Kinga kwa Rais aliyeko madarakani na wastaafu ni kichocheo cha uvunjaji haki, Iangaliwe upya

Ukweli ni kuwa kama siyo sheria kunibana basi ningekuwa nimeshafungua kesi kadhaa dhidi ya rais Magufuli kutokana na mwenendo wa matamko yake.

Kwanza nikiri kuwa yapo maeneo machache ambayo rais anafanya vizuri kama mkuu wa nchi na eneo hilo ni nidhamu ya kazi ingawa imechangishwa na uoga hivyo kukosa matokeo chanya kwa kiwango kikubwa juu ya ukuaji wa uchumi. Lakini kwa ukweli ulio mchungu kabisa, rais Magufuli kama ataendelea hivi basi huenda akawa ni rais wa bahati mbaya kabisa kwa nchi kuwahi kuwa naye na mbaya zaidi huenda hadi mwaka 2020 tukajikuta tuna taifa lenye taswira tofauti kabisa na wengi wetu wakabaki wakijiuliza kulikoni?

Kauli nyingi sana za rais Magufuli zinaliweka taifa katika mashaka makubwa sana, zinavutia mgawanyiko wa hali ya juu.

Kama kiongozi mkuu wa nchi pale unapoongea au kufanya jambo, ni tofauti kabisa na watu wengine hata kina Lowassa, Mbowe na Maalim Seif. Kiongozi wa nchi kama atashindwa kuchochea umoja basi ni heri ajiuzulu mapema kwani ameshindwa kuwa mkuu wa nchi kwa hatua za awali kabisa, umoja haujengwi kwa kuwatisha watu wenye ufuasi mkubwa nchini wala kuwatisha wafuasi wao. Kuendelea kuyatisha makundi mbalimbali kuna siku yanaweza kuungana na kuwa kitu kimoja kwa ajili ya kujibu mapigo na hapo ndipo yanapotokea mambo kama ya kaskazini mwa Uganda, Mashari mwa Congo na Sudan ya kaskazini vs Sudan ya kusini.

Sasa basi, kwa kuwa mheshimiwa rais anaonyesha kutokubadilika huku kasi hiyo ikizidi, ni bora akabanwa na mhimili wa kutekeleza sheria na ule mwingine wa kutunga sheria ingawa umeingiliwa ila bado unaweza kujipa meno ikiwa utakuwa kitu kimoja kwa wengi wao.

Ikiwa wabunge wataungana na kubadili sheria ama kuonyesha waziwazi kuwa yapo matamshi wasiyokubaliana nayo kutoka kwa rais (najua kwa sasa wapo wengi kutoka CCM) basi wanaweza kubadili sheria na kuifanya mahakama iwe na meno juu ya rais aliyeko madarakani na hapo kama nchi tutakuwa tumepiga hatua kubwa kwa mustakabali wa taifa. Ama kwa kuonyesha tu uimara wao na kupaza sauti.

Haya yakiendelea hivi, basi ni majaaliwa mbeleni.

Tatizo akidi haitatimia bungeni
 
Wote tunajua moja ya vitu ambavyo Rais anaapa vizuri kuvilinda siku anapokabidhiwa nchi in Katiba.

Ivi chombo gani kinatakiwa kumwajibisha pindi anapo ivunja katiba ya jamhuri ya Muungano?

Na je nani mwenye mamlaka ya kutambua kuwa Rais amevunja katiba hatua zichukuliwe?

Je baada ya kustafu kosa la kuvunja katiba linaweza kumfikisha mahakamani Rais was Jamhuri ya muungano?
 
Ni muda mrefu watu wamekuwa na malalamiko juu ya Rais aliyemadarakani na ilishawahi kujadiliwa Bungeni juu ya kumshtaki au kutomshtaki aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu.

Hata hivyo kwa mujibu wa Ibara ya 46(1) na (3) ya Katiba yetu ya 1977 ni marufuku kumshtaki Rais kwa kosa alilofanya akiwa madarakani wakati bado anaongoza Ib. 46(1) na baada ya kuondoka madarakani Ib. 46(3).

Pamoja na kwa chini ya Ibara 46A kunauwezekano wa kumshtaki Rais wakati na baada ya uongozi wake, utaratibu huu ni mgumu sana kutimiza masharti yake haswa ukizingatia uwiano wa vyama Bungeni.

Je, ni wakati sasa wa kubadilisha msimamo huu haswa wakati huu wa sera za uwajibikaji? je, hatutaondoa amani ya moyo kwa Rais aliyemadarakani inayomsaidia kutekeleza majukumu yake ipasavyo.
 
Haya yameandikwa na aliyekuwa Mbunge Mzalendo aliyepigania nchi hii na hatimaye kutishiwa hata maisha na mwishowe kupokwa ushindi wake wa Ubunge. Prof David Kafulila. Hawa ndiyo waliopaswa kuwa Maprofesa ukiachana na wale ma Pro-pesa.

Anasema bado watanzania wanamlilia JPM aokeo hasara tunayoingia ya Bilion 7 anazolipwa Singasinga kila mwezi ambazo ina maana kwa miezi miezi kumi na mbili ni tsh bil 84 tungeweza kununua ndege mpya kila mwaka ikiwa tunataka ndege. Lakini tungeweza kubomoa nyumba zilizopo buguruni kwa mnyaman halafu tukaanza kujenga mji wa kisasa pale na kuwapatia wananchi na nyingine kupangisha kila mwaka.

Hapo ukiacha Bil 305 alizopewa na ikulu ya kikwete pamoja na viongoz wengine nadhan ikiwa ni mgao. Kukosekana kwa nguvu katika Bunge letu,maslah binafs,kukosa uzalendo n.k kunafanya lishindwe kumwajibisha rais fisadi,mfujaji au mwizi. Hapa tudai katiba nzuri.

CAG na TAKUKURU walithibitisha pesa za ESCROW hazikuwa za singa singa. Kikwete peke yake na watu wako waliofaidika na pesa hizi walisimamia kidete kusema ni za singasinga.

Jambo hili tu lilitosha kumchunguza ndugu kikwete. Lakini anadunda tu mitaani mpaka leo hii. Na ndio maana kwa uzalendo Gen Ulimwengu alisema huyu jamaa alipaswa achunguzwe au awekwe ndani.

Inaumiza sana wakati serikali inawakamua wananchi kodi /damu mpaka tone la mwisho wakati kuna ambao walipaswa walipe hizo pesa. Ni Afrika tu mgonjwa wa malaria anatolewa damu ili iwe sadaka kwa miungu ambao wameshakunywa sana damu mpaka wanaamua hii wanayopata wawe wanaoga.
 
Huu uzi Life Span yake JF ni Masaa kadhaa.
Umejaa uchochezi na uchonganishi na pia unafungua mageti yanayoelekea Kisutu
#Hatuna_Milioni_7
 
Kuna vitu vingine ukifikiria vinaumiza sana. Vijana inabidi tujifunze kuwa wazalendo katika umri huu wa sasa ili tabia nzuri ikomae ndani yetu. Pia tusome kwa bidii tupate maarifa ya kutosha Kwasababu hawa wazee wanataka siku wakifa wawe wametuachia nchi ambayo ni 00
 
Ila kwa sasa wanakamua damu kwa wagonjwa kweli kukusanya kodi.... yaani magari yaliyo isha kuwa scraped tangu 2008 unayalipia motor vehicle na kodi leo...
 
Hata akiondolewa kinga unadhani atashitakiwa? labda chama cha upinzani ndio kiwe katika utawala ila kama chama chake ndio kinaongoza nchi bado ataendelea ku enjoy maisha mazuri.
CCM ni chama cha mafisadi ndio maana wote katika system lazima waekwe watu ambao ni wanachama wa CCM na wenye kadi za CCM ili kuwalinda viongozi wa CCM
DPP ni Mwana CCM
Takukuru ni Mwana CCM
Msajili wa vyama ni Mwana CCM
IGP ni Mwana CCM
Mwenyekiti wa NEC ni Mwana CCM
Mwanasheria na Naibu wake ni Mwana CCM
 
Katika nchi yetu kuna sheria za ajabu sana, mojawapo ni hii ya kumlinda Rais Mstaafu kutokana na makosa aliyoyafanya akiwa Rais. Habari juu ya Ufisadi uliofanyika katika awamu ya tatu ya Uongozi wa nchi yetu ni dira tosha ya kutufanya tufikirie upya juu ya Kinga ya Rais Mstaafu ya kutoshitakiwa.

Kashfa za kufanya biashara akiwa Ikulu, Wizi wa Mgodi wa Kiwira uliokuwa na thamani ya mabilioni ya shilingi kwa Mkapa-Yona kujiuzia kwa shilingi milioni 700 tu, Uundaji wa Kampuni za wizi na utapeli za Meremeta na Tangold, Wizi wa EPA BoT na Ujenzi wa Twin Towers za BoT, Ubinafsishaji wa NBC kwa Bei ya kutupa,Ununuzi wa Rada kwa bei ya kuruka, Ununuzi wa ndege ya Rais kwa gharama ya Watanzania "kula nyasi" na nyinginezo ni sababu za kutosha kabisa za kutufnaya Watanzania kupigania kuondolewa kwa sheria ya kinga inayomlinda Raisi mstaafu kutoshiotakiwa kwa wizi, ubadhirifu na Ufisadi aliofanya Rais Mstaafu wakati akiwa madarakani.

Sheria ya Kinga ni Msingi mkuu wa Ufisadi na Utawala wa hovyohovyo kwa gharama za Watanzania kama kashfa hizo nilizotaja hapo juu zilivyotugharimu Kiuchu na Kimaadili. Kuvuja kwa Habari za juzi kuhusu Utajiri wa Waziri Chenge kumiliki dola milioni moja katika akaunti nje ya nchi ni ushuhuda mwingine juu ya Sheria hii Fisadi ambayo inaweka misingi ya Wizi na Uhujumu wa mali ya Umma kwa hasara ya Wananchi wa Tanzania. Hebu tujiulize; Je, itawezekana kumshitaki Chenge aliyekuwa MWanasheria Mkuu wakati wa Mkapa bila kumgusa Mkapa (ambaye sheria inamkinga dhidi ya kushitakiwa?), Tunaweza kumshitaki Daniel Yona kwa kujiuzia Kiwira kwa bei ya bure bila kumshitaki Mkapa ambaye ni "Mjasiriamali" na Mbia mwenzake? KAtika haya mawili haiwezekani kutenda haki maana haiyumkiniki na ni vigumu sana kuwatia watu hawa hatiani (Yona na Chenge) na kumwachia huru Mkapa ambaye ama alishirikiana nao au alishindwa kuwajibika kwa Makusudi na kuwaachia "Wajasiriamali" na Mafisadi kama Chenge kujineemesha kupitia mikataba hewa na feki ambayo naamini kuwa Aliisaini kwa ahadi ambazo ndizo leo imemfanya Chenge kutuhumiwa kuwa na USD Milioni 1 kwenye akaunti zake nje ya nchi!

Kuondolewa kwa shria hii Fisadi, pia kutasaidia kupunguza idadi ya Wagombea urais ambayo wakati wa kinyam]ng'ang'anyioro cha kwenda kugombe Urasi huwa kunakuwa na orodha ndefu ya watu wanaotaka kuwa Marais maana wanajua fika kuwa wakipata nafasi hiyo Ufisadi wao hautakumbukwa milele. Hii itatusaidia kuwa na Wagombea safi na wnaojiamini kuwa ni Waadilifu na ni safi.

Wito wangu kwa Viongozi wa Dini, NGOs, Wananchi, Wabunge na Wanaharakati wengine ni kuwa wakati umefika wa Kushinikiza kufutwa kwa sheria FISADI inayomkinga Rais dhidi ya Rais Mstaafu. Tuanze sasa na ikiwezekana hata kutumia Mahakama ili sheria hiyo iondolewe haraka na kabla hatujapata Rais wa Awamu ya Tano.

Tukifanikiwa kuondoa sheria hiyo Fisadi, tuanze na Mkapa ambaye ndiye chimbuko, Founder na Pioneer wa Ufisadi tunaouona sasa na unaotula kama kansa Watanzania.
WaTz mnapenda kumshitaki Nyani kwa Tumbiri ili aonekane mwizi wa mahindi tu lakini mkijua hawezihata kukemewa . Katiba pendekezwa ya Waryoba ilikuwa imefungia kinga zote za kijingaza rais ndaniya jeneza tayari kwenfakuzikwa. Hamtaki kumsema Tumbiriwenu chaujanja aliyefungua jeneza hilo kwa lugha ya porojo na hata kusababisha vijana eetu kurushiana makonde na viti kutetea kufunuliwa kwa jeneza hilo. Hamkumlaani Kikwete kwa kudai eti mnampenda na kumsifu kuwa kiongozi bora. Mbona alihofia zaidi kuondolewa kwa kinga hizo? Angeacha mkamshitaki Mkapa wenu na sisi tukamshitaki Kikwete wetu ndiyo mngejua yupi alikuwa fisadi ndani ya Ikulu. Aliyerukia kuzuia Katiba ya Waryoba ndiyo ana kesi kubwa ya kujibu kwa waTz.
 
Ďu
Katiba Mpya inataka Rais apunguziwe madaraka ya kuteua. Sawa lakini mfumo wa watu kuingia holela katika idara hata wasipoweza kufanya kazi (siyo wasizoziweza-tofautisha hapa) ni hatari.

(Mfano mwepesi ni kumpa Mchaga ajira huria namna hiyo, nchi itaingizwa biashara na mwenendo usio na mwelekeo sahihi kama ukabila, wizi wa fedha na hata maangamizi ya makabila mengine. Siyo kuwa mchaga hawezi kazi bali akiipata anafanya mambo mengine yenye madhara kwa raia wengine (sasa hivi nimenunua butter ya karanga kutoka Super Market ya Mchaga amefungua makopo yale na kuongezea madawa ya kupoteza fahamu)).

Kasoro iko katika namna Rais anavyochaguliwa na kinga anazopewa. Rais anachaguliwa na wananchi halafu katika ndoto za ujinga wote wananchi wanashangilia kuwa wana demokrasia ya kuchagua mpaka Rais wao.Lakini Rais huyo huyo akishaingia Ikulu anakuwa kama Mungu-Mtu, wananchi waliomchagua hawawezi kumfukuza na hashauriwi na yeyote katika kazi zake isipokuwa akina-Rweyemamu. Na kama Bunge likijazwa mahela ya kwenda mpaka Dubai kukutanisha wapendanao basi hata ukasirike namna gani kuhusu tabia ya Jakaya Ikulu unapoteza wakati wako. Sana sana ukionyesha wazi chuki zako kwa Jakaya unajipalia makaa utaishia kama Ulimboka au Kibanda.

Mahela yamejaa Uswiss lakini Rais hata aibe na wewe ukapata data zote huna chombo cha kumsikiliza raia wa kawaida kuhusu tabia ya wizi wa Rais. Mahakama yote anateua yeye, na Jaji Kiongozi ni Mstaafu aliyepewa Ruzuku na Rais huyo huyo kurudi kazini.Ukifungua madai Jaji Kiongozi anakubana, jinai huwezi kwa sababu Rais hashitakiwi kwa jinai, na Yeye Rais ndiyo Mwendesha Mashitaka Mkuu wa jinai, ndiyo anamteua DPP.

Hivyo -------- yeyote akishapata kura za wananchi kuwa Rais kaula na hana kikwazo mpaka miaka mitano ipite. Wakati wa kutoa mapendekezo kuhusu Katiba Mpya mimi niliwahi kupendekeza kwenye mtandao wa Tume husika kuwa:

!.Kuwe na utaratibu Rais kufukuzwa na wale waliomchagua. Sheria zote za ajira nchini zinasema hivyo, kila mwajiriwa atafukuzwa na mamlaka iliyomwajiri.

2. Rais asitokane na Chama cha Siasa kwa sababu majukumu yake ni ya Kitaifa siyo ya kisiasa wala kimkoa. Hivyo Rais achaguliwe na ushirika wa nyanja zote zinazounganisha wana siasa wote na asasi zote zinazoweka mskumo katika nchi. Tukishindwa kueleka huko basi Rais achaguliwe na Bunge kama ambavyo anafukuzwa na Bunge.

3. Rais anapokurupuka kwa wiki mbili kwenda kuomba kura kwa watu wasiomjua kuna hatari ya Rais huyo huyo kurudi huko akigawa pesa za walipakodi kwa wakulima wa korosho kama shukrani kwa kumsaidia kuingia Ikulu.

4.Utawala wa ki-Demokrasia ndiyo unaotokana na wananchi moja kwa moja na hapa wananchi ndiyo wanaweza kuonyesha tofauti kati ya ubora wa mawazo yao. Hata ndani ya nyumba tofauti za kimawazo zipo lakini baba huwa hazitakiwi kumfanya mbaguzi. wote ni watoto na huyo ni Mama yao. Na mtoto mmoja akimpenda kaka yake na mama yake na kumchukia HUYO ZURIAT haina noma, nyumba itadumu tu. Hivyo watawala wa kisiasa ndiyo wachaguliwe na wananchi. Na hapa ilitosha kabisa Mmasai kuchagua Mbunge wake Monduli kwa sababu anamjua, siyo mkazi wa Mpanda kumchagua mtu wa Kilosa aliyepita siku moja tu akijinadi kwake, ni urongo huo. Waziri Mkuu akitokana na Chama Chenye Majority Bungeni ndiyo utaratibu unaotumika na kwingine. Waziri Mkuu wa namna hiyo atakuwa makini kuhakikisha Chama chake hakiingii migogoro ya uchumi na raia kwa ujumla kwa sababu chama kitapoteza umaarufu.

5. Raia wamshitaki Rais mahakamani na Mahakama iwe na uwezo wa kumpa mdai hukumu dhidi ya Rais, halafu hukumu hiyo apewe Spika wa Bunge kwa ajili ya kuona hukumu inatekelezwa kwa kiwango cha hata kumwondoa Rais madarakani. Hapo Rais atawaheshimu hata raia wa nchi yake.

Mkiendelea na utaratibu wenu wa sasa itakuwa Rais anateua Mawaziri halafu wahuni na mafisadi waliomweka Rais madarakani wanaharibu na waziri husika anajiuzulu halafu Rais anateua Mawaziri wengine. Huo ndiyo huitwa mzunguko wa umaskini.
Duh! Hii namubaliana nayo 100% kama niliandika mimi. Lazima ilikuwa saa sita usiku na nilikuwa nimechelewa kulala. Lakini wakuu huo ndiyo fact!
 
Katika katiba yetu ya Tanzania,kuna kinga maalum ya Rais kutoshtakiwa. Kinga hii uhusu Rais anapomaliza muda wake wa uongozi kutoshtakiwa kwa makosa aliyoyatenda akiwa madarakani,katika kutekeleza wajibu wake

Mambo mengi yanayofumuka sasa yameanza kwenye awamu zilizopita. Wastaafu wetu wasingekuwa na kinga wangechunguzwa,kuhojiwa na hata kuburuzwa mahakamani. Mengi yangejulikana na kurekebishwa kwa tawala zilizopo na zijazo. Ingekuwa somo

Madudu yote ya sasa yamezaliwa na yaliyopita. Katiba yetu inatulazimisha kuamini na kufuata methali: yaliyopita si ndwele,tugange yajayo. Katiba yafanya wakuu kujisahau.

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Songea,Ruvuma)
 
Back
Top Bottom