Suzy Elias
JF-Expert Member
- Nov 9, 2021
- 1,067
- 6,193
Kwanza ieleweke, kisasi ni haki!
Kwa namna Paul alivyotengwa na kunangwa, kutwezwa na hata kusilibiwa na mahasimu wake kipindi alipokuwa hana kazi ni wazi kama lipo kosa atalitenda ni kutolipa kisasi kwalo.
Paul, kwanza anapaswa aelewe watesi wake walianza kumtafutia namna ya kummaliza tena tokea waliposikia tetesi ya kurejeshwa kwake.
Paul, pili atambue vita vimhusuzo sasa ni zaidi ya vile vilivyopita hapo nyuma!
Paul, tatu asithubutu kumwamini yeyote awaye baada ya fursa ya kiuongozi aliyoipata kwa mara nyingine.
Mwisho ( na si kwa u-muhimu ), Paul ni lazima alipe kisasi cha haja na kuwatenga mbali watesi wake ili kuwanyima wasaa wanao weza kuutumia kumwangamiza kwa ukaribu alio nao sasa.
Kwa namna Paul alivyotengwa na kunangwa, kutwezwa na hata kusilibiwa na mahasimu wake kipindi alipokuwa hana kazi ni wazi kama lipo kosa atalitenda ni kutolipa kisasi kwalo.
Paul, kwanza anapaswa aelewe watesi wake walianza kumtafutia namna ya kummaliza tena tokea waliposikia tetesi ya kurejeshwa kwake.
Paul, pili atambue vita vimhusuzo sasa ni zaidi ya vile vilivyopita hapo nyuma!
Paul, tatu asithubutu kumwamini yeyote awaye baada ya fursa ya kiuongozi aliyoipata kwa mara nyingine.
Mwisho ( na si kwa u-muhimu ), Paul ni lazima alipe kisasi cha haja na kuwatenga mbali watesi wake ili kuwanyima wasaa wanao weza kuutumia kumwangamiza kwa ukaribu alio nao sasa.