funzadume
JF-Expert Member
- Jan 28, 2010
- 13,565
- 21,046
Funza naingia, ukumbini kuelezea
Utamu wa kitumbua, hakika mnaujua
Nikila nafurahia,na usingizi unijia
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
Nenda kwa mama Maria, lazima utarudia
Jinsi anavyoumua, na sukari kukitia
Kinanoga kitumbua, kwa chai ukishushia
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
Zilikuja Kalimati, lakini haziku chati
Zikaja na chapati, zenye nyingi hanjumati
Pia vikaja visheti, na kupitwa na wakati
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
Upole watakinana, kitumbua kukichana
kile ukiwa wima hata kwa kuchutama
Kukosa utalalama, na moyo kukusosoma
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
Ukikiona kimevimba, utapenda kukilamba
kwa mchele si pumba, namna ya kukiumba
ni kinene si chembamba, hakika kinabamba
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
Vingine vinakilanga, ukila vina mchanga
Asili yake ni Tanga, sehemu za Kibaranga
Meno yatakubanga, ukivamia kijinga
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
(c) Funzadume (Soli ya Mbingu)
Utamu wa kitumbua, hakika mnaujua
Nikila nafurahia,na usingizi unijia
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
Nenda kwa mama Maria, lazima utarudia
Jinsi anavyoumua, na sukari kukitia
Kinanoga kitumbua, kwa chai ukishushia
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
Zilikuja Kalimati, lakini haziku chati
Zikaja na chapati, zenye nyingi hanjumati
Pia vikaja visheti, na kupitwa na wakati
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
Upole watakinana, kitumbua kukichana
kile ukiwa wima hata kwa kuchutama
Kukosa utalalama, na moyo kukusosoma
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
Ukikiona kimevimba, utapenda kukilamba
kwa mchele si pumba, namna ya kukiumba
ni kinene si chembamba, hakika kinabamba
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
Vingine vinakilanga, ukila vina mchanga
Asili yake ni Tanga, sehemu za Kibaranga
Meno yatakubanga, ukivamia kijinga
Malenga nawaambia, hakuna kama kitumbua
(c) Funzadume (Soli ya Mbingu)