Kikwete Amedanganya wananchi hawa

mkongo

Member
Nov 21, 2009
19
9
Tanzania haki iko wapi? Tutaiendekeza CCM mpaka lini?

Najumuika Ulingoni kuwaonyesha link yenye video ya yaliyotokea mwaka 1996 huko Bulyanhulu wakati wananchi walivyoondelewa kwa nguvu bila huruma na uvunjaji wa haki, tena nchini kwao kumbuka serikali yao walioiweka madarakani ndiyo waliofanya vitendo hivi.

Pia Rais wao Jakaya Mrisho Kikwete amewadanganya wakati wa kampeni... nasema NAMCHUKIA kwasababu ni Mnafiki.

Hata faida inayopatikana na machimbo haya haiwafaidishi wananchi hawa ni kwa viongozi wachache ambao wanapenda kujinunulia magari ya kifahari. kuishi maisha ya kifahari, kujilipa mishahara minono, wenye sifa ya umimi na sio mimi na wewe na yule. Jamani tuwaonee huruma asilimia kubwa ya wananchi vijiji wanaoishi kwa maisha ya tabu.

Asante kwa waliotengeneza video hii kutuonyesha yaliyotokea huko. Mimi binafsi nimesikitika sana na imenigusa.

Asante

[ame]http://vimeo.com/7690704[/ame]
 
Tanzania haki iko wapi? Tutaiendekeza CCM mpaka lini?

Najumuika Ulingoni kuwaonyesha link yenye video ya yaliyotokea mwaka 1996 huko Bulyanhulu wakati wananchi walivyoondelewa kwa nguvu bila huruma na uvunjaji wa haki, tena nchini kwao kumbuka serikali yao walioiweka madarakani ndiyo waliofanya vitendo hivi.

Pia Rais wao Jakaya Mrisho Kikwete amewadanganya wakati wa kampeni... nasema NAMCHUKIA kwasababu ni Mnafiki.

Hata faida inayopatikana na machimbo haya haiwafaidishi wananchi hawa ni kwa viongozi wachache ambao wanapenda kujinunulia magari ya kifahari. kuishi maisha ya kifahari, kujilipa mishahara minono, wenye sifa ya umimi na sio mimi na wewe na yule. Jamani tuwaonee huruma asilimia kubwa ya wananchi vijiji wanaoishi kwa maisha ya tabu.

Asante kwa waliotengeneza video hii kutuonyesha yaliyotokea huko. Mimi binafsi nimesikitika sana na imenigusa.

Asante

http://vimeo.com/7690704

Karibu sana ndugu, naona umekuja na kasi mpya, post ya kwanza tu imegonga Ikulu!
 
Video yenyewe ipo wapi?

Sie tulikuwa na hasira kuliko zako hizo kule Nyenzi.com mpaka BCS, ila tumepoa kwa sasa hatuna misimamo mikali. Tumegundua kuwa waTanzania ndo wajinga kukubali kudanganywa.

Asante mkuu
 
Aisee video hii inasikitisha sana...watu wanaposhika silaha msifikiri hawana akili
 
Mwanangu Mkongo haya ndiyo mambo yaliyomtoa Naomi machozi, Tanzania is a police state, hatuwezi kubisha.

Inabidi watu wapelekwe mahakamani, hata ikibidi katiba kurekebishwa ili watu waweze kuisue serikali.

Wanasheria wa bongo mbona wamelala?

Huyu Generali Kiwelu Kawajibishwa vipi?

Kuna watu katika video wanasema "Muheshimiwa tunaomba turuhusiwe kuuliza maswali" "Tanzania nchi huru uhuru wenyewe ndio huu?" "Tanzania nchi ya amani amani yenyewe ndiyo hii?"

Inatia huruma sana!
 
Video yenyewe ipo wapi?

Sie tulikuwa na hasira kuliko zako hizo kule Nyenzi.com mpaka BCS, ila tumepoa kwa sasa hatuna misimamo mikali. Tumegundua kuwa waTanzania ndo wajinga kukubali kudanganywa.

Asante mkuu
Umenikumbusha hii site enzi hizo ilkuwa bomba kishenzi, hivi iliishia wapi ?.
 
Nilisikia tetesi kuwa Che Nkapa ni shareholder katika kampuni ya dhahabu ya Kahama.
Baada ya kuangalia hii video naelewa kwa nini nguvu zilitumika chini ya utawala wake kuwafukuza wananchi hao.
 
Naomba niulize jamani tumlaumu nani? kama Wasukuma wenyewe wenyeji ndo wanaongoza kupigia kura CCM, jamani hivi Wasukumu hata nusu ya namba yao wangepigia kura upinzani si wasingejikomboa jamani? Hao wawakilishi wao wa CCM wakina Chenge na Mwanyika wamewasaidia vipi au wamejishibisha bila aibu na kuacha umaskini huu ukiendelea na ajabu Chenge ataingia bungeni tena 2010! Endeleeni kulia tu labda muendelee kuua albino kwa vile kwenu nyie ni rahisi zaidi ya kujikomboa (samahani nitakayemkwaza) kuondoa CCM madarakani wakija Chadema na CUF ku washauri mnadai ati chama cha Wachagga na Uislamu kwani hawa watu si Watanzania wenzenu? wapeni nafasi muone kama watawaangusha au endeleeni kula propaganda huku mkimezwa na kufisidiwa! Inasikitisha
 
Bluray, acha usingizi huo! Hivi unafikiri kwamba kwa sasa huwezi kuishtaki Serikali mpaka Katiba ibadilishwe? Kasome The Government Proceedings Act uone kawa huwezi kuishtaki Serikali!
 
Video yenyewe ipo wapi?

Sie tulikuwa na hasira kuliko zako hizo kule Nyenzi.com mpaka BCS, ila tumepoa kwa sasa hatuna misimamo mikali. Tumegundua kuwa waTanzania ndo wajinga kukubali kudanganywa.

Asante mkuu

FairPlayer huoni hiyo video hapo mwanzoni?
 
kwani pale wapemba wakiikataa ccm si mnaona ni wajinga sasa ndio muone wapemba wameuliwa na nyinyi mlikuwa kimya bado mtaipigia ccm mkipewa pombe na flana tu basi mmeridhika amkeni bado mmelala mkidanganywa tu kidogo basi sasa hiyo ndio hali muuone wapemba wao wameshajijua na ndio maana ccm anafanya afanyalo pemba hana kitu
 
Tanzania haki iko wapi? Tutaiendekeza CCM mpaka lini?

Najumuika Ulingoni kuwaonyesha link yenye video ya yaliyotokea mwaka 1996 huko Bulyanhulu wakati wananchi walivyoondelewa kwa nguvu bila huruma na uvunjaji wa haki, tena nchini kwao kumbuka serikali yao walioiweka madarakani ndiyo waliofanya vitendo hivi.

Pia Rais wao Jakaya Mrisho Kikwete amewadanganya wakati wa kampeni... nasema NAMCHUKIA kwasababu ni Mnafiki.

Hata faida inayopatikana na machimbo haya haiwafaidishi wananchi hawa ni kwa viongozi wachache ambao wanapenda kujinunulia magari ya kifahari. kuishi maisha ya kifahari, kujilipa mishahara minono, wenye sifa ya umimi na sio mimi na wewe na yule. Jamani tuwaonee huruma asilimia kubwa ya wananchi vijiji wanaoishi kwa maisha ya tabu.

Asante kwa waliotengeneza video hii kutuonyesha yaliyotokea huko. Mimi binafsi nimesikitika sana na imenigusa.

Asante

http://vimeo.com/7690704
Picha na taarifa kama hizi husikitisha na kuhuzunisha sana, Mbali na ubadhirifu wa mali za Taifa uliojitokeza kwa Nguvu mno wakati wa uongozi wa Mkapa pia Wananchi wamepoteza maisha kwa sababu za kisiasa au za kujaribu kutetea baadhi ya haki zao, Vyombo vya dola vimeariwa kutumia nguvu ambazo zimesababisha vifo. Kama tunavyoona katika video hii, na kadhaa zimepita kama Pemba na Mwembe Chai. Uongozi wa Serekali iliyopo unaelekea umeshindwa kuchukua hatua zozote na Wanasheri wetu inaelekea wanaogopa kutia Kitumbua cha Mchanga. Kwa hali hiyo labda tujaribu kufungua Kesi nje ya nchi katika Mahakama za kimataifa ili kuongeza Presure/mbinyo kwa viongozi kuwa they can run, but they cant hide/Wanaweza kukimbia lakini hawawezi kujificha.
 
Tanzania haki iko wapi? Tutaiendekeza CCM mpaka lini?

Najumuika Ulingoni kuwaonyesha link yenye video ya yaliyotokea mwaka 1996 huko Bulyanhulu wakati wananchi walivyoondelewa kwa nguvu bila huruma na uvunjaji wa haki, tena nchini kwao kumbuka serikali yao walioiweka madarakani ndiyo waliofanya vitendo hivi.

Pia Rais wao Jakaya Mrisho Kikwete amewadanganya wakati wa kampeni... nasema NAMCHUKIA kwasababu ni Mnafiki.

Hata faida inayopatikana na machimbo haya haiwafaidishi wananchi hawa ni kwa viongozi wachache ambao wanapenda kujinunulia magari ya kifahari. kuishi maisha ya kifahari, kujilipa mishahara minono, wenye sifa ya umimi na sio mimi na wewe na yule. Jamani tuwaonee huruma asilimia kubwa ya wananchi vijiji wanaoishi kwa maisha ya tabu.

Asante kwa waliotengeneza video hii kutuonyesha yaliyotokea huko. Mimi binafsi nimesikitika sana na imenigusa.

Asante

http://vimeo.com/7690704


Hii video ya 2008, lengo la kuitengeneza sijui kama limefikiwa zaidi ya hzi posts za blogs, it seems was posted from Canada ......


Kwa ya Buly Mining Report zipo kibao ikiwemo "Special Investigation Report" ya 2002http://www.miningwatch.ca/sites/miningwatch.ca/files/Bulyanhulu.pdf

Council of Canadians, Sept 27, 2001 http://www.canadians.org/



Documentary Film ya Mattias Ylstra, Stan van Houcke, 2004
http://www.ylstra.nl/bulyanhulu.html

Just you can see jinsi gani hao hao Wazungu wanavyafanya juu ya tabu zetu....
 
Bila ya kuingia msituni hakuna haki itakayopatikana. Naona maneno matupu hayazai kitu.
 
Nilisikia tetesi kuwa Che Nkapa ni shareholder katika kampuni ya dhahabu ya Kahama.
Baada ya kuangalia hii video naelewa kwa nini nguvu zilitumika chini ya utawala wake kuwafukuza wananchi hao.

Che Nkapa alikuwa ni shareholder katika Mabangu Investiment ambayo ndiyo ilikuwa Prospecting Lincense Holder ya eneo hilo na kuna uwezekano kuwa bado wanahold shares zoa kwenye maning Company iliochukuwa jukumu la uchimbaji. Mabangu Investment inamilikiwa na Prof. Mbilinyi
 
Huko misituni mnataka kwenda kulina asali ama kutafuta kuni?
Acha kudhihaki watu bwana. Umeelewa fika kuwa wanasema nini. Mimi nadhani wewe u mmoja wa watu wanaolinda 'status quo' ya wanaodhalilisha wananchi.
 
Back
Top Bottom