Habari wana JF.
Mpaka sasa sijapata jibu kulikoni serikali inashindwa kuweka kipengele cha dini ya mtu kwenye fomu za sensa ilihali kuna kipengele cha kuhesabu makanisa na misikiti-utata huu ni kukwepa kitu gani?
Kwa mtazamo wangu -ikiwa niko sahihi-wakiristu na serikali wanataka kipengele cha dini kisiwepo (kama ilivyo sasa) wakati ambapo waislam wanataka kipengele hicho kiingizwe ili wakati wa sensa ijulikane wazi kuwa nchi hii ina waislam wangapi na wakristo wa ngapi.
Kwangu mimi naunga mkono suala hili kwa sababu sensa ni kujua idadi ya watu kwa namna ilivyo-wawe walemavu, watoto, wanawake (vipengele vya hawa vipo kwenye fomu). Ikiwa kweli hakuna mkono wa kanisa, na ikiwa kweli kwamba wakristo wanaitakia mema nchi hii na kwamba hakuna udini kama inavyodaiwa, ni vipi wakristo hwaungi mkono hoja ya waislam ya kuingizwa kipengele cha dini ikiwa hawana ajenda ya siri nyuma ya pazia?
inashangaza kuona serikali inakomaa kuwa kujua dini ya watu si suala la kimaendeleo-inasikitisha saaana. Kwa muda sasa waislam nchini wamekuwa wanadai kuonewa katika sehemu nyingi, na kwa kuwa wakristo walikwisha toa sensa yao na kutangazwa na serikali kupitia TBC1, ni kwa nini sasa serikali haioni busara kuingiza kipengele cha dini ili iwe na takwimu sahihi kutokana na chanzo chake yenyewe? Au ndo kanisa limekwisha amua?
kwa kutumia sensa ya kanisa ambapo inaonesha wakristo ni karibu mara mbili ya waislam ina maana (kwa wenye akili) kuwa wakristo kushika nyadhifa zote muhimu ni sahihi kwa sababu (1) wamesoma -kama ambavyo wamekuwa anadai tangu ukoloni na (2) ni wengi nchini. Mwenye akili pekee ndo analiona hili.
Woga wa kuwa watu wakijua idadi yao kwa dini zao inaleta uvunjifu wa amani ni propanga ya kitoto saaaana. Mbona baada ya wakristo kutoa takwimu zao na kubarikiwa na serikali hakuna uvunjifu wa amani uliotokea? Tutende haki, tuache upuuzi na propanganda za kinafiki.
Ole wao masheikhe wanaotumia undumilakuwili wao kulinda hadhi yao kwa kanisa/serikali kwani adhabu kali itawathibitikia siku ya malipo (kiama). Ahadi ya Allah ni kamilifu-hakika itatekelezwa juu yao. Tuchukue tahadhari mapema kwa kuzingatia maslahi ya wengine hata kama hawapendwi.
Mpaka sasa sijapata jibu kulikoni serikali inashindwa kuweka kipengele cha dini ya mtu kwenye fomu za sensa ilihali kuna kipengele cha kuhesabu makanisa na misikiti-utata huu ni kukwepa kitu gani?
Kwa mtazamo wangu -ikiwa niko sahihi-wakiristu na serikali wanataka kipengele cha dini kisiwepo (kama ilivyo sasa) wakati ambapo waislam wanataka kipengele hicho kiingizwe ili wakati wa sensa ijulikane wazi kuwa nchi hii ina waislam wangapi na wakristo wa ngapi.
Kwangu mimi naunga mkono suala hili kwa sababu sensa ni kujua idadi ya watu kwa namna ilivyo-wawe walemavu, watoto, wanawake (vipengele vya hawa vipo kwenye fomu). Ikiwa kweli hakuna mkono wa kanisa, na ikiwa kweli kwamba wakristo wanaitakia mema nchi hii na kwamba hakuna udini kama inavyodaiwa, ni vipi wakristo hwaungi mkono hoja ya waislam ya kuingizwa kipengele cha dini ikiwa hawana ajenda ya siri nyuma ya pazia?
inashangaza kuona serikali inakomaa kuwa kujua dini ya watu si suala la kimaendeleo-inasikitisha saaana. Kwa muda sasa waislam nchini wamekuwa wanadai kuonewa katika sehemu nyingi, na kwa kuwa wakristo walikwisha toa sensa yao na kutangazwa na serikali kupitia TBC1, ni kwa nini sasa serikali haioni busara kuingiza kipengele cha dini ili iwe na takwimu sahihi kutokana na chanzo chake yenyewe? Au ndo kanisa limekwisha amua?
kwa kutumia sensa ya kanisa ambapo inaonesha wakristo ni karibu mara mbili ya waislam ina maana (kwa wenye akili) kuwa wakristo kushika nyadhifa zote muhimu ni sahihi kwa sababu (1) wamesoma -kama ambavyo wamekuwa anadai tangu ukoloni na (2) ni wengi nchini. Mwenye akili pekee ndo analiona hili.
Woga wa kuwa watu wakijua idadi yao kwa dini zao inaleta uvunjifu wa amani ni propanga ya kitoto saaaana. Mbona baada ya wakristo kutoa takwimu zao na kubarikiwa na serikali hakuna uvunjifu wa amani uliotokea? Tutende haki, tuache upuuzi na propanganda za kinafiki.
Ole wao masheikhe wanaotumia undumilakuwili wao kulinda hadhi yao kwa kanisa/serikali kwani adhabu kali itawathibitikia siku ya malipo (kiama). Ahadi ya Allah ni kamilifu-hakika itatekelezwa juu yao. Tuchukue tahadhari mapema kwa kuzingatia maslahi ya wengine hata kama hawapendwi.