Kiwanda Cha TPI Chafungiwa

2mbaku

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
316
67
Mamlaka ya chakula na dawa TFDA imesimamisha uzalishaji pamoja na usambazaji wa dawa bandia za kupunguza makali ya ukimwi ARVs zilizokuwa zikizalishwa na kiwanda cha TPI kilichopo Arusha kutokana na kubainika kuwa ni dawa bandia ambazo tayari zilikuwa katika soko.

Hayo yamesemwa na mkurugunzi wa TFDA Hiiti Silo wakati akito ufafanuzi juu ya usitwaji wa uuzwaji wa dawa hizo mbele ya waandishi wa habari Jijini dar es salaam.

Dawa hizo ambazo kiwanda cha TPI lTd kiliuzia bohari ya dawa MSD na kugundulika kuwa ni bandia zilisitishwa kutengenezwa na kusambazwa October 4 mwaka huu kutokana na ukaguzi kufanyika mara mbili kwa lengo la kujiridhisha kutokana na wizara ya afya na ustawi wa jamii kutoa taarifa kwa uma juu ya uwepo wa dawa hizo katika mfumo wa biashara.

Silo amesema kuwa licha ya kukifungia kiwanda hicho lakini taratibu za kutoa adhabu nyingine kama kufuta leseni ndio zitafuatwa baada ya uchunguzi kukamilika kwa kuangalia kwa kiasi gani dawa hizo zilisambazwa.

Dawa hizo ambazo zinatumia jina la kibiashara TT-VIR 30 tayari zilikuwa sokoni ingawa bado madhara yake hayajathibitika kwa watumiaji lakini tayari TFDA imesema kuwa ipo katika hatua za uchunguzi.

Tayari wizara ya afya na ustawi wa jamii ilitoa taarifa kwa uma juu 7 mwaka huu juu ya uwepo wa dawa bandia za kupunguza makali ya ukimwi ingawa kumekuwepo na mkanganyiko wa taarifa ambazo zinaonekana kuwa kiwanda cha Tanzania pharmaceutical Industries TPI kinaendelea na uzalishaji wa dawa hizo

Source: Star TV
 
Hivi watu ambao wamekuwa wanatumia hizo dawa bandia wanaweza kuungana na kuweka wakili, na kudai fidia? Hii itawashikisha adabu watu wanachezea maisha ya watu.
 
Wagonjwa hapa kuna mihela ya bure ushahidi uko wazi kwamba kiwanda kimefungiwa changamkeni....
 
Anganya toto mchana kweupe,huu ni mradi wa CCM wanakusanya pesa ajili uchaguzi ujao,Madabida ameshapewa ulaji mwingine na njia kuwa karibu na watawala na chama,hatudanganyiki kitoto namna hiyo;
 
Anganya toto mchana kweupe,huu ni mradi wa CCM wanakusanya pesa ajili uchaguzi ujao,Madabida ameshapewa ulaji mwingine na njia kuwa karibu na watawala na chama,hatudanganyiki kitoto namna hiyo;
Mimi kidogo natofautiana na baadhi ya watu.
Tukikuta noti feki kwenye mzunguko basi hatuwezi kuifungia BOT hata kidogo. Siipendi CCM na viongozi wake mpaka rangi zake na Timu ya Yanga ikiwemo but kwa hili nafikiri TPI hawana makosa.

Nimemsikiliza Zarina Madabida anasema wao hawana mitambo ya kutengeneza dawa zenye leya mbili, wala hawajawahi kua na chupa za aina ile. Hii issue wameipiga watu wa MSD. Au pengine wakati mzigo unatoka njiani kuja MSD wataalamu wakaupiga "change quarter". Mi hawa jamaa wanaojiitaga Papaa sinaga imani nao kabisa.
 
Mimi kidogo natofautiana na baadhi ya watu.
Tukikuta noti feki kwenye mzunguko basi hatuwezi kuifungia BOT hata kidogo. Siipendi CCM na viongozi wake mpaka rangi zake na Timu ya Yanga ikiwemo but kwa hili nafikiri TPI hawana makosa.

Nimemsikiliza Zarina Madabida anasema wao hawana mitambo ya kutengeneza dawa zenye leya mbili, wala hawajawahi kua na chupa za aina ile. Hii issue wameipiga watu wa MSD. Au pengine wakati mzigo unatoka njiani kuja MSD wataalamu wakaupiga "change quarter". Mi hawa jamaa wanaojiitaga Papaa sinaga imani nao kabisa.

hapa ndio nachoka na wabongo siasa imetawala kila kona hadi serious issue kama hii tunaleta siasa unataka ubadilishe mawazo wabongo wataanza kubishana kisiasa kuhusu hii issue na authorities nazo zitaingia kwenye mjadala wa hizi dawa kisiasa na mwisho wa siku kwa vile ilijadiliwa kisiasa mjadala huu utakufa km mijadala mingine ya kisiasa na watu wataendelea kuzitengeneza dawa feki na wabongo tutaendelea kuathirika km kawa,
 
Back
Top Bottom