Kikwete Akataa Balali Asiletwe!

Chifu,

Sinuii kukukatisha tamaa, kamwe hiyo si hulka yangu. Hata kama sintokubaliana nawe, sitaota kukukatisha tamaa. Kitu ninachotaka uelewe ni kwamba, jinsi ulivyoandika inaonyesha inataka mambo yafanywe kienyeji.

Hata kama serikali ya Marekani itataka kumrudisha Ballali, haiwezi ikajiamulia tu kufanya hivyo bila kuombwa rasmi na serikali ya Tanzania. Hata kama wakiombwa, ujue kuwa kwa vile Ballali ni mkazi wa kudumu wa Marekani, serikali ya Marekani inaweza ishindwe kumrudisha kwani huko kutakuwa ni njia panda kati ya kuingilia mambo ya ndani ya Tanzania na kumlinda mtu mwenye kustahili kuishi na kufanya kazi huku.

Kama nilivyoeleza hapo awali, suala hili ni nyeti na lina mtandao wa watu wengi na kufanya mambo kienyeji kutapelekea kukosa hata hilo suluhisho la kudumu. Cha msingi ni kuendelea kuihoji serikali ni kwanini hawawafungulii mashtaka wahusika wote (japo Ballali ni conduit tuu), kina Patel, Lukaza, Mushis (not sure if you're related), na hata wale walioidhinisha malipo haya na Ballali, watu kama kina Mramba, Mgonja etc. Kuishinikiza serikali kwa kila namna ndio njia pekee ya kutafuta suluhisho lakini sio propaganda na udaku wa kutoa tafsiri isiyo sahihi na yenye kuleta uchochezi.
 
Chifu,

Sinuii kukukatisha tamaa, kamwe hiyo si hulka yangu. Hata kama sintokubaliana nawe, sitaota kukukatisha tamaa. Kitu ninachotaka uelewe ni kwamba, jinsi ulivyoandika inaonyesha inataka mambo yafanywe kienyeji.

Hata kama serikali ya Marekani itataka kumrudisha Ballali, haiwezi ikajiamulia tu kufanya hivyo bila kuombwa rasmi na serikali ya Tanzania. Hata kama wakiombwa, ujue kuwa kwa vile Ballali ni mkazi wa kudumu wa Marekani, serikali ya Marekani inaweza ishindwe kumrudisha kwani huko kutakuwa ni njia panda kati ya kuingilia mambo ya ndani ya Tanzania na kumlinda mtu mwenye kustahili kuishi na kufanya kazi huku.

Kama nilivyoeleza hapo awali, suala hili ni nyeti na lina mtandao wa watu wengi na kufanya mambo kienyeji kutapelekea kukosa hata hilo suluhisho la kudumu. Cha msingi ni kuendelea kuihoji serikali ni kwanini hawawafungulii mashtaka wahusika wote (japo Ballali ni conduit tuu), kina Patel, Lukaza, Mushis (not sure if you're related), na hata wale walioidhinisha malipo haya na Ballali, watu kama kina Mramba, Mgonja etc. Kuishinikiza serikali kwa kila namna ndio njia pekee ya kutafuta suluhisho lakini sio propaganda na udaku wa kutoa tafsiri isiyo sahihi na yenye kuleta uchochezi.
Taratibu tu..mwishowe naona tutakubaliana.Nitajaribu kukujibu kama ifuatavyo;

Hakuna mahali popote kwenye thread hii ambapo nimesema mambo yaamuliwe kienyeji!Kama umekuwa ukifuatilia postings kwenye thread toka mwanzo..ni wazi utaona kuwa sijapingana na hiyo bodi iliyoundwa ya uchunguzi.

Mahali ambapo napingana ni very wazi..Kwanini serikali ya Kikwete haimuhitaji Balali kwenye mahojiano haya wakati ni wazi kuwa yeye ndiye mtu wa kwanza kuwajibishwa na rais?We huoni kwamba hayo makampuni yenyewe yaliomba hizo fedha then yakapewa?

Sasa huyo aliyezitoa hatakiwi kuhojiwa?HIVI UNAFIKIRI WATANZANIA NI PUMBAVU KIASI HICHO?

WAKINA MUSHI'S,MRAMBA'S,MGONJA'S..NA WAPANDA MERIKEBU WENGINE NAO WAHOJIWE KAMA WAMEHUSIKA..HAYA NI MASWALA YA KITAIFA NA SIO KINA FLANI!MUSHI'S NA MRAMBA'S WAKO WENGI..

SINA HAJA YA KUWA RELATED NA MAFISADI!NAPOPITA KWENYE MITAA YA BONGO NA KUONA HALI HALISI YA WANANCHI MACHOZI HUWA YANANITOKA!

NDIYO HIVYO NILIVYOZALIWA

!MAMBO NI MBAYA BONGO..HALAFU HUU UPUUZI UFUMBIWE MACHO!

HAIWEZEKANI!TUTAPAMBANA!KAMA SUALA HILI NI NYETI KAMA UNAVYODAI...THEN KIKWETE ALITAKIWA AFANYE SOMETHING THAT MAKES SENSE!

SOMETHING ABOVE ALL POLITICS!SOMETHING TO DO WITH PATRIOTISM "BRING BALALI HOME SO HE CAN FACE JUSTICE"

Mwisho kwa kumalizia,nataka upate time na kufuatilia habari kabla ya kukurupuka tu na kutoa madai ambayo hayana msingi!"

SERIKALI YA MAREKANI IMESAINI MAKUBALIANO NA TANZANI..HIVYO HATA KAMA BALALI ANA HUO URAIA AMA GREENCARD KAMA UNAVYOTAKA TUAMINI BADO TU ATARUDISHWA KAMA KIKWETE AKIKUBALI..NI MAKUBALIANO KATI YA NCHI HIZO MBILI!

YA KUKABIDHIANA WATU WANAOHITAJIKA KATIKA UCHUNGUZI ETC!
 
Mushi unaweza kusema kwa uhakika kabisa "Kikwete Akataa Balali asiletwe"? Tumia maneno yako vizuri basi arawa! Otherwise unaonekana kama kituko hivi.
Kituko ni wewe unayeongea kama msukule!Kwanini unapenda laini laini?Sasa kama Kikwete hajakataa kwanini alikuwa anasema hajui aliko?

Marekani wakaulizwa wakesema yuko kwetu!Tukamuomba Mh Rais kwamba amrudishe..akagoma..akanyamaza kimya!

Tukadhani labda wamarekani ndo wayeyushaji..kumbe wapi ni Kikwete mwenyewe na serikali yake.WAMAREKANI WAKATUMIA LUGHA YA KIDIPLOMASIA"SERIKALI IKIOMBA TUTAMRUDISHA!

UNAFIKIR MAREKANI HAWAJUI KUWA WANANCHI WANATAKA BALALI ARUDISHWE NA KIKWETE HATAKI?

WE HUWEZI KUONA KUWA KIKWETE NDIO HATAKI ALETWE?HIVI WE UNAFIKIRI WATU WAKO KIMYA TU KUHUSU HII ISSUE?

UMEKOSEA "ARAWA"!
 
nilikuwa natafuta wapi Kikwete kakataa kuwa Balali asiletwe!!...............oooh my God what a waste of time!!!

jmushi1

Balozi kusema serikali haijasema/haijaomba kuwa wanamuhitaji Balali haina maana kuwa JK kakataa.....this is what all others here are telling you........SERIKALI HAIJAOMBA BADO haina maana kuna mtu kakataa........unless unajua ya ndani/jikoni zaidi
 
nilikuwa natafuta wapi kikwete kakataa kuwa balali asiletwe!!...............oooh my god what a waste of time!!!

Jmushi1

balozi kusema serikali haijasema/haijaomba kuwa wanamuhitaji balali haina maana kuwa jk kakataa.....this is what all others here are telling you........serikali haijaomba bado haina maana kuna mtu kakataa........unless unajua ya ndani/jikoni zaidi
"serikali haijaomba bado"hizo ni lugha za kisiasa ambazo watu wenye upeo kama ninyi mnatakiwa muelewe!wametumia lugha laini tu!

Hawataki kuwachonganisha wananchi na rais wao..ni lugha ambayo kama we si mwelewa utapata shida kidogo!kalugha tu kaki politics kanakuchanganya!yani kweli unataka serikali ya marekani ituambie kuwa kikwete ndio kakataa?

Utaratibu huo wa kidiplomasia waliouchukua marekani ni ambao wanaamini kabisa kuwa sasa tutamuuliza mh rais wazi kuwa ni kwanini hawaulizi wamarekani wamlete balali?

Mbona hamumuulizi mh rais ni kwanini hawaombi wamarekani wamlete balali?

Atueleze basi ili tujue kuwa si kweli amekataa asiletwe!jamani mbona tunatreat each other kama watoto?
 
Mimi naona Mushi anahitaji msaada hapa, tusimsakame sana. Ikibidi kumsamehe katika suala la lugha au kupindisha heading ya habari ya gazetini tufanye hivyo, lakini tuitazame hoja anayotaka kutufikishia. Hoja niliyoiona kwake ni kwamba serikali (inayoongozwa na JK of course) haijawa proactive katika suala la kurudishwa kwa Balali nchini Tanzania. Lakini ndugu Mushi unapaswa kukumbuka pia kwamba serikali hiyohiyo bado haijawachukulia hatua watuhumiwa wengine walioko Tanzania wa sakata hilohilo. Zimetajwa kampuni zaidi ya 20 zenye wakurugenzi na wahusika wake wako Tanzania. Rais kaamuru kwamba uchunguzi ufanyike wa kutosha na hatua zichukuliwe bila kumwogopa mtu yeyote, na katoa miezi sita kwa shughuli hiyo. Muda huo haujaisha, kwa hiyo bado hakuna mapendekezo ya majina rasmi ya watuhumiwa wanaopaswa kukamatwa. Ingekuwa Mwanasheria mkuu na wenzake wameshasema watuhumiwa rasmi ni Balali etc, hapo ndipo amri ya kukamatwa kwao ingetolewa, na hapo suala la kuomba Balali arudishwe lingekuwa na mantiki. Kwa hiyo kutokutolewa amri ya kukamatwa Balali sasa hivi si sababu Kikwete kakataa, ni suala la utawala wa sheria, zinatakiwa kufuata taratibu zote ili amri ya kumkamata kama itabidi kutolewa basi iwe halali. Usichukulie kitendo cha kufukuzwa kwake ugavana kuwa ndio ushahidi wa kuwa yeye ni fisadi, hiyo ni hatua ya kiutawala kwanza, hatua za kisheria ndizo hizo tunazosubiri. Elewa hivyo ndugu Mushi, tumia lugha nzuri, na hutagombana na yeyote hapa.

Yapo tunayolalamikia wengi kwenye hii forum kuhusu sakata hili, kama vile kutogundulika kwa hili tatizo mapema, kupuuzwa kwa sauti za awali zilizopigia kelele ufisadi huu, na hata sasa mimi binafsi nadhani muda wa miezi sita ni mwingi mno kwa suala ambalo liko wazi kiasi hicho. Pengine wengine wangeendelea kujibu mashtaka wakati uchunguzi unaendelea kwa wenzao. Labda vyombo vya dola vingepaswa kufanya kazi yake mapema zaidi kabla ya hiyo kampuni ya uhasibu kugundua ufisadi huo. Na je PCCB, IGP, AG nk wanasubiri maagizo ya Rais ndipo wafanye kazi yao walioajiriwa kufanya? Kama Rais asipowaagiza hawachunguzi? Sasa kama hivyo, kazi yao nini? Nilitegemea hao watu (PCCB, IGP, AG, etc) wafanye kazi yao mapema (kabla sakata halijatufikia walalahoi) wamfikishie rais ripoti katika briefings, naye angetangaza uamuzi wa serikali badala ya kuanza kutoa maagizo ya moja kwa moja kwa watu ambao katika kuapishwa tu hayo ndio majukumu yao wanayotarajiwa kuyafanya. Hayo ndiyo tunayojadili hapa. Haya ndugu zanguni, tuendelee sasa, taratibu tusiumizane!
 
Masatu JF Senior Expert Member Join Date: Mon Jan 2007

Re: Kikwete Akataa Balali Asiletwe!

Ur either sarcastic or plain idiot, kindly take ur pick....
__________________
The greatest lesson in life is to know that even fools are right sometimes

Hii nilikuwa sijaiona hii, lakini baada ya kuisoma kwa makini imenifanya nishindwe kujua mjinga na mwenye akili ni yupi? Matusi yamerushwa weee bila ya watu kuzingatia the context politically, sina uhakika na the juice ya hii topic, lakini for the sake of a political argument au debate, ambayo ndio hasa the goal ya kuwepo hapa JF kwa kweli it is unfair the way guys mlivyo-jump on the man Mushi,

Kwa mfano, kungekuwa na article kichwa kinasema "..Tanzania yamrudisha Obote Madarakani.." mtasema kuwa huyo aliyeandika ni mjinga maana sisi wabongo wote hatukushiriki kwenye kuamua kuwa ile vita na Idd Amini, nia na madhumuni pamoja na mengine ilikuwa Mwalimu, kumrudisha rafiki yake kwenye power? No Mwalimu, politically, aliamua kwa niaba yetu wananchi wote hata kama hakuna hotuba yakle yoyote alisema hivyo kuanzia wakati wa vita na hata baada ya vita kuisha, na kwamba sisi as wananchi kuanzia bunge, hatukukaaa chini kuamua kuwa tumpige Amin, mpaka tumuondoe kwenye power badala ya kuheshimu sheria za kimataifa za kututaka tumtoe kwenye mipaka yetu tu, kama balozi wa US anasema serikali yetu haijamuomba kumrudisha Balali, maana yake kwa maneno mengine ya kisasa ni kwamba rais wetu hajamuomba, period na tena a big FULL STOP! Je rais wetu hataki Balali, arudi ndipo either Mushi alipo-fall short kidogo kwenye kuelezea au kuexplain exactly his point of view au hatukubaliani tu na maelezo yake on the topic!

Lakini kumshambulia tuuu tena mpaka watu wanaoaminika hapa JF, wengine kwa matusi mazito mazito what is the message kwa wananchi wengine? Mushi, sikubaliani na hoja zako kwenye hii topic kuwa zinatosha ku-define maana ya kichwa chako cha habari, lakini I respect your bold stand ya kusimamia hoja yako, na hapa JF tunahitaji watu zaidi kama wewe, sio watu wa kuogopa ogopa na kujikomba komba kwa wengine kihoja ili waonekane wana akili, NO! stand for what you believe, and that is exactly what you did, Bravo and keep it up!

Mushi, thank You kwa Your stand, na tunahitaji wengine zaidi kama wewe hapa JF!

Salute!
 
Kithuku
hichi ndicho ambacho nimejaribu kufanya.....kumsaidia.....lakini wapi, pengine + msaada wako ataelewa
 
................, kama balozi wa US anasema serikali yetu haijamuomba kumrudisha Balali, maana yake kwa maneno mengine ya kisasa ni kwamba rais wetu hajamuomba, period na tena a big FULL STOP! Je rais wetu hataki Balali, arudi ndipo either Mushi alipo-fall short kidogo ..............!

Uzuri wa JF ni pamoja kuwekana sawa ......pengine na hiyo hapo juu itasaidia arawa kuelewa....kumhukumu Muungwana kuwa amekataa ni kinyume na standards za judgement zetu wengi hapa.....kijana (arawa)amefall short................PERIOD!!

tuendelee kukata ishus
 
1.
kumhukumu Muungwana kuwa amekataa ni kinyume na standards za judgement zetu wengi hapa.....

Not 100%, kwa sababu who cares na hizo standards ambazo most of the time zinategemea amesema nani na amemtukana nani, na nani anajikomba kwa nani? Mushi had all the right kusema rais amekataa kwa sababu balozi wa US hawezi kusema publicly kuwa rais wenu hataki, kwenye diplomatic language haikubaliki hiyo, Clinton, amesema Obama kushinda South Carolina, ni sawa na Jesse Jackson, alivyoshinda kwenye miaka ya 1884, na 1988, lakini akaishia kutopata nomination, lugha hii kisiasa dunia nzima imeamuliwa kuwa huyu ni racist na anajaribu kutumia race card, je is that exactly what he Clinton said? Je ingekuwa hapa JF Mushi ameamua kuwa hivyo dunia ilivyoamua ndivyo Clinton alivyosema, which is his right ingekuwaje?

2.
kijana (arawa)amefall short................PERIOD!!

Kwenye hili la pili, ndiyo hasa accademically na politically iliyotakiwa kuwa the fine line ya kushambulia hoja za Mushi, na sio kumtukana mpaka kumwambia ajichague kama ni idiot, hizo ni lugha za choooni zisiruhusiwe hapa JF kwenye mijadala ya elimu, watu wengine tunasoma hapa jamani, na wengine tunaangalia anga za PHD ikiwezekana, sasa tusaidiane kielimu, sio kimatusi!

Ahsante Mkuu Ogah na wengine kwa kunielewa, na Mushi keep it up!
 
Mushi,

Chifu, sihoji hata kidogo ni jinsi gani ulivyo na uchungu wa nchi yako. Lakini nafikiri Bw. Ogah amenisaidia kufafanua kuwa ni jinsi gani ninavyopingana nawe; kichwa cha habari chenye kupotosha.

Kitu ninachopenda kwetu sote ni kutokukubali kupumbazwa na jinsi serikali yetu jinsi inavyofanya mambo au kutufanya tuwe na tofauti na kufarakana. Naamini Ballali ni fisadi lakini siamini yeye ndio star wa hii movie. Yeye katumiwa tu, kama alivyomtumia Meghji kusaini nyaraka. Imetokea kuwa yeye ndio anakuwa kafara na yeye yupo nje ya nchi. Jaribu kujiuliza, hivi angekuwepo nchini ni nini kingetokea? Angekamatwa au tungesubiri miezi sita hiyo hiyo waliyopewa kina AG, IGP na wengineo kukamilisha uchunguzi? Kikubwa zaidi ya hilo ni hivi: Ballali aliwasaidia watu kadhaa kuchota fedha. Hawa watu wanahitaji kushtakiwa kama Ballali. Basi ni kwanini hawa watu hawazungumziwi au kuandamwa kama anavyoandamwa Ballali? Cha zaidi, watu hawa wako nchini (kama hawajakimbia bado), je serikali imechukua hatua gani kama vile kuwanyang'anya pasi za kusafiria, kufreeze mali zao mpaka uchunguzi ukamilike? Kwanini macho yote yapo kwa Ballali aliye mbali lakini walio karibu na mkono wa sheria wanafumbiwa macho? Isichukuliwe kana kwamba namtetea Ballali, ninachotaka ni kuwa tusifanywe mabwege zaidi ya vile tulivyofanywa na hawa mafisadi.
 
Shukran kwa Field Marshall ES,pamoja na Kithuku.

Nashukuru sana kwasababu atleast kuna waheshimiwa hapa JF ambao mmenielewa kwa kiasi kikubwa.

Nashukuru pia kwa maelezo yenu ambayo sasa yamenipa moyo zaidi wa kujadili thread hii kwa hoja ambazo tutakuwa tukizidadili na kuelimishana kwa taarifa zozote ambazo tutakuwanazo zenye kuchangia dhana yetu kuu ya kuhakikisha kwamba justice is to prevail!

Nimajukumu yetu sisi watanzania..kwa niaba ya raia wote wa ulimwengu huu..wenye kupenda uhuru na demokrsia ya kweli!Wasiokumbatia siasa za uchochezi,ubaguzi,unyanyasaji,rushwa,matengano,chuki na ufisadi.Waheshimiwa; watoto wetu na vizazi vijavyo watazijadili hizi mada kwa namna hii tonayofanya hapa.

Maybe watasoma madarasani..kwamba kwenye historia ya nchi hii kashfa ya mamia ya mabilioni ilitokea hapa nchini kwetu!Kwamba kulishawahi kuwa na vita dhidi ya mafisadi!

Lakini jambo moja nataka tukumbushane waungwana;ili historia yetu hii ipate kutukuzwa na watoto wetu na vizazi vijavyo katika taifa letu hili changa,then ni lazima tubadilishe matokeo ya mwisho ya historia hii!

Vizazi vijavyo vijivunie historia ya kizazi hiki kuwa kilipigana vita dhidi ya ufisadi na kushinda vita hivyo!Wajue kuwa accountability ndio mojawapo ya nguzo kuu za uhuru na maendeleo!

Kwamba mafisadi hao walifikishwa kunako sheria na wananchi walipewa haki zao!Ndio picha tunayotaka kuwajengea vizazi vijavyo!

Turudi kwenye issue;
Ni hivi juzi tu waziri Meghji huko bungeni amesema kuwa hayo makampuni yaliyohusika na ufisadi yafuatiliwe kama yamelipa kodi..Sasa hiisi ni moja ya hatua za awali za kuhalalisha ufisadi pamoja na kuzitakasa hizo pesa walizochukua?

Badala ya kodi..alitakiwa aseme hivi;MAKAMPUNI YOTE YALIYOPOKEA KIASI FLANI MNAMO TAREHE FLANI WAZIRUDISHE KWASABABU ZILIPELEKWA KWENYE AKAUNTI ZAO KIMAKOSA!

Sasa kwasababu uchunguzi ndio unafanyika wa hayo makosa haina maana kwamba hizo pesa ni halali!Hizo pesa zinajulikana zilipo..zirudishwe kwanza halafu uchunguzi uendelee wa kuwa ni kwanini watu waliandika barua na kutia saini utoaji na ulipaji pesa kwa makampuni na yoyote yule aliyehusika!

Uchunguzi wa kwamba ni nani ashitakiwe nao upo wazi.Kwani si wazi kuna taratibu zinazofuatwa wakati wa procedure kama hizo?

Waungwana;

Naomba pia nijibiwe hili; kwanini watu wote walioidhinisha hayo malipo..kuanzia hizo fedha zilipokuwa huko kwenye akaunti ya madeni ya nje(kumbuka kwamba kuna barua ambazo ilibidi ziandikwe kuidhinisha utoaji wa fedha hizo kwani ilikuwa sio utaratibu wa kawaida),kutolewa na kupelekwa kwenye hizo akaunti za makampuni,hadi wakati ambapo makampuni ama watu hao binafsi walipozichukua pesa hizo kutoka kwenye akaunti za mabenki yao.Hao watu wako wapi?Walitakiwa wakamatwe,wapewe mdhamana kwa mujibu wa sheria,then waendelee kuhojiwa!Na kama sio makosa yao..sheria ndiyo itakayoamua.

Issue kubwa kama hii si ya kupiga dana dana!Ni issue ya kitahadhari!Inayotakiwa attention ya hali ya juu!Kwasababu ni wazi kuwa kila kampuni inajulikana ilipewa kiasi gani then mali ama akaunti zao zenye kufikia kiasi cha fedha za umma walizopewa zitaifishwe na kurudishwa mikononi mwa wananchi!

Tuhakikishe kuwa hizo bilioni zaidi ya 130 zinakwenda kwenye kusaidia matatizo ya wananchi ikiwemo umasikini!Kuwajengea hospitals,schools,roads,kuwasaidia katika kilimo cha kisasa..ili waweze kujikimu na tatizo la njaa ,zipelekwe kusaidia kulinda mazingira ili kuepuka maradhi,ukame na mafuriko!Kulisadia taifa letu!

Hatutaki hizo pesa zirudishwe huko kwenye akaunti ya nje!Hiyo haina maana tena kwasababu serikali ilikuwa haioni umuhimu huo hadi Dk Slaa alipowashtua watanzania!
 
1.

Not 100%, kwa sababu who cares na hizo standards ambazo most of the time zinategemea amesema nani na amemtukana nani, na nani anajikomba kwa nani? Mushi had all the right kusema rais amekataa kwa sababu balozi wa US hawezi kusema publicly kuwa rais wenu hataki, kwenye diplomatic language haikubaliki hiyo, Clinton, amesema Obama kushinda South Carolina, ni sawa na Jesse Jackson, alivyoshinda kwenye miaka ya 1884, na 1988, lakini akaishia kutopata nomination, lugha hii kisiasa dunia nzima imeamuliwa kuwa huyu ni racist na anajaribu kutumia race card, je is that exactly what he Clinton said? Je ingekuwa hapa JF Mushi ameamua kuwa hivyo dunia ilivyoamua ndivyo Clinton alivyosema, which is his right ingekuwaje?

2.

Kwenye hili la pili, ndiyo hasa accademically na politically iliyotakiwa kuwa the fine line ya kushambulia hoja za Mushi, na sio kumtukana mpaka kumwambia ajichague kama ni idiot, hizo ni lugha za choooni zisiruhusiwe hapa JF kwenye mijadala ya elimu, watu wengine tunasoma hapa jamani, na wengine tunaangalia anga za PHD ikiwezekana, sasa tusaidiane kielimu, sio kimatusi!

Ahsante Mkuu Ogah na wengine kwa kunielewa, na Mushi keep it up!

Mkuu FMES,

Nakubaliana nawe mkuu kuwa Mushi ana haki ya kutoa hoja na kuitetea kwa nguvu zake zote. Lakini naomba tuangalie mambo mawili...mosi, ni vile ulivyosema kutumia lugha za chooni bali tutumie mijadala ya elimu. Kwa jinsi Mushi alivyoandika kichwa cha habari huku kikiwa kinatofautiana na kilichoandikwa, ni mfano wa kuwa na mjadala usio wa elimu.

Lakini tunaweza kusema alisema kwa context ya kisiasa. Hili linanipelekea kuangalia jambo la pili, kwa nini tuwe tunaandika mada kama hii (isiyo ya kisiasa) kwa kutumia context ya siasa? Naelewa logic aliyotaka kutumia ili kuwa na conclusion aliyotoa lakini kwa bahati mbaya sidhani kama yaliendana.

Kwa heshima na taadhima!
 
Mkuu FMES,

Nakubaliana nawe mkuu kuwa Mushi ana haki ya kutoa hoja na kuitetea kwa nguvu zake zote. Lakini naomba tuangalie mambo mawili...mosi, ni vile ulivyosema kutumia lugha za chooni bali tutumie mijadala ya elimu. Kwa jinsi Mushi alivyoandika kichwa cha habari huku kikiwa kinatofautiana na kilichoandikwa, ni mfano wa kuwa na mjadala usio wa elimu.

Lakini tunaweza kusema alisema kwa context ya kisiasa. Hili linanipelekea kuangalia jambo la pili, kwa nini tuwe tunaandika mada kama hii (isiyo ya kisiasa) kwa kutumia context ya siasa? Naelewa logic aliyotaka kutumia ili kuwa na conclusion aliyotoa lakini kwa bahati mbaya sidhani kama yaliendana.

Kwa heshima na taadhima!
Kichwa changu cha habari kingetofautiana na habari kama Mh Rais mwenyewe angekuwa ameshawaomba wamarekani wamlete Balali..na si kutuambia kuwa hajui mahali alipo!Angetakiwa awe ameshawaomba wamarekani wamlete Balali na si kusubiri mpaka wamarekani watuambie kuwa serikali ya Rais wetu haijawaomba kufanya hivyo!

Rais na serikali yake wanadiriki kutuambia hawajui Balali alipo.Wamarekani wakaja wakatuambia..ala..yumo humu..kwanza na viza tunamfutia!Rumours zikaanza yuko kisiwani Malta!Tukawauliza wamarekani kwanini mnafanya mambo haya ya kuruhusu aende kisiwani?

wakasema no..bado yumo humu nchini mwetu!

Tukasema alah..kumbe!?Sasa mbona hamumleti aje kuhojiwa?Wakasema serikali yenu haimhitaji!SASA BADALA YA KULETA SIASA ZAKO ZA VITENDAWILI NAOMBA UFUMBUE HIKI KWANZA..BADALA YA KUENDELEAZA SIASA ZA KUTUKUZANA HUKU MAMILIONI YA WANANCHI WAKITESEKA KWA HALI NGUMU YA MAISHA!HUKU MAMIA YA MABILIONI YAKIGAWANWYA KAMA NJUGU!

NI BORA UZINGATIE SIASA ZA COMMON SENSE..MUULIZE MH RAIS NI KWANINI ALIONA NI MUHIMU KUWAHOJI WANANCHI KABLA YA BALALI?
 
Hamna mtu amekuomba uje kuchangia matusi kwenye hii thread..however unaonyesha udhaifu wako..kwamba uko hapa kwa maslahi flani!JF niliamua kujiunga baada ya kuona ni uwanja mpana wenye kuruhusu mijadala ya hoja kwa hoja bila kuget personal!Sio nia yangu kujibu matusi kwa matusi..kama umeshindwa kunijibu maswali niliyouliza then pls dont contribute to this thred.Siasa za matusi na chuki binafsi unazozileta hapa jf ni za kichefuchefu..zirudishe ulikozitoa..Nitawaomba jf waongeze freedom in the middle ili iweze kuwa JAMBO FREEDOM FORUMS!WHERE WE DARE TO TALK!

Where the hell u got this mandate of total ban? for ur inf Im here to stay and ur dealing with the beast u dont know!
 
Kichwa changu cha habari kingetofautiana na habari kama Mh Rais mwenyewe angekuwa ameshawaomba wamarekani wamlete Balali....Angetakiwa awe ameshawaomba wamarekani wamlete Balali na si kusubiri mpaka wamarekani watuambie kuwa serikali ya Rais wetu haijawaomba kufanya hivyo!
....!NI BORA UZINGATIE SIASA ZA COMMON SENSE..MUULIZE MH RAIS NI KWANINI ALIONA NI MUHIMU KUWAHOJI WANANCHI KABLA YA BALALI?

Brother Mushi taratibu Mangi:Kwanza msee wangu inabidi hilo swali lako nililolinukuu hapo juu inabidi ujiulize wewe mwenyewe. Wewe ndiye inabidi uzingatie what you are calling "Siasa za Common Sense" and if that is the case then naamini kabisa utafika wakati wa kuwaomba wamerekani wamrudishe Balali. Sasa kama kwako "common sense" ni kumleta sasa hivi, wakati criminal investigations into the matters is going on,then sawa.

Kwa mfano ndugu yangu ikiwa kibaka kakukwapulia simu yako na aka kamatwa je ni "commonn sense" gani utaitumia; kumchakaza na kumchoma moto au "common sense" ya kumpeleka kituoni ambako possibility ya kuachiwa kwa sababu nyingi tu.

Nilalosema ni kuwa ingawa mamilioni yamechotwa na wengi wetu pamoja na ndugu zetu tunasota, huku mafisadi wakitanua, ukweli ni kwamba sheria huwa siku zote inampendelea mkosaji hasa akiwa na uwezo. That is a reality of life and therefore ku-reverse that immediately lazima "Common Sense" unayoizungumzia tuitupilie mbali and replace it with Anarchy/Mob Justice. In that case so long as audit report imeshasema kuwa kuna watu waliochota mabilioni, the wakusanywe, hata mahakamani kuwapeleka ni kupoteza muda, kwa vile wanaweza wakahonga, tuwafilsi mali zao zote na kuwafunga miaka 30 kazi nguumu na viboko 12 juu. Hiyo ndiyo "KOMONI SENSI"?.
 
He he he he he umisahau jinsi Bunge lilivyotumia billion 1 kuwapatanisha Mengi na Malima, its de same path, finding de proper way kubilali Tanzanian money in de name of investigation, God have mercy
 
Mushi,

Tuachane na siasa za common sense na twende na facts. Common sense inatutuma kuamini kuwa ubalozi wa Marekani unafanya kila liwalo kumrudisha Ballali ila tu wanasubiri maombi ya JK. Sasa nikuulize, mbona walikimbilia kusema kuwa wamemfutia Ballali visa huku wakijua hiyo ni technicality ya kudanganya toto? Kitu alichofanyiwa ni kuwa kwa kupotedha wadhifa wake, Ballali amepoteza diplomatic passport na privilege zote including going in and out of the US as a URT official. That's it.

Lakini, ubalozi huohuo haukusema kuwa Ballali ana hadhi ya ukaazi wa kudumu (permanent residency) hivyo kupoteza kwake diplomatic passport, haimzuii kuingia na kutoka (au kuishi Marekani). Au hata kama hakuwa nayo hiyo permanent residency, bado angeweza kuomba visa (kama mtu binafsi)na kuna nafasi kuwa angeipata (kwani hajashtakiwa rasmi na serikali). Hivyo basi, tuwe makini katika kushabikia mambo ili tusije tukaonekana kuwa kwa vile mzungu amesema jambo fulani, basi yeye ndio sahihi. As far as I am concerned, ubalozi wa Marekani nao unacheza siasa (kwa namna kama ya serikali yetu na wala wasitake kutupia lawama serikali ya JK pekee. Kwa nini balozi Green alipoulizwa mahali alipo Ballali akayeyusha kwa kusema kuwa sheria za Marekani hazimruhusu kusema nyendo za watu walioko nchini mwao? Wamarekani na law enforcement agencies zao kweli hawajui Ballali alipo?
 
Mushi,

Tuachane na siasa za common sense na twende na facts..... Kwa nini balozi Green alipoulizwa mahali alipo Ballali akayeyusha kwa kusema kuwa sheria za Marekani hazimruhusu kusema nyendo za watu walioko nchini mwao? Wamarekani na law enforcement agencies zao kweli hawajui Ballali alipo?

Now you are talking. Common sense is not that common even if you have open facts as it is relative. Kwa fisadi common sense ni kuchota size yake na kujihami kwa kila mbinu kukilinda kile alichokwapua. Na sheria zipo kuwalinda wale waliozitunga. Kama common sense ingekuwa inatumika, sheria zisingekuwa na maana. Balozi anochosema ni kuwa pamoja na Balali "kuiba", pamoja na Balali kuwepo marekani, pamoja na Babali kunyang'anywa visa, lakini SHERIA ambayo ni mbadala wa Common sense ndiyo inatumika and there is nothing you and me can do about that! Ni mpaka pale mwenzake JK akohoe, hiyo ndiyo "common sense" inayotumika kwenye anga za ufisadi. Wewe ukiuliza utapewa majibu ..sijui, no comments, ask you goverment nk.

Wewe common sense zako zinakuambia kuwa haiwezekani kuwa wamerakani hawajui Balali yuko wapi, lakini Balozi yuko sawa kwa vile yeye anzungumzia kwa misingi ya sheria ambayo inamlinda Balali pamoja na kujulikana wazi kuwa yupo wapi!

Hiyo ndiyo demokrasia - ni kuwaweka watu madarakani ili walinde masilahi ya wale waliowaweka. Matajiri wameiweka serikali ya CCM madarakani kwa hivyo ni "common sense" and it is a FACT that serikali hiyo italinda masilahi ya hao matajiri. Wale asilimia 80 walikuwa wanasindikizaji wa mdundiko tu sana saana kuambulia ubwabwa. Dawa ni moja tu, wakipiga ngoma hiyo ya uchaguzi usikubali kuicheza!
 
where the hell u got this mandate of total ban? For ur inf im here to stay and ur dealing with the beast u dont know!
sawa tu!ila no matusi!jf embraces fair discussion!and if its politics..we embrace the ones that makes sense!

Nataka nikuhakikishie kuwa sina uwezo wa kumban yeyote!

However nilishtushwa na matusi yaliyokuwa yakielekezwa kwangu..na badala ya kujibu kwa matusi,nilishauri aache kuendelea kuchangia matusi!

I am ready to deal with whoever!as long as we dont distort the real meaning of us coming here on jf!

This is my new slogan.."jambo freedom forums"where we dare to speak!
 
Back
Top Bottom