Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Na. M. M. Mwanakijiji
Ili Kikwete aweze kuliongoza taifa kuielekea mabadiliko tunayoyataka ni lazima kwanza kabisa atambue kuwa ipo haja ya mabadiliko. Ninapozungumzia mabadiliko nazungumzia mfumo mzima wa utawala ambao nimeuita ni "MFUMO WA UTAWALA WA KIFISADI". Matatizo yetu mengi kama taifa yanatokana na mfumo huu ambao umejikita katika taratibu za sheria, fikra, na taratibu mbalimbali.
Mabadiliko haya ni lazima yaanzie kwenye kuelewa haja ya kuandika upya Katiba. Jambo hili Kikwete halioni au hataki kuliona kwani kufanya hivyo ni kukiri kuna mapungufu makubwa ya Kikatiba. Mabadiliko haya ni lazima yaingie katika mfumo wa kuwajibishana na kusimamiana kitu ambacho Kikwete na chama chake bado hawajaona ulazima wa kushughulikia na matokeo yake kwa kutumia mfumo ule ule ulioshindwa kwa miaka 50 wanafikiria wataweza kujenga taifa la karne ya ishirini na moja.
Lakini jambo la pili ni lazima kutambua kuwa aina ya viongozi wanaoingia madarakani huamua kabisa jinsi gani taifa linatawaliwa. Kwa muda mrefu nimekuwa nikisema na sitojuta kurudia tena kuwa tatizo kubwa la Tanzania na uongozi wake siyo elimu, fedha, mipango, au tafiti za kuelezea matatizo yetu. Tatizo letu kubwa ni aina ya viongozi tunaowaingiza madarakani. Mojawapo ya hofu zangu kubwa ni kwamba mwaka huu tunaweza tukajikuta tunaingiza kundi la ajabu sana kutuongoza na tutakuwa watu wa kwanza kulalamika "viongozi wetu vipi?".
Kuanzia utendaji kazi wa Bunge lililopita, kura za maoni na sasa kampeni za uchaguzi naweza kuona ndani ya CCM aina ya viongozi ambao hawana tofauti na watawala wetu walioshndwa wa miaka mitano au kumi iliyopita. Matokeo yake ni kuwa mabadiliko tunayoyataka hayawezi kutokea kwa sababu viongozi wenyewe wanaoingizwa hasa kutoka upande wa CCM wao wenyewe nao hawatambui au hawako tayari kukiri kuwa kuna haja ya mabadiliko. Wao kama ilivyo Kikwete wanafurahia hali iliyopo sasa (status quo).
Ndio maana basi utaona kuwa katika kampeni za Rais Kikwete na wagombea wa CCM dhima hii ya Mabadiliko haipo. Kutaka kupigia kelele mabadiliko ni kujaribu kusema kuwa kilichopo hakiko sawasawa na hivyo kukiri udhaifu. CCM na Kikwete hawako tayari kukubali kuwa kuna mapungufu yanayohitaji mabadiliko makubwa isipoikuwa yale ya kimapambo (cosmetic change). Tanzania inahitaji mabadiliko makubwa ya kimuundo na kimfumo ambayo yataliweka taifa katika nafasi ya kuwa taifa la kisasa kwani ilivyo sasa, njia tuliyoichagua ni njia ya Nigeria; upande mmoja kuna mafanikio ya namna mbalimbali, na upande mwingine kuna ufisadi ambao umeuwa ni utamaduni. Kwa kuendelea kuchagua watu wale wale tunazidi kurasimisha ufisadi na kuufanya kuwa ni sehemu ya maisha yetu hasa unaposikia viongozi wa CCM wakituambia kuwa "hakuna aliye msafi" na hivyo kujaribu kuhalalisha uchafu wao.
Swali kubwa kumbe kwa wapiga kura wetu linazunguka katika suala hili la mabadiliko. Je umeridhika na hali iliyopo? Je unaridhika na mfumo uliopo wa utendaji kazi wa serikali na watumishi wake? Je unaridhika na uongozi unaotolewa kwa taifa letu. Ukijibu "Ndiyo" kwa maswali yote hayo maana yake ni kuwa na wewe huoni haja ya mabadiliko na hivyo una uwezekano mkubwa wa kuchagua wagombea wote wa CCM ambao mtazamo wao unashirikiana nao.
Kwa sasa, naweza kusema kwa uhakika mkubwa tu kwamba bado Rais Kikwete na uongozi wa juu wa CCM hawajashawishi kuonesha kuwa wanatambua kuwa muda wa mabadiliko umefika. Itakuwaje lakini kama ni kweli bado hatujafikia huko kwani hadi tutapojikuta tumesukumizwa katika kona ya dhulma, ufisadi, na uonevu ndipo tutakapoamua kusema "imetosha"? Labda ni kweli muda wa mabadiliko bado haujafika na hilo CCM wanalitumia kwa manufaa yao.
Lakini, hata leo hii bado kizazi cha Watanzania kinaitwa kuamua kama kinataka mabadiliko na kama mabadiliko hayo yanaweza kuletwa na watu wale wale, wenye fikra zile zile, kutoka chama kile kile chenye sera zile zile. Ukijibu "hapana", basi ni lazima uongozwe na dhamira yako kupiga kura kuchagua mabadiliko kwa kupigia wagombea wenye kuwakilisha mabadiliko.
Itakuwaje hata hivyo kama sisi na wao tumeshindwa kutambua uwepo wa muda huo sasa?
Ili Kikwete aweze kuliongoza taifa kuielekea mabadiliko tunayoyataka ni lazima kwanza kabisa atambue kuwa ipo haja ya mabadiliko. Ninapozungumzia mabadiliko nazungumzia mfumo mzima wa utawala ambao nimeuita ni "MFUMO WA UTAWALA WA KIFISADI". Matatizo yetu mengi kama taifa yanatokana na mfumo huu ambao umejikita katika taratibu za sheria, fikra, na taratibu mbalimbali.
Mabadiliko haya ni lazima yaanzie kwenye kuelewa haja ya kuandika upya Katiba. Jambo hili Kikwete halioni au hataki kuliona kwani kufanya hivyo ni kukiri kuna mapungufu makubwa ya Kikatiba. Mabadiliko haya ni lazima yaingie katika mfumo wa kuwajibishana na kusimamiana kitu ambacho Kikwete na chama chake bado hawajaona ulazima wa kushughulikia na matokeo yake kwa kutumia mfumo ule ule ulioshindwa kwa miaka 50 wanafikiria wataweza kujenga taifa la karne ya ishirini na moja.
Lakini jambo la pili ni lazima kutambua kuwa aina ya viongozi wanaoingia madarakani huamua kabisa jinsi gani taifa linatawaliwa. Kwa muda mrefu nimekuwa nikisema na sitojuta kurudia tena kuwa tatizo kubwa la Tanzania na uongozi wake siyo elimu, fedha, mipango, au tafiti za kuelezea matatizo yetu. Tatizo letu kubwa ni aina ya viongozi tunaowaingiza madarakani. Mojawapo ya hofu zangu kubwa ni kwamba mwaka huu tunaweza tukajikuta tunaingiza kundi la ajabu sana kutuongoza na tutakuwa watu wa kwanza kulalamika "viongozi wetu vipi?".
Kuanzia utendaji kazi wa Bunge lililopita, kura za maoni na sasa kampeni za uchaguzi naweza kuona ndani ya CCM aina ya viongozi ambao hawana tofauti na watawala wetu walioshndwa wa miaka mitano au kumi iliyopita. Matokeo yake ni kuwa mabadiliko tunayoyataka hayawezi kutokea kwa sababu viongozi wenyewe wanaoingizwa hasa kutoka upande wa CCM wao wenyewe nao hawatambui au hawako tayari kukiri kuwa kuna haja ya mabadiliko. Wao kama ilivyo Kikwete wanafurahia hali iliyopo sasa (status quo).
Ndio maana basi utaona kuwa katika kampeni za Rais Kikwete na wagombea wa CCM dhima hii ya Mabadiliko haipo. Kutaka kupigia kelele mabadiliko ni kujaribu kusema kuwa kilichopo hakiko sawasawa na hivyo kukiri udhaifu. CCM na Kikwete hawako tayari kukubali kuwa kuna mapungufu yanayohitaji mabadiliko makubwa isipoikuwa yale ya kimapambo (cosmetic change). Tanzania inahitaji mabadiliko makubwa ya kimuundo na kimfumo ambayo yataliweka taifa katika nafasi ya kuwa taifa la kisasa kwani ilivyo sasa, njia tuliyoichagua ni njia ya Nigeria; upande mmoja kuna mafanikio ya namna mbalimbali, na upande mwingine kuna ufisadi ambao umeuwa ni utamaduni. Kwa kuendelea kuchagua watu wale wale tunazidi kurasimisha ufisadi na kuufanya kuwa ni sehemu ya maisha yetu hasa unaposikia viongozi wa CCM wakituambia kuwa "hakuna aliye msafi" na hivyo kujaribu kuhalalisha uchafu wao.
Swali kubwa kumbe kwa wapiga kura wetu linazunguka katika suala hili la mabadiliko. Je umeridhika na hali iliyopo? Je unaridhika na mfumo uliopo wa utendaji kazi wa serikali na watumishi wake? Je unaridhika na uongozi unaotolewa kwa taifa letu. Ukijibu "Ndiyo" kwa maswali yote hayo maana yake ni kuwa na wewe huoni haja ya mabadiliko na hivyo una uwezekano mkubwa wa kuchagua wagombea wote wa CCM ambao mtazamo wao unashirikiana nao.
Kwa sasa, naweza kusema kwa uhakika mkubwa tu kwamba bado Rais Kikwete na uongozi wa juu wa CCM hawajashawishi kuonesha kuwa wanatambua kuwa muda wa mabadiliko umefika. Itakuwaje lakini kama ni kweli bado hatujafikia huko kwani hadi tutapojikuta tumesukumizwa katika kona ya dhulma, ufisadi, na uonevu ndipo tutakapoamua kusema "imetosha"? Labda ni kweli muda wa mabadiliko bado haujafika na hilo CCM wanalitumia kwa manufaa yao.
Lakini, hata leo hii bado kizazi cha Watanzania kinaitwa kuamua kama kinataka mabadiliko na kama mabadiliko hayo yanaweza kuletwa na watu wale wale, wenye fikra zile zile, kutoka chama kile kile chenye sera zile zile. Ukijibu "hapana", basi ni lazima uongozwe na dhamira yako kupiga kura kuchagua mabadiliko kwa kupigia wagombea wenye kuwakilisha mabadiliko.
Itakuwaje hata hivyo kama sisi na wao tumeshindwa kutambua uwepo wa muda huo sasa?