Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,232
- 113,610
Moja ya vitu vibaya sana katika mahusiano ya kimapenzi ni kuachwa na mpenzi wako (to get dumped). Mbaya zaidi ni pale unapoachwa kwa ghafla bila hata kuona dalili. Unastukia tu mwenzako anakata mawasiliano. Hakupigii tena simu. Ukimpigia yeye hapokei. Ukimwandikia waraka wa elektroniki (email) hakujibu wala nini. Haya yote yanatokea siyo kwamba kapotea na hakuna anayejua yuko wapi. Unajua yupo kabisa na jumbe zako zote unajua anazipata lakini hazijibu kwa makusudi tu.
Pole pole fikra za kuachwa zinaanza kukujia kichwani. Mara unaanza kushikwa na machungu moyoni. Unajiuliza mengi lakini hupati majibu. Unaanza kujiuliza pengine labda kuna kitu ulimkosea....unajiuliza weee hadi kichwa kinaanza kukuuma lakini hupati jibu. Hukumbuki hata kidogo kama ulimkosea kitu maana mara ya mwisho mlipokuwa wote kila kitu kilionekana kuwa shwari na mkaagana vizuri tu kama ilivyo desturi yenu.
Mwishowe unakuja kustukia tu kuwa umeachwa na hiyo ndiyo hali halisi na ndiyo ukweli wenyewe. Nguvu zinakuishia mwilini. Maumivu unayasikilizia kuanzia kwenye moyo hadi tumboni. Maisha unaanza kuyaona kama hayana thamani tena. Hata hamu ya kula inaisha. Unajiuliza hivi kwa nini mimi (why me).
Mdau, umewahi kuachwa au kumwacha mpenziyo? Kama uliwahi kuachwa ulijisikiaje na ulikabilianaje na hali hiyo? Ulilia? Ulijikaza tu kisabuni hadi ukapoa? Na kama umewahi kumwacha mpenziyo, ulimwacha achaje? Ulimwambia au ulitimka tu kimya kimya na yeye akaja kustukia baadaye?
Pole pole fikra za kuachwa zinaanza kukujia kichwani. Mara unaanza kushikwa na machungu moyoni. Unajiuliza mengi lakini hupati majibu. Unaanza kujiuliza pengine labda kuna kitu ulimkosea....unajiuliza weee hadi kichwa kinaanza kukuuma lakini hupati jibu. Hukumbuki hata kidogo kama ulimkosea kitu maana mara ya mwisho mlipokuwa wote kila kitu kilionekana kuwa shwari na mkaagana vizuri tu kama ilivyo desturi yenu.
Mwishowe unakuja kustukia tu kuwa umeachwa na hiyo ndiyo hali halisi na ndiyo ukweli wenyewe. Nguvu zinakuishia mwilini. Maumivu unayasikilizia kuanzia kwenye moyo hadi tumboni. Maisha unaanza kuyaona kama hayana thamani tena. Hata hamu ya kula inaisha. Unajiuliza hivi kwa nini mimi (why me).
Mdau, umewahi kuachwa au kumwacha mpenziyo? Kama uliwahi kuachwa ulijisikiaje na ulikabilianaje na hali hiyo? Ulilia? Ulijikaza tu kisabuni hadi ukapoa? Na kama umewahi kumwacha mpenziyo, ulimwacha achaje? Ulimwambia au ulitimka tu kimya kimya na yeye akaja kustukia baadaye?