Chaimaharage
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 211
- 78
Kutokana na hali ilivyo sasa ni bora wapenda mabadiliko wakaanza maandalizi mapema ili kukabliana na udhalimu ambao umeanza kujitokeza. Msidhanie walioficha mabilioni ya pesa Uswiss na maovu mengine watakuwa tayari kuona utawala unao walinda uanguke. Wako radhi hata kumwaga damu ili maslahi yao yasihujumiwe. Wanajua mkono wa sheria utakuwa juu yao baada ya anguko la utawala ambao wanatumia udhaifu wake kujikita mizizi ya unyonyaji.
Kutegemea sanduku la kura pekee halita tosha, ni budi kufanya maandalizi zaidi kuondoa udhalimu kwa sababu vyombo vya ulinzi na mahakama mwelekeo wake siyo mzuri. 2010 bilashaka mlishuhudia tume ya uchaguzi madudu iliyofanya. Mpaka tunafika 2015 hali itakuwa mbaya sana kwa wanaounga mkono M4C. Nchi yetu tunako elekea siyo muda mrefu tutaanza kushuhudia matukio ya ugaidi. Matukio ya aina hii hufanywa kama tunavyo shuhudia kwenye nchi nyingine na watu ambao wameona maisha hayana thamani tena kutokana na ugumu na kupoteza matumaini na wako radhi kujitoa mhanga ili kutetea haki za wanyonge.
Kutegemea sanduku la kura pekee halita tosha, ni budi kufanya maandalizi zaidi kuondoa udhalimu kwa sababu vyombo vya ulinzi na mahakama mwelekeo wake siyo mzuri. 2010 bilashaka mlishuhudia tume ya uchaguzi madudu iliyofanya. Mpaka tunafika 2015 hali itakuwa mbaya sana kwa wanaounga mkono M4C. Nchi yetu tunako elekea siyo muda mrefu tutaanza kushuhudia matukio ya ugaidi. Matukio ya aina hii hufanywa kama tunavyo shuhudia kwenye nchi nyingine na watu ambao wameona maisha hayana thamani tena kutokana na ugumu na kupoteza matumaini na wako radhi kujitoa mhanga ili kutetea haki za wanyonge.