Kete Ngumu
JF-Expert Member
- Nov 21, 2014
- 6,644
- 6,830
Serikali au Wizara husika angazieni kwa kufuatilia uhujumu uchumi unaoendelea katika soko kubwa kabisa Tanzania la Kariakoo.
Utaratibu ambao sio rasmi ila unafuatwa upo hivi, Kariakoo kwa mtu anaetaka kuanzisha biashara. Kwanza kuonana na madalali na kuwaambia unataka kufungua biashara gani ili wakutafutie kwenye eneo linaloendana na biashara yako, namaanisha kama unataka kufungua duka la kuuza jeans za kiume basi kuna maeneo ambayo wafanyabiashara wa aina hiyo wapo ili muende sawa kibiashara hasa katika kupata wateja.
Ukishapata fremu unaambiwa kuna KILEMBA, hii kilemba ni pesa utakayoitoa aidha kwa mfanyabiashara anaekuachia hiyo frem au kwa mwenye nyumba, kiasi cha chini kabisa cha fremu ni kuanzia milioni 20-30 fremu za ndani na milioni 30-80 kwa fremu za nje yaani fremu zinazotizamana na barabara.
Pointi yangu ni hii, siku hizi kumeibuka wimbi la wenye nyumba kuwaondoa wafanya biashara wote katika nyumba kwa kigezo cha kukarabati nyumba na kutangaza KILEMBA kipya kwa anaetaka kurudi kwa uwiano wa hisabu ya kilemba ilioainishwa hapo juu.
Ikumbukwe kilemba sio kodi ya pango, unalipa kilemba na kodi ya pango unalipa. Wafanyabiashara wengi wameathirika na hili na wengine wamezifunga kabisa biashara zao kwa kushindwa kulipa kilemba kipya na kodi mpya kwa wakati mmoja.
Nyumba mbili zilizopo mtaa wa Raha na Mchikichi moja ilijengwa upya nyingine ikafanyiwa marekebisho kidogo tu na watu wote hao wakaumizwa.
Nyumba moja yenye underground inaweza kuwa na fremu zaidi ya 60 sasa ukizidisha kwa kilemba tu cha milioni 20 mara 60 unaona kabisa hawa wenye nyumba au wanaojiita wajenzi wanavyopata pesa nyingi kwa njia zisizo halali.
Serikali au wizara husika tafadhalini fuatilieni swala hili na hatua kali zichukuliwe kunusuru uchumi wa Taifa na familia kwa ujumla.
Utaratibu ambao sio rasmi ila unafuatwa upo hivi, Kariakoo kwa mtu anaetaka kuanzisha biashara. Kwanza kuonana na madalali na kuwaambia unataka kufungua biashara gani ili wakutafutie kwenye eneo linaloendana na biashara yako, namaanisha kama unataka kufungua duka la kuuza jeans za kiume basi kuna maeneo ambayo wafanyabiashara wa aina hiyo wapo ili muende sawa kibiashara hasa katika kupata wateja.
Ukishapata fremu unaambiwa kuna KILEMBA, hii kilemba ni pesa utakayoitoa aidha kwa mfanyabiashara anaekuachia hiyo frem au kwa mwenye nyumba, kiasi cha chini kabisa cha fremu ni kuanzia milioni 20-30 fremu za ndani na milioni 30-80 kwa fremu za nje yaani fremu zinazotizamana na barabara.
Pointi yangu ni hii, siku hizi kumeibuka wimbi la wenye nyumba kuwaondoa wafanya biashara wote katika nyumba kwa kigezo cha kukarabati nyumba na kutangaza KILEMBA kipya kwa anaetaka kurudi kwa uwiano wa hisabu ya kilemba ilioainishwa hapo juu.
Ikumbukwe kilemba sio kodi ya pango, unalipa kilemba na kodi ya pango unalipa. Wafanyabiashara wengi wameathirika na hili na wengine wamezifunga kabisa biashara zao kwa kushindwa kulipa kilemba kipya na kodi mpya kwa wakati mmoja.
Nyumba mbili zilizopo mtaa wa Raha na Mchikichi moja ilijengwa upya nyingine ikafanyiwa marekebisho kidogo tu na watu wote hao wakaumizwa.
Nyumba moja yenye underground inaweza kuwa na fremu zaidi ya 60 sasa ukizidisha kwa kilemba tu cha milioni 20 mara 60 unaona kabisa hawa wenye nyumba au wanaojiita wajenzi wanavyopata pesa nyingi kwa njia zisizo halali.
Serikali au wizara husika tafadhalini fuatilieni swala hili na hatua kali zichukuliwe kunusuru uchumi wa Taifa na familia kwa ujumla.