1800
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 2,215
- 603
watanzania tuwe macho na viongozi ambao wapo tayari kuingia ikulu kwa kukanyaga damu zetu, viongozi wanaochochea vurugu ili tu wapate kutimiza malengo yao ya kisiasa tuwaepuke viongozi wa namna ni hatari kwa taifa letu, amani ikitoweka wao huondoka na familia zao nje ya nchi na kutuachia vurugu, tunataka mabadiliko kwa njia ya Amani. Mpenda Amani.
Unacho ongea ni sahihi kabisa kwako kwa vile uko thoughtlessness,ndio maana unaona kuhoji wizi wa kodi yako unaofanywa mchana kweupe na watu wachache kwa maslahi ya familia zao wakati wewe na nduguzo mmepigika kimaisha mpaka kifikra,au kupaza sauti ili huduma za kijamihi kama elimu,afya,barabara,kuheshimu haki za raia,kuhoji uadilifu uliopotea kwenye vyombo vyetu vya dola kwako wewe ndio unaona ni uchochezi,its a shame kwa kua watu wenye iq kama yako ndio mnaofurahiwa na ili genge la wahuni na matapeli wa rasilimali zetu walio chini ya kimvuli cha uongozi!haya maneno yako wewe si wa kwanza kuyatoa,walishayatoa watu wenye dhamana na chama chao na wenye kufahamika nchi nzima kama Wassira,Nnauye nk lakini wamekuja kujigundua Watanzania wamewapuuza kwa vile vichwa vyao vimefunguka siku hz,hawako tena katika dimbwi la ujinga wa kudanganywa kwa hoja za kitoto eti machafuko,udini,ukabila etc!cream ya watu wenye mawazo kama yako kwa Tanzania ya leo ndio inaelekea ukingoni,watu wanakimbilia kujikomboa kifikra na kimaisha mkuu,na hawataki kubaki tena kwenye ignorance siku hizi!