu wengi. Kwa kuanzia, nawasilisha mawazo ya mwana JF ambaye amedhihaki CV ya Dr Slaa. Ningependa kumwalika ndugu huyu kushiriki katika mjadala ili kujaribu kujibu maswali yafuatayo ambayo yametokana na dhihaka juu ya PhD ya kusomea ya Dr. Slaa.
Barubaru aliandika kwa kubeza CV hii ya Dr. Slaa hivi:
''Profile ya Dr Slaa EDUCATION
International Eye H. Centre Certificate in Eye Health 1993-1993
TransWorld Tutorial College, London Certificate in Management 1985-1985
St. Thomas Aquinas University Advanced Diploma in Rural Development 1980-1981
St. Urban University, Rome PhD (JCD) Law 1977-1981 [Doctor of Canon Law (Latin: Juris Canonici Doctor or JCD)]
Kipalapala Seminary Certificate in Theology 1974-1977
Kibosho Seminary School Certificate in Philosophy 1972-1973
Itaga Seminary School A-Level Education 1970-1971
Dung'unyi Seminary School O-Level Education 1966-1969
Karatu Primary School Primary Education 1962-1965
Daudi Primary School Primary Education 1961-1961
Kwermusl Primary School (Mbulu) Primary Education 1958-1960''
Maswali kwa Barubaru na wachangiaji wengine:
1. Je kuna tofauti gani ya kifalsafa na ki-empirical katika NADHARIA zinazoongoza utafiti wa sheria za kanisa na sheria nyingine?
2. Je kuna tofauti gani ya kifalsafa na ki-empirical katika njia za kufanya UTAFITI katika sheria za kanisa na sheria nyingine?
3. Je ndugu anayedhihaki PhD ya Dr. Slaa anamfahamu vipi Thomas Aquino?
4. Je ndugu anayedhihaki kisomo cha darasani cha PhD ya Dr. Slaa anafahamu jinsi St. Thomas Aquino (Dr. Slaa amesomea chuo cha St. Thomas Aquino mwasisi wa elimu ya sheria ya nchi za Magharibi kama alivyoonyesha ndugu anayetoa dhihaka) alivyochangia katika maendeleo ya elimu ya sheria katika nchi za Magharibi? Kwa kujibu maswali hayo utaona dhahiri ubora wa hali ya juu wa PhD ya sheria na ya kusomea ya Dr. Slaa.
Kuna watu wengine mlisoma lkn elimu zenu hazina maana kwa nchi yenu, ulifikia hadi cheo ya RDD lkn udini haukukutoka. Hebu fikiria kama waislamu ndio wangejenga shule wakati wa ukoloni si nchi nzima mngewalazimisha wawe waislamu. Samahani sana baba yangu lkn uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana na elimu yako hiyo ya kujifungia na madesa kwenye msikiti wa udsm ndio iliyokuharibu huko nyuma.Awali ya yote napenda kukufahamisha mimi sio Mhasibu bali ni mchumi kuanzia Bcom (Udsm-Tz) MBA (Ontario- Can) na PhD (Sofia- JPN). Sijawahi kuwa Mhasibu popote pale katika maisha yangu zaidi kufanya kazi Wizara ya Mipango na baadae kuwa RDD(Regional Development Director- Mwanza. Kabla kurudi Nyumbani Oman (kuukana uraia wa Tz na kuchukua uraia wa Oman).
ndugu yangu Sikonge,
Si kuwa naipenda CCM au chama chochote huko Tz bali nazungumzia hali halisi enu ya Uchumi kama field yangu kwani naguswa sana na maisha ya jamaa, marafiki na hata ndugu zngu huko wanavyoishi na namna nchi inavyoendeshwa.
Kama kawaida yangu kwangu kuimarisha uchumi ni jambo la kwanza na mengine kama siasa ni baadae nacho ni kitu kilichonifanya niondoke TZ. Lakini napenda kukujuza Biashara zangu zoooote ni clean kabisa tunafata sheria zote za nchi yenu na hata ukitaka waambie TRA wakaangalie na kama una ushahidi wowote basi peleka kwenye vyombo husika ili hakhi itendeke. Tupo wazi kwa hilo. Na Mke wangu yapo kama mwanasheria basi mkaonane mahakamani.
Lakini kama mwanadamu ulie sahihi kabisa unatakiwa uhoji kila kitu. Haingii akilini mchumi kama mimi unaniweka kwenye mambo ya medicine ni lazima ujiulize mara mbili.
Nikirudi kwa Dr Slaa , kila wakti namuuliza kwa elimu yako hiyo Je madhehebu mengine huko TZ au waislam watakuwa salama kama wewe ukipewa nchi? Ni nani asiyejua kanisa katoliki na Mtandao wake kuanzia jumuiya zake za Mitaa, kigango, parokia mpaka Taifa.
Je angekuwa Mtu amesomea Uislam kama Prof Juma Mikidadi (aliyewahi kuwa Mbunge wa Kibiti- Rufiji ) ambaye alisomea Islamic Law mpaka masters ake na kisha PhD. Je wakatoliki wangekuwa kimya.
Lakini yote hayo yanataka mtu makini katika kuhoji na hata kujua ukweli wa mambo na kujiridhisha kwa nia ile ile ya mustakabali mzuri wa ustawi wa nchi yako.
Usione Khaya kuhoji kwani ndiko kunakokupa mwangaza wa baadae. Usipende kitu kiasi cha kuona kwenye chongo ukasema kengeza.
By The way, ndugu zangu huko Sikonge wazima? nasikia kuna njaa sana na inshallah nitapeleka chochote soon kuwasaidia.
Kuna watu wengine mlisoma lkn elimu zenu hazina maana kwa nchi yenu, ulifikia hadi cheo ya RDD lkn udini haukukutoka. Hebu fikiria kama waislamu ndio wangejenga shule wakati wa ukoloni si nchi nzima mngewalazimisha wawe waislamu. Samahani sana baba yangu lkn uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana na elimu yako hiyo ya kujifungia na madesa kwenye msikiti wa udsm ndio iliyokuharibu huko nyuma.
Sawa kabisa kaka, kama mtu akitaka kuelewa kitu afanye utafiti kwanza kabla ya kuongea. Na utafiti unaweza kufanyika kwa kumhoji Dr. Slaa. Na swala jingine ni kwamba Chuo kilichompa Dr Slaa hiyo PhD kipo na amekitaja sasa kwa nini asiulize huko anatafuta majibu sehemu nyingine?
hatufanyi utafiti kwa kumuuliza tu lakini hata kuangalia makuzi yake ya utotoni na ujana wake pia kuangalia elimu yake na mtiririko mzima wa maisha yake .
hayo yanaweza kabisa kukupa mwanga wa kuweza kumtambua mtu. Japo watu huwa wa badilika lakini ukweli utabaki kuwa ukweli.
Nilipo Blue,
Je unajuwa CAN LAW?