hivi kwan nini redio na/au tv stations zinakuwa na vipindi vinavyofana wakati fulani? mfano jumapili jioni redio nyingi utakuta vipindi vya nyimbo za zamani(wenyewe wanaita flash back).jee hii inatokana na mahitaji au ukosefu wa ubunifu tu?
Huo ni upoyoyo mkuuu tena mkubwa saana kwanini wanashindwa kuwa creative tv kama 4 woote taarifa ya habari saaa 2 kamili duuuu! Hampishani hata nusu saa hv.
Jamani nami nimefuatilia kuna radio 2 hivi zinaigana kila kitu ahdi program zao....clouds na magic fm.....fuatilieni yaani kila kitu...kuna wakati asubuhi wanaigana hata mada kujadili
Wa tz sio wabunifu., kisha inakera mfano kipindi cha komed cha TBC, EATV na channel ten yaani wanaigana kila kitu muda niuleule hata siku za marudio. Hadi wanaume kuvaa magauni. Yani unaweza kufikiri ndo walewale. Ujinga mtupu.
maproducer wa bongo hawataki kuumiza vichwa kwa ubunifu that is why wanaigana sijui na ukosefu wa elimu nao unachangia refer to KIBONDE ana div 0 form 4 unategemea nini
Ni kawaida yetu wabongo, hata hapa JF siku hizi utakuta habari moja inaanzishiwa Threads hata tanotofauti.. Mtu anaweza kuchukua habari kutoka kwenye Jukwaa la hoja Mchanganyiko akaipeleka kwenye Jukwaa la siasa halafu akaiita Breaking news! Vile vile Blog nyingi za kibongo mambo ni yale yale, wanafanya copy and paste. Ubunifu utawapotezea muda, i guess!!!!!!!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.