Kipa Ally Salim anapaswa afundishwe jinsi ya kukaa golini penati zinapopigwa

political monger senior

JF-Expert Member
Nov 26, 2020
1,801
5,788
β€Ίβ€Ί 'π™ˆπ˜½π™„π™‰π™ 𝙃𝙄𝙄 𝙉𝙄 π™ƒπ˜Όπ™π˜Όπ™ˆπ™'

Ameandika mchambuzi Jemedari Said

"Nawapongeza Simba SC kwa kutwaa ngao ya jamii, nampongeza kijana wangu, Ally Salim kwa kuzuia penati (3) ni ushujaa mkubwa.

"Zaidi nampongeza Ally Salim kwa mbinu yake ya kutoka hatua moja mbele kabla mpira haujapigwa na kumuibia mpigaji na mwamuzi msaidizi ambaye ndio huwa mwenye shughuli ya kuangalia kama kipa ametoka kabla ya mpira kupigwa.

"Ukiangalia penati zote Ally Salim alikuwa anatangulia kutoka kabla mpira haujapigwa, hata ile moja (Ya Azizi Ki) aliyofungwa ni vile tu mpira ulikuwa na kasi.

"Nampongeza Ally Salim kwa mbinu hii ambayo leo imemsaidia kwa kutokuwa na waamuzi makini pia. Lakini nampa tahadhari, mbinu hii siku hizi ni HARAMU na ikitokea ukaokoa basi penati inarudiwa, hivyo leo penati zote (3) zingerudiwa. Ukibisha angalia video kwa umakini.

"Diarra anaweza kuwa mwalimu mzuri kwa namna alivyookoa penati yake kwa kuhakikisha mguu mmoja unabaki kwenye mstari wakati mpira unapigwa na sio kutokea mbele hatua moja.

"Simba furahieni leo na Ngao mmebeba, ila kwenye mechi zenye waamuzi makini msije mkarusha ngumi tu, kipa anatokea mbele hatua moja kabla mpira kupigwa ambayo ni makosa."

Jemedari Said
Mchambuzi wa Efm Radio

"Ally Salim anastahili pongezi nyingi kwa kile alichokionesha katika mchezo dhidi ya Yanga, kudaka penati (3) dhidi ya wanafainali sio mchezo.

"Lakini kuna jambo ambalo halikuwa sawa kwa upande wa waamuzi ambao ndio wenye jukumu la kusimamia sheria zote uwanjani.

"Ki kawaida golikipa wakati wa kudaka penati hapaswi kutoa miguu yake yote kabla mpigaji hajapiga mpira, lakini kwa Ally Salim ilikuwa tofauti alikuwa anatoka hata kabla mpira haujapigwa.

"Katika penati zote (3) alizocheza zilistahili kurudiwa kwani zilikuwa zinapigwa wakati ambao ameshatoka kwenye mstari.

"Bado tuna safari ndefu sana kuhusu waamuzi wetu na sheria hizi"

Edgar Kibwana
Mchambuzi wa Clouds fm radio
1691985547188.jpg
 
Vyovyote vile, Yanga hawana wapigaji penati.

Aziz K aliweza kufunga kwa sababu lilikua ni shuti kali, ila na yeye angepiga kinyoronyoro kama wenzake kipa pia angedaka. Hawa wengine wameshaona kipa ni mwepesi upande wa kulia, bado wanamuelekeza wanapopiga, halafu wanapiga ki star, lazima umpe kipa sifa.

Hizo za kuanza kutoka hatua moja sioni kama ni sababu, sababu ni Yanga kutokuwa na wapiga penati.
 
Vyovyote vile, Yanga hawana wapigaji penati.
Aziz K aliweza kufunga kwa sababu lilikua ni shuti kali, ila na yeye angepuga kinyoronyoro kama wenzake kipa pia angedake. Hawa wengine wameshaona kipa ni mwepesi upande wa kulia, bado wanamuelekeza wanapopiga, halafu wanapiga ki star, lazima umpe kipa sifa.
Hizo za kuanza kutoka hatua moja sioni kama ni sababu, sababu ni Yanga kutokuwa na wapiga penati.
Yanga awakujipanga kwa ajili ya penalty walijua mechi wanaimaliza ndani ya dk90 kwa jinsi walivyokuwa wanaumiliki mchezo..
 
Ninakubaliana na Mawazo yake lakini UZEMBE WA WACHEZAJI KUTOJUA KUPIGA PENALT NDIO TATIZO, MIGUU 12 NI JIRANI MNO.

1. kwanini yanga Wasilalamike mapema PENALT ya kwanza au ya pili???????

2. Kwani kwa wydad Hakutokaa au alitoka na Akafungwa na kupotezwa MABOYA kwa PENALT zote .???????

3. HUONI kwamba Uwezo wa kupiga PENALT upo chini kwa wachezaji wa timu zetu?????

Hizo sheria ni mpya sana Miguu 12 ni JIRANI mno kufunga PENALT

Ni uzembe tu kwa HAO wapigaji.
Ukiwa unajua kupiga PENALT HAIJALISHI GOLIKIPA AMEKAA WAPI UTAFUNGA TU .

YANGA WAMEKUWA WAZEMBE KUPIGA PENALT NA WAMEFUNGWA FULL STOP.
 
Yote kwa yote mtani kashinda
Ndo mpira huwezi kufurahi kila siku
Kwenye mpira makosa na maumivu yapo
Acha utani unoge makolo washinde wachukue hilo sinia
Walikaa kinyonge muda mrefu
Watani
 
Ni penati Moja tu Ally Salim aliibia nyingine zote alikaa kwenye mstari, huyu jemedari ni bingwa wa kukosoa wachezaji wengine ila wachezaji walio chini yake hata wafanye madudu gan7 hawagusi na Boko ni mmoja wapo .
 
Vyovyote vile, Yanga hawana wapigaji penati.

Aziz K aliweza kufunga kwa sababu lilikua ni shuti kali, ila na yeye angepiga kinyoronyoro kama wenzake kipa pia angedaka. Hawa wengine wameshaona kipa ni mwepesi upande wa kulia, bado wanamuelekeza wanapopiga, halafu wanapiga ki star, lazima umpe kipa sifa.

Hizo za kuanza kutoka hatua moja sioni kama ni sababu, sababu ni Yanga kutokuwa na wapiga penati.

Au nungunungu aliwaambia Ali ni mbovu upande ule….? Maana haiwezekan wote wapige kule kule
 
Ishapita ndugu zangu,marefa wa kibongo sometimes sijui wanafikiria nini, mtu mara nne kavunja sheria.

Ila cha msingi kocha kajitahidi kutengeneza muunganiko wa timu na hata sub anazo zifanya unaona zina impact,cha msingi pale ajaribu kuongea na washambuliaji wake kuhusu umaliziaji.
 
Back
Top Bottom