Kufufuka na kurudi msukule.

Kaitaba

JF-Expert Member
Jun 30, 2009
916
52
Nafikiri kuna tofauti kati ya kufufuka na kurudi msukule,

Mara nyingi tunachanganya, Binti wa mwanza na yule wa moshi hawajafufuka ila wamerudi msukule,

Aliyefufuka ni yule aliyekufa kweli kwelii na kisha kurudia uhai,( Mfano Jesus)

Ila aliyechukuliwa msukule, akionekana tena huyo anakuwa amerudi msukule sio kafufuka

Tusihalibu kiswahili.
 
Aksante Kaitaba kwa kuweka hii kitu sawa! Ishu ya kufufuka ni tofauti kabisa, na isifananishwe na mambo ya misukule.Big up mkuu!
 
utajuaje kwamba hakufa kweli kweli, embu elezea hapo mkuu

Ni hivi, huyu wa mwanza alikufa wakamzika, baada ya miaka kadhaa akaonekana amekatwa ulimi nk, huyu ni msukule

Mwingine wanapokuwa wanataka kuzika anapiga chafya na kuanza kuongea, huyo kafufuka,

bila shaka umenielewa.
 
Aksante Kaitaba kwa kuweka hii kitu sawa! Ishu ya kufufuka ni tofauti kabisa, na isifananishwe na mambo ya misukule.Big up mkuu!

Nakushukuru sana, ukweli utabaki kuwa ukweli na uongo utakuwa uwongo daima,
 
Huyo aliyesema kuwa mtoto mwanza kafufuka, afute/alekebishe thread yake haraka kama anakubaliana na mimi,
 
Back
Top Bottom