Lukansola
JF-Expert Member
- Sep 5, 2010
- 5,435
- 1,597
Kwenye CCM nampigania EL kwa nguvu zangu zote kwa sababu naamini ni kwa kupitia yeye, Tanzania itapata ule ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania na pia ili litimie lile neno kuwa "rais wa 2015" lazima atatoke Kaskazini.
Pasco.
Pasco tujipe muda wa kufikiri kidogo, hivi katika miaka yote ambayo Lowassa amekuwepo alisuburi nini kuleta huo ukombozi wa pili? sangarara kauliza kama akifa je, nadhani wale wote waliokwisha kujaribu na kushindwa hawapaswi kupewa nafasi tena, Tanzania ina watu wengi tu wenye uwezo nina amini, kwa hiyo tupumzisheni na huyo Lowassa jamani, kwanza nasikia alitakiwa na ccm aondoke kwa maana kwamba yeye ndo anachafua chama chao na bado hajafanya hivyo, na ccm imeshindwa kumfanya lolote hatutaki kuongozwa na watu wanaolindana, unataka El awe rais ili aje amlinde jk kwa kumlipa fadhila za yeye kutokufikishwa mbele ya sheria kwa ufisadi, Tanzania haitaendelea kwa mtindo huu. na pili nadhani ccm wakubali tu kupumzika wajipange upya badala ya ku force kung'ang'ania madaraka mpaka kufikia kuiweka nchi yetu hapa ilipo sasa including hali ya amani.