Kodi ya mishahara ya watumishi wa muungano kubaki zanzibar waziri wa fedha zanzibar.

Kakke

JF-Expert Member
Dec 4, 2010
1,883
1,482
[h=2][/h] Waziri wa Fedha Zanzibar Omar Yussuf Mzee


Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imo katika hatua za mwisho za kujua idadi ya wafanyakazi wa taasisi za muungano wanaofanya kazi Zanzibar ili kuwatoza kodi kwenye mishahara yao.
Waziri anaeshughulikia masuala ya fedha na uchumi Omar Yussuf Mzee amesema kodi hizo zitasaidia kuimarishaji utoaji wa huduma za kijamii kama vile, maji, afya na elimu.
Akijibu suala katika kikao cha baraza la wawakilishi amesema mpango huo utasaidia kupatikana kwa zaidi ya shilingi bilioni 21 katika mwaka huu wa fedha 2012/2013.
Amesema katika kikao cha kujadili kero za muungano hivi karibuni kiliagiza kurekebisha sheria ya kodi ya mapato ili kuruhusu kodi za ajira kuhamishiwa sehemu anayofanyia kazi muhusika
[h=3]Like this:[/h]Like
 
Back
Top Bottom