Kozi ya Diploma ya Mineral Processing inatolewa chuo gani?

Mnyunguli

JF-Expert Member
Dec 21, 2020
1,570
3,909
Wanazengo naomba kujua ni chuo gan kinatoa hiyo kozi ya Mineral processing ngazi ya diploma (stashahada).

Bodi ya mikopo inayotoa mikopo kwa diploma wamesema hii kozi itapewa kipaombele ila mpaka sasa sijaiona inatolewa chuo gani, nimewauliza National Council for Technical Education (NACTE) kuhusu hiyo kozi ya diploma kuwa inatolewa chuo gani nao wanashangaa.

Zingatia kozi ni mineral processing kama ilivyoelekezwa.

Kozi nyingine ni ya railway constructions and maintanance hii nayo sijui inatolewa wapi....Mtalaamu anayejua anisadie
 
Angalia UDOM kuna diploma in mineral exploration and mining....

So mineral processing itakua ndani humo.

Udom kuna mineral exploration and geology pamoja na kozi ya diploma in mining engineering...


So mineral processing nadhani still inajitegemea.
 
Mineral Resources Institute MRI ila kwa sasa kipo chini ya ya UDSM...kipo Dodoma karibu na chuo cha mipango, masomo mema ukakaze msuli pale.
 
Hiko ni chuo kinatambulika na nacte?
Lazima hawa jamaa wamejipanga sana, ila jibu langu lisiwe source ya jibu la swali lako anyone interested awafuate hapo Mwanza au kama ni mbali cheki website yao na simu zao kwa maelezo kamili.
 
Mineral Resources Institute MRI ila kwa sasa kipo chini ya ya UDSM...kipo Dodoma karibu na chuo cha mipango, masomo mema ukakaze msuli pale.
Nimechek prospectus ya nacte sijakiona aisee
 
Udom kuna mineral exploration and geology pamoja na kozi ya diploma in mining engineering...


So mineral processing nadhani still inajitegemea.
Hakuna diploma ya mineral processing.

Mineral processing ipp ndani ya mineral exploration and mining.

Angalia module zake utaipata ipo ndani humo.

Nimekusaidia kuangalia vyuo karibu vyote inaanzia bachelor...
 
Back
Top Bottom