Omona Wanyu
Member
- Feb 29, 2012
- 51
- 6
Ndugu watanzania wenzetu sisi wanakijiji wa kijiji cha Ruhita wilayani Karagwe ambao ni wafugaji hivi sasa navyoandika tunapigwa na kuchomewa Nyumba zetu hali ni mbaya sana zaidi ya Nyumba zetu 93 zimeshachomwa moto mpaka jana, Ngombe zaidi ya 163 zimepotea katika vurugu, watoto wamepotea, wake zetu wamepigwa na kunyanyaswa kijinsia, watu wanapata vilema vya maisha, familia zimekuwa wakimbizi ndani ya nchi yao wenyewe, wanapika na kulala nje na kuishi vichakani kwa hofu ya kukamatwa, Jeshi la Polisi Mkoa wanatekeleza amri na unyanyasaji huu wa kutisha, wakituita sisi wahamiaji haramu, huku Wanyarwanda MATAJIRI waliovamia na kupora ardhi yetu wamekwisha waweka sawa, kwa kuwapa mboga na kuachwa wakiendelea kupora ardhi yetu adhimu na kutuacha sisi wakiwa mbele ya serikali yetu, mpaka sasa hatuna Chakula watoto wanalia, Chakula kimechomwa moto, na wamepotezana na wazazi. WATANZANIA MLIOKO HUKO MJINI MTUSAIDIEEE! WENZENU TUNATESEKA NA HATUNA MATUMAINI NA SERIKALI YETU! Mheshimiwa Prof Anna Tibhaijuka binti yetu sisi wenyewe kweli hii ndio fadhila ya Usomi wako kwetu Mama?