Zulqarnayn
Senior Member
- Oct 17, 2011
- 107
- 50
Habari zilizotufikia hivi punde na ambazo tumezithibitisha zinasema kwamba Mbunge wa Nzega yuko katika hali mbaya ndani ya chama chake. Kwenye Kikao cha Kamati ya wabunge wa CCM (party caucus) hapo jana jioni ambacho pamoja na mambo mengine kilijadili sakata la mgomo wa madaktari, hakikusita kujadili suala la nidhamu ndani ya chama hususan miongoni mwa baadhi ya wabunge. Hapo mjadala kuhusiana na ushiriki wa Mbunge huyu kijana, msomi na mwanaharakati ambaye amekuwa akifanya mambo yanayosemekana kushabihiana na harakati za vyama vya upinzani kwa misimamo yake na michango mikali ndani na nje ya bunge. Kijana huyu alijikuta kwenye wakati mgumu pale hoja ya kumtaka ashughulikiwe, kama ile ya kikao cha namna hiyo cha jumapili iliyopita, ilirudi tena.
Safari hii alipewa nafasi ya kujitetea na ndipo alivyoanza kupangua tu hoja za wabunge wenzake moja baada ya nyingine lakini kabla hajafika popote alikatizwa na mwenyekiti wa kikao hicho na kumtaka ake kwanza asomewe maelezo ya taarifa ya usalama aliyokuwa nayo Mhe. Pinda, baada ya hapo Mbunge wa Sikonge kwa kuangalia hali ilivyokuwa imechafuka mule ndani kufuatia baadhi ya wabunge wa CCM kusikitika, aliokoa jahazi na kmuomba waziri mkuu asitishe zoezi la kumtaka Kigwangalla kujieleza, na badala yake asaidiwe, alisema: 'mwenyekiti mimi ni mwenyekiti wa wabunge wa Tabora, naomba nikuombe sana umsaidie mdogo wangu Kigwangalla, ni kijana mzuri lakini sema ana spidi kali sana, anahitaji busara zenu, akina Mkuchika, Wassira, naomba mumsaidie mdogo wangu huyu jamani...hapa naona kama mnazidi kumbomoa tu hamumsaidii, mimi ningekuwa yeye kwanza nisingeongea humu hata kwa miezi sita hivi....' Waziri Mkuu alisitisha mchakato huu na Kigwangalla, ambaye alikuwa ameanza kwa kuomba radhi watu wote aliowakwaza kwa namna yoyote ile, na kusema anaomba aweke rekodi straight ili tatizo lionekane kwa uhalisia wake na siyo kumuangalia yeye kama msaliti ama 'Rebel' kwa chama........alionekana kutoridhika na uamuzi huu na hivyo alitulia na kusononeka.
Kikao hicho kilikuwa kikali sana na kilijadili mambo mengi sana mazito likiwemo la posho na jinsi serikali inavyojichanganya. Wachunguzi wa mambo ya kisiasa wanasema, sasa ni kwa nini anaendelea kubaki kwenye CCM wakati ananyanyasika kiasi hicho bila hata huruma, bila hata kupewa nafasi ya kujieleza kwa kina? CCM sasa inaonesha kuchoka na pengine kuanza safari ya kuelekea kuanguka, maana kama inawapiga vita vijana makini, wasomi na machachari kama Kigwangalla, inataka kutueleza nini kuhusu wapambanaji wake katika siku za usoni? Inabidi wawe ni watu wa ndiyo tu? Ili hiki chama kishamiri na kiendelee kushika hatamu za uongozi wa nchi, inabidi kijirekebishe, kiwakumbatie watu walioonesha vipaji vya uongozi wa kisiasa na wenye mvuto kwa umma kama akina Khamis Kigwangala!
Safari hii alipewa nafasi ya kujitetea na ndipo alivyoanza kupangua tu hoja za wabunge wenzake moja baada ya nyingine lakini kabla hajafika popote alikatizwa na mwenyekiti wa kikao hicho na kumtaka ake kwanza asomewe maelezo ya taarifa ya usalama aliyokuwa nayo Mhe. Pinda, baada ya hapo Mbunge wa Sikonge kwa kuangalia hali ilivyokuwa imechafuka mule ndani kufuatia baadhi ya wabunge wa CCM kusikitika, aliokoa jahazi na kmuomba waziri mkuu asitishe zoezi la kumtaka Kigwangalla kujieleza, na badala yake asaidiwe, alisema: 'mwenyekiti mimi ni mwenyekiti wa wabunge wa Tabora, naomba nikuombe sana umsaidie mdogo wangu Kigwangalla, ni kijana mzuri lakini sema ana spidi kali sana, anahitaji busara zenu, akina Mkuchika, Wassira, naomba mumsaidie mdogo wangu huyu jamani...hapa naona kama mnazidi kumbomoa tu hamumsaidii, mimi ningekuwa yeye kwanza nisingeongea humu hata kwa miezi sita hivi....' Waziri Mkuu alisitisha mchakato huu na Kigwangalla, ambaye alikuwa ameanza kwa kuomba radhi watu wote aliowakwaza kwa namna yoyote ile, na kusema anaomba aweke rekodi straight ili tatizo lionekane kwa uhalisia wake na siyo kumuangalia yeye kama msaliti ama 'Rebel' kwa chama........alionekana kutoridhika na uamuzi huu na hivyo alitulia na kusononeka.
Kikao hicho kilikuwa kikali sana na kilijadili mambo mengi sana mazito likiwemo la posho na jinsi serikali inavyojichanganya. Wachunguzi wa mambo ya kisiasa wanasema, sasa ni kwa nini anaendelea kubaki kwenye CCM wakati ananyanyasika kiasi hicho bila hata huruma, bila hata kupewa nafasi ya kujieleza kwa kina? CCM sasa inaonesha kuchoka na pengine kuanza safari ya kuelekea kuanguka, maana kama inawapiga vita vijana makini, wasomi na machachari kama Kigwangalla, inataka kutueleza nini kuhusu wapambanaji wake katika siku za usoni? Inabidi wawe ni watu wa ndiyo tu? Ili hiki chama kishamiri na kiendelee kushika hatamu za uongozi wa nchi, inabidi kijirekebishe, kiwakumbatie watu walioonesha vipaji vya uongozi wa kisiasa na wenye mvuto kwa umma kama akina Khamis Kigwangala!