Kisa cha Kweli: Sitasahau nilivyopendwa na mchawi nikaishia kurogwa

Inaendelea sehemu ya tano.

Nilitembea moja kwa moja hadi getto, nikafika nikajilaza kichwa kilikuwa kina mawazo mengi sana. Naamini watu wengi ambao nilikutana nao njiani inawezekana walibaini siko sawa. Nilikaa sikuwa hata na nguvu ya kupika, nilikuwa nawaza tu. Baadae washkaji tuliokuwa tunakaa nao getto walirudi kutoka shule ilikuwa mida ya saa tisa hivi. Jamaa walilalamika kwa nini nimewahi kurudi kutoka shule lakini sijapika,nikawaambia naumwa. Jamaa walipika ugali dagaa nikala kidogo kwa kujilazimisha. Baadaye nikaona nimfate Vumilia getto kwake ili twende alikokuwa anasema, niliona siwezi kusubiri wakati niko kwenye mdomo wa Simba.

Uzuri alipokuwa anakaa haikuwa mbali sana, nilitembea kwa dakika kadhaa chache nikawa nimefika. Nilibisha hodi akafungua mlango nikaingia ndani. Nilivyoingia, nikaketi chini kwenye godoro lililopo chumbani kwake, nikawa namtazama. Nilimuona kama mtu aliyekuwa amebaki kama tumaini langu la mwisho. Moja kwa moja, nikamwambia twende ulikokuwa unasema. Alikataa akasema nitakuja kukuchukua mwenyewe usiwe na haraka. Nilimbembeleza lakini alikataa katakata akasema atakuja baadae usiku. Niliamua kurudi getto, nikafika nikalala nikimsubiri aje anichukue. Ilifika hadi usiku saa tatu alikuwa hajaja, nikajikuta nimepitiwa na usingizi. Baadae nilishtuka usingizini, kuna mtu alikuwa kama ananivuta mkono. Niliangalia na kumkuta alikuwa mtu ambaye amevaa nguo nyeusi tii, nilipiga kelele kwa nguvu hadi mshikaji wangu mmoja aliyekuwa amelala akashtuka kutoka usingizini. Mshikaji mwingine alikuwa mezani amewasha kibatari anapiga kitabu naye aliniangalia, akaniuliza.

"Vipi unaota?"

Nilimtazama Yule mtu na kugundua alikuwa ni Vumilia. Usoni alikuwa amepaka dawa nyeupe za unga unga. Alinifanyia ishara ya kuniambia nikae kimya. Kilichonishangaza licha ya kwamba Vumilia alikuwa pembeni kidogo tu ya jamaa anayesoma mezani lakini mshikaji alionyesha haoni chochote. Ilikuwa ni kama mimi tu ndiye niliyekuwa namuona. Alinifanyia ishara nisimame, niliwaza kidogo kuona kama nachokifanya ni sahihi. Ghafla kuna wazo lilikuja kichwani likaniambia hivi kwa nini nimemuamini Vumilia ghafla, je kama ndio yeye anataka kunichukua kunipeleka kwa wachawi wenzie wakanimalize, si ndio naenda kufa kirahisi rahisi tena kwa kujipeleka mwenyewe. Wazo hili lilianza kama utani lakini lilinishawishi, nikajikuta natikisa kichwa kuashiria kwamba nimekataa na sikuwa tayari twende naye. Ni kama vile aliyasoma mawazo yangu.

"Vipi umeogopa, au unadhani nataka nikufanyie kitu kibaya, kumbuka nilikuambia uwe jasiri" aliniuliza kwa sauti kubwa

Nilipigwa butwaa na kumuangalia mshikaji aliyekuwa anasoma, lakini macho alikuwa amekodolea kwenye kitabu, ni wazi hakusikia chochote. Nilishangaa nikajisemea moyoni ama kweli duniani kuna mengi. Nilikaa kimya kwa kuogopa nikijibu jamaa angesikia na kuanza kuwaza tofauti.

"Sikia nikwambie mr the dragon, hata hapa nimefanya ustaarabu tu. Ningeamua ningekuchukua kimya kimya hadi ninakotaka kukupeleka bila wewe kujua. Hujiulizi jana umepelekwa makaburini na kuchanjwa bila kujitambua, sasa nikitaka kukupeleka unadhani nitashindwa. Kama hauamini subiri"

Aliongea vile na kuanza kurudi kinyumenyume hadi kwenye kona moja ya chumba na kupotea. Sijui kilitokea nini lakini nilijikuta nashikwa na usingizi mzito ghafla na nilipokuja kushtuka nilijikuta nilikuwa nje ya ile nyumba, Vumilia akiwa pembeni yangu amenishika mkono.

"Umeamini sasa kwamba naweza kukupeleka popote. Sikiliza Mimi napambania maisha yako kwa hiyo fuata kila nitakachokwambia"

Mpaka hapo sikuwa na ujanja zaidi ya kutii amri, niliamua sasa liwalo na liwe. Vumilia alinitangulia na kuniamuru nimfate kwa nyuma. Alianza kutembea kwa miguu halafu mimi nikawa namfata kwa nyuma. Tulitembea kwa mwendo wa dakika chache tukawa tumeshafika kijijini kwetu. Yalikuwa ni maajabu yaani sehemu ambayo huwa tunatembea sio chini ya masaa mawili na nusu tulitembea kwa dakika zisizozidi kumi na tano.

Tulipofika kwenye kijiji chetu alininong'oneza "tunaenda kwa mzee Nkelebe"

Mzee Nkelebe alikuwa ni mganga maarufu wa kienyeji pale kwenye kijiji chetu.

Tulipiga hatua ndani ya dakika chache tulikuwa tumeshafika.

Itaendelea kesho asubuhi!

Leo nimeandika kwa kifupi kuonyesha bado tuko pamoja maana watu washaanza kupata wasiwasi, kwamba sitamalizia. Jamani niko hapa mwanzo mwisho.

Na kesho ni weekend nina muda mwingi wa kuandika kwa hiyo ni bandika bandua.

Usingizi nipumzike. Good night
Usije kuwa kama Mzee wa yunge mdogo na yunge mkubwa.
 
Inaendelea sehemu ya sita.

Tulikuwa tumeshafika kwenye mlango wa kuingia kwa mganga. Unajua familia nyingi za usukumani zinakuwa na wigo au tuseme uzio ambao mara nyingi unakuwa wa miti fulani inaitwa minyaa au "manara" kwa kisukuma, lakini pia wigo mwingine ulikuwa wa mkonge "katani" kwa kisukuma. Na kwenye wigo huu huwa kuna sehemu ya kutokea ambao ndio kama geti la kuingilia. Sasa tulikuwa tumesimama kwenye hiyo sehemu ya kuingilia, lakini tulivyopita tu kuingia Sasa kwa mganga tukawa hatuoni chochote. Nyumba tulizokuwa tunaziona za mganga pindi tukiwa nje ya ule wigo tukawa hatuzioni, ni miti na vichaka tu ndio tukawa tunaona.

"Oooh! nini hiki" alisema Vumilia kwa sauti iliyoashiria kufadhaika na hali ile.

Nilimuangalia kwa sababu nilikosa sababu hata nimjibu nini, kwangu kila kitu kilionekana kama mazingaombwe. Baadaye aliniambia unajua mganga huyu ameweka madawa ya kuzindika eneo lake kwa hiyo sitaweza kupita, hadi nivue nguvu za kichawi nije kawaida ndio nitapita.

"Utavuaje?" Nilimuuliza

"Inabidi tuende kwa bibi"

Tulianza kutembea kwenda kwa bibi yake ambapo ilikuwa ni palepale kijijini kwetu. Sio muda mrefu tulikuwa tumeshafika. Aliingia ndani kwenye moja ya nyumba za pale kwao, akakaa kidogo halafu akarejea.

Safari hii alikuwa amevaa nguo za kawaida . Alikuwa amejifunga kitenge kiunoni na kitenge kingine amekizungusha kwa juu kifuani. Alinyoosha mkono na kunionyesha kopo, akaniambia nichote na kujipaka usoni. Nilichota kitu ambacho ni kama yalikuwa mafuta yakiwa yamechanganywa dawa, ambayo yalifanya kuwa kama mchanganyiko wa mafuta na unga unga. Yalikuwa ni mafuta yenye harufu kali ya kama kitu kilichooza lakini sikujali nilijipaka bila kujiuliza mara mbili. Aliniambia yalikuwa ni mafuta ya aina fulani ya mjusi ambaye kwa kiswahili sijui jina lake yamechanganywa na unga wa mizizi ya miti minne ambayo hakunitajia wala hakunambia matumizi yake.

"Inabidi tutembee haraka, nahisi tuko hatarini" aliongea huku uoga ukiwa dhahiri machoni mwake.

"kwa nini"

" Nahisi wanakutafuta kukuchukua na sasa wako njiani wanakuja, inabidi tufanye haraka tufike kwa mganga. Wakitukuta njiani kabla hatujafika utakuwa hatarini"

"Wamejuaje tumekuja huku" niliuliza nikionyesha mshangao kidogo.

"Wewe huyajui haya mambo, tafadhali tuwahi tuondoke"

Safari hii hatukutembea kama mwanzo isipokuwa tulikuwa tunakimbia ili tuwahi kufika. Na miongoni kati ya vitu vilivyonishangaza mwanzoni tulikuwa tunatumia muda kidogo sana kutembea umbali mrefu, lakini safari hii tulitumia muda mrefu. Haikuchukua muda mrefu toka tuanze ile safari, akaniambia wako nyuma yetu wanatufata. Wakitupata tu umekwisha. Niliogopa sana nikawa natamani hadi kupaa. Niliwaza pia vipi tukifika tena kwa mganga halafu tusipaone halafu huku nyuma tunafukuziwa.

It was probably the most terrifying moment in my life.

Muda sio mrefu nikaanza kusikia vishindo vya watu vinatufuata kwa nyuma. Wakati akili haijakaa sawa nikasikia kishindo kwa mbele yetu ni kama kitu fulani kilikuwa kimerushwa. Tokea pale tukawa tunapata ugumu sana wa kukimbia, miguu ilikuwa mizito sana au niseme ni kama kuna nguvu fulani unakuvuta kwa hiyo unapiga hatua kwa tabu sana. Tulijikongongoja hadi tulipovuka pale ambapo kile kitu kilikuwa kimedondokea. Tulipokivuka tu tukaanza kukimbia tena kwa kasi. Kufupisha story zoezi hili likawa endelevu ikawa kila tukivuka muda sio mrefu, kile kitu (ambacho kwa wakati huo bado sikukijua ni kitu gani) kinarushwa tena, tukivuka baada ya dakika chache kinarushwa tena. Lakini tukikivuka kasi yetu ya kukimbia inaongezeka, kikirushwa kasi inapungua inakuwa kama tunavutwa. Tulihangaika hivyo hadi tulipofika kwenye geti la kuingilia kwa mganga.

"rudini sasa watoto wangu mmewashindwa"

Ilikuwa ni sauti ya kiume ambaye nilikuja kumugundua ni mzee Nkelebe. Alikuwa akiwaamuru wale wachawi warudi walikotoka. Alitupokea na kutupeleka hadi kwenye mojawapo ya kijumba kilichopo pale kwake kilichojengwa kwa nyasi mwanzo mwisho.

Aliingia kwenye nyumba na kuja na viti vidogo aina ya vigoda viwili akatupatia na kutuamuru tukae.

"Unajua mwanzoni niliwaona mlivyokuja mkarudi. Wewe Vumilia ni mwenyeji hapa nilijua umekuja kwa nia njema Na lazima kuna shida hivyo nilijua lazima utarudi tu, hivyo nilikaa kukusubiri"

"Na huyu msabato umemtoa wapi, hadi akawa anakimbizana na wajanja usiku huu" aliendelea kusema huku akiniangalia Kwa unafiki fulani

Ni kama alikuwa ananikumbusha mwaka mmoja uliopita tu, nikiwa na brother mmoja mwinjilisti wa kanisani kwetu muuza vitabu vya dini ambapo nikiwa naye tuliwahi kumtembelea huyo mganga kumhubiri neno la Mungu. Nilikumbuka mwinjilisti yule aliyekuwa hamung'unyi maneno akimwambia mganga wewe unafanya kazi ya shetani utachomwa moto. Na sisi tunaofanya kazi ya Mungu tutaenda mbinguni. Sasa ilikuwaje mtoto wa Mungu anayesubiri mbingu, kwenda kutafuta msaada kwa wachomwa moto.

Ukistaajabu ya Musa, utayaona ya firauni.

"Tuachane na hayo baba huyu kijana anahitaji msaada" alisema Vumilia

"Sawa"

Mzee alisogeza maji kwenye karai dogo akaweka dawa fulani. Akamaliza akachukua kitu kama mkia wa mnyama wenye rangi nyeusi. Kama unaujua mkia wa ng'ombe kule chini huwa unakuwa kama una manyoya manyoya marefu, alichukua mkia wa hivyo sasa. Akamaliza akaanza kupiga manyanga huku akiimba nyimbo na kuongea ongea kama aliyepandwa na wazimu. Baada ya dakika kadhaa akanipa kakipande ka mti wa mnyaa na kuniambia nizungumze shida zangu bila kutoa sauti. Ni kama mtu anavyonuia kitu fulani.

Baada ya kumaliza zoezi lile alikichukua kile kipande akakiloweka kwenye yale maji. Akamaliza akakitoa kisha akaanza kukiangalia.

Akaanza kuniambia.

"Kijana una matatizo makubwa sana. Umefanya vizuri kuja hapa leo la sivyo leo ulikuwa mwisho wako. Kwanza ninaona watu wameandaa sherehe sehemu fulani kufurahia kukukaribisha huko kwenye makazi ya misukule"

"Na ninawaona hadi sasa wamekaa pale nje ya wigo wangu wanakusubiri utoke hapa"

Alisema na kuniangalia, nilikaa kimya sikuwa na la kuongea bado.

Alichukua kopo fulani akalisogeza kwenye mdomo wake, akaongea maneno fulani halafu akachukua dawa nyeusi na kunipaka usoni kisha akaniambia nitoke nje na kuangalia angani. Huku akinielekeza maneno fulani ya kutamka hadi mara tatu. Nilitoka nje huku nikiogopa nikafika nikatazama hewani na kutamka maneno aliyoniambia mara tatu. Yalikuwa maneno sio ya kiswahili wala kisukuma.

Ghafla kilijitokeza kitu cha ajabu angani, ambacho sikukitarajia. Ni kama ilitokea luninga iliyokuwa inaonyesha matukio mbali mbali. Kwa ufupi niliwaona wachawi kuanzia siku ile walivyonichukua wakanipeleka makaburini na kunichanja chale na kila kitu walichokifanya. Kilichonisikitisha zaidi niliwaona bibi yangu na mama yangu mdogo wakiwa na mwanamke mwingine ambaye naye alikuwa wa palepale kijijini. Bibi huyu alikuwa ni mmojawapo wa wake za babu yangu mzaa mama ambaye kwa wakati huo alikuwa marehemu na mama mdogo ni mtoto wa kuzaliwa na huyo bibi. Nilivyoona tu nilijua sababu ya yale yote ni nini.

Kulikuwa na mgogoro baina ya watoto wa mke wa kwanza wa babu yangu ambao ni mjomba wangu, mama mkubwa na mama yangu mzazi ambaye alikuwa ni kitinda mimba. Huyu bibi niliyemuona kwenye luninga ya mzee Nkelebe alikuwa ni mke wa pili kuolewa. Sababu ilikuwa ni mgogoro wa ardhi ambapo mke huyu alidai kuna sehemu ambayo mama yangu na mama mkubwa walichukua, ambayo ilinunuliwa yeye akiwa ndio ameolewa hivyo yeye ndiye haki nayo.

Kumbe nalogwa kisa mgogoro wa ardhi niliwaza!

Baada ya muda luninga ile ilikata matangazo nikarudi kwenye kijumba cha mganga. Kufika tu Vumilia alifungua mdomo wake na kuniambia.

"Nafikiri sasa umeanza kuniamini, mwanzoni nilipokuambia ndugu zako wanakutafuta labda hukunielewa"

Mzee Nkelebe alimtuliza Vumilia kisha akaanza kuniambia.

"Una matatizo mawili ambayo nimeyaona kwako yanayotakiwa kushughulikiwa. Tunaanza na tatizo la kwanza"

Mganga aliniangalia kisha akanambia nikunje suruali yangu. Aliliona kovu ambalo nililipata miaka mingi, siku ile nimeona wachawi nikiwa darasa la tatu. Aliniambia

"Kuna kitu uliwekewa kwenye mwili wako muda mrefu sana nimekiona unacho, tatizo lenu wafiadini hamtembeagi hadi mambo yawafike shingoni, ulitakiwa uwe umeshakiondoa muda mrefu sana" alisema mganga huku akiniangalia kwa umakini pale kwenye kovu.

"Labda nikuulize swali" alisema mganga akatulia kidogo kisha akaendelea

"hivi unadhani kwa nini siku ile unaona wachawi wakati ukiwa bado mdogo, kwa nini wewe peke yako ndio ulizisikia zile kelele za wachawi?. Na unadhani kwa nini ulipotoka nje ulifanikiwa kuwaona wachawi pasipo kutumia dawa yoyote, wakati kikawaida huwezi kuwaona wachawi bila Dawa?"

Aliniuliza lakini niliona dhahiri sikuwa na jibu kamili. Hivyo nikamwambia sijui chochote.

Akaniambia ulipokuwa mtoto ulikuwa na nguvu za asili na ukoo wenu una mizimu mikali sana. Hizo nguvu ndio zilikusaidia kuwaona na kusikia zile kelele, japo sasa hivi zimepungua na ni kawaida kupungua kadri unavyozidi kukua.

"Sasa wachawi hawakufurahishwa na wewe kuwaona, ilibidi wakufate baadae ulipokuwa umelala wakuchane mguu na kukuwekea dawa fulani iliyo kwenye kakipande kadogo ka mti"

"Kazi ya dawa hizo ni kukuzuia wewe ushindwe kusema chochote kila unaposhuhudia tukio la kichawi. Hebu niambie tokea ulivyoona tukio lile ulishawahi kumsimulia mtu kama ulitokewa na jambo kama lile"

"hapana" nilijbu kwa mshangao huku nikikumbuka jinsi moyo ulivyokuwa unakuwa mzito na kuogopa sana kila nilipotaka kumwambia mtu yeyote kuhusu tukio lile.

"Kumbe dawa zile zilikuwa zinafanya kazi" niliwaza

"Amini hata hili tukio la kuchanjwa usingeweza kumwambia yeyote. Na hautaweza kuja kumwambia yeyote kuhusu tukio la kishirikina utakalolishuhudia hadi siku unaingia kaburini, kama tusipoitoa hiyo dawa mwilini mwako" alisema mganga

"Hata baba yako najua usingemwambia, najua ungepata nia ya kumwambia lakini usingethubutu, hivyo watu wasingejua shida yako na usingepata msaada"

Baada ya kumaliza alichukua wembe na kunichana kidogo kwenye kovu.Alipaka dawa kisha akachomoa kipande cha mti kidogo kama vimisumari vile vidogo.

" Sasa uko huru kuongea. Tunaenda kwenye tatizo la pili".alisema kisha akaendelea

"Hili nadhani umejionea mwenyewe, wachawi tayari wana mamlaka juu ya mwili wako maana wameshamaliza maagano na mizimu ya kwenu, kwa tambiko lililofanyika makaburini. Kazi iliyobaki ni kukuchukua. Sasa ili tukurudishe kuna damu yako waliichukua wakati wanafanya tambiko inabidi tuirudishe kwanza" alitulia kidogo kisha akaendelea

"damu hiyo mwanzoni ilikuwa imefichwa kwenye dari la nyumba ya kwa bibi yako. Ila baada ya kujua umeshaanza kutembea kwa waganga kuna sehemu imepelekwa kufichwa pa siri zaidi ambayo mimi kwa uwezo wangu siwezi kuichukua huko. Inabidi nikupeleke kwa mganga ambaye naamini yeye anaweza kukusaidia. Ila ni mpaka nimtaarifu kwanza baba yako kwanza ajue kila kitu. Maana kuna vitu vitahitajika"

Nilikubali kwa sababu sikuwa na ujanja. Hata hivyo nilijua kama mama yangu angejua ndio angeleta kipingamizi lakini baba yangu hakuwa na shida, hakuwa mtu wa dini sana. Nilimshauri wasimshirikishe mama kwenye hilo, kwa sababu nilijua kwanza ni lazima angepinga kwenda kwa mganga. Pili sikutaka kumuona akiyajua matatizo yangu yangemfanya asononeke sana.

Mganga aliniambia nisiondoke pale kwake maana ndio ilikuwa sehemu salama kwangu. Hadi ile damu yangu irudishwe, lakini akamwambia Vumilia aondoke kesho asubuhi ila asipite kwenye njia ya kutokea kwa mganga wakati anatoka. Yaani apite sehemu pasipo na njia rasmi, mganga alihofia kuna mitego imeachwa ni mpaka aitegue kwanza.

Itaendelea
 
Inaendelea sehemu ya sita.

Tulikuwa tumeshafika kwenye mlango wa kuingia kwa mganga. Unajua familia nyingi za usukumani zinakuwa na wigo au tuseme uzio ambao mara nyingi unakuwa wa miti fulani inaitwa minyaa au "manara" kwa kisukuma, lakini pia wigo mwingine ulikuwa wa mkonge "katani" kwa kisukuma. Na kwenye wigo huu huwa kuna sehemu ya kutokea ambao ndio kama geti la kuingilia. Sasa tulikuwa tumesimama kwenye hiyo sehemu ya kuingilia, lakini tulivyopita tu kuingia Sasa kwa mganga tukawa hatuoni chochote. Nyumba tulizokuwa tunaziona za mganga pindi tukiwa nje ya ule wigo tukawa hatuzioni, ni miti na vichaka tu ndio tukawa tunaona.

"Oooh! nini hiki" alisema Vumilia kwa sauti iliyoashiria kufadhaika na hali ile.

Nilimuangalia kwa sababu nilikosa sababu hata nimjibu nini, kwangu kila kitu kilionekana kama mazingaombwe. Baadaye aliniambia unajua mganga huyu ameweka madawa ya kuzindika eneo lake kwa hiyo sitaweza kupita, hadi nivue nguvu za kichawi nije kawaida ndio nitapita.

"Utavuaje?" Nilimuuliza

"Inabidi tuende kwa bibi"

Tulianza kutembea kwenda kwa bibi yake ambapo ilikuwa ni palepale kijijini kwetu. Sio muda mrefu tulikuwa tumeshafika. Aliingia ndani kwenye moja ya nyumba za pale kwao, akakaa kidogo halafu akarejea.

Safari hii alikuwa amevaa nguo za kawaida . Alikuwa amejifunga kitenge kiunoni na kitenge kingine amekizungusha kwa juu kifuani. Alinyoosha mkono na kunionyesha kopo, akaniambia nichote na kujipaka usoni. Nilichota kitu ambacho ni kama yalikuwa mafuta yakiwa yamechanganywa dawa, ambayo yalifanya kuwa kama mchanganyiko wa mafuta na unga unga. Yalikuwa ni mafuta yenye harufu kali ya kama kitu kilichooza lakini sikujali nilijipaka bila kujiuliza mara mbili. Aliniambia yalikuwa ni mafuta ya aina fulani ya mjusi ambaye kwa kiswahili sijui jina lake yamechanganywa na unga wa mizizi ya miti minne ambayo hakunitajia wala hakunambia matumizi yake.

"Inabidi tutembee haraka, nahisi tuko hatarini" aliongea huku uoga ukiwa dhahiri machoni mwake.

"kwa nini"

" Nahisi wanakutafuta kukuchukua na sasa wako njiani wanakuja, inabidi tufanye haraka tufike kwa mganga. Wakitukuta njiani kabla hatujafika utakuwa hatarini"

"Wamejuaje tumekuja huku" niliuliza nikionyesha mshangao kidogo.

"Wewe huyajui haya mambo, tafadhali tuwahi tuondoke"

Safari hii hatukutembea kama mwanzo isipokuwa tulikuwa tunakimbia ili tuwahi kufika. Na miongoni kati ya vitu vilivyonishangaza mwanzoni tulikuwa tunatumia muda kidogo sana kutembea umbali mrefu, lakini safari hii tulitumia muda mrefu. Haikuchukua muda mrefu toka tuanze ile safari, akaniambia wako nyuma yetu wanatufata. Wakitupata tu umekwisha. Niliogopa sana nikawa natamani hadi kupaa. Niliwaza pia vipi tukifika tena kwa mganga halafu tusipaone halafu huku nyuma tunafukuziwa.

It was probably the most terrifying moment in my life.

Muda sio mrefu nikaanza kusikia vishindo vya watu vinatufuata kwa nyuma. Wakati akili haijakaa sawa nikasikia kishindo kwa mbele yetu ni kama kitu fulani kilikuwa kimerushwa. Tokea pale tukawa tunapata ugumu sana wa kukimbia, miguu ilikuwa mizito sana au niseme ni kama kuna nguvu fulani unakuvuta kwa hiyo unapiga hatua kwa tabu sana. Tulijikongongoja hadi tulipovuka pale ambapo kile kitu kilikuwa kimedondokea. Tulipokivuka tu tukaanza kukimbia tena kwa kasi. Kufupisha story zoezi hili likawa endelevu ikawa kila tukivuka muda sio mrefu, kile kitu (ambacho kwa wakati huo bado sikukijua ni kitu gani) kinarushwa tena, tukivuka baada ya dakika chache kinarushwa tena. Lakini tukikivuka kasi yetu ya kukimbia inaongezeka, kikirushwa kasi inapungua inakuwa kama tunavutwa. Tulihangaika hivyo hadi tulipofika kwenye geti la kuingilia kwa mganga.

"rudini sasa watoto wangu mmewashindwa"

Ilikuwa ni sauti ya kiume ambaye nilikuja kumugundua ni mzee Nkelebe. Alikuwa akiwaamuru wale wachawi warudi walikotoka. Alitupokea na kutupeleka hadi kwenye mojawapo ya kijumba kilichopo pale kwake kilichojengwa kwa nyasi mwanzo mwisho.

Aliingia kwenye nyumba na kuja na viti vidogo aina ya vigoda viwili akatupatia na kutuamuru tukae.

"Unajua mwanzoni niliwaona mlivyokuja mkarudi. Wewe Vumilia ni mwenyeji hapa nilijua umekuja kwa nia njema Na lazima kuna shida hivyo nilijua lazima utarudi tu, hivyo nilikaa kukusubiri"

"Na huyu msabato umemtoa wapi, hadi akawa anakimbizana na wajanja usiku huu" aliendelea kusema huku akiniangalia Kwa unafiki fulani

Ni kama alikuwa ananikumbusha mwaka mmoja uliopita tu, nikiwa na brother mmoja mwinjilisti wa kanisani kwetu muuza vitabu vya dini ambapo nikiwa naye tuliwahi kumtembelea huyo mganga kumhubiri neno la Mungu. Nilikumbuka mwinjilisti yule aliyekuwa hamung'unyi maneno akimwambia mganga wewe unafanya kazi ya shetani utachomwa moto. Na sisi tunaofanya kazi ya Mungu tutaenda mbinguni. Sasa ilikuwaje mtoto wa Mungu anayesubiri mbingu, kwenda kutafuta msaada kwa wachomwa moto.

Ukistaajabu ya Musa, utayaona ya firauni.

"Tuachane na hayo baba huyu kijana anahitaji msaada" alisema Vumilia

"Sawa"

Mzee alisogeza maji kwenye karai dogo akaweka dawa fulani. Akamaliza akachukua kitu kama mkia wa mnyama wenye rangi nyeusi. Kama unaujua mkia wa ng'ombe kule chini huwa unakuwa kama una manyoya manyoya marefu, alichukua mkia wa hivyo sasa. Akamaliza akaanza kupiga manyanga huku akiimba nyimbo na kuongea ongea kama aliyepandwa na wazimu. Baada ya dakika kadhaa akanipa kakipande ka mti wa mnyaa na kuniambia nizungumze shida zangu bila kutoa sauti. Ni kama mtu anavyonuia kitu fulani.

Baada ya kumaliza zoezi lile alikichukua kile kipande akakiloweka kwenye yale maji. Akamaliza akakitoa kisha akaanza kukiangalia.

Akaanza kuniambia.

"Kijana una matatizo makubwa sana. Umefanya vizuri kuja hapa leo la sivyo leo ulikuwa mwisho wako. Kwanza ninaona watu wameandaa sherehe sehemu fulani kufurahia kukukaribisha huko kwenye makazi ya misukule"

"Na ninawaona hadi sasa wamekaa pale nje ya wigo wangu wanakusubiri utoke hapa"

Alisema na kuniangalia, nilikaa kimya sikuwa na la kuongea bado.

Alichukua kopo fulani akalisogeza kwenye mdomo wake, akaongea maneno fulani halafu akachukua dawa nyeusi na kunipaka usoni kisha akaniambia nitoke nje na kuangalia angani. Huku akinielekeza maneno fulani ya kutamka hadi mara tatu. Nilitoka nje huku nikiogopa nikafika nikatazama hewani na kutamka maneno aliyoniambia mara tatu. Yalikuwa maneno sio ya kiswahili wala kisukuma.

Ghafla kilijitokeza kitu cha ajabu angani, ambacho sikukitarajia. Ni kama ilitokea luninga iliyokuwa inaonyesha matukio mbali mbali. Kwa ufupi niliwaona wachawi kuanzia siku ile walivyonichukua wakanipeleka makaburini na kunichanja chale na kila kitu walichokifanya. Kilichonisikitisha zaidi niliwaona bibi yangu na mama yangu mdogo wakiwa na mwanamke mwingine ambaye naye alikuwa wa palepale kijijini. Bibi huyu alikuwa ni mmojawapo wa wake za babu yangu mzaa mama ambaye kwa wakati huo alikuwa marehemu na mama mdogo ni mtoto wa kuzaliwa na huyo bibi. Nilivyoona tu nilijua sababu ya yale yote ni nini.

Kulikuwa na mgogoro baina ya watoto wa mke wa kwanza wa babu yangu ambao ni mjomba wangu, mama mkubwa na mama yangu mzazi ambaye alikuwa ni kitinda mimba. Huyu bibi niliyemuona kwenye luninga ya mzee Nkelebe alikuwa ni mke wa pili kuolewa. Sababu ilikuwa ni mgogoro wa ardhi ambapo mke huyu alidai kuna sehemu ambayo mama yangu na mama mkubwa walichukua, ambayo ilinunuliwa yeye akiwa ndio ameolewa hivyo yeye ndiye haki nayo.

Kumbe nalogwa kisa mgogoro wa ardhi niliwaza!

Baada ya muda luninga ile ilikata matangazo nikarudi kwenye kijumba cha mganga. Kufika tu Vumilia alifungua mdomo wake na kuniambia.

"Nafikiri sasa umeanza kuniamini, mwanzoni nilipokuambia ndugu zako wanakutafuta labda hukunielewa"

Mzee Nkelebe alimtuliza Vumilia kisha akaanza kuniambia.

"Una matatizo mawili ambayo nimeyaona kwako yanayotakiwa kushughulikiwa. Tunaanza na tatizo la kwanza"

Mganga aliniangalia kisha akanambia nikunje suruali yangu. Aliliona kovu ambalo nililipata miaka mingi, siku ile nimeona wachawi nikiwa darasa la tatu. Aliniambia

"Kuna kitu uliwekewa kwenye mwili wako muda mrefu sana nimekiona unacho, tatizo lenu wafiadini hamtembeagi hadi mambo yawafike shingoni, ulitakiwa uwe umeshakiondoa muda mrefu sana" alisema mganga huku akiniangalia kwa umakini pale kwenye kovu.

"Labda nikuulize swali" alisema mganga akatulia kidogo kisha akaendelea

"hivi unadhani kwa nini siku ile unaona wachawi wakati ukiwa bado mdogo, kwa nini wewe peke yako ndio ulizisikia zile kelele za wachawi?. Na unadhani kwa nini ulipotoka nje ulifanikiwa kuwaona wachawi pasipo kutumia dawa yoyote, wakati kikawaida huwezi kuwaona wachawi bila Dawa?"

Aliniuliza lakini niliona dhahiri sikuwa na jibu kamili. Hivyo nikamwambia sijui chochote.

Akaniambia ulipokuwa mtoto ulikuwa na nguvu za asili na ukoo wenu una mizimu mikali sana. Hizo nguvu ndio zilikusaidia kuwaona na kusikia zile kelele, japo sasa hivi zimepungua na ni kawaida kupungua kadri unavyozidi kukua.

"Sasa wachawi hawakufurahishwa na wewe kuwaona, ilibidi wakufate baadae ulipokuwa umelala wakuchane mguu na kukuwekea dawa fulani iliyo kwenye kakipande kadogo ka mti"

"Kazi ya dawa hizo ni kukuzuia wewe ushindwe kusema chochote kila unaposhuhudia tukio la kichawi. Hebu niambie tokea ulivyoona tukio lile ulishawahi kumsimulia mtu kama ulitokewa na jambo kama lile"

"hapana" nilijbu kwa mshangao huku nikikumbuka jinsi moyo ulivyokuwa unakuwa mzito na kuogopa sana kila nilipotaka kumwambia mtu yeyote kuhusu tukio lile.

"Kumbe dawa zile zilikuwa zinafanya kazi" niliwaza

"Amini hata hili tukio la kuchanjwa usingeweza kumwambia yeyote. Na hautaweza kuja kumwambia yeyote kuhusu tukio la kishirikina utakalolishuhudia hadi siku unaingia kaburini, kama tusipoitoa hiyo dawa mwilini mwako" alisema mganga

"Hata baba yako najua usingemwambia, najua ungepata nia ya kumwambia lakini usingethubutu, hivyo watu wasingejua shida yako na usingepata msaada"

Baada ya kumaliza alichukua wembe na kunichana kidogo kwenye kovu.Alipaka dawa kisha akachomoa kipande cha mti kidogo kama vimisumari vile vidogo.

" Sasa uko huru kuongea. Tunaenda kwenye tatizo la pili".alisema kisha akaendelea

"Hili nadhani umejionea mwenyewe, wachawi tayari wana mamlaka juu ya mwili wako maana wameshamaliza maagano na mizimu ya kwenu, kwa tambiko lililofanyika makaburini. Kazi iliyobaki ni kukuchukua. Sasa ili tukurudishe kuna damu yako waliichukua wakati wanafanya tambiko inabidi tuirudishe kwanza" alitulia kidogo kisha akaendelea

"damu hiyo mwanzoni ilikuwa imefichwa kwenye dari la nyumba ya kwa bibi yako. Ila baada ya kujua umeshaanza kutembea kwa waganga kuna sehemu imepelekwa kufichwa pa siri zaidi ambayo mimi kwa uwezo wangu siwezi kuichukua huko. Inabidi nikupeleke kwa mganga ambaye naamini yeye anaweza kukusaidia. Ila ni mpaka nimtaarifu kwanza baba yako kwanza ajue kila kitu. Maana kuna vitu vitahitajika"

Nilikubali kwa sababu sikuwa na ujanja. Hata hivyo nilijua kama mama yangu angejua ndio angeleta kipingamizi lakini baba yangu hakuwa na shida, hakuwa mtu wa dini sana. Nilimshauri wasimshirikishe mama kwenye hilo, kwa sababu nilijua kwanza ni lazima angepinga kwenda kwa mganga. Pili sikutaka kumuona akiyajua matatizo yangu yangemfanya asononeke sana.

Mganga aliniambia nisiondoke pale kwake maana ndio ilikuwa sehemu salama kwangu. Hadi ile damu yangu irudishwe, lakini akamwambia Vumilia aondoke kesho asubuhi ila asipite kwenye njia ya kutokea kwa mganga wakati anatoka. Yaani apite sehemu pasipo na njia rasmi, mganga alihofia kuna mitego imeachwa ni mpaka aitegue kwanza.

Itaendelea
Leo jumapili achia za kutosha
 
Ushauri Bora kabisa , mleta Uzi chukua hii
Sidhani kama unaweza kuandika story nzima kwa note book, note book ina limitation ya maneno kwa idadi fulani.

Changamoto nyingine ni jinsi ya kucopy na kuja kupaste huku. Nilishajaribu kudownload app ya microsoft word unaandika vizuri lakini kuicopy kuitoa huko na kuipaste huku ndio changamoto.

Ningekuwa na computer ndio rahisi.
 
Inaendelea sehemu ya sita.

Tulikuwa tumeshafika kwenye mlango wa kuingia kwa mganga. Unajua familia nyingi za usukumani zinakuwa na wigo au tuseme uzio ambao mara nyingi unakuwa wa miti fulani inaitwa minyaa au "manara" kwa kisukuma, lakini pia wigo mwingine ulikuwa wa mkonge "katani" kwa kisukuma. Na kwenye wigo huu huwa kuna sehemu ya kutokea ambao ndio kama geti la kuingilia. Sasa tulikuwa tumesimama kwenye hiyo sehemu ya kuingilia, lakini tulivyopita tu kuingia Sasa kwa mganga tukawa hatuoni chochote. Nyumba tulizokuwa tunaziona za mganga pindi tukiwa nje ya ule wigo tukawa hatuzioni, ni miti na vichaka tu ndio tukawa tunaona.

"Oooh! nini hiki" alisema Vumilia kwa sauti iliyoashiria kufadhaika na hali ile.

Nilimuangalia kwa sababu nilikosa sababu hata nimjibu nini, kwangu kila kitu kilionekana kama mazingaombwe. Baadaye aliniambia unajua mganga huyu ameweka madawa ya kuzindika eneo lake kwa hiyo sitaweza kupita, hadi nivue nguvu za kichawi nije kawaida ndio nitapita.

"Utavuaje?" Nilimuuliza

"Inabidi tuende kwa bibi"

Tulianza kutembea kwenda kwa bibi yake ambapo ilikuwa ni palepale kijijini kwetu. Sio muda mrefu tulikuwa tumeshafika. Aliingia ndani kwenye moja ya nyumba za pale kwao, akakaa kidogo halafu akarejea.

Safari hii alikuwa amevaa nguo za kawaida . Alikuwa amejifunga kitenge kiunoni na kitenge kingine amekizungusha kwa juu kifuani. Alinyoosha mkono na kunionyesha kopo, akaniambia nichote na kujipaka usoni. Nilichota kitu ambacho ni kama yalikuwa mafuta yakiwa yamechanganywa dawa, ambayo yalifanya kuwa kama mchanganyiko wa mafuta na unga unga. Yalikuwa ni mafuta yenye harufu kali ya kama kitu kilichooza lakini sikujali nilijipaka bila kujiuliza mara mbili. Aliniambia yalikuwa ni mafuta ya aina fulani ya mjusi ambaye kwa kiswahili sijui jina lake yamechanganywa na unga wa mizizi ya miti minne ambayo hakunitajia wala hakunambia matumizi yake.

"Inabidi tutembee haraka, nahisi tuko hatarini" aliongea huku uoga ukiwa dhahiri machoni mwake.

"kwa nini"

" Nahisi wanakutafuta kukuchukua na sasa wako njiani wanakuja, inabidi tufanye haraka tufike kwa mganga. Wakitukuta njiani kabla hatujafika utakuwa hatarini"

"Wamejuaje tumekuja huku" niliuliza nikionyesha mshangao kidogo.

"Wewe huyajui haya mambo, tafadhali tuwahi tuondoke"

Safari hii hatukutembea kama mwanzo isipokuwa tulikuwa tunakimbia ili tuwahi kufika. Na miongoni kati ya vitu vilivyonishangaza mwanzoni tulikuwa tunatumia muda kidogo sana kutembea umbali mrefu, lakini safari hii tulitumia muda mrefu. Haikuchukua muda mrefu toka tuanze ile safari, akaniambia wako nyuma yetu wanatufata. Wakitupata tu umekwisha. Niliogopa sana nikawa natamani hadi kupaa. Niliwaza pia vipi tukifika tena kwa mganga halafu tusipaone halafu huku nyuma tunafukuziwa.

It was probably the most terrifying moment in my life.

Muda sio mrefu nikaanza kusikia vishindo vya watu vinatufuata kwa nyuma. Wakati akili haijakaa sawa nikasikia kishindo kwa mbele yetu ni kama kitu fulani kilikuwa kimerushwa. Tokea pale tukawa tunapata ugumu sana wa kukimbia, miguu ilikuwa mizito sana au niseme ni kama kuna nguvu fulani unakuvuta kwa hiyo unapiga hatua kwa tabu sana. Tulijikongongoja hadi tulipovuka pale ambapo kile kitu kilikuwa kimedondokea. Tulipokivuka tu tukaanza kukimbia tena kwa kasi. Kufupisha story zoezi hili likawa endelevu ikawa kila tukivuka muda sio mrefu, kile kitu (ambacho kwa wakati huo bado sikukijua ni kitu gani) kinarushwa tena, tukivuka baada ya dakika chache kinarushwa tena. Lakini tukikivuka kasi yetu ya kukimbia inaongezeka, kikirushwa kasi inapungua inakuwa kama tunavutwa. Tulihangaika hivyo hadi tulipofika kwenye geti la kuingilia kwa mganga.

"rudini sasa watoto wangu mmewashindwa"

Ilikuwa ni sauti ya kiume ambaye nilikuja kumugundua ni mzee Nkelebe. Alikuwa akiwaamuru wale wachawi warudi walikotoka. Alitupokea na kutupeleka hadi kwenye mojawapo ya kijumba kilichopo pale kwake kilichojengwa kwa nyasi mwanzo mwisho.

Aliingia kwenye nyumba na kuja na viti vidogo aina ya vigoda viwili akatupatia na kutuamuru tukae.

"Unajua mwanzoni niliwaona mlivyokuja mkarudi. Wewe Vumilia ni mwenyeji hapa nilijua umekuja kwa nia njema Na lazima kuna shida hivyo nilijua lazima utarudi tu, hivyo nilikaa kukusubiri"

"Na huyu msabato umemtoa wapi, hadi akawa anakimbizana na wajanja usiku huu" aliendelea kusema huku akiniangalia Kwa unafiki fulani

Ni kama alikuwa ananikumbusha mwaka mmoja uliopita tu, nikiwa na brother mmoja mwinjilisti wa kanisani kwetu muuza vitabu vya dini ambapo nikiwa naye tuliwahi kumtembelea huyo mganga kumhubiri neno la Mungu. Nilikumbuka mwinjilisti yule aliyekuwa hamung'unyi maneno akimwambia mganga wewe unafanya kazi ya shetani utachomwa moto. Na sisi tunaofanya kazi ya Mungu tutaenda mbinguni. Sasa ilikuwaje mtoto wa Mungu anayesubiri mbingu, kwenda kutafuta msaada kwa wachomwa moto.

Ukistaajabu ya Musa, utayaona ya firauni.

"Tuachane na hayo baba huyu kijana anahitaji msaada" alisema Vumilia

"Sawa"

Mzee alisogeza maji kwenye karai dogo akaweka dawa fulani. Akamaliza akachukua kitu kama mkia wa mnyama wenye rangi nyeusi. Kama unaujua mkia wa ng'ombe kule chini huwa unakuwa kama una manyoya manyoya marefu, alichukua mkia wa hivyo sasa. Akamaliza akaanza kupiga manyanga huku akiimba nyimbo na kuongea ongea kama aliyepandwa na wazimu. Baada ya dakika kadhaa akanipa kakipande ka mti wa mnyaa na kuniambia nizungumze shida zangu bila kutoa sauti. Ni kama mtu anavyonuia kitu fulani.

Baada ya kumaliza zoezi lile alikichukua kile kipande akakiloweka kwenye yale maji. Akamaliza akakitoa kisha akaanza kukiangalia.

Akaanza kuniambia.

"Kijana una matatizo makubwa sana. Umefanya vizuri kuja hapa leo la sivyo leo ulikuwa mwisho wako. Kwanza ninaona watu wameandaa sherehe sehemu fulani kufurahia kukukaribisha huko kwenye makazi ya misukule"

"Na ninawaona hadi sasa wamekaa pale nje ya wigo wangu wanakusubiri utoke hapa"

Alisema na kuniangalia, nilikaa kimya sikuwa na la kuongea bado.

Alichukua kopo fulani akalisogeza kwenye mdomo wake, akaongea maneno fulani halafu akachukua dawa nyeusi na kunipaka usoni kisha akaniambia nitoke nje na kuangalia angani. Huku akinielekeza maneno fulani ya kutamka hadi mara tatu. Nilitoka nje huku nikiogopa nikafika nikatazama hewani na kutamka maneno aliyoniambia mara tatu. Yalikuwa maneno sio ya kiswahili wala kisukuma.

Ghafla kilijitokeza kitu cha ajabu angani, ambacho sikukitarajia. Ni kama ilitokea luninga iliyokuwa inaonyesha matukio mbali mbali. Kwa ufupi niliwaona wachawi kuanzia siku ile walivyonichukua wakanipeleka makaburini na kunichanja chale na kila kitu walichokifanya. Kilichonisikitisha zaidi niliwaona bibi yangu na mama yangu mdogo wakiwa na mwanamke mwingine ambaye naye alikuwa wa palepale kijijini. Bibi huyu alikuwa ni mmojawapo wa wake za babu yangu mzaa mama ambaye kwa wakati huo alikuwa marehemu na mama mdogo ni mtoto wa kuzaliwa na huyo bibi. Nilivyoona tu nilijua sababu ya yale yote ni nini.

Kulikuwa na mgogoro baina ya watoto wa mke wa kwanza wa babu yangu ambao ni mjomba wangu, mama mkubwa na mama yangu mzazi ambaye alikuwa ni kitinda mimba. Huyu bibi niliyemuona kwenye luninga ya mzee Nkelebe alikuwa ni mke wa pili kuolewa. Sababu ilikuwa ni mgogoro wa ardhi ambapo mke huyu alidai kuna sehemu ambayo mama yangu na mama mkubwa walichukua, ambayo ilinunuliwa yeye akiwa ndio ameolewa hivyo yeye ndiye haki nayo.

Kumbe nalogwa kisa mgogoro wa ardhi niliwaza!

Baada ya muda luninga ile ilikata matangazo nikarudi kwenye kijumba cha mganga. Kufika tu Vumilia alifungua mdomo wake na kuniambia.

"Nafikiri sasa umeanza kuniamini, mwanzoni nilipokuambia ndugu zako wanakutafuta labda hukunielewa"

Mzee Nkelebe alimtuliza Vumilia kisha akaanza kuniambia.

"Una matatizo mawili ambayo nimeyaona kwako yanayotakiwa kushughulikiwa. Tunaanza na tatizo la kwanza"

Mganga aliniangalia kisha akanambia nikunje suruali yangu. Aliliona kovu ambalo nililipata miaka mingi, siku ile nimeona wachawi nikiwa darasa la tatu. Aliniambia

"Kuna kitu uliwekewa kwenye mwili wako muda mrefu sana nimekiona unacho, tatizo lenu wafiadini hamtembeagi hadi mambo yawafike shingoni, ulitakiwa uwe umeshakiondoa muda mrefu sana" alisema mganga huku akiniangalia kwa umakini pale kwenye kovu.

"Labda nikuulize swali" alisema mganga akatulia kidogo kisha akaendelea

"hivi unadhani kwa nini siku ile unaona wachawi wakati ukiwa bado mdogo, kwa nini wewe peke yako ndio ulizisikia zile kelele za wachawi?. Na unadhani kwa nini ulipotoka nje ulifanikiwa kuwaona wachawi pasipo kutumia dawa yoyote, wakati kikawaida huwezi kuwaona wachawi bila Dawa?"

Aliniuliza lakini niliona dhahiri sikuwa na jibu kamili. Hivyo nikamwambia sijui chochote.

Akaniambia ulipokuwa mtoto ulikuwa na nguvu za asili na ukoo wenu una mizimu mikali sana. Hizo nguvu ndio zilikusaidia kuwaona na kusikia zile kelele, japo sasa hivi zimepungua na ni kawaida kupungua kadri unavyozidi kukua.

"Sasa wachawi hawakufurahishwa na wewe kuwaona, ilibidi wakufate baadae ulipokuwa umelala wakuchane mguu na kukuwekea dawa fulani iliyo kwenye kakipande kadogo ka mti"

"Kazi ya dawa hizo ni kukuzuia wewe ushindwe kusema chochote kila unaposhuhudia tukio la kichawi. Hebu niambie tokea ulivyoona tukio lile ulishawahi kumsimulia mtu kama ulitokewa na jambo kama lile"

"hapana" nilijbu kwa mshangao huku nikikumbuka jinsi moyo ulivyokuwa unakuwa mzito na kuogopa sana kila nilipotaka kumwambia mtu yeyote kuhusu tukio lile.

"Kumbe dawa zile zilikuwa zinafanya kazi" niliwaza

"Amini hata hili tukio la kuchanjwa usingeweza kumwambia yeyote. Na hautaweza kuja kumwambia yeyote kuhusu tukio la kishirikina utakalolishuhudia hadi siku unaingia kaburini, kama tusipoitoa hiyo dawa mwilini mwako" alisema mganga

"Hata baba yako najua usingemwambia, najua ungepata nia ya kumwambia lakini usingethubutu, hivyo watu wasingejua shida yako na usingepata msaada"

Baada ya kumaliza alichukua wembe na kunichana kidogo kwenye kovu.Alipaka dawa kisha akachomoa kipande cha mti kidogo kama vimisumari vile vidogo.

" Sasa uko huru kuongea. Tunaenda kwenye tatizo la pili".alisema kisha akaendelea

"Hili nadhani umejionea mwenyewe, wachawi tayari wana mamlaka juu ya mwili wako maana wameshamaliza maagano na mizimu ya kwenu, kwa tambiko lililofanyika makaburini. Kazi iliyobaki ni kukuchukua. Sasa ili tukurudishe kuna damu yako waliichukua wakati wanafanya tambiko inabidi tuirudishe kwanza" alitulia kidogo kisha akaendelea

"damu hiyo mwanzoni ilikuwa imefichwa kwenye dari la nyumba ya kwa bibi yako. Ila baada ya kujua umeshaanza kutembea kwa waganga kuna sehemu imepelekwa kufichwa pa siri zaidi ambayo mimi kwa uwezo wangu siwezi kuichukua huko. Inabidi nikupeleke kwa mganga ambaye naamini yeye anaweza kukusaidia. Ila ni mpaka nimtaarifu kwanza baba yako kwanza ajue kila kitu. Maana kuna vitu vitahitajika"

Nilikubali kwa sababu sikuwa na ujanja. Hata hivyo nilijua kama mama yangu angejua ndio angeleta kipingamizi lakini baba yangu hakuwa na shida, hakuwa mtu wa dini sana. Nilimshauri wasimshirikishe mama kwenye hilo, kwa sababu nilijua kwanza ni lazima angepinga kwenda kwa mganga. Pili sikutaka kumuona akiyajua matatizo yangu yangemfanya asononeke sana.

Mganga aliniambia nisiondoke pale kwake maana ndio ilikuwa sehemu salama kwangu. Hadi ile damu yangu irudishwe, lakini akamwambia Vumilia aondoke kesho asubuhi ila asipite kwenye njia ya kutokea kwa mganga wakati anatoka. Yaani apite sehemu pasipo na njia rasmi, mganga alihofia kuna mitego imeachwa ni mpaka aitegue kwanza.

Itaendelea
Simiyu hatari
 
Inaendelea! Sehemu ya 2

Niliendelea na ratiba zingine za shule kama kawaida. Ilipofika mchana saa sita nilirudi nyumbani kupata chakula cha mchana, kisha nikarudi tena shule kwa ajili ya vipindi vya jioni. Wakati wa kutawanyishwa jioni ulipofika nilirudi nyumbani kama kawaida, nilienda moja kwa moja hadi chumbani nikabadilisha nguo kisha nikatoka kwa ajili ya kwenda kucheza mpira. Wakati nikiwa ninatoka nilikutana na mtoto wa mama mdogo ambaye tulikuwa tunaishi nae pale nyumbani akanambia.

"Babu anakuita kule" alisema huku akinionyesha kwenye nyumba ya nyasi ambayo ilikuwa nyuma ya nyumba kubwa. Nilienda moja kwa moja hadi ndani ya nyumba. Nilivyoingia nilikuta ndani kulikuwa na watu watatu. Kulikuwa na Babu, mjomba Elias (yule aliyechanjwa chale usiku uliopita na mzee mmoja aliyekuwa amevaa kibagarashia ambaye sikumtambua. Niliwasalimia, nikamaliza nikauliza " Babu Elikana ameniambia unaniita" Babu aliniambia kaa hapo chini. Nilikaa chini nikatega sikio kuwasikiliza.

Kumbe yule mzee mwenye kibagarashia alikuwa ni mganga wa kienyeji. Baada ya mjomba kuchanjwa chale Babu alimpeleka kwa mganga kuangaliwa kama kutakuwa na shida yoyote. Kule kwa mganga waliaguliwa, halafu yule mganga akawaaambia Babu na mjomba nimeona kuna mtoto hapo kwako wachawi walimfanyia jambo jana. Sasa hilo jambo ambalo mganga aliwaambia nimefanyiwa ndio ilikuwa sababu ya mimi kuitwa pale.Babu aliniangalia machoni halafu kwa sauti ya upole sana akaniuliza

"mwanangu naomba utuambie ukweli jana usiku uliona nini" . Hii haikuwa kawaida ya Babu kumuona akiwa anaongea kwa upole kiasi kile. Licha ya kwamba alikuwa ni mtu mwenye upendo na watoto, wajukuu na ndugu wengine lakini Babu pia alikuwa ni mtata sana. Jambo la kukaripia na kuchapa viboko ilikuwa kama mlevi kugugumia chupa ya konyagi, hakujiuliza mara mbili. Alikuwa ni mkali asiyependa masihara hata kidogo, mpaka alikuwa amebatizwa jina akawa anaitwa "serikali" kwa lafudhi ya kisukuma "serekale". Hivyo aliponiuliza hivyo nilijua hilo ni ombi kwa mara ya kwanza tu, lakini nisipotoa majibu anayoyataka kinachofuata ni mkong'oto. Nilijiandaa kujibu lile swali aliloniuliza lakini moyo uliogopa sana mapigo ya moyo yakawa yanaenda kwa kasi.

Hali hii ilinishangaza kidogo kwani ni mara ya pili sasa kila nikitaka kuongelea hilo jambo, nakuwa naogopa sana. Nilitamani kujibu lakini uoga ulinizidi nikabaki kutoa macho na kujiumauma mdomo.

"Mr the dragon hebu nijibu mwanangu kuna kitu chochote uliona jana" aliuliza tena babu.

Nilitaka kukubali lakini bado nafsi yangu iliogopa na kugoma kabisa, hadi nikaanza kutetemeka kwa hofu. Nilishindwa hata kukubali angalau kwa kutikisa kichwa. Mganga yule alinikodolea macho kama ananichunguza kwa makini, halafu akasema.

"Mzee Manumbu nafikiri wewe mwenyewe umeona, nilikwambia huyu hawezi akasema lolote hata umwekee bunduki, si unaona anavyotetemeka, Kuna kitu amefanyiwa huyu" aliniangalia kidogo kisha akaendelea

"Nafikiri cha msingi tuharakishe twende nae kwangu, tukalifanyie utaratibu hili jambo kabla mambo hayajawa mabaya".

Baada ya pale niliamriwa niondoke pale niende nikamuite mama yangu. Niliondoka nikaenda hadi kwenye nyumba nyingine yenye jiko ambapo pembeni yake kuna mti wa "mhare" na ndio sehemu wanawake walipendelea kukaa. Nilimkuta mama amekaa nikampa maelekezo kwamba anaitwa kisha nikaondoka zangu kwenda kucheza. Kuna muda nilikuwa napata wasiwasi lakini kuna muda pia niliona kawaida tu. Nadhani ni kwa sababu ya akili zile za kitoto. Mpira tulikuwa tunacheza barabarani umbali kama wa mita miamoja na hamsini kutoka nyumbani. Baadae nilikuja kuitwa niende nyumbani mama ananiita.

Nilikimbia kwenda nyumbani kumsikiliza mama. Nilikuwa nimeshapata hisia ananiita juu ya suala hilohilo. Nilipofika swali la kwanza kuulizwa lilikuwa

"eti mwanangu jana usiku kuna kitu uliona" . Nilitaka kujibu lakini nilipatwa na hofu nikaishia tu kujibu "sijaona chochote mama". Mama aliniangalia kwa huruma kisha akasema

"Eti babu yako analazimisha uende kwa mganga ukaangaliwe" sikujibu chochote nilikaa kimya tu. Kiukweli nafsi ilikuwa inaniuma sana kwa kumficha ukweli mama yangu. Lakini ningefanya nini wakati kila nikitaka kuongea moyo unaingiwa baridi kama la Antarctica. Najua mtu mwingine anaweza ajiulize hofu tu ndio ilifanya ushindwe kuongea, mimi mhusika ndio najua jinsi nilivyokuwa najisikia.

"Hebu twende huku" aliniambia mama huku akinivuta kuelekea kwenye nyumba kubwa. Tulienda moja kwa moja hadi ndani ya chumba alichokuwa analala mama yangu. Tulipofika mama akaniambia

"Hata nisipokuwepo, babu yako akikwambia muende kwa mganga ukatae kabisa, jifunze kumtegemea Mungu kwenye maisha yako"

Nilishangazwa kidogo na kauli ile ya mama, maana kwa jinsi babu alivyokuwa mtata sidhani kama ningeweza kumgomea endapo angeamua jambo lake. Nilijua hata mimi hajanichukua kwa lazima kwenda kwa mganga kwa sababu ya babu alimpenda sana mama yangu hivyo hakutaka kulazimisha. Mama yangu alikuwa ni kipenzi cha babu yangu inawezekana kuliko watoto wote wa huyo mzee. Hili jambo hata watoto wengine walikuwa wanalijua. Inawezekana kwa sababu mama yangu alikuwa ni kitindamimba wa mke wake wa kwanza kuoa, ambaye alifariki akamwacha mama yangu bado ananyonya.

Lakini kuhusu suala la kumtegemea Mungu sikushangazwa sana na hilo, pamoja na akili yangu ya kitoto lakini nilitegemea hilo kutoka kwa mama yangu. Kwa sababu mama yangu alikuwa ni mtu wa dini msabato aliyeishika imani haswa. Sio wale wasabato wa kusubili jumamosi ndio wavae suruali nyeusi, shati jeupe na tai nyeusi huku wakikung'uta biblia iliyojaa vumbi ndio waende kanisani. Yeye kusali na kusoma neno ilikuwa ni jadi yake. Baada ya hapo aliniambia nifumbe macho akapiga ombi moja refu la uchungu sana lililoishia na sala ya bwana. Kisha akasema kauli moja tu

"MUNGU ATATENDA"

Itaendelea kesho mida kama hii

NB: huu ulikuwa ni utangulizi tu kesho ndio tutalianza sakata lenyewe. Kuanzia nilivyolazimishwa kuwa kwenye mahusiano na mchawi hadi alivyoniroga.

Usiku mwema.

Sawa
 
Inaendelea sehemu ya sita.

Tulikuwa tumeshafika kwenye mlango wa kuingia kwa mganga. Unajua familia nyingi za usukumani zinakuwa na wigo au tuseme uzio ambao mara nyingi unakuwa wa miti fulani inaitwa minyaa au "manara" kwa kisukuma, lakini pia wigo mwingine ulikuwa wa mkonge "katani" kwa kisukuma. Na kwenye wigo huu huwa kuna sehemu ya kutokea ambao ndio kama geti la kuingilia. Sasa tulikuwa tumesimama kwenye hiyo sehemu ya kuingilia, lakini tulivyopita tu kuingia Sasa kwa mganga tukawa hatuoni chochote. Nyumba tulizokuwa tunaziona za mganga pindi tukiwa nje ya ule wigo tukawa hatuzioni, ni miti na vichaka tu ndio tukawa tunaona.

"Oooh! nini hiki" alisema Vumilia kwa sauti iliyoashiria kufadhaika na hali ile.

Nilimuangalia kwa sababu nilikosa sababu hata nimjibu nini, kwangu kila kitu kilionekana kama mazingaombwe. Baadaye aliniambia unajua mganga huyu ameweka madawa ya kuzindika eneo lake kwa hiyo sitaweza kupita, hadi nivue nguvu za kichawi nije kawaida ndio nitapita.

"Utavuaje?" Nilimuuliza

"Inabidi tuende kwa bibi"

Tulianza kutembea kwenda kwa bibi yake ambapo ilikuwa ni palepale kijijini kwetu. Sio muda mrefu tulikuwa tumeshafika. Aliingia ndani kwenye moja ya nyumba za pale kwao, akakaa kidogo halafu akarejea.

Safari hii alikuwa amevaa nguo za kawaida . Alikuwa amejifunga kitenge kiunoni na kitenge kingine amekizungusha kwa juu kifuani. Alinyoosha mkono na kunionyesha kopo, akaniambia nichote na kujipaka usoni. Nilichota kitu ambacho ni kama yalikuwa mafuta yakiwa yamechanganywa dawa, ambayo yalifanya kuwa kama mchanganyiko wa mafuta na unga unga. Yalikuwa ni mafuta yenye harufu kali ya kama kitu kilichooza lakini sikujali nilijipaka bila kujiuliza mara mbili. Aliniambia yalikuwa ni mafuta ya aina fulani ya mjusi ambaye kwa kiswahili sijui jina lake yamechanganywa na unga wa mizizi ya miti minne ambayo hakunitajia wala hakunambia matumizi yake.

"Inabidi tutembee haraka, nahisi tuko hatarini" aliongea huku uoga ukiwa dhahiri machoni mwake.

"kwa nini"

" Nahisi wanakutafuta kukuchukua na sasa wako njiani wanakuja, inabidi tufanye haraka tufike kwa mganga. Wakitukuta njiani kabla hatujafika utakuwa hatarini"

"Wamejuaje tumekuja huku" niliuliza nikionyesha mshangao kidogo.

"Wewe huyajui haya mambo, tafadhali tuwahi tuondoke"

Safari hii hatukutembea kama mwanzo isipokuwa tulikuwa tunakimbia ili tuwahi kufika. Na miongoni kati ya vitu vilivyonishangaza mwanzoni tulikuwa tunatumia muda kidogo sana kutembea umbali mrefu, lakini safari hii tulitumia muda mrefu. Haikuchukua muda mrefu toka tuanze ile safari, akaniambia wako nyuma yetu wanatufata. Wakitupata tu umekwisha. Niliogopa sana nikawa natamani hadi kupaa. Niliwaza pia vipi tukifika tena kwa mganga halafu tusipaone halafu huku nyuma tunafukuziwa.

It was probably the most terrifying moment in my life.

Muda sio mrefu nikaanza kusikia vishindo vya watu vinatufuata kwa nyuma. Wakati akili haijakaa sawa nikasikia kishindo kwa mbele yetu ni kama kitu fulani kilikuwa kimerushwa. Tokea pale tukawa tunapata ugumu sana wa kukimbia, miguu ilikuwa mizito sana au niseme ni kama kuna nguvu fulani unakuvuta kwa hiyo unapiga hatua kwa tabu sana. Tulijikongongoja hadi tulipovuka pale ambapo kile kitu kilikuwa kimedondokea. Tulipokivuka tu tukaanza kukimbia tena kwa kasi. Kufupisha story zoezi hili likawa endelevu ikawa kila tukivuka muda sio mrefu, kile kitu (ambacho kwa wakati huo bado sikukijua ni kitu gani) kinarushwa tena, tukivuka baada ya dakika chache kinarushwa tena. Lakini tukikivuka kasi yetu ya kukimbia inaongezeka, kikirushwa kasi inapungua inakuwa kama tunavutwa. Tulihangaika hivyo hadi tulipofika kwenye geti la kuingilia kwa mganga.

"rudini sasa watoto wangu mmewashindwa"

Ilikuwa ni sauti ya kiume ambaye nilikuja kumugundua ni mzee Nkelebe. Alikuwa akiwaamuru wale wachawi warudi walikotoka. Alitupokea na kutupeleka hadi kwenye mojawapo ya kijumba kilichopo pale kwake kilichojengwa kwa nyasi mwanzo mwisho.

Aliingia kwenye nyumba na kuja na viti vidogo aina ya vigoda viwili akatupatia na kutuamuru tukae.

"Unajua mwanzoni niliwaona mlivyokuja mkarudi. Wewe Vumilia ni mwenyeji hapa nilijua umekuja kwa nia njema Na lazima kuna shida hivyo nilijua lazima utarudi tu, hivyo nilikaa kukusubiri"

"Na huyu msabato umemtoa wapi, hadi akawa anakimbizana na wajanja usiku huu" aliendelea kusema huku akiniangalia Kwa unafiki fulani

Ni kama alikuwa ananikumbusha mwaka mmoja uliopita tu, nikiwa na brother mmoja mwinjilisti wa kanisani kwetu muuza vitabu vya dini ambapo nikiwa naye tuliwahi kumtembelea huyo mganga kumhubiri neno la Mungu. Nilikumbuka mwinjilisti yule aliyekuwa hamung'unyi maneno akimwambia mganga wewe unafanya kazi ya shetani utachomwa moto. Na sisi tunaofanya kazi ya Mungu tutaenda mbinguni. Sasa ilikuwaje mtoto wa Mungu anayesubiri mbingu, kwenda kutafuta msaada kwa wachomwa moto.

Ukistaajabu ya Musa, utayaona ya firauni.

"Tuachane na hayo baba huyu kijana anahitaji msaada" alisema Vumilia

"Sawa"

Mzee alisogeza maji kwenye karai dogo akaweka dawa fulani. Akamaliza akachukua kitu kama mkia wa mnyama wenye rangi nyeusi. Kama unaujua mkia wa ng'ombe kule chini huwa unakuwa kama una manyoya manyoya marefu, alichukua mkia wa hivyo sasa. Akamaliza akaanza kupiga manyanga huku akiimba nyimbo na kuongea ongea kama aliyepandwa na wazimu. Baada ya dakika kadhaa akanipa kakipande ka mti wa mnyaa na kuniambia nizungumze shida zangu bila kutoa sauti. Ni kama mtu anavyonuia kitu fulani.

Baada ya kumaliza zoezi lile alikichukua kile kipande akakiloweka kwenye yale maji. Akamaliza akakitoa kisha akaanza kukiangalia.

Akaanza kuniambia.

"Kijana una matatizo makubwa sana. Umefanya vizuri kuja hapa leo la sivyo leo ulikuwa mwisho wako. Kwanza ninaona watu wameandaa sherehe sehemu fulani kufurahia kukukaribisha huko kwenye makazi ya misukule"

"Na ninawaona hadi sasa wamekaa pale nje ya wigo wangu wanakusubiri utoke hapa"

Alisema na kuniangalia, nilikaa kimya sikuwa na la kuongea bado.

Alichukua kopo fulani akalisogeza kwenye mdomo wake, akaongea maneno fulani halafu akachukua dawa nyeusi na kunipaka usoni kisha akaniambia nitoke nje na kuangalia angani. Huku akinielekeza maneno fulani ya kutamka hadi mara tatu. Nilitoka nje huku nikiogopa nikafika nikatazama hewani na kutamka maneno aliyoniambia mara tatu. Yalikuwa maneno sio ya kiswahili wala kisukuma.

Ghafla kilijitokeza kitu cha ajabu angani, ambacho sikukitarajia. Ni kama ilitokea luninga iliyokuwa inaonyesha matukio mbali mbali. Kwa ufupi niliwaona wachawi kuanzia siku ile walivyonichukua wakanipeleka makaburini na kunichanja chale na kila kitu walichokifanya. Kilichonisikitisha zaidi niliwaona bibi yangu na mama yangu mdogo wakiwa na mwanamke mwingine ambaye naye alikuwa wa palepale kijijini. Bibi huyu alikuwa ni mmojawapo wa wake za babu yangu mzaa mama ambaye kwa wakati huo alikuwa marehemu na mama mdogo ni mtoto wa kuzaliwa na huyo bibi. Nilivyoona tu nilijua sababu ya yale yote ni nini.

Kulikuwa na mgogoro baina ya watoto wa mke wa kwanza wa babu yangu ambao ni mjomba wangu, mama mkubwa na mama yangu mzazi ambaye alikuwa ni kitinda mimba. Huyu bibi niliyemuona kwenye luninga ya mzee Nkelebe alikuwa ni mke wa pili kuolewa. Sababu ilikuwa ni mgogoro wa ardhi ambapo mke huyu alidai kuna sehemu ambayo mama yangu na mama mkubwa walichukua, ambayo ilinunuliwa yeye akiwa ndio ameolewa hivyo yeye ndiye haki nayo.

Kumbe nalogwa kisa mgogoro wa ardhi niliwaza!

Baada ya muda luninga ile ilikata matangazo nikarudi kwenye kijumba cha mganga. Kufika tu Vumilia alifungua mdomo wake na kuniambia.

"Nafikiri sasa umeanza kuniamini, mwanzoni nilipokuambia ndugu zako wanakutafuta labda hukunielewa"

Mzee Nkelebe alimtuliza Vumilia kisha akaanza kuniambia.

"Una matatizo mawili ambayo nimeyaona kwako yanayotakiwa kushughulikiwa. Tunaanza na tatizo la kwanza"

Mganga aliniangalia kisha akanambia nikunje suruali yangu. Aliliona kovu ambalo nililipata miaka mingi, siku ile nimeona wachawi nikiwa darasa la tatu. Aliniambia

"Kuna kitu uliwekewa kwenye mwili wako muda mrefu sana nimekiona unacho, tatizo lenu wafiadini hamtembeagi hadi mambo yawafike shingoni, ulitakiwa uwe umeshakiondoa muda mrefu sana" alisema mganga huku akiniangalia kwa umakini pale kwenye kovu.

"Labda nikuulize swali" alisema mganga akatulia kidogo kisha akaendelea

"hivi unadhani kwa nini siku ile unaona wachawi wakati ukiwa bado mdogo, kwa nini wewe peke yako ndio ulizisikia zile kelele za wachawi?. Na unadhani kwa nini ulipotoka nje ulifanikiwa kuwaona wachawi pasipo kutumia dawa yoyote, wakati kikawaida huwezi kuwaona wachawi bila Dawa?"

Aliniuliza lakini niliona dhahiri sikuwa na jibu kamili. Hivyo nikamwambia sijui chochote.

Akaniambia ulipokuwa mtoto ulikuwa na nguvu za asili na ukoo wenu una mizimu mikali sana. Hizo nguvu ndio zilikusaidia kuwaona na kusikia zile kelele, japo sasa hivi zimepungua na ni kawaida kupungua kadri unavyozidi kukua.

"Sasa wachawi hawakufurahishwa na wewe kuwaona, ilibidi wakufate baadae ulipokuwa umelala wakuchane mguu na kukuwekea dawa fulani iliyo kwenye kakipande kadogo ka mti"

"Kazi ya dawa hizo ni kukuzuia wewe ushindwe kusema chochote kila unaposhuhudia tukio la kichawi. Hebu niambie tokea ulivyoona tukio lile ulishawahi kumsimulia mtu kama ulitokewa na jambo kama lile"

"hapana" nilijbu kwa mshangao huku nikikumbuka jinsi moyo ulivyokuwa unakuwa mzito na kuogopa sana kila nilipotaka kumwambia mtu yeyote kuhusu tukio lile.

"Kumbe dawa zile zilikuwa zinafanya kazi" niliwaza

"Amini hata hili tukio la kuchanjwa usingeweza kumwambia yeyote. Na hautaweza kuja kumwambia yeyote kuhusu tukio la kishirikina utakalolishuhudia hadi siku unaingia kaburini, kama tusipoitoa hiyo dawa mwilini mwako" alisema mganga

"Hata baba yako najua usingemwambia, najua ungepata nia ya kumwambia lakini usingethubutu, hivyo watu wasingejua shida yako na usingepata msaada"

Baada ya kumaliza alichukua wembe na kunichana kidogo kwenye kovu.Alipaka dawa kisha akachomoa kipande cha mti kidogo kama vimisumari vile vidogo.

" Sasa uko huru kuongea. Tunaenda kwenye tatizo la pili".alisema kisha akaendelea

"Hili nadhani umejionea mwenyewe, wachawi tayari wana mamlaka juu ya mwili wako maana wameshamaliza maagano na mizimu ya kwenu, kwa tambiko lililofanyika makaburini. Kazi iliyobaki ni kukuchukua. Sasa ili tukurudishe kuna damu yako waliichukua wakati wanafanya tambiko inabidi tuirudishe kwanza" alitulia kidogo kisha akaendelea

"damu hiyo mwanzoni ilikuwa imefichwa kwenye dari la nyumba ya kwa bibi yako. Ila baada ya kujua umeshaanza kutembea kwa waganga kuna sehemu imepelekwa kufichwa pa siri zaidi ambayo mimi kwa uwezo wangu siwezi kuichukua huko. Inabidi nikupeleke kwa mganga ambaye naamini yeye anaweza kukusaidia. Ila ni mpaka nimtaarifu kwanza baba yako kwanza ajue kila kitu. Maana kuna vitu vitahitajika"

Nilikubali kwa sababu sikuwa na ujanja. Hata hivyo nilijua kama mama yangu angejua ndio angeleta kipingamizi lakini baba yangu hakuwa na shida, hakuwa mtu wa dini sana. Nilimshauri wasimshirikishe mama kwenye hilo, kwa sababu nilijua kwanza ni lazima angepinga kwenda kwa mganga. Pili sikutaka kumuona akiyajua matatizo yangu yangemfanya asononeke sana.

Mganga aliniambia nisiondoke pale kwake maana ndio ilikuwa sehemu salama kwangu. Hadi ile damu yangu irudishwe, lakini akamwambia Vumilia aondoke kesho asubuhi ila asipite kwenye njia ya kutokea kwa mganga wakati anatoka. Yaani apite sehemu pasipo na njia rasmi, mganga alihofia kuna mitego imeachwa ni mpaka aitegue kwanza.

Itaendelea
Nina kufuatilia kwa umakini na ukaribu sana...wafia dini wnakufa sana hasa pale wanapousahau ushauri wa mhubiri 7:15-18. Mkuu yaliwahi kunipata, Mimi nilioa mchawi enzi hizo nikiwa nimfia dini.

Anyway nisikutoe kwenye kisa chako kinachoelimisha labda wengi watatokwa tongotongo kwenye ubongo...Tutambue Kuna jamii isiyoonekana na inafanya mambo yasiyoweza kuonekana kwa jicho la kawaida.
 
Back
Top Bottom