Kipaumbele katika maisha

Kisusi Mohammed

JF-Expert Member
Aug 10, 2009
563
468
Imekuwa ni kama kasumba kwa watu wengi waliofikia rika la kujitegemea kukosa uchaguzi sahihi wa kuyaendea maisha yao kwa usahihi endelevu utakao mjenga na kumuendeleza katika kuyakabili maisha yake ya kila siku.

Wengi wamekuwa wanashindwa kuamua ni kipi haswaa ni cha kipaumbele katika mambo mengi ya msingi ya kufanya ili maisha yawe bora na yenye furaha.

Kwa Mfano: Kuoa au kuolewa, kuwa na usafiri (gari, pikipiki, baiskeli), kujenga nyumba, kununua shamba, kununua kiwanja, kuwekeza katika hisa, kusafiri nje ya nchi katika kutafuta kipato cha ziada au kufanya lolote lenye muelekeo wa kimaendeleo.

Hivyo basi kwa mtazamo wa haraka haraka nikiwa kama mmoja wa waliopata tabu sana katika kuamua kipaumbele, nikaonelea haitakuwa vibaya faida hii nikaifikisha mikononi mwa wanaJF ili kila mwenye wazo lake na atupe alichonacho ili kesho na keshokutwa kwa watakaopata mawazo haya mazuri wayatumie na wasiishie kuapata tabu kama mimi.

Swali la msingi: NI KIPI CHA KUKIPA KIPAUMBELE KATIKA HAYO MENGI NILIYOYATAJA HAPO JUU?

Natumai nimeeleweka.
 
Hahahahaaaa kaka Franki umeme ni nyongeza tu, na hauleti maendeleo bali unarudisha maendeleo nyuma "MGAO"!
 
mimi nadhani bila nyumba nzuri ya kukaa mwanadam hujawa na maisha mazuri. gari badae na vingine vingi ila nyumba ni muhim iwe kijini au mjini
 
Hi inategema na mtu na mtu.

Kuna watu kipaumbele chao ni Kuoa kwanza wengine kununua gari na wengine mpka wanunue Shamba. Kwa hiyo kujibu swali lako ni kwamba Kilamtu ana kitu ambacho anakipa kipaumbela zaidi ya kingine.

Wewe unaweza ukawa unapenda sana ujenge nyumba yako kabla ya kuoa na mtu wengine mambo ya kujenga nyumba wala hayapo sana kwenye akili yake
 
Nionavyo mimi:
1 kuwa na hisa au shughuli yoyote ya kuongeza kipato
2 kiwanja
3 kujenga nyumba
4 usafiri
kuoa/kuolewa kunaingia popote baada ya namba moja
 
The best is what will make you as effective and efficient as possible....Ukianza na gari nadhani utakuwa faster zaidi kufikia malengo yako. After all...ukiwa na 8,000,000 unaweza kupata gari litakalokusaidia mambo yako, the same haiwezi kujenga nyumba. Next ni Mke mwenye kipato na serious.....ukimpata mke serious na akiwa na income mtajenga nyumba nzuri na kubwa kihalali kabisa. Mimi nilifanya hivyo; TOYOTA COROLLA, WIFE and finally HOUSE. I have two houses na sijawahi kupitisha vocha ya mtu wala kutoa na kupokea rushwa kama kina nanihii
 
Kwa kweli nazidi kuelimika na kufaidika kila baada ya mchango wa mdau. Hii itawasaidia wale wote ambao bado wana maswali juu ya kipi kitangulie kabla ya kingine. Ahsanteni sana na bado nataraji mawazo zaidi ili iwe faida kwetu na wengineo wote.
 
Kisusi, hongera kwa kuibua haka kamada kazuri na muhimu kwa wengi mimi nikiwemo. Naomba kumuunga mkono Joste kwa asilimia 70.

Kwa mtazamo wangu Kipaumbele katika Maisha kitategemea na mipangilio ya mtu mwenyewe.Wakati mwingine angependa atangulie kuoa mwingine anafikiria gari kwanza na mwingine angedhani nyumba kwanza. Familia zetu ni extra extended, mara unapopata kakibarua unafuatwa na msululu wa wategemezi nyuma yako, wapo watakao hitaji ada ya shule, mtaji, matibabu na mengine yanayofanana na hayo.Hivyo wakati unaweka Vipaumbele vyako huwezi kuyaweka hayo niliyoyataja kando hata kidogo. Ili Upeo au elimu uliyoipata iweze kutricle down into your family/community lazima uwasaidie hao ili nao angalau wapate macho ya kuona maili kadhaa mbele yao, vinginevyo utakuwa na gari halafu wakwenu hata asprin hawawezi kununua itakuwa haina maana sana.

Biblia inasema asiyejali wa kwao ni sawa mtenda maovu mwingine yeyote yule.

Best regards.
 
Ahsante sana kaka Grey, pamoja na utashi wa mtu binafsi nilitegemea nawe utoe orodha yako kulingana na kipaumbele kwa maisha yako ya extra extended family na hali halisi ya familia zetu. Kwa sababu wengi wetu tupo kwenye status kama hiyo, ukitusaidia kuorodhesha priorities waweza tusaidia kufunguka kimawazo.
 
Back
Top Bottom