Kipi kinakatika umeme au waya

moja, kwa mazoea ni kuwa chenye kukatika ni kile chenye umbo lenye kuonekana..ni kwa kwa mantiki hiyo unapata tabu kufikiri kuwa umeme nao hukatika kwa vile hauna umbo lenye kuonekana(tunaona nyaya na athari ya umeme lakini si umeme wenyewe).

nadhani hapa kiswahili kilikosa neno stahiki na hivyo kikaazima kutoka lugha ya kiingereza(power cut off) na kwa makubaliano kwa vile kitu kinapokatika kunakuwa na ends mbili zisizo na muunganiko basi hewala kukosekana kwa huduma ya umeme wacha kuwe ni umeme kukatika!

kwa hiyo mkuu..umeme unakatika, maji yanakatika kadhalika simu inakatwa.

kuhusu waya mkuu..unakatika..ingawa kuna mkuu wangu mmoja amesema waya unavunjika, sidhani!
 
@Al Zagawi:
Asante kwa ufafanuzi fasihi. Hii mada ukiiangalia kwa pupa inaoneka kama ni rahisi vile, lakini ukiikaribia zaidi ndio ugumu wake unavyoziidi kuongezeka. Swali langu la nyongeza ni: ipi tofauti kati ya kukatika na kuvunjika? Kijiti cha kiberiti kinakatika au kinavunjika?
 
moja, kwa mazoea ni kuwa chenye kukatika ni kile chenye umbo lenye kuonekana..ni kwa kwa mantiki hiyo unapata tabu kufikiri kuwa umeme nao hukatika kwa vile hauna umbo lenye kuonekana(tunaona nyaya na athari ya umeme lakini si umeme wenyewe).nadhani hapa kiswahili kilikosa neno stahiki na hivyo kikaazima kutoka lugha ya kiingereza(power cut off) na kwa makubaliano kwa vile kitu kinapokatika kunakuwa na ends mbili zisizo na muunganiko basi hewala kukosekana kwa huduma ya umeme wacha kuwe ni umeme kukatika!kwa hiyo mkuu..umeme unakatika, maji yanakatika kadhalika simu inakatwa.kuhusu waya mkuu..unakatika..ingawa kuna mkuu wangu mmoja amesema waya unavunjika, sidhani!
............nashukuru kwa ufafanuzi,
 
Umeme unakatika, waya unavunjika!
.............rungu,usichanganye lugha na wewe unapokuwa kazini,maana unapokuwa kazini hata maji yanaweza kuvunjika,jaribu kudhibitisha kwa kumuuliza mtu aliyepigwa rungu uone................ha........haa........haaaa,nashukuru kwa jibu.
 
@Al Zagawi: Asante kwa ufafanuzi fasihi. Hii mada ukiiangalia kwa pupa inaoneka kama ni rahisi vile, lakini ukiikaribia zaidi ndio ugumu wake unavyoziidi kuongezeka. Swali langu la nyongeza ni: ipi tofauti kati ya kukatika na kuvunjika? Kijiti cha kiberiti kinakatika au kinavunjika?
.....tusubiri wataalamu wa lugha......................,rungu na kirungu.............pia itafuata
 
@Al Zagawi:
Asante kwa ufafanuzi fasihi. Hii mada ukiiangalia kwa pupa inaoneka kama ni rahisi vile, lakini ukiikaribia zaidi ndio ugumu wake unavyoziidi kuongezeka. Swali langu la nyongeza ni: ipi tofauti kati ya kukatika na kuvunjika? Kijiti cha kiberiti kinakatika au kinavunjika?

mkuu wangu rungu, asante kwa kushukuru...

sasa tuendelee na mada...tofauti ya kukatika na kuvunjika!

kukatika...kwa mazoea(sijui kwenye kamusi wanasemaje, hapa natumia uzoefu tu) tunatumia neno hili katika vitu visivyo na maumbile yenye kuonekana kama huduma mbalimbali mfano huduma ya umeme imekatwa, huduma ya maji imekatwa, huduma ya simu imekatwa. na neno mbadala kwa baadhi ya huduma ni kusitisha..mfano kuduma ya kusajili namba za simu imesitishwa kuanzia tarehe fulani mpaka tarehe fulani. tanbihi; kwa makosa watu hutumia neno imesimamishwa badili ya imesitishwa.

Kuvunjika...kwa mazoea tunatumia neno hili kwa vitu vyenye maumbile yenye kuonekana na ambavyo ends mbili zinapokosa kuungana kwa kutenganishwa na ikiwa katika tendo la kutenganisha kuna sauti inazalishwa. ni kwa mantiki hiyo njiti ya kiberiti inavunjika na waya unakatika(kumbuka waya unapokatika huwa hakuna sauti yenye kusikika kwa uwazi.

lakini kama alivyosema mkuu Rungu hapo juu...hii mada ni ngumu pengine wakija wataalamu humu wataweza kutusaidia...bahati mbaya mzee wetu wa mbinu za kiswahili katika TBC1, Suleiman Hegga, sidhani kama anapita maeneo haya.
 
kuvunja :1- tunaweza kusema ni kwa kutumia kitu kisicho na makali, mfano vunja mlango kwa kutumia jiwe , vunja nyumba kwa kutumia mitaimbo nk.
2- kuvunja kwa kutumia nguvu za mwili , beki wa timu A kamvunja mguu mshambuliaji wa timu B.

kukata : 1- ni kuvunja ila hili linatumika kwa kitu chenye makali, panga,kisu shoka nk . kata mti ,tawi
2- kusita kwa huduma kama maji ,umeme nk.
 
kuvunja :1- tunaweza kusema ni kwa kutumia kitu kisicho na makali, mfano vunja mlango kwa kutumia jiwe , vunja nyumba kwa kutumia mitaimbo nk.
2- kuvunja kwa kutumia nguvu za mwili , beki wa timu A kamvunja mguu mshambuliaji wa timu B.

kukata : 1- ni kuvunja ila hili linatumika kwa kitu chenye makali, panga,kisu shoka nk . kata mti ,tawi
2- kusita kwa huduma kama maji ,umeme nk.
Matumizi mengine ya kuvunja na kukata ni:
- Kuvunja mahusiano
- Kuvunja ungo
- Kuvunja mkutano
- Kuvunja (kukata) mbavu
- Kuvunja sheria
- Kuvunja mkataba
- Kuvunja mwiko
- Kuvunja pesa
- Kuvunja mgongo
- Kuvunja moyo
- Kuvunja rekodi
- Kukata shauri
- Kukata mawasiliano
- Kukata viuno
- Kukata karata
- Kukata sala
- Kukata tamaa
- Kukata roho
- Kukata mshahara
- Kukata kauli
- Kukata kamba
- Kukata maji
.................
Hii ni kusema kuwa hata "umeme unakatika", na hili tusilichukulie kama ni upungufu wa Kiswahili bali ni utajiri wa lugha yetu.
 
Matumizi mengine ya kuvunja na kukata ni:
- Kuvunja mahusiano
- Kuvunja ungo
- Kuvunja mkutano
- Kuvunja (kukata) mbavu
- Kukata shauri
- Kukata mawasiliano
- Kukata viuno
- Kukata karata
- Kukata sala
.................
Hii ni kusema kuwa hata "umeme unakatika", na hili tusilichukulie kama ni upungufu wa Kiswahili bali ni utajiri wa lugha yetu.
-Kukata kiu
-Kukata mbuga
-Kuvunja ukimya
 
Matumizi mengine ya kuvunja na kukata ni:- Kuvunja mahusiano- Kuvunja ungo- Kuvunja mkutano- Kuvunja (kukata) mbavu- Kukata shauri- Kukata mawasiliano- Kukata viuno- Kukata karata- Kukata sala.................Hii ni kusema kuwa hata "umeme unakatika", na hili tusilichukulie kama ni upungufu wa Kiswahili bali ni utajiri wa lugha yetu.
Duh,amakweli kukatika kwa umeme na waya,sasa imekuwa tena kuvunja na kukata,mara ungo,haya tena viuno.Rungu nisaidie,kwani Mammamia kama alivyotujuza huu ni utajiri wa lugha yetu.kirungu na rungu tofauti ni nini?.................,Kwa haraka haraka tuu si kila kukatika kuna hasara,hata pia kuvunja.......................ukichukulia maneno ya Mammamia hapo juu utaona kuwa,kweli lugha yetu inautajiri mkubwa,unaweza kubisha lakini tafakari na chukua hatua.......................jaribu kukata,si umeme ila kiuno uone...............,vilevile waulize waliovunja ungo........je,wanajuta...............Nikupongeze sanaaaaa Mammamia,si kwa kukata kiuno au kuvunja ungo,bali kwa kutujuza upana wa lugha yetu..............kiswahili hoyeeeeeeeeeeee
 
kwa mazoea rungu na kirungu ni kitu cha namna inayofanana lakini saizi ndiyo inatofautisha baina ya vitu hivyo viwili...ikiwa ni kidogo huitwa kirungu na kinyume chake ni rungu.

lakini maneno yote mawili yanatumika katika lugha za msimu kumaanisha vitu au hali tofauti na asili ya maneno yenyewe mfano..rungu litakushukia ni tamathali ya semi ikimaanisha utapata adhabu kali mfano wa kupigwa na rungu. mfano mwingine ni...alinipiga kirungu hutumika kumaanisha aliniomba pesa.

kiswahili lugha adhimu, ngumu kwa wasoipa umuhimu...nawasilisha
 
Wana JF mnijuze,kipi kinakatika umeme au waya?

Vyovyote utakavyotamka au kutumia neno lakini maanake ni nchi kuwa gizani kwa sababu context iko wazi. Unafikiri neno likikosewa wakati kwa situation iliopo ujumbe ni clear Jairo, Ngeleja, Malima na JK wata-escape punishment kutoka kwa wananchi?
 
Back
Top Bottom