Jana usiku nilifurahi sana. Nilikuwa natazama Mlimani TV mtangazaji alikuwa anapita maeneo mbalimbali kuzungumza na wananchi. Alifika mahali fulani akamhoji mjumbe wa CCM. Alinikuna sana kwa maneno yake. Alionyesha visima vyenye vyura na akachukua kabisa chura akaonyesha na kusema hapo ndio CCM ilipowafikisha. Akasema maji yamepelekwa kwenye mashamba makubwa na wananchi wanakunywa maji machafu sana. Akasema CCM iliwaahidi muda mrefu kupeleka maji lakini hakuna lililo fanyika. Alinikuna zaidi aliposema CCM wanakuja hapa wanasema viongozi wa ccm tuwaokoe lakini itakuwa ngumu kwani watu wana shida nyingi lakini muda wote huo CCM hawajafanya chochote na wanavyojaribu kuwaambia wananchi waichague CCM wanakosa hoja za kutetea.
My take: kama hao ndio viongozi wa CCM wanasema hivyo kazi ipo.
My take: kama hao ndio viongozi wa CCM wanasema hivyo kazi ipo.