Filosofia ya Rorya
JF-Expert Member
- Sep 20, 2021
- 3,214
- 3,587
Ole wako unayenunua simu ya kiganjani kwa mtu badala ya dukani.
Wengi wanatambia simu za mkopo na wanaoshindwa kumaliza mkopo baadhi yao hujitoa akili kwa kuziuza na kutokomea.
Makampuni ya simu za mikopo yanaanza operesheni maalum rasmi ya kukusanya madeni na ku-recover simu hizo kwenye robo ya kwanza ya mwaka 2024.
Makampuni ya mikopo ya bodaboda nayo yanajifua kuanza operesheni mwakani. Usinunue bodaboda mikononi bila ya kuwa na uhakika na ununuzi wake wa awali.
Maisha ya Mtz yanazidi kuwa kwenye hotspot. Mtz anadiwa kimataifa, kitaifa na kibinafsi.
Mtz ana simu ya mkopo, boda ya mkopo, servant quarter ya mkopo benki, sufuria za mkopo za Waturuki, vifaa vya ujenzi vya mkopo kwa Massawe wa Kishimundu, TV set ya mkopo kwy duka la Mkinga wa kutoka Makete, ticket ya mkopo ya Precision Air, digrii ya mkopo ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu, malimbikizo ya ada ya uanachama wa CCM ambayo kwa mwezi ni 100/ kwa mwaka ni 1,200/ tu, mke wa mkopo (anadaiwa mahari), anadaiwa marejesho vicoba sehemu 4 tofauti (1. Kaushadamu, 2. Usiku wa deni mfupi, 3. Kopauchizike, 4. Vunjandoa)
NB: Wachumi wa nchi hii mliosomeshwa kwa kodi zetu mko wapi? Mnafanya nini kuokoa taifa na hali hii? Nyie ni sehemu ya kuifikisha nchi kwy hali hii au?
Wengi wanatambia simu za mkopo na wanaoshindwa kumaliza mkopo baadhi yao hujitoa akili kwa kuziuza na kutokomea.
Makampuni ya simu za mikopo yanaanza operesheni maalum rasmi ya kukusanya madeni na ku-recover simu hizo kwenye robo ya kwanza ya mwaka 2024.
Makampuni ya mikopo ya bodaboda nayo yanajifua kuanza operesheni mwakani. Usinunue bodaboda mikononi bila ya kuwa na uhakika na ununuzi wake wa awali.
Maisha ya Mtz yanazidi kuwa kwenye hotspot. Mtz anadiwa kimataifa, kitaifa na kibinafsi.
Mtz ana simu ya mkopo, boda ya mkopo, servant quarter ya mkopo benki, sufuria za mkopo za Waturuki, vifaa vya ujenzi vya mkopo kwa Massawe wa Kishimundu, TV set ya mkopo kwy duka la Mkinga wa kutoka Makete, ticket ya mkopo ya Precision Air, digrii ya mkopo ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu, malimbikizo ya ada ya uanachama wa CCM ambayo kwa mwezi ni 100/ kwa mwaka ni 1,200/ tu, mke wa mkopo (anadaiwa mahari), anadaiwa marejesho vicoba sehemu 4 tofauti (1. Kaushadamu, 2. Usiku wa deni mfupi, 3. Kopauchizike, 4. Vunjandoa)
NB: Wachumi wa nchi hii mliosomeshwa kwa kodi zetu mko wapi? Mnafanya nini kuokoa taifa na hali hii? Nyie ni sehemu ya kuifikisha nchi kwy hali hii au?