Goodluck Mshana
JF-Expert Member
- Aug 7, 2011
- 1,271
- 1,119
Habari kwenu Wadau!
Kituo cha Mafuta cha Total ambacho kipo eneo la Mlimani City imekuwa na utaratibu wa hovyo wa kuwanyanyasa Watembea kwa Miguu kwa muda mrefu!
Utaratibu huo umeanza tangu kipindi cha sherehe za Christmas mpaka leo hii! Ukiwa unatembea kwa Miguu, unaendesha baiskeli au ukiwa Mazoezini hauruhusiwi kupita kwenye eneo la kituo cha mafuta!
Wapo Walinzi wa Kampuni (nitaweka Jina soon) wenye Silaha ambao wamejipanga pande zote za Sheli kuzuia watembea kwa Miguu! Utaratibu huo haukuwepo miaka yote! Iweje leo unakuja utaratibu wa ovyo kiasi hiki?
Utaratibu huo wa hovyo umepelekea watu kutengeneza njia mbadala ya kuzunguka kituo cha Mafuta kitendo ambao kimeendeleea kuharibu Mazingira kwa Wananchi kujitengenezea njia zao wenyewe!
Tunataka kujuzwa kama utaratibu huu ni mpya kwa Sheli za Mkoa wa Dar es Salaam na kwingineko Nchini au ni Ubabe wa wenyefedha? Itakumbukwa Sheli hii bado ipo kwenye hifadhi ya Barabara na hivyo kuzuia Service Road inayotokea Mlimani City kuja roundabout ya kuelekea kwa Mama Kamche to Calabash! Kitendo cha kuzuia muendelezo wa service road ndio maana watu wamekuwa wakipita chini ya Paa la Sheli hiyo!
Lakini kwenye Sheli kuna huduma za Kibenki, Supermarket na Biashara ya Vilainishi vya Magari nk.
Tunaomba Mamlaka zinazohusika, ikiwemo Ofisi ya RC Kunenge kuingilia kati unyanyasaji na uzalilishaji unaoendelea kwenye Sheli ya Total pale Mlimani City!
Goodluck Mshana
Kituo cha Mafuta cha Total ambacho kipo eneo la Mlimani City imekuwa na utaratibu wa hovyo wa kuwanyanyasa Watembea kwa Miguu kwa muda mrefu!
Utaratibu huo umeanza tangu kipindi cha sherehe za Christmas mpaka leo hii! Ukiwa unatembea kwa Miguu, unaendesha baiskeli au ukiwa Mazoezini hauruhusiwi kupita kwenye eneo la kituo cha mafuta!
Wapo Walinzi wa Kampuni (nitaweka Jina soon) wenye Silaha ambao wamejipanga pande zote za Sheli kuzuia watembea kwa Miguu! Utaratibu huo haukuwepo miaka yote! Iweje leo unakuja utaratibu wa ovyo kiasi hiki?
Utaratibu huo wa hovyo umepelekea watu kutengeneza njia mbadala ya kuzunguka kituo cha Mafuta kitendo ambao kimeendeleea kuharibu Mazingira kwa Wananchi kujitengenezea njia zao wenyewe!
Tunataka kujuzwa kama utaratibu huu ni mpya kwa Sheli za Mkoa wa Dar es Salaam na kwingineko Nchini au ni Ubabe wa wenyefedha? Itakumbukwa Sheli hii bado ipo kwenye hifadhi ya Barabara na hivyo kuzuia Service Road inayotokea Mlimani City kuja roundabout ya kuelekea kwa Mama Kamche to Calabash! Kitendo cha kuzuia muendelezo wa service road ndio maana watu wamekuwa wakipita chini ya Paa la Sheli hiyo!
Lakini kwenye Sheli kuna huduma za Kibenki, Supermarket na Biashara ya Vilainishi vya Magari nk.
Tunaomba Mamlaka zinazohusika, ikiwemo Ofisi ya RC Kunenge kuingilia kati unyanyasaji na uzalilishaji unaoendelea kwenye Sheli ya Total pale Mlimani City!
Goodluck Mshana