The unpaid Seller
JF-Expert Member
- Oct 27, 2019
- 1,876
- 5,443
" KITU GANI ULICHOKIONA MAISHANI MWAKO KILICHOKUHUZUNISHA ZAIDI ?!"
Peace be with you all,
Maisha yana mengi ya kufurahisha, kushangaza, kuchekesha lakini pia kuhuzunisha. Leo niwashirikishe jambo lililonihuzunisha zaidi maishani, pia wewe tuambie nini kilikuhuzunisha zaidi.
Mwaka 2009 nilipata kuona video ya mwandishi wa habari akichinjwa na watu wenye msimamo mkali wa dini fulani wakiwa wamevalia mavazi meusi waliwa na bendera nyeusi pia yenye maandishi ya kiarabu. Video ili ilikua ndefu, ya kikatili sana sana. Walimchinga kwa kisu butu ili kumzidishia mateso yule mwandishi, video ya zaidi ya dakika 13 jamaa anateseka. aise daa !!
Nakumbuka alivyokua akitikisa miguu iliyofungwa bara bara ni kama alikua akiwasihi wasimuue, lakini haikusaidia jambo, muuaji aliendelea na ukatili ule huku mara kadhaa akimgeuza huku na kule kukwepa damu iliyokua ikiruka kwa kasi isitue kwenye mavazi yake.
Cha kuuzunisha zaidi wakati mateka yule anachinjwa walikuwepo mateka wengine wawili (watalii na daktari waliokwenda kutembelea nchi hiyo) pembeni wamepigishwa magoti wakitazama mwenzao anavyochinjwa na kisha na wao kuchinjwa, hebu fikiria mateso ya kisaikolojia kwa wale wawili (sikuona wao wakifanyiwa ukatili baada ya kufuatilia taarifa zao nilikuja kujua nao waliuawa kwa mtindo ule ule)
Baada ya kuitazama nilipata mawenge kila nikilala kwa wiki mbili mfululizo, nilikua nikuona tukio lile kila nikifumba macho. Tukio lile lilinijaza huzuni sana moyoni, kila nilipowatizama watu mitaani nilitafakari jinsi binadamu tuna roho za kikatili kuliko hata wanyama. What a shame to humanity !!
Niliwaza mengi sana kwa mfululizo na hasa kujiuliza ni kosa gani walifanya mateka wale kustahili mateso makali kiasi kile ?! na kwa kiasi nilipata hasira. Ilinichukua miaka kadhaa kwa picha za tukio kunitoka kichwani na sitaki tena kupitia kipindi cha huzuni kama kile.
Peace be with you all,
Maisha yana mengi ya kufurahisha, kushangaza, kuchekesha lakini pia kuhuzunisha. Leo niwashirikishe jambo lililonihuzunisha zaidi maishani, pia wewe tuambie nini kilikuhuzunisha zaidi.
Mwaka 2009 nilipata kuona video ya mwandishi wa habari akichinjwa na watu wenye msimamo mkali wa dini fulani wakiwa wamevalia mavazi meusi waliwa na bendera nyeusi pia yenye maandishi ya kiarabu. Video ili ilikua ndefu, ya kikatili sana sana. Walimchinga kwa kisu butu ili kumzidishia mateso yule mwandishi, video ya zaidi ya dakika 13 jamaa anateseka. aise daa !!
Nakumbuka alivyokua akitikisa miguu iliyofungwa bara bara ni kama alikua akiwasihi wasimuue, lakini haikusaidia jambo, muuaji aliendelea na ukatili ule huku mara kadhaa akimgeuza huku na kule kukwepa damu iliyokua ikiruka kwa kasi isitue kwenye mavazi yake.
Cha kuuzunisha zaidi wakati mateka yule anachinjwa walikuwepo mateka wengine wawili (watalii na daktari waliokwenda kutembelea nchi hiyo) pembeni wamepigishwa magoti wakitazama mwenzao anavyochinjwa na kisha na wao kuchinjwa, hebu fikiria mateso ya kisaikolojia kwa wale wawili (sikuona wao wakifanyiwa ukatili baada ya kufuatilia taarifa zao nilikuja kujua nao waliuawa kwa mtindo ule ule)
Baada ya kuitazama nilipata mawenge kila nikilala kwa wiki mbili mfululizo, nilikua nikuona tukio lile kila nikifumba macho. Tukio lile lilinijaza huzuni sana moyoni, kila nilipowatizama watu mitaani nilitafakari jinsi binadamu tuna roho za kikatili kuliko hata wanyama. What a shame to humanity !!
Niliwaza mengi sana kwa mfululizo na hasa kujiuliza ni kosa gani walifanya mateka wale kustahili mateso makali kiasi kile ?! na kwa kiasi nilipata hasira. Ilinichukua miaka kadhaa kwa picha za tukio kunitoka kichwani na sitaki tena kupitia kipindi cha huzuni kama kile.