Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Huku akionekana mwenye furaha tofauti na wakati alipokuwa analalamikia Chadema walipodai SYNOVATE wameficha matokeo, Abdulrahaman Kinana ameikosoa REDET kwa kile alichokiita ni kutumia mtindo wa kimikoa badala ya majimbo na hivyo kupunguza wastani wa kukubalika kwa CCM hususani mgombea wake wa uraisi.
Akihoji utaratibu wa kura hiyo ya maoni alidai CCM itaibuka na asilimia 88 badala ya ile ya 71% ambayo wengi wanaona ilikuwa imechakachuliwa na hivyo kutowatendea haki watanzania.
La kushangaza, Kinana hakuelezea ni vipi majimbo yaliyo ndani ya mikoa yawe hayakujumuishwa kwenye utafiti huo. Hivyo, alishindwa kuthibitisha hoja yake ni vipi CCM ilikuwa imeathirika na utafiti huo wa REDET iwe ya kimikoa au ya kimajimbo.
Vilevile, Kinana alikuwa bubu juu ya inakuwaje Dr. Slaa awe ana mvuto mkubwa kwa wananchi kwenye kampeni zake lakini asiweze kuwa anakubalika kuliko JK ambaye watu huenda kwenye mikutano yake kusikiliza burudani za kizazi kipya.
Akihoji utaratibu wa kura hiyo ya maoni alidai CCM itaibuka na asilimia 88 badala ya ile ya 71% ambayo wengi wanaona ilikuwa imechakachuliwa na hivyo kutowatendea haki watanzania.
La kushangaza, Kinana hakuelezea ni vipi majimbo yaliyo ndani ya mikoa yawe hayakujumuishwa kwenye utafiti huo. Hivyo, alishindwa kuthibitisha hoja yake ni vipi CCM ilikuwa imeathirika na utafiti huo wa REDET iwe ya kimikoa au ya kimajimbo.
Vilevile, Kinana alikuwa bubu juu ya inakuwaje Dr. Slaa awe ana mvuto mkubwa kwa wananchi kwenye kampeni zake lakini asiweze kuwa anakubalika kuliko JK ambaye watu huenda kwenye mikutano yake kusikiliza burudani za kizazi kipya.