Killings in custody

Katika msako wake baba yule akabahatisha kuzikuta pesa zile kwenye begi la nguo za Mussa.

Zilikuwa bideni zipatazo 31,500
Mbona unatuchanganya Sasa, hizo 31,500 si zilichukuliwa nusu kwenda kubadilishwa mjini, zinabaki vipi tena 31,500 ?
 
Askari Polisi wa Tanzania mikono yao imejaa damu ya Watanzania wenginwasio na hatia kabisa
Mimi siku zote huwa nalaumu sana mfumo uliopo kwenye vituo vya police wa kuingiza na kutoa watuhumiwa. Hivi inashindikanaje vituo vya ma wilayani au vituo vikuuu kutumia mfumo wa Komputa with special programs za kipolisi kum sajili mtuhumiwa? Mfumo ambao mhalifu ataingizwa records zake zote, namba ya NIDA, vitambulisho vingine, picha yake na finger prints? Details za aliyemkamata, makosa yake nk? Na hii ingekuwa connected kwenye server ya HQ na Mkoani. Hii ingefanya watu washindwe kuwabambikia wengine kesi. But it seems for some reasons huu mfumo hautakiwi kabisa.
 
Naanza kwa kunukuu Barua ya rais Mstaafu Ally Hassan Mwinyi (Kipindi akiwa ni waziri wa mambo ya ndani), aliyomwandikia Rais Julius Nyerere kumtaarifu nia yake ya kujiuzuru baada ya mauaji ya wananchi mikononi mwa polisi Mwanza na shinyanga Mwaka 1977

“Polisi ni chombo cha kulinda amani,mali na maisha ya watu wake. Si chombo cha kuwaua.”

“Pia polisi ni chombo cha kuhifadhi na kudumisha usalama na haki. Si chombo cha kudhulumu, kuonea na kuwatesa wananchi wale wale wanaogharamia kukiweka”

Barua inaendelea

“Kwa bahati mbaya,maovu kama haya ndiyo haswa yalitendwa na vyombo vya serikali huko mikoa ya Shinyanga na Mwanza”

Mwinyi akaendelea
emoji116.png


“Kijinai, mimi binafsi nisingehusika kwani sikushiriki wala sikushauri, Sikuagiza wala kuelekeza mambo yale yafanywe kama hivyo yalivyofanywa”

Mwinyi akaonyesha uungwana
emoji116.png


“Hata hivyo,kisiasa nakiri kuwa nahusika. Siwezi kukwepa kwa sababu dhamana yangu ya uwaziri inaambatana na wajibu unaonitaka nijue yanayotendeka wizarani na pia niweze kudhibiti na kuhakikisha mwenendo mwema wa Jeshi la Polisi.”

Mwinyi akanukuu msaafu
emoji116.png


“Msaafu unatuusia kwa kusema “WALA HATABEBA MZIGO WA MWINGINE”

“Kisiasa MZIGO HUU NI WANGU NA NAKUBALI KUUBEBA KWANI HAKUNA MWINGINE WA KUUBEBA”

Then Mwinyi threw the towel
emoji116.png


“Kwa hiyo,Mwalimu nakuomba mambo matatu.Kwanza naomba radhi mimi nafsi yangu na pia naomba radhi kwa niaba ya askari wote wema walipo. Pili naomba vilevile uelewe sehemu yangu katika kosa hili.Tatu kwa fedheha hii,naomba unikubalie kujiuzuru”.

Mwinyi akawa amemaliza barua yake.
Nitaendelea kumuheshimu Mzee Ruksa. Allah amuongoze katika njia iliyonyooka yeye na sisi, amsamehe makosa yake, amuongezee umri na ampe siha njema.

Nampenda sana Mzee Ruksa kwa ajili ya Allah.
 
A THREAD BY FORTUNATUS BUYOBE

KILLINGS IN CUSTODY

Hit me!

Jab Me!

Make me say I did it.

When you pour Cold water on me,

I’ll Sign the Paper.





This is a two in one Thread

Yes!

Huu ni Uzi wenye mikasa miwili

Naanza kwa kunukuu Barua ya rais Mstaafu Ally Hassan Mwinyi (Kipindi akiwa ni waziri wa mambo ya ndani), aliyomwandikia Rais Julius Nyerere kumtaarifu nia yake ya kujiuzuru baada ya mauaji ya wananchi mikononi mwa polisi Mwanza na shinyanga Mwaka 1977

“Polisi ni chombo cha kulinda amani,mali na maisha ya watu wake. Si chombo cha kuwaua.”

“Pia polisi ni chombo cha kuhifadhi na kudumisha usalama na haki. Si chombo cha kudhulumu, kuonea na kuwatesa wananchi wale wale wanaogharamia kukiweka”

Barua inaendelea

“Kwa bahati mbaya,maovu kama haya ndiyo haswa yalitendwa na vyombo vya serikali huko mikoa ya Shinyanga na Mwanza”

Mwinyi akaendelea

“Kijinai, mimi binafsi nisingehusika kwani sikushiriki wala sikushauri, Sikuagiza wala kuelekeza mambo yale yafanywe kama hivyo yalivyofanywa”

Mwinyi akaonyesha uungwana

“Hata hivyo,kisiasa nakiri kuwa nahusika. Siwezi kukwepa kwa sababu dhamana yangu ya uwaziri inaambatana na wajibu unaonitaka nijue yanayotendeka wizarani na pia niweze kudhibiti na kuhakikisha mwenendo mwema wa Jeshi la Polisi.”

Mwinyi akanukuu msaafu

“Msaafu unatuusia kwa kusema “WALA HATABEBA MZIGO WA MWINGINE”

“Kisiasa MZIGO HUU NI WANGU NA NAKUBALI KUUBEBA KWANI HAKUNA MWINGINE WA KUUBEBA”

Then Mwinyi threw the towel

“Kwa hiyo,Mwalimu nakuomba mambo matatu.Kwanza naomba radhi mimi nafsi yangu na pia naomba radhi kwa niaba ya askari wote wema walipo. Pili naomba vilevile uelewe sehemu yangu katika kosa hili.Tatu kwa fedheha hii,naomba unikubalie kujiuzuru”.

Mwinyi akawa amemaliza barua yake.

Naiita barua hii kama barua ya kiungwana na ya Kihistoria.

Ni barua pekee ya Kiongozi wa Taifa letu aliyejiuzuru huku akikubali makosa bila kumtupia mzigo mtu mwingine.

Barua hiyo ilifuatiwa na kustaafishwa kwa manufaa ya umma, Director wa Tiss, Mzena, IGP, Pundugu, na maofisa kibao.

Mtiti huu ukahamia Mwanza kulikotokea vifo vya watuhumiwa wawili wa mauaji ya vikongwe, Masanja Makhula Mazengenuka na Issack Mwanamkoboko.

RC wa Mwanza, Peter Kisumo,
RSO Andrew Mayalla, DSO Ihuya, RPC Mkwawa, na OCD, wakastaafishwa kwa manufaa ya umma, kisha wakapandishwa kizimbani kwa Kesi ya Mauaji Mwanza. Washitakiwa wote walikutwa na hatia, isipokuwa Andrew Mayalla aliyekuwa akitetewa na wakili Murtaza Lakha.

Je Tangu mwaka 1977 mpaka leo, ni matukio mangapi yametukia kwa watu kuuwawa wakiwa mikononi mwa polisi?

Je, alishawajibika kiongozi yeyote wa kisiasa?

Alishawajibishwa kiongozi yeyote kwa ngazi ya RPC, RSO, RCO nk?

Sasa nakukaribisha katika uzi huu kuyaangazia matukio mapya

Sheria inasema

“When a person in in trusted as a custodian of a suspect or convict. He or she will be liable of anything that might befall to that suspect /Convict”

Kwa tafsiri isiyo rasmi maneno hayo yanamaanisha”

“Mtu aliyeaminiwa kumshikilia mahabusu au mfungwa atawajibika kwa lolote litakalomtokea mahabusu au mfungwa wakati yuko chini ya uangalizi wake”

Tuendelee

Nianze na mkasa wa kwanza

Mkuu wa gereza la Liwale mkoani Lindi alikuwa amesafiri kikazi kwenda mkoani Dar Es salaam.

Huko nyuma katika gereza lake kukawa kuna kazi ya kuvuna mahindi katika shamba la gereza.

Wafungwa wakifanya kazi hiyo chini ya usimamizi wa askari Magereza

Baada ya kuvuna ikafata kazi ya kusomba mahindi hayo kupeleka kwenye ghala la gereza na mengine yalipaswa kupelekwa nyumbani kwa Bwana jela ACP Gilbert Sindani ambaye kwa wakati huo alikuwa safarini Dar es salaam.


Mkuu wa gereza akiwa bado yuko Dar es salaam akapigiwa simu na “vichomi” wake kuwa katika mahindi yake yaliyovunwa kuna mengine yameibiwa.

Mkuu wa gereza akarudi Liwale.

Akamuita msaidizi wake na kumhoji juu ya taarifa mahindi yake kuibiwa.

Msaidizi akakubali ni kweli tuhuma hizi amezipata lakini bado hajazichunguza hivyo bado hakuna yeyote aliyetuhuniwa kuiba mahindi au kupokea mahindi ya wizi.

Taarifa hii haikumridhisha mkuu wa gereza.


Kesho yake tarehe 8 june 2022 Mkuu huyu akawaita Nyampala wa gereza pamoja na “Kiherehere” wake,

Usishangae ndugu msomaji,

Kiherehere ni cheo gerezani na huyu huwa ni mpambe wa Nyampala na muda wowote anaweza kupanda cheo kuwa Nyampala.

Nyampala alikuwa ni mfungwa namba 70/2020 ABDALAH NGATUMBALA

Kiherehere alikuwa ni mfungwa namba 76/2021 SIABA MBONJOLA

Hawa wote waliitwa na mkuu wa gereza na kuhojiwa akiwataka wampe taarifa kamili juu ya wizi wa mahindi yake.

Wawili hawa wakakana kujua lolote.

Baada ya majibu hayo Palepale Mkuu wa gereza akaanza kuwapiga akiwataka wamtaje aliyechukua mahindi na amechukua kiasi gani.

Alipochoka Mkuu wa gereza akawaita askari wawili;

1.SGT.YUSUPH SELEMANI

na

2.CORPORAL FADHILI MAFOWADI

wamsaidie kuwapiga hadi watakapotaja wezi

Kipigo hicho hakikuwafurahisha askari wengine ambao waliwazuia Sajenti Yusuph na Koplo Fadhili wasiendelee kuwapiga, wakihoji iwapo wana uhakika kweli kuna wizi umetokea?

Wengi waliamini kuwa uchache wa mavuno ya mwaka huu ndiyo sababu ya kudhani kwamba wizi umefanyika.

Mkuu wa gereza alipobaini kuwa wafungwa wale wameumizwa sana, akaondoka.

Muda mfupi baadaye akarudi na kuwapakia kwenye gari kuwapeleka hospitalini hospitali ya wilaya Liwale.

Pale hospitali kwa kuwa walipelekwa wakiwa na hali mbaya madaktari wakashauri kwanza wapatiwe Form ya polisi namba 3 PF3 ndio waendelee na matimabu.

Wakati haya yanaendelea mmoja ya Wagonjwa alimfahamu Nyampala Ngatumbara

Akampigia simu ndugu yake aitwaye SAID MOHAMED

Baadaye madaktari wakabaini kuwa tayari Nyampala Ngatumbala alikuwa amekwisha kufariki dunia.

Na kwa kuwa hali ya kiherehere ilizidi kuwa mbaya wakamwandikia rufaa akimbizwe hospitali ya Mifupa Moi

Ndugu wa Nyampala akiambatana na diwani wao Nassoro wakaenda hospitali ya liwale lakini wakazuiwa kumuona mgonjwa wao (marehemu) bila ya kibali cha mkuu wa gereza.

Wakampigia simu Mkuu wa wilaya aliyewataka waende ofisini kwake.

Walipofika Mkuu wa wilaya akawaeleza kuwa tayari ana taarifa hizo na kwamba ameshawasiliana na mkuu wa Mkoa ili atume timu kuchunguza sakata hilo.

Kesho yake Mkuu wa gereza akawapigia simu diwani na ndugu wa marehemu waende Kipute (liliko gereza la Liwale)

Walipoenda wakamkuta Mkuu wa gereza akiwa na Mkuu wa gereza wa mkoa wa Lindi (RPO)FELSCHEME MASSAWE

Mbele ya RPO mkuu wa gereza akawaeleza kuwa ndugu yao amefariki kutokana na maradhi ya shinikizo la damu.

Ndugu hawakuridhika na maelezo hayo ambapo wakaomba postmortem ifanyike

Ripoti ya daktari ikabainisha kuwa marehemu alikuwa kavunjika mguu mmoja, mshipa wa nyuma wa mguu mwingine umechanika huku damu ikiwa imeganda maeneo ya mikononi.

Ripoti ikahitimisha kuwa marehemu alifariki kwa kipigo na sio shinikizo la damu.

Mfungwa huyo aliyeuwawa alikuwa akitumikia kifungo cha miaka mitano tu jela baada ya kukutwa na hatia ya kukamatwa na nyama pori ya nguruwe.

Lakini askari hao wakaamua kubadilisha adhabu yake kugeuka kuwa ya kifo.

Mfungwa huyo aliyeuwawa alikuwa akitumikia kifungo cha miaka mitano tu jela baada ya kukutwa na hatia ya kukamatwa na nyama pori ya nguruwe.

Lakini askari hao wakaamua kubadilisha adhabu yake kugeuka kuwa ya kifo.

Katika nusa nusa ndipo ikabainika kuwa Mfungwa huyu aliuwawa kwa bahati mbaya tu Wakati watu wakitaka kutekeleza visasi vyao.

Nanukuu

“Kuna watu ambao Mkuu wa Gereza hapatani nao. Kuna askari anawatafutia sababu awafukuzishe kazi. Ni bahati mbaya kuwa askari hao hawakutajwa na Marehemu Ngatumbara na mwenzake,”

Quoted from a source within, under anonymity conditions

Hili sio tukio la kwanza kwa mfungwa kufia mikononi mwa askari Magereza.

Mwaka 2010 Mfungwa namba 214 Khassim Kumchaya aliuwawa na askari wanne mwenye namba B 5147 WDR Swalehe, A 854 Sajenti Mohamed, 4264 Sajenti Jason aka Machozi na askari mwenye namba A 5294 Sajenti Shaibu.

Mfungwa huyu aliuwawa katika gereza la Lilungu mkoani Mtwara.

Mwaka 2019 askari wa gereza la Kilombero walimuua mfungwa Basiri Makungu.

Mnahisi nimemaliza?

Hapana ndio naanza!

Sasa Nageukia tukio la mauaji ya Kijana mfanyabiashara wa madini aliyeuwawa na Polisi mkoani Mtwara.

Ilikuwa hivi;

Mussa Hamisi alikuwa akijishughurisha na biashara ndogo ndogo ikiwemo kuuza mitumba katika kijiji cha Luponda wilayani Nachingwea mkoani Lindi.

Baadae Mussa akaondoka kijijini Luponda Kwenda kwenye machimbo ya dhahabu kijiji cha Mpiruka B hukohuko Nachingwea.

Mungu amtupi mja wake na penye nia pana njia.

Mwezi october 2021 Mussa akapata bahati ya kengewa baada ya shimo lao kutema.

Baada ya kusafisha dhahabu musa akapata dhahabu ya kutosha kubadili maisha yake.

Madalali wakamuunganisha Mussa na mnunuzi wa dhahabu yake raia wa kigeni

Kweli biashara ikafanyika!

Mussa akiibuka na kiasi kikubwa cha pesa ambayo hakupata kuiota.

Naam!

Alilipwa kiasi kikubwa cha dola za Kimarekani yapata 31,500 usd

Ukikileta kikwetu kwetu ni sawa na milioni 74 na ushee.

Musa akaondoka machimboni na kurudi kijijini kwao Luponda.

Kule akamnunulia mama yake Battery Solar na Inverter

Kichwani akipanga kupabadilisha kabisa pale nyumbani kwao.

Akaficha nusu ya pesa ile pale nyumbani.

Akaondoka na nusu ya pesa kwenda kuibadilisha Mtwara mjini.

Alipofika Mtwara akamjulisha mjomba wake aitwaye SALUM NG’OMBO kuwa yuko Mtwara.

Huyu mjomba wake alikuwa ni dalali wa kwenye mabasi akifanyia kazi yake kituo cha mabasi MKANALEDI pale pale Mtwara Mjini.

Mussa alamjuza sababu ya ujio wake na akamuomba amsindikize kwenda Bank

Wakaona benki ya BMN (code) ndiyo ingefaa kutumika kubadilisha Biden kuwa Samia.

Mussa akazama BMN bank Mtwara

Pale Bank akahudumiwa na mdada flani hivi

Biden wakageuka Samia kama milioni 30 hivi

Baada ya kubadili yule dada akamuuliza anaishi wapi?

Mussa akasema kuwa anaishi Nachingwea na anapanga kuondoka siku ile ile.

Mdada akamshauri kuwa sio salama kusafiri na pesa ile kuwa kuwa muda umeenda.

Akamshauri aende nyumba ya wageni aliyomtajia ili kesho mapema arudi Nachingwea

Mussa Akakubali kiroho safi


Jioni Mussa akatoka kujivinjari na akaenda kwenye Club maarufu pale Mtwara Kama Triple V

Sasa hapa ndipo ndugu msomaji inabidi nirudie kauli moja ambayo niliwahi kumnukuu Kachero mmoja wakati “tunabadilishana kahawa”

Nanukuu

“Makachero huwa tunavutiwa sana na mtu anayekunywa “bia msitu” awapo bar... Sio kwamba tunamuonea wivu.. Hapana! Bali huwa ni msingi mkubwa wa kuanza kuwa suspicious kutaka kujua anafanya kazi gani inayompa kipato cha kunywa “bia msitu””.

Hapa bia msitu anamaanisha ile tabia ya kuagiza vinywaji vingi kwa wakati mmoja na kutapanya kwenye meza huku ukitoa offer kwa wanaokuzunguka”

Ndicho alichokifanya Mussa pale Club

This was his grave mistake

What a coincidence!

Ilitokea kuwa pale Club yule mhudumu wa Bank aliyemhudumia Mussa naye alikuwepo.

Naam alikuwepo pale akipata kinywaji na jamaa yake mmoja ambaye ni “njagu”

Njagu huyu alikuwa meza moja na yule mhudumu pamoja na manjagu wenzake.

Hivyo wakati Mussa anamwagilia Moyo kwa “bia msitu” na wakati manjagu wale wanavutiwa naye walianza kumjadili mbele ya yule Mhudumu.

Mhudumu bila kujua akasema Mussa ana kisu cha kutakata kwani ni yeye alibadili pesa zake.

Akasema anatokea Nachingwea na Lodge aliyofikia

Naam!

Mhudumu akawaambia Mussa amefikia SADINA hotel

Mhudumu aliyasema yale “in good faith” bila kujua kama anauza ramani ya vita kwa wale manjagu.

Mussa akaondoka muda ukiwa umeenda sana kurudi lodge kwake.

Bila ya kujua tayari kuna manjagu yamemuundia mkia.

Majira ya saa 7 kwenda saa 8 usiku Mussa akashangaa mlango wa chumba chake unagongwa kwa fujo.

Alipofungua wakaingia watu waliojitambulisha kuwa wao ni polisi na yuko chini ya ulinzi.

Alipouliza kosa lake hakutajiwa akaambiwa anahitajika kituoni.

Manjagu wakasachi chumba chake lakini wakaishia kukuta milioni 2.5 pekee.

Hii haikuwaridhisha!

Wao walikuwa na story nzima kutoka kwa mhudumu wa benki kuwa Mussa kaondoka na kiasi gani.

Walikuwa wanajua pia kuwa Mussa alibadili kiasi tu cha pesa kati ya pesa aliyokuwa nayo.

Mussa alipohojiwa kilipo kiasi kingine alikana kabisa kuwa na pesa nyingine.

Mussa seemed to be a very brave young boy.

He might have hidden the rest of the “package” somewhere within his room.

Mussa alipokaidi akachukuliwa na kupelekwa korokoroni Mtwara Central police.

Sasa unajua mtu anapoingia kituoni ni lazima aandikwe kwenye Detention Register kuwa anaingia ndani kwa kosa gani.

Askari wale wakaandika kuwa Mussa anashikiliwa kwa kosa la Wizi wa pikipiki.

Musa akalala korokoroni siku hiyo.

Sasa msomaji inabidi uelewe kitu kimoja,

Kulala korokoroni usiku mpaka asubuhi sio issue

Issue ni kuwa ikifika kesho yake asubuhi mpaka mchana swala lako linakuwa nje ya waliokukamata.

Swala linaanza kupata “nzi” wengi kwani mwenye kituo “OCS” ni lazima ajue umeingiaje.

Ukiacha “OCS” mwingine ambaye ni lazima ajue ni mkuu wa upelelezi “OC- CID” na lazima mkuu wa polisi wa wilaya OCD lazima ajue idadi ya mahabusu wake wilayani ili aweze kutoa ripoti kwenye “morning brief” kwa mkuu wa wilaya ambaye ndiye Mwenyekiti wa kamati ya usalama wilayani.

So mpaka inafika kesho yake asubuhi Swala la Mussa lazima tayari lilishafika kwenye Meza za vigogo wa polisi niliowataja.

(Save for the DC kwani yeye anaweza kupewa “fabricated infos)

Lakini niliowataja kwa nyadhifa zao ni lazima walipata taarifa toka kwa wakamataji na Mussa.

Ni kwa sababu Mussa asingeendelea kukaa ndani bila maelezo yake kuchukuliwa.

Na ni lazima Mussa alijitoa kwenye kesi ya wizi wa Pikipiki na akaeleza uhalisia kuwa yeye ni nani, anatokea wapi, na kafata nini Mtwara hadi kuishia korokoroni.

Tuendelee

So wale wakamataji wakawashirikisha wakubwa wao kuwa issue ya Mussa inaweza kuwafanya waibuke na “donge nono”

Swala hili likawavutia wakubwa wale.

Wakubwa wakaona wa “adjust” vipimo vya kumuhoji Mussa

Then they started to “forgive” Mussa mpaka aseme pesa nyingine ilipo.

After a severe “forgiveness” Mussa akataja alipoficha pesa nyingine SADINA lodge.

Manjagu walipoenda kweli wakakuta pesa ikiwa imefichwa kwenye dari ya choo kwenye chumba alichokikodi Mussa.

What a Bingo!

Sasa manjagu wale wakaanza kuamini Story ya yule mfanyakazi wa Bank kuwa Mussa alimweleza kuwa anabadili nusu na pesa na nyingine angeenda kubadili sometimes afterwards.

Sasa bingo ikawa utamu kolea!

Wakapata hamu kwenda kuzifata Nachingwea.

Lakini kikaibuka kikwazo!

Yes kikwazo!

Wanaenda Vipi kufanya kazi wilaya nyingine huku wao wanatokea wilaya nyingine?

Wakaona hiyo haiwezekani without prior notice of RCO na RCIO

Ndio!

Wasingeweza kwenda bila kumjulisha mkuu wa Upelezi na Mkuu wa intelejensia wa Mkoa.

“Nzi” wakaongezeka kwenye chain


Naam!

Ilibidi hawa nao wafahamu swala la Mussa kinaga ubaga kama kweli wanazitaka zile pesa.

Baada ya watu hawa kuwekwa sawa na baada ya mussa kuwa ametepeta wakapiga simu Nachingwea.

Namba ya simu wasingeipata kokote zaidi ya kuitoa kwa Mussa.

Namba ile ilikuwa ni ya Mama yake Mussa

Ndugu Msomaji, nakurudisha nyuma kidogo

Yule mjomba wake Mussa anayefanya kazi kituo cha mabasi cha MKANALEDI pale Mtwara alishangaa ukimya wa mpwa wake tangu jana yake.

Huku akiwa hapatikani kwenye simu.

Katika jitihada za kumtafuta ndio akawa ameenda hadi kituo cha polisi kumuulizia kama labda alikamatwa kwa shida yoyote.

Hisia zake zikazaa matunda.

Akabaini Mussa yuko pale kituoni kwa siku mbili nzima.

Akaambiwa kesi ya Mussa ni nzito ya wizi wa pikipiki so hawezi kumuona.

Kipindi hicho namba ya Mama wa Mussa imeshachukuliwa.

Yule mjomba wake akamtafuta mzee mmoja maarufu kwa jina la Ng’itu asaidie kumnusuru mpwa wake

Kweli yule mzee akampambania Musa lakini huku akifata anayoelekezwa na wale Manjagu.


Siku ya tatu toka Mussa ashikiliwe Manjagu wakampa yule Mzee namba ya Mama Mussa aitwaye Hawa Ally ili aipige na walishamwambia cha kusema.

Yule mzee akampa maelezo mama yule kuwa Mussa amekamatwa na inahitajika shilingi laki tatu kwa ajili ya dhamana.

Mama wa watu na mmewe(Baba wa Mussa wa kufikia) wakajichanga wakatuma ile laki tatu ili kumsaidia Mussa apate dhamana.

Hawakuuliza sababu ya kukamatwa kwake

Wao walichojali ni mtoto wao awe huru.

Wakamnunulia Mussa Uhuru tunaoambiwa ulishapatikana mwaka 1961

Let’s pause at this juncture ndugu msomaji.


just imagine,

Hawa manjagu tayari walishapata pesa nyingi tu kutoka kwa Mussa pale Mtwara mjini.

Lakini hawakuridhika!

Wakamkamua pia mama wa watu shilingi laki tatu.

With due respect, these cops were animals.

Tuendelee

So baada ya muda Mzee yuleyule akapiga simu na kumwambia kuwa Mussa ameshaachiwa.

Lakini,

Mzee yule akamwambia Mama Mussa kuwa kwa mujibu wa maelezo ya Mussa ameeleza kuwa ana pesa nyingine kaacha kule nyumbani so polisi wanaenda kuzifata.

Baada ya simu ile baba wa kambo wa Mussa akaona ule ni ushenzi,

Akaingia kwenye chumba cha Mussa na kuanza kusaka pesa zile popote zilipo.

Nia yake ilikuwa azichukue azifiche ili polisi wakifika wasizikute.

Katika msako wake baba yule akabahatisha kuzikuta pesa zile kwenye begi la nguo za Mussa.

Zilikuwa bideni zipatazo 31,500

Mzee akahamisha pesa zile na kuzificha anakopajua.

Mida ya jioni Polisi kutoka Mtwara wakafika na gari lao Nachingwea nyumbani kwa kina Mussa.

Naam!

Walikuwa wameambatana na Mussa akiwa kapigwa pingu chini ya ulinzi mkali kama wamekamata gaidi hatari.

Ukiwaona unaweza kusema wako serious kumbe wako kwenye armed robbery.

The people we entrusted with our lives and properties, were now conspiring and executing armed robbery shamelessly in a broad daylight.

Mussa akashushwa garini

Wazazi wake wakishangaa kulikoni

Manjagu wale hawakuwa na maneno mengi wakawataka wazazi wale wajitambulishe.

Wazazi wale wakasema wao ndio baba na mama wa “gaidi” aliyepo mbele yao.

Funny but not funny

Manjagu wake wakasema wako pale kwenye mission moja tu ya kuhakikisha Mussa anawaonyesha alikoacha fedha nyingine pale nyumbani.

Nafikiri manjagu wale walikuwa kwenye zoezi la malezi wakiwasaidia wazazi wake kumlea Mussa.

Labda waliona kwa umri wake hapaswi kuwa na fedha zile kwani zingeweza kumharibu kwenye makuzi.

Kweli Mussa alikuwa Mdogo,

Mussa alizaliwa mwaka 1996

Basi bwana Mussa akaingia kwenye chumba chake huku akiwa chini ya ulinzi.

Akaongoza moja kwa moja kwenye begi lake la nguo alikokuwa kaacha pesa zile.

Musa akabaki na mshangao kama anasoma talaka baada ya kuzikosa pesa zile!

Akawaambia manjagu kuwa aliziacha pale lakini anashangaa hazipo.

Wale manjagu wenye njaa kama wametoa mimba hawakutaka kuelewa lolote.

Njagu mmoja akamulekezea Mussa bunduki kisogoni na kumwambia asilete mzaha kwani atakuwa anaiweka roho yake kwenye kamali kwa dau dogo.

Sura za manjagu wale zilikuwa mbali kabisa na masikhara na yote haya yalifanyika huku wazazi wa Mussa wakishuudia.

Uchungu wa mwana aujuaye Mzazi!

Mama Mussa akapiga magoti kuwasihi manjagu wale wasimzuru mwanae.

Mama akaanza kuropoka huku akimwambia mmewe awaonyeshe pesa ziliko.

Akasema mmewe ndio alizihamisha ili kunusuru nafsi ya mwanae.

Dear reader,

Despite the fact that it is me who is jotting down this thread, this captivating and hollow scene didn’t exonerate me from sobbing.

Naomba nimnukuu Mama Mussa

“Wakamuuliza hela umeweka wapi, akasema kwenye begi, wakamuonyesha bunduki, maana walikuja na bunduki. Kwa hiyo kwa kuona mimi nina uchungu wa mtoto wasimpige wasimuue wakati mimi niko pale, ndipo nikamwambia (mume wangu) katoe hela uwape. Ndipo wakapewa, wakazichukua wakawa wanazihesabu, mimi nilikuwa nalia kwa sababu ya uchungu, mtoto ametiwa pingu.”

Polisi walipozipata pesa zile hawakuridhika.

Wakaanza kuangalia chochote chenye thamani pale nyumbani kwa kina Mussa.

Wakaona battery ya solar na Inveter ndio vyenye thamani navyo wakavibeba.

Vitu hivi Mussa alikuwa amemnunulia mama yake baada tu ya kupata pesa zake.

Lakini navyo vikabebwa.

Njaa! Njaa! Njaa!

Kama watoto wa Mamba.

Si unajua mtoto wa mamba hanyonyi?

Baada ya kupata bingo kwa mara ya pili manjagu wale wakamrudisha Mussa kwenye gari lao kisha wakamchukua na baba yake aliyekuwa ameficha pesa zile wakisema anaenda kuisaidia polisi wakaenda nao Kituo cha polisi Nachingwea.

Pale Kituoni wakamwacha yule mzee arudi kijijini bila hata nauli.

Hata kazi ya kuisaidia polisi hawakumpa tena kama walivyoahidi.

Kisha gari ikaunganisha mpaka Kituo cha polisi Mtwara wakiwa na Mussa.

Pale kituoni Mtwara manjagu wakamwambia Mussa kosa lake ni kukutwa na Dola za Marekani.

Lakini wakamkataza kutangaza suala hilo.

Badala yake wakampa kesi ya wizi wa pikipiki.

Wakamruhusu aondoke na wakampatia laki Moja kama “chenji” ya kukutwa na kosa la kumiliki dola wakati yeye ni mmatumbi.

Akaambiwe asionekane pale mjini na arudi tarehe 6 Nov kuangalia status ya kesi yake.

Mussa akarudi Nachingwea akiwa na laki moja tu akiwa kapauka.


Siku hazigandi,
Be blessed kaka
 
Nitaendelea kumuheshimu Mzee Ruksa. Allah amuongoze katika njia iliyonyooka yeye na sisi, amsamehe makosa yake, amuongezee umri na ampe siha njema.

Nampenda sana Mzee Ruksa kwa ajili ya Allah.
Na ndiyo maana Allah amempa afya njema na maisha marefu. Hakuna kitu muhimu kwenye maisha ya binadamu kama HAKI.
 
Maybe tatizo heading... (Maybe)
Mkuu wala usisumbuke kuhusu heading iko sahihi kabisa, hasa kwa mtu yeyote makini. Tatizo lililopo miaka hii ni watu kupenda kushabikia mambo ya hovyo hovyo. Ingekuwa hapa ile issue ya Masanja, mkewe na Katibu thread ingeshajaa watu. Yaani nimeusoma huu uzi several times na ku share na jamaa mpaka kikao hapa ofisini kimesimama kwa muda. Halafu kitu ambacho kinaumiza ni kwamba kijana wa watu kauwawa kwa milioni nearly 80, na kwa jinsi hiyo chain ilivyo ndefu labda aliyepata nyingi ni milioni 6 au 7. Pia it seems polisi hawajifunzi maana tukio la akina Zombe na wenzake na wale vijana wa madini wa Mahenge lilikuwa hivi hivi.
 
ni vp uzi kama huu umepata wasomaji wahache, umefichwa au?
Watu si wanapenda sana mambo ya kipuuzi kupuuzi mkuu? Weka hapa msanii kafumaniwa utaona uzi utakavyokimbia.. Pia kingine ambacho nimejifunza, hasa hasa uhasama ulioanzia kwenye siasa za awamu ya tano, ni kwamba watu wanaona mwenzao kufanyiwa unyama na kupotezwa ni jambo la kawaida tuu... Yaani nowadays ni kawaida kusikia vijana kwenye majukwaa wakijiapiza kuwashughulikia/kuwapoteza wenzao. Akina Sabaya walitesa sana wenzao mpaka kuwatia vilema but kuna watu wanawaona ni mashujaa na role models.
 
Mimi siku zote huwa nalaumu sana mfumo uliopo kwenye vituo vya police wa kuingiza na kutoa watuhumiwa. Hivi inashindikanaje vituo vya ma wilayani au vituo vikuuu kutumia mfumo wa Komputa with special programs za kipolisi kum sajili mtuhumiwa? Mfumo ambao mhalifu ataingizwa records zake zote, namba ya NIDA, vitambulisho vingine, picha yake na finger prints? Details za aliyemkamata, makosa yake nk? Na hii ingekuwa connected kwenye server ya HQ na Mkoani. Hii ingefanya watu washindwe kuwabambikia wengine kesi. But it seems for some reasons huu mfumo hautakiwi kabisa.
Mkuu tayari umeshayasahau ya "Lugumi", mbona ni juzi juzi tu?
 
Back
Top Bottom