Mkuu nadhani hapo ulipitiwa, ni BAKITA (Baraza la Kiswahili la Taifa).Watanzania wenzangu,
Kuanzia leo, napenda kuwatangazia kuwa neno 'digital' kama litumikavyo kwenye lugha ya Kiingereza katika maswala ya teknolojia, tafsiri yake ya Kiswahili ni 'puru'.
Ifuatayo ni unyambulishaji wa neno hilo kweny matumizi katika Kiingereza na tafsiri yake kwa kiswahili.
--digital world : ulimwengu wa puru
--digitalisation : upurukushaji
--digitalised : imepurushika
--digital : puru
--digitally : kipuru
Wahakiki wa Kiswahili na BAKWATA, naomba kutoa hoja.
Shukrani.
SteveD.
Du, tutakuwa na tafsiri za kumwaga.Mzee digital ni tarakimu. K wa hiyo digital technology ni technolojia tarakinishi.
Huwezi kuwa na tafsiri ya neno "Digital" bila ya kuwa na tasfiri ya neno "analog."
Je "analog" inatafsirijwe kwa kiswahili?
Mkuu nadhani hapo ulipitiwa, ni BAKITA (Baraza la Kiswahili la Taifa).
Nawasilisha!
Na neno digital kuwa ni tarakimu linatokana na ukweli kuwa technolojia ya digital inatumia number maalumu ziitwazo binary digits,yaani unapoandika maandishi yanageuzwa katika mfumo wa 0 1010101 ili yaweze kusafiri kwenda upande mwingine.Rejea herufi za html online.
Ndugu, naomba mnipatie tafsiri au ufafanuzi wa neno 'thread' kwa kiswahili kama itumikavyo kwenye forum hii.
Je,neno jarida/daftari/ukurasa yanaweza kufaa kama tafsiri yake ya kiswahili?
Nyongeza; kwa sababu nauliza swali hii karibia na mwisho wa juma kuanza na kwenye shamlashamla za Eid, nawasihi basi kwa wale wepesiwepesi wa kuchombeza na maneno kuwa tayari nimeshafikiria neno 'kamba' na 'uzi' na nafikiri hayafai kuwakilisha neno thread kama litumikavyo kwenye forum hii. Ahsanteni.
SteveD.