Kontena la futi 40 lililosheheni meno ya tembo lakamatwa Unguja!

Adrian Stepp

JF-Expert Member
Jul 1, 2011
2,764
2,581
Kontena lenye urefu wa futi 40 lililojaa pembe za ndovu limekamatwa kisiwani Unguja mchana huu likitokea bandari ya Dar es Salaam.

Mpaka sasa haijajulikana mzigo huo una thamani ya kiasi gani na raia wawili wa Tanzania wamekamatwa kuisaidia polisi .

Kwa mujibu wa Waziri Kagasheki, kontena hilo pia linahisiwa kumilikiwa na raia wa China.

Tukio hilo limeshudiwa na Waziri wa nchi tawala za mikoa Zanzibar pamoja na Waziri wa maliasili na Utalii Balozi Hamisi Kagasheki.

Source: Eatv/ Radio

==================
Picha
==================




date.png
7:42 PM
comments.png





IMG_0149.JPG


Kamanda wa Kikosi cha Polisi Bandarini Zanzibar akiongoza Operesheni wa kukagua magunia yaliokuwa na Pembe za Tembo yaliokamatwa katika bandari hiyoleo yakiwa katika harakati ya kusafirishwa nje ya Nchi kupitia bandari hiyo, zoezi hilo limefanywa chini ya Jeshi la Polisi Bandari Kikosi cha KMKM, yalikuwa katika Kontena la futi 40.


Askari wa jeshi la Polisi wakitowa Pembe za Tembo katika makunia wakati wa zoezi hilo leo asubuhi katika bandari ya Malindi Zanzibar.

Magunia haya yakiwa na sehena na makombe ya pwani wakati katikati yakiwa na viroba vya mPembe za Tembo ambayo yakiwa yamehifadhiwa katika Kontena likiwa tayari kusafirishwa nje ya Nchi, limegunduliwa katika bandari ya Zanzibar leo asubuhi.

Zoezi likiendelea kupekuwa makunia ya Makombe ya Pwani kutowa magunia yaliohifadhiwa Pembe za Tembo

Baadhi ya Pembe za Tembo zilizokamatwa katika bandari ya Malindi Zanzibar yakisubiri kuhisabiwa kupata idadi kamali na thamani yake na uzito kwa ujumla.

Operesheni ukiendelea kuhesabu Pembe za Tembo zilizokamatwa katika bandari ya Zanzibar wakiweka hesabu sawa kuhakikisha hesabu iliokamilika na kupata thamani yake halithi.
IMG_0186.JPG

Zikipimwa uzito kujuwa uzito wake kila gunia likipimwa kupata uzito wake wote.



source; Paparazi

 
Adrian Stepp embu chunguza kwanza mmiliki wa meli iliyobeba kontena ni nani? Taharifa yako nzuri inaitaji nyama nyama tuone kama kaa mbali na tembo anahusika kivipi.
 
Last edited by a moderator:
Kontena lenye urefu wa futi 40 lililojaa pembe za ndovu limekamatwa kisiwani Unguja mchana huu likitokea bandari ya Dar es Salaam

Mpaka sasa haijajulikana mzigo huo una thamani ya kiasi gani na raia wawili wa Tanzania wamekamatwa kuisaidia polisi

Kwa mujibu wa Waziri Kagasheki, kontena hilo pia linahisiwa kumilikiwa na raia wa China.

Source: Eatv/ Radio

Hadi pale ccm itakapoondoka madarakani, na hasa pale katibu mkuu wake Kinana atakapotiwa ndani ndipo tutakuwa na uhakika kuwa tembo wetu watanusurika.

Vinginevyo hadi kufikia mwaka 2015 tutakuwa hatuna tembo hata mmoja kwa spidi hii wanayoendelea nayo ya kuwaua tembo wetu.

Huu ushirika wa ccm na wachina ndio umezidi kutumalizia tembo wetu kwahiyo tunatakiwa tuwatimue nchini wachina kama hatua ya kwanza ya kuwanusuru tembo wetu kabla ya kuwatimua madarakani ccm 2015.
 
Back
Top Bottom