Kikwete azungumza na wazee wa Dar; ajiandaa kwa mgongano na TUCTA

Tulichagua sura (mvuto) na si busara na hekima ya kuongoza nchi. Hiaya ndo faida na matunda tunayoyapata sasa.
 
Mazungumzo ya mwisho yamefanyika tarehe 30 Mwezi April TUCTA walianzia kutaka kima cha chini kiwe 315,000 wakajadiliana kushusha TUCTA wakashusha kiwango serikali nayo ikakubali kupanda lakini hawakufikia kiwango cha TUCTA. Ndipo TUCTA wakashuka tena. Serikali ikasisitiza bado haiwezi kumudu kiwango hicho. Ndipo serikali na TUCTA wakakubaliana kutokubaliana. JK akasema ameshangazwa na kauli ya TUCTA kuendeleza kitisho cha mgomo. Huku akishangiliwa na umati wa watu, akiwabeza kibagamoyo. Bagamoyo kuwa hao wana lao jambo.
 
JK ameelezea kwa nini serikali imekataa kiwango cha 315,000 hakiwezekani kwa sababu zitahitajika Trilioni 6 kulipa mishahara ya serikali wakati mapato ya serikali ni Trilioni 5. Utapangaje mishahara mikubwa kuliko uwezo. Ameuliza tukakope?
 
Anaelezea kwa nini serikali haiwezi kutekeleza kiwango cha kima cha chini cha mshahara cha 315,000 eti kwa kigezo kuwa mapato ya serikali kwa mwaka ujao ni trilioni 5.7 wakati mishahara kwa kiwangu walichopendekeza tucta ni trilioni 6 na ushee hivyo malipo ya hiki kima cha chini hayatekelezeki.

Pia anaeleza kuwa TUCTA walipendekeza kima cha chini kwa 315,000 lakini baada ya mazungumzo na serikali walikubali kushuka chini mara mbili lakini walipotoka nje wakawaleleza wafanyakazi kuwa wameafikiana na serikali kiwango cha 315,000 hivyo TUCTA ni waongo na vigeugeu
 
Hotuba nimeanza kuisikiliza kati lakini naona topic muhimu anayozungumzia ni mugomo wa Wafanyakazi (watumishi, waajiliwa) kama ulivyotangazwa na TUCTA.

Sijui itaishia wapi lakini naona hapo alipo nimeshangaa. Kwanza ni choice ya audience yake, 'wazee wa Dar es Salaam' Kama ni wazee kwa maana ya siku zote naona kama siyo watumishi wa Serikali. Muenendo naona anatoa hotuba kwa washabiki (nilitegemea hili) maana wanashangilia hata bila sababu.

Baya ambalo sikutegemea, ni jinsi alivyoahidi kwamba wakigoma na kuandamana, watapigwa na polisi. Huyu ni Rais na naamini anafahamu nguvu ya maneno yake, Sijui ni kwa nini anaelekeza tendo kama hilo. Anazidi kusema Polisi watawaumiza. Kakumbusha uwezo wa polisi kuua kama ilivyowahi kutokea huko nyuma.

Ok, vyovyote itakavyokuwa ktk hotuba hii, binafsi sifahamu ni kwa nini hotuba za viongozi wetu hazitofautiani na zile za Mugabe. Tusubiri anakoishia.
Kumbe nilikuwa simjui vizuri sana huyu raia eeh!...Badala ya kujibu hoja unawatisha wananchi waliokuchagua kwa kutumia POLISI?...kWELI mvi SIO BUSARA!
 
Anasema kama ni kura zao TUCTA basi ashazikosa, atazipata kwa wengine
 
Anasema kwa kejeli kuwa hana haja na kura za wafanyakazi wanaodai ongezeko la kima cha chini cha 315,000 kwani serikali ya CCm haina uwezo wa kutimiza ahadi hiyo hivyo kura zao ndio amezikosa hivyo wakitaka wawapigie upinzani
 
Daa kweli watanzania tu wapumbavu,wanavyomshangilia Jk na hotuba yake wala siamni kam kweli wao ndio wazee wa Dar.Yaani wanamshangilia mpaka JK mumkari inampanda na kuzidi kubwabwaja kama yuko jukwaani vile.Lol
 
Anasema kwa kejeli kuwa hana haja na kura za wafanyakazi wanaodai ongezeko la kima cha chini cha 315,000 kwani serikali ya CCm haina uwezo wa kutimiza ahadi hiyo hivyo kura zao ndio amezikosa hivyo wakitaka wawapigie upinzani
Mkwere ni mkwere tu bana...Jasiri haachi asili...Huu ni ushakunaku wa juu kabisa!
In the first place, nani aliyesema tungempa yeye kura zetu, who the hell is he?...mburaaa!
 
Anasema Tanzania ina wafanyakazi takribani laki 3.5 kati ya Watanzania 45m hivyo hawezi kutumia mapato ya Watanzania wote kuwaridhisha wafanyakazi wachache hiyo ni DHULUMA. Wafanyakazi hata wakigoma bado mshahara hautapanda...kwani madai yao hayatekelezeki.
 
JK amesema atawashangaa sana watumishi wa serikali watakaogoma. Amesema kama wafanyakazi hawampigia kura kwa kuzikosa hizi 315,000 then wasimpigie kura, amebainisha yuko tayari kuzikosa kura hizo lakini Watanzania wengine wote watampa kura zake. Wajameni hii sasa ni pre-mature campaign, tena leo ;' anaongea with serious tone very convincing hata mimi naanza kumuona. JK is worth come back!.
 
basi kama amesema hivyo ni mpuuzi sana yaanii anawadharau tukta?

kwanza kesho si mwisho halafu tar 5 tuko bara barani

raisi ganni huyu?
 
Anasema Tanzania ina wafanyakazi takribani laki 3.5 kati ya Watanzania 45m hivyo hawezi kutumia mapato ya Watanzania wote kuwaridhisha wafanyakazi wachache hiyo ni DHULUMA. Wafanyakazi hata wakigoma bado mshahara hautapanda...kwani madai yao hayatekelezeki.

Kuhusu hela walizokalia mafisadi anasemaje?...
Asikwepe hoja..
Kwanini awaite wazee, ambao hawawezi kuhiji chochote?..kwanini asiitishe pressconference na kuruhusu maswali?..
Jibu ni..TOO MUCH USWAHILI!
 
kasema hana haja na kura za watumishi wa serikali na mgomo ni batili na kinyume na sheria
 
"Mgomo ni batili na kinyume cha sheria"=JK

Sheria ya ajira inaelezahaki za mwajiri na mwajiliwa
 
Mkwere ame-panic na anadhihirisha uwezo wake, ni muda mzuri wa Tanzania kumjua huyu bwana kwa undani.
 
Back
Top Bottom