Invisible
JF Admin
- Feb 26, 2006
- 16,294
- 8,327
Kuna mjadala ulikuwa unaendelea baina ya wakenya nami nilikuwa mfuatiliaji wa karibu. Hivi ndivyo mjadala ulivyoanzishwa na nikahisi ni somo kwa wengi!
Na haya chini ndiyo maoni ya baadhi ya waliochangia mpaka sasa:
Mwingine naye:
Mwingine akachangia hivi:
Na huyu akawa na maoni haya:
Naye huyu akaona atie neno:
Haikuishia hapo, huyu akiwa Dar es Salaam akatoa maoni hivi:
Mtanzania mwingine akatia neno:
Mwingine toka Tanzania akakunwa akatoa maoni yake hivi:
Huyu naye hakuwa nyuma:
Na huyu hakuwa nyuma akachangia hivi:
Hawakuishia hapo wakaendeleza wengine hivi:
Huyu ni mpenzi wa ICT akadakia hivi:
Nilikuwa napenda kuendelea lakini niishia hapa kwa kuwaomba wadau maoni yenu juu ya michango ya wenzetu hawa. Bahati mbaya wanatumia Mkundi wa Google hivyo mijadala mingi huwa naipata kwenye barua pepe. Kuna baadhi nimewaalika huenda tukawa nao hapa tukaona maoni yao zaidi.
Asiyeonekana!
Swahili name for resilience is ukakamavu.
Speaking of swahili,I have a challenge to all of us.
Maybe its a high time we as Kenyans cultivate more interest of this language.
It was only jana nilipokutana na mmarekani mmoja mweusi ambaye amejibatiza Otieno.Jamaa huyu ana uchu wa kijifunza Kiswahili.wazungu pia wanajikakamua kujifunza lugha 'yetu'.
Wenzangu, tuna raslimali muhimu, yaani lugha ya Kiswahili, lakini tumefumba macho jamani...
Pokeeni changa moto,mimi nikiwa mstari wa mbele kujikemea..
Ni aibu wala si ushupavu viongozi kufanya makosa ya kisarufi katika usemi wao.
Ni aibu kununua tu magazeti na majarida yaliyochapishwa kwa kiingereza.
Ni aibu kuzungumza kizungu pekee na kutupilia mbali Kiswahili sanifu.
Ni aibu kama wadau wenzangu kuwasiliana tu kwa Kiingereza.
Na ni aibu si haba kwamba ukidurusu maandishi yangu utajikwaa kwa makosa labda ya ngeli au uchaguzi wa nomino mwafaka.
Na ili tujue, ni makosa Kujibu Mzuri unaporejelea maamkio-niligundua (hivi majuzi tu)kwamba Kiswahili sanifu inatushurutisha kuitika Nzuri...kwa sababu ya uwiano wa kingeli baina ya Habari na jawabu lako..
Na haya chini ndiyo maoni ya baadhi ya waliochangia mpaka sasa:
Nakubaliana nawe.
Mbona tumetupilia mbali asili yetu - yaani lugha ya Kiswahili?
Mimi hutafsiri jarida fulani ambalo sisi huchapisha hapa Westlands. Mbona wageni kutoka nje wawe na ari sana ya kuijua lugha yetu, ilhali sisi hapa tumejitia hamnazo, kana kwamba sisi ni wageni?
Lahaula! haya basi, tuanze kwa kusoma gazeti liitwalo Taifa Leo, kisha tuingilie vitabu mbali mbali ambavyo vinaweza kupatikana katika maduka ya kuuza vitabu maalum hapa mjini.
Uwanja ni wenyu wadau wenzangu. Je, mtaipokea changamoto hii?
Sarah
ukweli mtupu,
shida iliyopo sasa hivi ni kwamba sheng imekita mizizi.
sijui tukiamua kuangamiza sheng tutaanzia wapi. Haiwezekani!
Labda tukubali sheng iwe lugha ya kiswahili ya kisasa, tusahau lugha sanifu.
English evolved from latin anyway.
Heshima zako Ndugu,
Maoni yangu ni kuwa hatuhitaji kuangamiza sheng au lugha yoyote ile, ndio maana tunakazana kuikita lugha Kiswahili. Chenye ningependekeza ni kuwa tuzidi kuikuza lugha ya Kiswahili kwa usanifu wake. Sheng inavutia kwa sababu ya kukosa nidhamu makhsusi ya kuisimamia na kuiendeleza ni kuendeleza kuashia wengine kama hatuwezi au hatutaki kutii sheria zozote za nidhamu za taaluma yoyote ile na uishi kwa ujumla basi tunaweza kupuuza hizo kanuni na kubugia raha ya utovu wa nidhamu.
Wasemaje?
Mwingine naye:
And now, Mwanzishaji, would you kindly say all that in English. I'd love to speak Kiswahili well but it is one language I have a problem with. Much like French and German. I can understand it but I am not one for heavy vocabulary like what I can see in your email.
HELP!!!
Mwingine akachangia hivi:
Come on!!! Kiswahili is too pedestrian for any serious person to use in holding a serious conversation!!!
Why do you think Jaramogi never even bothered to learn it?!
Na huyu akawa na maoni haya:
Dr ...., be a serious man. what do you mean too pedestrian? the fact that majority of us can't speak it does not mean that one cannot use it to hold a serious conversation. a big percentage of Kenyan population can only understand Kiswahili as opposed to English. then Daktari what you are saying is that your communication is limited to English speakers only, meaning you cannot reach majority of Keyans therefore you are mean with information. that is my take, do members agree with me?
Naye huyu akaona atie neno:
Kwa wanachama,
Nitarajio langu kuwa haya mazungumzo ya lugha ya Kiswhili ni muhumi sana wakati huu kuliko wakati mwingine. Kwa nini nasema hivyo? Kiswahili ni ligha ya Kitaifa na hata mataifa zaindi ya 125 zimeanza kutumia au kuhimiza watu wajifunze hii lugha.
Kwangu mimi naunga K'Ogutu mkono kuwa hii ni lugha ambayo inaeleweka na wengi hata serikali yetu imeanza kukienzi katika mambo rasmi. Kama fomu za kuchukua pasipoti sasa ziko kwa lugha mbili: Kiswahili na Kiiengereza. Na Daktari kusema kuwa hii ni ligha ya wanaotembea ni matusi kwa mwafrika na hasa Mkenya wa kawaida ambaye anakitumia kama njia yake ya mawasiliano kila siku.
Changamoto; tukienzi lugha na pia tukiuze kama lugha ya mawasiliano. Hata umoja wa mataifa inahitaji kukiorodhesha kama lugha moja ya mawasiliano. Kwa wale wanaosoma taifa leo, kulikuwa na makala jana kuhusu Afrika Mashariki yaweza kukipoteza lugha ya Kiswahili kwa mataifa ya magharibi. Kwa sababu wanakifunza na pia wamewachukua wahadhiri wa lugha ya Kiswahili na wanafunza katika vyuo vikuu.
Kama mwangaza wa jamii wacha tukiendeleze lugha hii yetu.
siku njema
Haikuishia hapo, huyu akiwa Dar es Salaam akatoa maoni hivi:
Mwingine akaendeleza mjadala hivi:Habari wote!
"Hakuna nchi yoyote duniani isiyojivunia lugha yake, na maendeleo ya nchi yanawezekana zaidi pale ambapo luagha ya nchi hiyo inapotumika katika tafiti na uvumbuzi mbalimbali"
Tutake tusitake sisi watu wa afrika Mashariki hasa Tanzania tuna kila sababu ya kujivunia na kukienzi Kiswahili, acheni firkra potofu ya kutukuza lugha za mataifa mengine na kukashifu lugha zenu.
KISWAHILI HUTUUNGANISHA DAIMA
Kwenu wadau,
Mimi binafsi siwezi nikajidai kuwa mkwasi wa lugha ya kiswahili, lakini nakienzi lugha hichi. Na fursa kama hii inanijenga kimsamiati. kile nafahamu mimi ni kwamba lugha yoyote ile kinahitaji ubunifu wa maneno fulani au majina fulani. Hii ni sababu kwamba kuna uzinduzi wa mambo kila wakati." we are in a world of discoveries". majina au maneno fulani hayakwemo kwenye msamiati ya lugha zetu. Kwa mfano Komputa kwa Kijaluo
Mtanzania mwingine akatia neno:
Okay,
si kawaida yangu kujibu kwenye hizi forums, but dr ....., those are your views,
kwangu mimi na watanzania wenzangu wote, tunajivunia kuongea kiswahili kinachotuunganisha na makabila yote nchini na kujenga umoja wa kitaifa, kiswahili kinafundishwa mpaka chuo kikuu, hatuwezi kung'ang'ania lugha za pili, kiswahili kwetu ni heshima ni utaifa na umoja, sijui kwako...............
proud swahili speaker.
Mwingine toka Tanzania akakunwa akatoa maoni yake hivi:
Kwa kweli huu mjadala umenifanya hata mimi nitoe maoni yangu, ingawa si kawaida kufanya hivyo. Sisi watanzania tunajivunia lugha yetu ya taifa sana. Tanzania tuna makabila mengi sana na kila moja linazungumza lugha yake. Iwapo tusingekuwa na lugha ya taifa mawasiliano kati yetu yangekuwa magumu kwa namna moja au nyingine. Rafiki zangu wa West Africa wanatuonea wivu sana maana wao iwapo sio kabila moja inabidi wawasiliane kwa kiingereza au kifaransa!
Nawashauri ndugu zangu wa afrika mashariki tuendeleze lugha ya kiswahili na kujitahidi kuitumia.
Huyu naye hakuwa nyuma:
Mwingine akahamasika akanena hivi:Sisi amepokea mtoto changa wenyu kuangaliana na mdomo ya Kiswahili.Anafurahi nyingi muno,kwa maongezo ya leo.
Kiswahili ndio kitukuzwe.... hapa nchini mwetu Kenya lilnalo adimu Kiswahili chetu ni lugha chipukizi mitaani kama vile sheng....Kando na hayo sisi tunalo ari ya kuitukuza lugha Kiswahili toka pwani hadi ninakotoka bara Kisumu.Tutajipa changa moto huu huu kudumisha ari yetu kama wazazi kuendeleza kiswahili sio tu kwa usemi bali kwa maandishi wa ufalsaha.
Kiswahili hoyeee......
Today, it is brick bats where I am concerned. Let me tell you one thing, wadau, challenge I have accepted. Karibuni, mutani sikia na kiswahili changu kiki ng'ara. Na haitakuwa sheng.
Na muwe na siku ya kuchangamuka!!! )
Na huyu hakuwa nyuma akachangia hivi:
Kwa kweli hii kiswahili chetu yeye ni lugha mzuri sana. yeye amefurahisha mimi sana mithili ya huyu mvua ambaye ananyesha. Lakin huyu mvua wetu amenyeshea blanketi wangu!! wololo yaye!!!!
Hawakuishia hapo wakaendeleza wengine hivi:
Nanu:
Have always wanted to know the kiswahili word for "catch up with me".
May be i left you doing some tasks behind but we were to go to a
certain place together, what should i say to him or her in swahili?
Hujambo Nanu,
Utamwambia "tafadhali nipate... au nikute... au ungana nami..." itategemea muktadha wa utendi wenyewe.
Kwa mfano, kwa mchanjari wa hapo juu ni katika muktadha wa kuwa unaenda, unamusubiri na unamtarajia.
Furahia kuzungumza na kuitumia lugha ya kiswahili.
shukrani na ubarikiwe.
Huyu ni mpenzi wa ICT akadakia hivi:
Kamau naye akachangia hivi katika kumjibu:Neno "facebook" limenipinga njenga! Hebu wasanii watutafsirie.
Naam katika ulimwengu wa teknolojia maneno mengi yatavumbuliwa na njia moja ya kuyatamka kutoka kimombo ni kuyatohoa au kuyatamka katika lugha chanzi.
Kwa uvumbuzi wa istilahai mwafaka wengi watasema tuwangoje Chimera na sheikh Nabahany watuundie istilahi na wengine kati yetu hawatakoma kusema tumuulize Swaleh Mdoe na Babuye.
Kwangu mimi Facebook nikitafsiri kunradhi nikiiundia jina jipya nitapendekeza Mtandaonyuso kwani Facebook ni mtandao ambao watu hutukana na kujuana kwanamna ya picha za nyuso zao.
Nilikuwa napenda kuendelea lakini niishia hapa kwa kuwaomba wadau maoni yenu juu ya michango ya wenzetu hawa. Bahati mbaya wanatumia Mkundi wa Google hivyo mijadala mingi huwa naipata kwenye barua pepe. Kuna baadhi nimewaalika huenda tukawa nao hapa tukaona maoni yao zaidi.
Asiyeonekana!