Kubomoa Naura Spring Hotel ni komoakomoa sio bomoabomoa

CCM ya magufuli siyo CCM ya JK,,huu ndio utawala wa haki na sheria..huyo mzee kama alitumia fedha kupindisha sheria kwenye utawala wa jk ngoja aonje joto ya jiwe!!!
Hakuna serikali ya mtu kama wajinga wengi tunavyotaka kuamini. Kama wakati wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa au Kikwete serikali iliingia mkataba na nchi,Kampuni au mtu fulani kwa niaba ya Tanzania jua na Magufuli anawajibika nao. Hatuwezi kuwa kila eti akichaguliwa Rais mpya na serikali nayo inakuwa mpya!
 
Kama watazingatia mita 60 kutoka mtoni central police, bot, diamond bank,nssf wajiandae
 
Sentensi yako hapo kwenye RED sijaielewa kabisa mkuu. Naomba ufafanuzi tafadhali.
Tazama eneo lilipo kanisa la St Theresa,Shule ya Naura,kituo cha polisi ,nyumba za polisi aka mabatini,Mt meru na zile nyumba usawa wa geti la Naura springs mpaka CEDHA .
Halafu kaangalie ile Gym na jiko,restaurant na swimming pool ya Naura springs ndio urudi hapa
 
Heshima yenu wakuu,

Mimi nimeanzisha hii thread kulaani kitendo cha Watanzania kushindwa kujiongeza na kurudishana nyuma. Mimi sioni kama kuna haja ya kukomoana kwa kutumia nafasi tulizonazo kisiasa au kiuchumi.



Nianze kwa kusema kwamba Tanzania ni Nchi ya Vyama vingi, na Mtanzania yupo huru kuunga Mkono chama chochote anachopenda.

Usitegemee kwamba utagombea nchi ya vyama vingi wote wakuunge mkono. Huu ni wakati wa kutibu majeraha ya Uchaguzi na Kujenga Nchi yetu iwe na Umoja amani na Maandeleo sio Muda wa Kukomoana.

Nitoe tahadhari katika hili, siku zote unaweza ukamkimbiza mjusi akakimbia, lakini akiona amezidiwa anageuka nyoka na kuanza kukukimbiza wewe.

Mimi kuna Maswali yananitatiza;

1.Hili Jengo hadi linajengwa Serikali haikuwepo?

2.Je, alipewa Vibali vya kujenga na wakaguzi walilikagua?

4.Aliyeruhusu kujengwa kwa jengo hili kachukuliwa hatua gani?.

5.Kwanini Serikali isiingie garama ya hili jengo?

6.Imekuaje Kuanzia Msingi jengo mnaliona hadi lifike hatua hii ndo ulibomoe? Huu ni uzalendo?

7.Hakuna njia mbadala ya kufanya ili hili jengo lisibomolewe?

Hili jengo Mahakama ndiyo ilimruhusu ajenge baada ya kushinda kesi dhidi ya Manispaa ya Arusha kumzuia Kujenga.

Eti inavunjwa kisa ipo bondeni. Mbona maji hayaingii ndani? Mto Sanawari Miaka yote upo na hili jengo halijawahi kusitisha shughuli kisa maji yameigia wala hapajawahi kutuwama maji.

Hii itakuwa Hotel yake ya pili kuwekewa X baada ya moja ya Mwanzo kuwekewa alama ya X.Impala Hotel, Leopard Tours Offices kuvunjwa.


Kama ndivyo, Basi tufanye hii Nchi iwe ya chama Kimoja. Nchi hii ni yetu sote. Nchi kwanza Vyama baadae. Roho za kukomoana zishindwe kwa jina la Yesu.

Arusha Wamechagua Mabadiliko, Wapigwe mabomu, wapigwe risasi, wabomolewe, wanyimwe huduma za kijamii, vyovyote vile mtakavyo fanya haisadii.

View attachment 315535 View attachment 315536


Kuna wakati tuliambiwa huyu mwenye hii hotel ametoa ufadhili kwa chama chetu alikijengea ofisi ya chama hapo karibu kabisa na jengo tajwa
 
Mleta mada umesema mwenye hotel alishinda kesi mahakamani baada ya manispaa kumzuia!?

Kumbe manispaa ilimzuia yeye akakimbilia mahakamani kuhonga hela sio? Avunjiwe haraka sana, tena hizo siku 90 ni nyingi sana!
 
Historia ya hilo jengo unalijua ?? Mimi tokea nikiwa mtoto lilikua limesimamishwa ujenzi wake Mkapa akaruhusu pale kuna mto na livunjwe tu
 
Mimi sio mwenyeji wa Arusha na siijui location ya hiyo hotel lkn kwa maelezo yako inaonekana huyo mmiliki alitumia nguvu ya pesa kushida huko mahakamani baada ya kuwekewa pingamizi la kujenga hiyo hotel bondeni!

Sasa acha aisome namba kwa jeuri yake ya pesa ya kudhani anaweza kuhonga wakati wote maishani. Na bahati mbaya, kwa mujibu wa baadhi ya wachangiaji humu, kuna watumishi waliosimamia zuio hilo lkn wakahamishwa kisa wanaleta kauzibe.
 
Kuna wakati tuliambiwa huyu mwenye hii hotel ametoa ufadhili kwa chama chetu alikijengea ofisi ya chama hapo karibu kabisa na jengo tajwa
Ufadhili wa kinafiki huo...hilo jengo hata halina tija kwa chama tajwa
 
Siku likiporomoka huku kukiwa na ugeni mtailaumu serikali.

Majipu yanayouma ndio haya sasa
Hili jengo bana lilisimama wakati wa ile kesi kati ya Mrema na Halmashauri kule mahakamani, na aliposhinda ndo mahakama ikampa kibali cha kuendelea kujanga, wakati huo sisi tukiwa tunaosha magari pale mtoni pale mtoni Sanawari na huku tukipata vabarua vya hapa na pale hapo ambappo leo ndo Naura spring,

Sasa swali ni kwamba mahakama ilimruhusu vipi kuendelea????? ilitumia vigezo gani kumruhusu ambavyo leo serikali ya JPM inavibatilisha????? mbona ule mto hauanzii pale Hotelini???
 
Zile hati za kufoji ndio alikuwa anaziongelea Magufuli?

Huyu jamaa ana katabia cha kukaa juu ya sheria hebu kaangalia ukuta wa ngurdoto ulivyo katika eneo la barabara.

Gharama za ujenzi amlipe nani?sanasana yeye ndio anatakiwa kufikishwa mahakamani kwa uchafuzi wa mazingira.
Hahaha kumbe hujui hata ngurdoto ni ya nani?
 
Impala bomoa, Naura bomoa, bado Ngurdoto. Zitaisha kama ulivyozipata. Ukiua kwa upanga, utakufa kwa upanga.
Du!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! huu nao ni upanga mkali sana, hebu upunguze makali kidogo ndugu.
 
KWa kiasi fulani nakumbuka mgogoro alioingia huyu mmiliki wa Naura Spring na serikali wakati wa ujenzi wa jengo hili, jamaa alishinda kesi mahakamani akaendelea na ujenzi hivyo inaonyesha huyu si mvamizi! Sasa hapa serikali isipotumia akili zake timamu itaingia kwenye kingi kirahisi sana.. Hili zoezi la bomoaboma lifanyike tukiweka busara zetu mbele sana!
 
Back
Top Bottom