Kosa hili ni kubwa sana, rais Magufuli kafanya

Safi sana mleta mada. Hata hivyo kicha cha habari kinamushkeli kidogo kulingana na mada yenyewe.

Tatizo wabongo hawawezi kutumia fikra zao kwa maslahi ya taifa lao. wanaamini kuwa kwao kambi ya upinzani wakati wa uchaguzi basi watabaki wapinzani daima, tena kwa kupinga kila kitu. Kwa maana nyingine ni kuwa kuna wapuuzi wasioitakia mema tanzania. kwao maendeleo ya taifa ni tusi. Hawana hata chembe ya uzaelendo.
Mbaya zaidi ni ulimbukeni wa baadhi ya wabongo. wanashabikia tu hata kitu kisicho cha kushabikia. Amini nakuambia, hata leo raisi aseme kila mtanzania apewe gari yake ya kutembelea watapinga tu, tena pasipo sababu ya msingi. Angalia hii mada, waswahili badala ya kumjibu mleta mada kulingana na habari aliyoleta waatukama matusi. Sijui lini tutafika
Mkuu hio heading niliiweka makusudi, ili wanaufipa wakimbilie ,niliiweka Kama bosheni tu,kila wakiingia holaa!
 
Badilisha kichwa cha Habari mkuu, Natamani uniambie usalama uko wapi kama Ben saanane hajapatikana hadi Leo, waliomshambulia lisu hawajulikana hadi Leo, waliomuua mawazo wako wapi?, risasi iliyouwa akwilina ilitoka wapi, wanaookotwa ufukweni wanauawa na nani, bombadye alishikiliwa kwa nn? 1.5 trillion imetumikaje?...........yapo meeeengi kama haya ndiyo yanasababisha watu waseme HAWAPO SALAMA!
NILITARAJIA UNGEKUJA NA MAJIBU YA HAYA ILI KUONYESHA USALAMA ULIVYO

pia naomba uniambie hadi ashambuliwe nani ndipo nchi kwako haiko salama?
Kichwa cha habari kiko Sawa, labda ulitaka kikupendeze wewe, najua ulikurupuka, kuingia ukakuta holaa!
 
Chadema wakati wa Dr Slaa walikuwa wapinzani kwelikweli lakini hawa wa sasa wamekuwa maharamia wa maendeleo.
 
Hata wakati Makonda anavamia Clouds media group nchi illikuwa alama. Hata wakati anatoa maelekezo mweye vyeti feki apige kazi nchi nilikuwa salama, hata wakati watu kutekwa,kuteswa na kuuawa kwa kuikosoa sérikali nchi nilikuwa salama.
Upotevu/wizi wa 1.5 trillion na mzalendo wa lumumba nchi ilikuwa salama..
U r not obliged, dame u!!
 
Magufuli bado anayo nafasi ya kufanya hayo yate mazuri pasipo kupoteza roho za watu.
 
hakuna maslahi bila kujali uhai wa mtu hayo maslahi ni kwa faida ya nani..... maslahi gani haswa unaweza yaweka hapa yanayogusa mwanach 1/1. Maji hola, umeme taabani, barabara ni zilezile za miaka yote... watusmishi mishahara ni ileile .. wakulima wameshindwa kuuza mazao yao yamedoda kwa hasara.. hawa ndo anapaswa kuwagusa si blablah bila facts
Bla bla naziona toka kwako, kodi nyingi Kwa wakulima zimeondolewa, hio ni hatua moja, mambo ni mengi, hatua Kwa hatua
 
Mleta uzi inasikitisha unapotumia uwezo wako wa kujenga hoja kwa kuleta uzi wa upotoshaji ili ionekane rais anafanya mambo mazuri lakini anapingwa. Hii inaonyesha wazandiki ni wengi na nyie ndio mnachangia kumpotosha rais ili muendelee kufaidi.

Ni mtanzania gani umemuona akipinga rais kutoa elimu bure? Ni mtanzania gani umemuona akienda kubomoa mradi wowote aliosimamia rais ili aonekane hafai? Kuna sisi tunaokosoa ununuzi wa ndege na tunasema angewekeza nguvu kwenye kilimo kwani huko angegusa watanzania zaidi ya 70%.

Rais anapingwa na kukosolewa na wengi kwa kubana demokrasia, kuongoza nchi kwa kuongopa mambo mengi, kujenga uhasama kwenye nchi tena kwa sababu za kiitikadi huku akikiri mwenyewe hadharani kwamba si mwanasiasa mzuri, na nyie watetezi wake mshindwe kumshauri hata kwenye udhaifu anaoukiri. Sasa hivi taasisi zote za kimamlaka kama bunge, mahakama,
majeshi nk ni kama zimefubaa yakisubiri kila kitu mpaka aamue yeye. Juzi tumeona chaguzi za marudio chama chake kikiendesha chaguzi za kikatili na kulazimisha kushinda kinyume na utaratibu. Ajira hakuna, maisha yanazidi kupanda, mfano mrahisi angalia bei ya sukari sasa na aliyokuta. Haya umetetea mambo mengi, inakuwaje kuna 1.5t yenye utata? Je hii nayo ni kwa sababu ya hayo malalamiko yako. Halafu hii tabia ya kusema watu wanatumika huku watu hao wakilalamikia mambo yaliyo wazi huwa mnaitoa wapi?
Hakuna elimu ya bure sisi tunalipia kodi watu wengine,bila sisi walipa kodi hakuna elimu hiyo ya msaada.Imefika wakati watu wajitambue kuwajibika siyo kulialia kila mara.
 
Mtoa mada na wwe jizi kubwa! Uhuru wa habar, democracy huru,Na usalama wa RAIA viko wapi vitu hivi!
Watanzania wanapumbazwa kwa vitusho vikari.
Ninawasiwasi na uwezo wako wa kung'amua mambo
 
Watanzania ni watu wa ajabu Sana, wakati nyara za taifa zinaporwa nchi ilikua salama, wakati, kodi za wananchi zikilipwa mishahara hewa nchi ilikua salama, wakati watoto wa maskini wengi walishindwa kupata elimu Kwa kua walishindwa kumudu Karo na michango, nchi ilikua salama, wakati serikali ilpolaumiwa Kwa kua na shirika la ndege lisilo na ndege nchi ilikua salama, wakati wakulima wakikomolewa na kodi nyingi katika mazao yao nchi ilikua salama ,wakati ujambazi nchini na biashara ya madawa ya kulevya ilishamiri nchi ilikua salama, wakati nidhamu ya watumishi wa sekta ya umma ilikua poor, nchi ilikua salama, wakati misamaha ya kodi ilikithiri nchi ilikua salama, wakati madini yalipokua yanatoroshwa Nje ya nchi, nchi ilikua salama ,ccm ilipopuuza madai ya wapinzani nchi ilikua salama, wakati bajeti ya huduma za afya ilikua chini, Nchi ilikua salama, wakati uvuvi haramu ulishamiri nchi ilikua salama, wakati migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji ilishamiri nchi ilikua salama,

Rais Magufuli umefanyia kazi changamoto hizi Kwa muda mfupi, kwa weledi wa hali ya juu, ukishirikiana na wasaidizi wako makini, , nchi si salama ,miradi mikubwa ya miundo mbinu imeanzishwa na inatekelezwa nchi sio salama. Lipi jema Kwa wanadamu?, usinge fanya kazi wangesema unaona ccm ni walewale

Ama kweli, duniani tenda wema wende zako , usingoje shukrani .

Mkuu rais, kuna kundi la watu wachache, wana nafasi nzuri kiuchumi ,tena baadhi si fedha halali walilipora taifa , waliamini nchi ni mali yao binafsi, walifanya watakavyo kulihujumu taifa, umegusa maslahi yao, wanatumia kila njia kuhakikisha unakwama, wananunua watu,na magazetini ya ndani na nje kuhakikisha nchi haisongi mbele, ili wapigiwe magoti.

Mkuu rais, songa mbele, ukisita tu,mahasimu watachukua point, usisite wananchi wengi wamekuelewa, wanaimani kubwa kwako, usituangushe,

Hizi kelele nyingi ni za wafa maji, waliozoea kitonga, ninyooshee mkuu!
Mkuu nikuulize tu, hayo uliyo ya taja yalifanywa na serikali gani? Na je walio fanya hayo hawajulikani? Kama wanajulikana wamechukuliwa hatua gani?
Pia naomba kujua hiyo miundo mbinu mikubwa unayo isema tofauti na railway ya SGR
 
Back
Top Bottom