Kikwete anawakwepa watanzania wa USA - tena!

Chief Charles A.Taku - anatafuta ulaji, sijui kama alishafanikiwa au ndio bado kinapikwa! Ajitaharidhishe, asije akajikuta mkataba wake na mahakama hiyo ya Rwanda unakwisha kabla maslahi yake hajapewa. Andrew Young, you are a slow learner. Some of us believed that way too; now we know better.
 
Andrew Young anatumia weusi wake kuendeleza unyonyaji na dhuluma dhidi ya Waafrika wenzake.

Hana tofauti na akina Bush, kazi zao ni kusifia viongozi wa Afrika, wanaokubaliana na mambo yao, au wanaolinda maslahi yao hata kama viongozi hao hawana mipango ya maana kwa nchi zao.
 
293159587.jpg


Alafu ndio mlikuwa mnataka muungwana aisubirie hii Award wakati wa mkutano?
 
Andrew Young anatumia weusi wake kuendeleza unyonyaji na dhuluma dhidi ya Waafrika wenzake.

Hana tofauti na akina Bush, kazi zao ni kusifia viongozi wa Afrika, wanaokubaliana na mambo yao, au wanaolinda maslahi yao hata kama viongozi hao hawana mipango ya maana kwa nchi zao.

Tunapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa. The awards hizi ni za kuchongwa. Hazina impact yoyote katika stature ya JK. He should see thru this.
 
Hahahahahahahaha....this is funny....(that boyz to men were there to entertain....)
 
Mr President Marekani,
umeenda zaidi ya mara nne, Mkoa wako wa Mbeya hujakanyaga since uchaguliwe...mambo gani sasa hayo, njoo utuone bwana hujafanya hata ziara moja, huku ni nyumbani kwako pia. Kumbuka wananchi wako wote.
 
jamani huyu BWANA SIDE AMEONYESHA WAZI ALIVYO KILAZA MWANAKIJIJI TUTAWASAIDIAJE WATU KAMA HAWA WALIONDOKA KWENYE MATATIZO YA ZANZIBAR KAMA ULIINGI AUBALOZINI NA AKILI ZAKO KWENDA KUSOMA UWEZI NENA YANAYONENWA

2)side huyo menosugu nakuhakikishia inawezekana hata us hayupo na kama yupo kaingia juzi na kama juzi huyo shule hakuna asikwambie mtu bwana nenda us ukajionee mwwenyewe,,mwambie watu wamerudi tule shule kwanza wengi vilaza wanaogopa vyuo vya bonngo noma,,kama ameshindwa kumzika baba yake atawezaje kutuongoza kwenda ikulu ya dar??au kuna ikulu uko ,,pili nahisi huyu jamaa anishi kiukimbizikimbizi kama si mtumwa
tunajribu kumsaiidia
 
Side Samahani Nimeandika Vibaya ,,nilikuwa Nakujulizsha Ukilaza Wa Huyu Menosugu,,nimemvumilia Nikaona Nimpashe Kidogo.......
Huyu Ukimleta Hata Cbe Ale Ka Diploma Wacha Advance Wanakula Kichwa,,jamani Mlio Marekani Elezeni Ukweli Halisi,,i Hav Been There,,hawa Ndugu Zetu Pesa Ipo Wala Si Utani,,ila Shule Wasikudanganye Kuna Watu Ndio Maana Wenye Akili Zao Wamekaa 5yrs Shule Awamalizi Wanaona Kuja Dar Na Kukimbiwa Utumwa,,kuwa Mtumwa Ukiwa Na Shule Yako Nakupa 5,,,,meno Sugu Namalizia Degree Udsm Nakuja Uko Tupambane Na Maisha Ila Natumaini Tutapishana Kidogo Ntakuwa Nabeba Mabegi Na Kusafisha Vyoo Kitaalamu Zaidi,,,,,,kuliko Wewe Ulieidanganya Ubalozi Unakwenda Kusoma,,hakika Mungu Akishusha Garika Kuondoa Wanaoishi Illegal Marekani Nafikiri Wengi Watakaokuja Watgeuka Majambazi Maana Life Ya Kule Ni Nzuri Jamani Sema Asilimia Ya Wengi Hatuendi Kusoma Tunalia Na Greencard,,,,all The Best Menosugu
 
Nina wasiwasi kama "mtoto wa mkulima" ni mtoto wa mkulima kikweli, labda mtoto wa kigogo akijifaragua kama mtoto wa mkulima au ana makovu ya kisaikolojia na safari.Mtoto wa mkulima wa kawaida Tanzania hata mtandao anausikia kwenye bomba, anataka kutuzuga nini?

Ingawa binafsi kama nilivyowahi kusema hapo nyuma sihudhurii vikao vya rais anapokuja huku (labda kujumuika na watanzania tu, sitegemei chochote cha kujenga) naamini Watanzania popote walipo wana haki ya kukutana na viongozi wao.

Hayo maneno ya mtoto wa mkulima yanaonyesha kukurupuka.


1.Nakubaliana na wewe, ingawa kwa sababu tofauti.Ni kupoteza muda kwa sababu maswali muhimu yanajibiwa kwa propaganda na "responses" badala ya kufanyiwa kazi.

2.Dead wrong, kuna watu huko bado wanafikiri Nyerere ndiye rais.Kama nilivyosema, labda wewe ni mkulima special kwenye shamba lake la minanasi au upo kwenye "ukulima wa vigogo" ndiyo maana una special access.

3.Sio lazima kurudi nyumbani ili mtu ashiriki katika mchakato wa siasa na uchumi.Kuhusu fedha kutokuwa na impact hapa unajionyesha ukosefu wako wa habari, remittance za Watanzania zinaleta fedha nyingi za kigeni kuliko dhahabu, kwa mujibu wa ofisi ya makamu wa rais 8% ya familia za Tanzania zinategemea remittance *. By October 2007 Unajua kwamba 2.4% ya GDP au $ 313m zilitokana na remittance (International Fund for Agricultural development)**


Tafadhali lete masuala yenye kina, sio vitu visivyoeleweka.

Sources

* http://www.sendmoneyhome.org/uploads/2007/04/uk-press-release-07a-updated.doc

** http://www.ifad.org/events/remittances/maps/africa.htm
2007 International Forum on Remittances at the IDB Conference Center in Washington DC, on 18-19 October 2007.

*** http://www.iht.com/articles/ap/2006/10/26/business/AF_FEA_FIN_Tanzania_Mining.php

http://www.livelihoods.org/hot_topics/docs/RemitTanzania.pdf
PUNDIT.

Labda nikupe taarifa inawezekana ukawa mmoja wa Tanzania walioondoka 10 or 20 yrs ago.
1; Hoja kua mtandao mkulima hatumii basi si hoja bcs now adays tuna TTCL wireless services kwetu kijijini hapa SHIGAMBA kwahiyo tunapata hudama ya mtandao.kwahiyo hiyo ni TAARIFA na naamini kama hujarudi nyumbani longtime basi vizuri ujue hilo.
2;Hoja kua kuna watanzania wanajua Nyerere ni Rais si kweli that is too theories mlionazo wenye fikra za KUSADIKIKA kua nchii hii bado ipo Gizani,Inamaana unashindwa kujua kua CCM inaofisi ktk kila kata Nchii HII?Hiyo nayo ni taarifa my be uliondoka wakati nyerere ni Rais wa nchi.
3;Hoja ya Ushiriki wa siasa na uchumi ukiwa nje au ndani naamini unapokua ndani hasa ktk eneo husika unashiriki more active kwa mifano halisi eg ukiwa na shamba unaweza kutuonyesha wenzio namna ya kua na kilimo bora,na kama sera ina mapungufu unaweza kutusaidia kutua mawazo ukiwa njee kama huko mlipo impact ya mnayoya sema ni ndogo bcs mawazo yenu yatakua (kama yalivo) more of theoretical kuliko hali halisi.Pia hoja yangu kua pesa mnazotuma hazina impact na Facts ulizotumia naamini umeonyesha kua remittence zenu hatuoni impact yake ktk uchumi wetu bcs either madini uliotumia as comparisson bado hatuoni impact yake kwetu sisi thats why i said remittence zenu hazi saidii uchumi wetu.Abt 2.4% ya GDP kua inatokana na IFAD hatupingi but hoja yangu remittence zenu mnaofanya hizo kazi za u house boy/Girl,kuosha magari,ulinzi ktk masupa maket etc hazina impact compered kama mngeli kua wakulima kama sisi na sasa mvua zimeanza u could contribute a lot to our economy,
Nashangaa wanao beza jembe la mkono while ni hilo lililowapatia nauli za kufika huko,but kwa taarifa sasa hivi serekali ya CCM imetuletea Trekta katika kila kata ili wakazi wa vijiji kati ya sita mpaka nane tutumie trekat moja ktk kililmo,Yameanzaishwa mashamba ya kata ili tulime kama kata i hope si muda mrefu tutakua tumemaliza ulimaji wa jembe la mkono.
Kwahiyo PUNDIT nasema kua Mkuu wetu hana sababu ya kupoteza muda hao waliokua wanamuhitaji bcs mawazo yao yatakua more of theories than practical.
3;
 
Wanabodi wa Jambo Forums,

Kwanza napenda kuwatakia Heri na Fanaka kwa Mwaka Mpya 2008. Napenda pia kuwaasa kufanya tathmini ya kiasi gani malengo mliyojiwekea kwa mwaka 2007 yalitimizwa, na jinsi ambavyo yale mtakayoyaweka kwa mwaka 2008 yatatimizwa.

Baada ya haya napenda kujibu hoja iliyopo hapo juu kwa kuwapa mwanga kuhusu ukweli wa mambo ambayo watendaji wakuu (wengi wao) wa Ikulu, pengine, wasingependa ujulikane.

Kwanza kabisa wengi wenu mnaelewa kwamba kuna utamaduni wa kila rais anayechaguliwa kuweka 'watu wake' kumshauri wakati akiwa kazini. Watu hawa huchaguliwa kutokana na ukaribu/uhusiano alionao (mara nyingi...) au pengine maoni ya baadhi ya 'maswahiba' wa rais, ambao wao wenyewe hawawezi (kwa sababu moja au nyingine) kuteuliwa kufanya kazi Ikulu. Hawa ndio hutoa maoni yao kwa rais nani ateuliwe kushika nafasi ambazo zinakuwa ziko wazi baada ya baadhi ya watendaji wa Ikulu kuondolewa.

Pili, kutokana na utamaduni huu, kinachotokea ni kwamba, wanaoteuliwa kushika nafasi hizo nyeti huwa hawana vigezo vya kiutendaji (professional qualifications, terms of refereence, etc.), hivyo huwa hawajui, kimsingi, wajibu wao na hata sifa zao za kikazi. Hili si jambo la kufanyia mzaha, kwani, kinachotokea ni kwamba wanateuliwa watu ambao hawana sifa au viwango vya kuwa washauri wa rais, au watendaji wa Ikulu. Hii inasababisha mambo mengi kuamuliwa kutokana na uzoefu wao, si uzoefu wa kitaalam kama inavyopaswa iwe.

Tatu, kutokana na watendaji hawa kutokuwa na sifa zinazowahalisha kuwa watendaji wa Ikulu, mara nyingi watu hawa hufanya kazi kwa 'kujipendekeza' kwa rais. Hawana mawazo mapya sembuse fikra za kibunifu, kwa hiyo wanafanya maamuzi ambayo mimi ninayaita 'kuziba nyufa' wakati inatakiwa 'kujenga upya ukuta'. Hawana mawazo mapya, wao ni kurejesha kila walichokikuta humo ndani ya lile kasri kubwa jeupe, na kukileta kikiwa na 'nembo mpya', kumbe rais anapelekewa mvinyo ule ule pasi na yeye mwenyewe kujua. Kwa yeyote ambaye atabisha juu ya hili, ninao mfano zaidi ya mmoja, ya utendaji huu mbovu wa watendaji wa Ikulu.

Sasa wengine pengine mtajiuliza, iwapo mambo ni shaghalabaghala kama haya? Kwa mtazamo wangu, itabidi watu walio karibu zaidi na Rais Kikwete, wamshauri kuangalia upya sifa za kitendaji (professional qualifications) za waajiriwa wa Ikulu, kwani, kama inavyoeleweka duniani kote, Ikulu ni mahali ambapo kila aliyeajiriwa hapo anastahili kuwapo, na hata kama aliitwa hapo kwa matakwa ya Rais, basi, Rais asiwe na mashaka naye hata kidogo. Kwa kila nafasi yake, mtendaji wa Ikulu anatakiwa kuwa na kiwango cha juu kabisa cha uwajibikaji, uzoefu na uadilifu. Asiwe mtu wa kuchukua 'uamuzi mwepesi' kwa kazi ngumu. Asiwe mtu wa kukwepa majukumu, na awe mtu wa kusema ukweli, kumshauri Rais ipasavyo, awe tayari kukataa kufanya kazi ambayo utendaji wake unachangia katika ushauri mbaya kwa Rais, na matokeo yake kuwa mabaya zaidi kwa mustakabali wa nchi husika. Asiwe mnafiki.

Jambo moja ambalo watendaji wa Ikulu (ikiwa ni pamoja na taasisi zote zinazohusiana na Ikulu) hawajalitambua ni kwamba, kisheria na kitendaji, wana nguvu nyingi sana. Wana uwezo wa kumwita mtu yeyote na kumpa kazi yoyote waitakayo aifanye, bila kuulizwa na mtu yeyote au taasisi yoyote. Si uongo, ukiwa Ikulu 'umeula', lakini kama ni 'kuula', basi uwe na uhalali wa 'kuula'. Hatupendi kusikia na kuona utendaji mbovu unaomdhalilisha na kumwaibisha Rais kila uchao; kama kulikuwa na nafasi ya Rais kuwaona Watanzania waishio Marekani, basi, nafasi hiyo ingetumika. Inawezekana watendaji hao wa Ikulu, pamoja na maswahiba zao wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani, waliona kwamba Watanzania wenzetu waliopo Marekani wangewaumbua kwa kutoa dukuduku zao mbele ya Rais iwapo wangepata nafasi ya kuzungumza na Rais, dukuduku ambazo pengine zingepaswa kufanyiwa kazi na watendaji hao wa Ikulu na ubalozini. Lakini wakaamua kukwepa majukumu; mimi namsifu mtendaji anayekubali kukosolewa, kuliko anayekwepa kukosolewa. Utajuaje kama utendayo ni sahihi kama hutaki kukosolewa? Ndio maana Rais Kikwete alisema malalamiko ya upinzani hayamnyimi usingizi, ni matokeo ya demokrasia; kwenye demokrasia lazima upinzani upige kelele, usipopiga kelele si demokrasia! Sijui nani kati yenu alimwelewa Rais Kikwete aliposema hayo.

Kabla ya kupata nafasi ya kufanya kazi (japo kwa mbali) na baadhi ya watendaji wa ngazi za juu za Ikulu, nilidhani kwamba Ikulu ni mahali patakatifu, ambapo kila aliye huko alistahili kuwa huko. Kwa leo, ule utakatifu wa Ikulu haupo tena. Watu wamekwenda huko kwa njia za ki-ajabu-ajabu. Hakuna "professional qualifiations" wala "terms of reference" zinazowawajibisha na kuwaruhusu kuwapo huko. Tutaendelea kufanya mzaha na Ikulu mpaka lini?

Rais Jakaya Kikwete, tafadhali safisha nyumba yako. Kama unahitaji ushauri wa kitaalam zaidi, tupo sisi huku nje, tutakushauri, tuite... tena tutaifanya kazi hiyo hata bila malipo, ili mradi ni kwa manufaa ya Taifa letu! Unastahili kufanya kazi na wataalam, sio watu wanaodhani ni wataalam. Wapo watu wachache sana ulionao huko Ikulu, ambao ni wataalam kweli kweli, lakini wana sauti ndogo kuliko hao uliowapa madaraka ya juu zaidi... hao mimi ninawaogopa... hao ndio wanaokupotosha.

Jambo Forums, tuendelee na kazi yetu. Uzi ni ule ule mwaka 2008! Sikukuu njema!
 
293399681.jpg

Boyz II Men na JK amekosekana Lowassa.

293399683.jpg

Haya mambo ndio Kikwete anapenda na anaweza kutumia hata billion zozote kuyapata. Aliposikia tu BIIM watakuwa ndani ya nyumba JK huyooooo.....

Watanzania hapa tumepotea kabisaaaaaa
 
Back
Top Bottom