Kuacha na kuachwa

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,232
113,610
Moja ya vitu vibaya sana katika mahusiano ya kimapenzi ni kuachwa na mpenzi wako (to get dumped). Mbaya zaidi ni pale unapoachwa kwa ghafla bila hata kuona dalili. Unastukia tu mwenzako anakata mawasiliano. Hakupigii tena simu. Ukimpigia yeye hapokei. Ukimwandikia waraka wa elektroniki (email) hakujibu wala nini. Haya yote yanatokea siyo kwamba kapotea na hakuna anayejua yuko wapi. Unajua yupo kabisa na jumbe zako zote unajua anazipata lakini hazijibu kwa makusudi tu.

Pole pole fikra za kuachwa zinaanza kukujia kichwani. Mara unaanza kushikwa na machungu moyoni. Unajiuliza mengi lakini hupati majibu. Unaanza kujiuliza pengine labda kuna kitu ulimkosea....unajiuliza weee hadi kichwa kinaanza kukuuma lakini hupati jibu. Hukumbuki hata kidogo kama ulimkosea kitu maana mara ya mwisho mlipokuwa wote kila kitu kilionekana kuwa shwari na mkaagana vizuri tu kama ilivyo desturi yenu.

Mwishowe unakuja kustukia tu kuwa umeachwa na hiyo ndiyo hali halisi na ndiyo ukweli wenyewe. Nguvu zinakuishia mwilini. Maumivu unayasikilizia kuanzia kwenye moyo hadi tumboni. Maisha unaanza kuyaona kama hayana thamani tena. Hata hamu ya kula inaisha. Unajiuliza hivi kwa nini mimi (why me).

Mdau, umewahi kuachwa au kumwacha mpenziyo? Kama uliwahi kuachwa ulijisikiaje na ulikabilianaje na hali hiyo? Ulilia? Ulijikaza tu kisabuni hadi ukapoa? Na kama umewahi kumwacha mpenziyo, ulimwacha achaje? Ulimwambia au ulitimka tu kimya kimya na yeye akaja kustukia baadaye?
 
1.SI USTAARABU KUMWACHA MTU GHAFLA .....KUNA MADHARA MENGI.
2.UNAWEZA KUMWACHA MTU TARATIBU....HASA WAAFRICA.
3.KABLA HUJAMUACHA MTU KWANZA TAHMINI ANAKUPENDA KIASI GANI.BAADA YA HAPO UTAJUA NAMNA YA KUMUACHA.
4.WAPO WANAOACHANA KWA UGOMVI MATUSI, KASHFA VIPI NYIE?HAIFAI na ni aibu
5.KUMBUKA KUWA MTU WAKO UNAEMPIGA CHINI LEO ANAWEZA VURUGA HUKO UNAKOENDA kuweni wastaarabu.
 
1.SI USTAARABU KUMWACHA MTU GHAFLA .....KUNA MADHARA MENGI.
2.UNAWEZA KUMWACHA MTU TARATIBU....HASA WAAFRICA.
3.KABLA HUJAMUACHA MTU KWANZA TAHMINI ANAKUPENDA KIASI GANI.BAADA YA HAPO UTAJUA NAMNA YA KUMUACHA.
4.WAPO WANAOACHANA KWA UGOMVI MATUSI, KASHFA VIPI NYIE?HAIFAI na ni aibu
5.KUMBUKA KUWA MTU WAKO UNAEMPIGA CHINI LEO ANAWEZA VURUGA HUKO UNAKOENDA kuweni wastaarabu.[/QUOTE]

Ulishawahi kushuhudia the most extreme case ya hapo pekundu? Kuna watu wan vurugu hadi milele!
 
NN unaamka asbh unajihisi kum=miss sana umpendaye unaamua kumwambia mara jibu linakuja aaaaaah hata mi nimekumiss sana lakini nimeoa last week!!!!!!!!

experience za kuachwa with no indicators ni mbaya sana!! u might end up doing something very stupid.
kidonda chake kigumu kupona, atahri zake huwa za muda mrefu saaana jamani!!
kitamu wewe unakiona shubili
una kuwa na vita against the whole world, kila mtu mbaya tu kwako......
.............................why am I recalling this???????????
 
NN unaamka asbh unajihisi kum=miss sana umpendaye unaamua kumwambia mara jibu linakuja aaaaaah hata mi nimekumiss sana lakini nimeoa last week!!!!!!!!

experience za kuachwa with no indicators ni mbaya sana!! u might end up doing something very stupid.
kidonda chake kigumu kupona, atahri zake huwa za muda mrefu saaana jamani!!
kitamu wewe unakiona shubili
una kuwa na vita against the whole world, kila mtu mbaya tu kwako......
.............................why am I recalling this???????????
Ehheeee shosti..endelea....
 
Ehheeee shosti..endelea....

mamii jamani mi sitaki kukumbuka kichwa kinaniuma afu naweza nikaanza kupunguza mapenzi yangu kwa Bala bure.....

hata ukikutana na mwanaume mwingine unahisi ndo wale wale tu maana mashairi yao vina na mizani ile ile tu!!!

kuachwa kusikie redioni na usome kwenye magazeti tu, yakikufika utajuuuuuuuuuta kupenda!!!
 
Kuacha kubaya sana;

Niliyemuacha sikupata nafasi ya kumwomba msamaha na sintoipata kwani aliji:HEHE ..........................nadhani nimeeleweka.:angry:
 
Kuacha kubaya sana;

Niliyemuacha sikupata nafasi ya kumwomba msamaha na sintoipata kwani aliji:HEHE ..........................nadhani nimeeleweka.:angry:

unaona sasa mnyalu................ni kitendo hatarishi sana kwa maisha ya mtu atii!!
 
Moja ya vitu vibaya sana katika mahusiano ya kimapenzi ni kuachwa na mpenzi wako (to get dumped). Mbaya zaidi ni pale unapoachwa kwa ghafla bila hata kuona dalili. Unastukia tu mwenzako anakata mawasiliano. Hakupigii tena simu. Ukimpigia yeye hapokei. Ukimwandikia waraka wa elektroniki (email) hakujibu wala nini. Haya yote yanatokea siyo kwamba kapotea na hakuna anayejua yuko wapi. Unajua yupo kabisa na jumbe zako zote unajua anazipata lakini hazijibu kwa makusudi tu.

Pole pole fikra za kuachwa zinaanza kukujia kichwani. Mara unaanza kushikwa na machungu moyoni. Unajiuliza mengi lakini hupati majibu. Unaanza kujiuliza pengine labda kuna kitu ulimkosea....unajiuliza weee hadi kichwa kinaanza kukuuma lakini hupati jibu. Hukumbuki hata kidogo kama ulimkosea kitu maana mara ya mwisho mlipokuwa wote kila kitu kilionekana kuwa shwari na mkaagana vizuri tu kama ilivyo desturi yenu.

Mwishowe unakuja kustukia tu kuwa umeachwa na hiyo ndiyo hali halisi na ndiyo ukweli wenyewe. Nguvu zinakuishia mwilini. Maumivu unayasikilizia kuanzia kwenye moyo hadi tumboni. Maisha unaanza kuyaona kama hayana thamani tena. Hata hamu ya kula inaisha. Unajiuliza hivi kwa nini mimi (why me).

Mdau, umewahi kuachwa au kumwacha mpenziyo? Kama uliwahi kuachwa ulijisikiaje na ulikabilianaje na hali hiyo? Ulilia? Ulijikaza tu kisabuni hadi ukapoa? Na kama umewahi kumwacha mpenziyo, ulimwacha achaje? Ulimwambia au ulitimka tu kimya kimya na yeye akaja kustukia baadaye?

Nimeisoma hii mara mbili mbili na nilipomaliza kuisoma nikabaki nasmile :smiling: tu maana nilidhani imeandikwa na mimi hahahahahahaha:behindsofa: ukitulia huwa unaandika vitu vizito sana. Maelezo yako jinsi unavyojisikia unapoachwa au kudhani umeachwa ni 100% accurate ndiyo maana nikakugongea kitu.
 
Kuacha kubaya sana;

Niliyemuacha sikupata nafasi ya kumwomba msamaha na sintoipata kwani aliji:HEHE ..........................nadhani nimeeleweka.:angry:
MJ Pole sana masikini......... jamani kuna maamuzi mengine huwa tunayatake for granted. Pole MJ
 
Mimi nafikiri nimeshawahi kuachwa mara mbili hivi lakini sikujisikia chochote yaani nilikuwa nadhani siamini kwa sababu waachaji walikuwa wanaacha na kurudi!! Sasa sijui niliachwa au la ila tu nilikuwa naona mabadiliko and then nikichunguza nakuta wameshaanzisha mahusiano mapya mwengine sasa nikiamua kukata mawasiliano kabisa wanarudi mbio kama wamefukuzwa huko walikokuwa walikokwenda !!
 
Ndio maana nimeacha kabisa kuingia kwenye mahusiano ambayo nina uhakika hayatadumu. Sitaki tena kumwacha mwanamke, ilishatokea lakini nafikiri ilikuwa lazima itokee lakini inaleta machungu sana. Ni mbaya kuacha na kuachwa ingawa sometimes huwa inabidi lakini jamani
 
Wakati mwingine huwa nahisi
mimi labda hata mapenzi yenyewe siyajui.......
Mimi mwanamke akiniacha huwa najisemea moyoni....\
wait till i become a billionaire.....my laugh will come last....
How stupid i am....
Wanasema mwanamke akikuacha it means u r not a good enough..
Mostly financially......
But offcourse kuna mengineyo yanachangia.....
 
Ktk mahusiano yangu NN nimeacha mara mbili na zingine zote nimetemwa. Kutemwa kwingine kulikuwa kuchungu kuliko uchungu wenyewe kuliambana na KASHFA na MATUSI. Samahani staki kukumbuka hayo matukio, ni hatari.
 
Jaman kuna watu wanaakili kuliko kuwa clever. sijapost entry siku nyingi sana. nakuja hv:
kuachwa au kuacha, hiv vitu tujitahid kuvifanya kwa mazungumzo ya pamoja, kwan mwenzenu niliachwa halafu kwa mbwe mbwe kibao,, lakin baada ya muda wa miaka miwil familia ya aliyeniacha walipata shida na mkombozi ni mimi kutokana kaz ninayofanya. je nisaidien kabla sijawambia what i did. je ningefanyeje, nimsaidie kutatua shida ama niponde za kichwa?????????????????:angry::painkiller::yuck:
 
moja ya vitu vibaya sana katika mahusiano ya kimapenzi ni kuachwa na mpenzi wako (to get dumped). Mbaya zaidi ni pale unapoachwa kwa ghafla bila hata kuona dalili. Unastukia tu mwenzako anakata mawasiliano. Hakupigii tena simu. Ukimpigia yeye hapokei. Ukimwandikia waraka wa elektroniki (email) hakujibu wala nini. Haya yote yanatokea siyo kwamba kapotea na hakuna anayejua yuko wapi. Unajua yupo kabisa na jumbe zako zote unajua anazipata lakini hazijibu kwa makusudi tu.

Pole pole fikra za kuachwa zinaanza kukujia kichwani. Mara unaanza kushikwa na machungu moyoni. Unajiuliza mengi lakini hupati majibu. Unaanza kujiuliza pengine labda kuna kitu ulimkosea....unajiuliza weee hadi kichwa kinaanza kukuuma lakini hupati jibu. Hukumbuki hata kidogo kama ulimkosea kitu maana mara ya mwisho mlipokuwa wote kila kitu kilionekana kuwa shwari na mkaagana vizuri tu kama ilivyo desturi yenu.

Mwishowe unakuja kustukia tu kuwa umeachwa na hiyo ndiyo hali halisi na ndiyo ukweli wenyewe. Nguvu zinakuishia mwilini. Maumivu unayasikilizia kuanzia kwenye moyo hadi tumboni. Maisha unaanza kuyaona kama hayana thamani tena. Hata hamu ya kula inaisha. Unajiuliza hivi kwa nini mimi (why me).

Mdau, umewahi kuachwa au kumwacha mpenziyo? Kama uliwahi kuachwa ulijisikiaje na ulikabilianaje na hali hiyo? Ulilia? Ulijikaza tu kisabuni hadi ukapoa? Na kama umewahi kumwacha mpenziyo, ulimwacha achaje? Ulimwambia au ulitimka tu kimya kimya na yeye akaja kustukia baadaye?

pole!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom