Kibosile SYNOVATE kikaangoni TBC1 leo asubuhi

Unajua neno "random" linapoteza maana pale unapoanza kuchagua mikoa, wilaya, kata na vigezo vingine.. it is not random when it is not random!

... poll researchers out there would concur. Furthermore, if one were to carry out a simple factor analysis, results would significantly converge to clear odds against CCM discarding the insignificant p<=0.61 or p<=0.79 of the two SPINNERS. A message to REDET and SYNOVATE: YOU are a shame to statistics. You might just be lucky in another trade.
 
Jamani hivi hakuna sheria inayoweza kuwatia hatiani kwa kupotosha jamii kwa makusudi?

wana sheria tusaidieni hapo ili hawa jamaa REDET na Synovate wafikishwe mahakamani kwa kosa la kutusababishia usumbufu, kosa la kutupotosha na kukiuka maadili ya tafiti?

Tusaidiane hapo jamani.
 
Hapa swala linabaki wazi kuwa,watanzania tunaanza kujengwa kisaikolojia kuwa CCM inakubalika,ili watakapochakachua matokeo ya uchaguzi mkuu waweze kujitetea kuwa hata tafitiza kitaalamu zilishaonyesha kuwa wanapendwa.
Nawaunga mkono wale waliokubali kutokudanganyika na wasomi wanaoaibisha taaluma zao.
 
sure kwa wale wataalam wa research nadhani mmeipata maana kamili ya random

PLEASE MAY I DECLARE INTREST THAT:Mimi si mfuasi wa chama chochote lakini nitoe maoni yangu kwamba hiki kinachofanywa na hawa Synovate na Redet ni aibu kubwa kwao na familia zao kwa sababu watu wazima wanaamua kuacha mambo ya msingi na kukimbilia pale Lumumba kuandaa tafiti za kuhuni kuganga njaa.Nasema ni za kihuni kwa sababu moja kwamba lengo lao ni moja tu kuhakikisha wanakatisha tamaa wafuasi wa upinzani wasiende kupiga kura.Hiyo ndiyo njama anayofanya Makamba na Kinana kwa kuwatumia hawa akina Synovate.
Lakini mimi niseme historia itakuja kuwahukumu hata kama sio leo lakini siku chache zijazo,hakuna dhambi mbaya kama kufanya hila kwa makusudi ili watu wasiende kupiga kura.Ni dhambi mbaya sana isiyosameheka.
Lakini niseme hawa akina Synovate wataanza kuumbuka mwaka huu baada ya uchaguzi.Kweli CCM inaweza kushinda lakini ushindi wake si zaidi ya asilimia 55%.CHADEMA inaweza kushindwa urais lakini haitakosa aslimia 35% ya kura zote.CUF nao si haba walau asilimia 10% watapata.mambo kama yatakuwa hivi tayari akina Synovate na manyang'au wenzao watakuwa wameshapata somo la kutosha.
 
hiyo sample unaweza kukuta aliye wahoji ni mgombea wa sisiemu na familia yake, na baadhi ya wafanyakazi wa ikulu mikoani, ambao walikuwa chini ya usimamizi wa tiss, sasa hapo unategemea utapata nini?
 
ANGALIA 'TRUE SCENARIO' ya Drama kati ya REDET, SINOVET na mikono michafu ya hao WaChakaChuaji-Maisha yetu -CCM!
Tatizo sio Usomi, ni utumwa wa fikra na kujikomba pasipo mental independence. Akina Dokta Bana washauri wa Kikwete kwa muda mrefu..kamwe hawakukosea, na baadaya Repoti, wanapigiana simu na JK na akina Kinana na Makamba na dole juu, ..eti "tumewamaliza"..halafu wanasemezana.....na pia wanaambizana "..tafuata na wale Jamaa Wakenya, Sinoveti tuwaamuru nao wabadili ripoti yao waiwasilishe kuwa mie JK nipo juu mapema la sivyo wajiandae kuondoka zao ktk ardhi hii wawahi Nairobi kabla ya Jumanne...." Sinovet wakakurupuka wakawahi ku-edit reports, jamaa wamewasimamia mgongoni...wakascreatch historical samples wakazi-blend na kufix wakasahau ku-edit maeneo mengine kama Pg 11 inasomeka JK anayo 70% (hii ikimaanisha ni ya utafiti mwingine kabisa, labda ule wake dhidi ya mawaziri wake), na ndio maana hata Sinovet walipowasilisha, walikuwa wanatetemeka, kila mtu kavaa kivyake, anaangalia kimang'amung'amu...yule dada ndio hata kimawazo hakuwa nao kabisaaaa...roho ilikuwa zake Kenyaaa....hadi anashtukashtuka, anarudi Tanzania....! NDIYO HALI HALISI KUUDHULUMU UTAIFA NA HAKI ZA WATANZANIA...WASHINDWE KAMA PHARAOH na jeshi lake chafu lilivyoliwa na ulimi wa maji ya bahari wa Mwenyezi Mungu ktk Bahari ya Sham, ndivyo wataangamizwa watu hawa. Sio SINOVET, sio REDET, sio CCM, wote hawa Fimbo ya mteule wa ukombozi MUSA wa Tanzania (Dr W.P. Slaa) itawapitisha Waana wa Israel ktk Bahari Kavu, ila Pharaoh na Jeshi lake Chafu, ovu, na vibaraka wao wawafuatapo Watanzania kuwadhulumu wataangamizwa ktk Maji ya Bahari....
KURA ZOTE KWA DR SLAA aivushe Tanzania na kuiokoa mikononi mwa WAOVU hawa! Sinovet watikimbia nchi kwa woga baada ya Oktoba 31 Slaa atapopita katikati yao, REDET na CCM YAO.
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU BARIKI UKOMBOZI WETU UNAOKUJA KWA KURA TUTAZOPIGA!
Yaani w
 
  • Jakaya Mrisho Kikwete (CCM)

    2,011 21.90%
  • Willibrod Slaa (CHADEMA)

    6,304 68.66%
  • Ibrahim Lipumba (CUF)

    262 2.85%
  • Hashim Rungwe (NCCR-Mageuzi)

    484 5.27%
  • Mutamwega Mugahywa (TLP)

    121 1.32%
  • Ata hii CCM hawaikubali
 
Nakubaliana na Mwanakijiji pamoja na Mkulima.

Idadin ya watu 2,000 ni nzuri sana na inatosha kabisa kwa kufanyia utafiti.

Ila kimekosekana neno RANDOM.

Kwa REDET nasikia walifikia kwa mabalozi wa nyumba 10 na huko mambo yakaishia (wa CCM).

Idadi inatosha sana ila kibaya ni NJIA ZILIZOTUMIKA ni MBAYA SANA kwa ufupi SI RANDOM.

Anyway, zimebaki siku chini ya 20.
 
hii ni aibu kubwa kwa wana taaluma wote Tanzania wanao husika na utafiti! Kwanza hivi nani anafanya quality control ya vitu kama hivi! miaka yote hiyo chuoni jumlisha na ma PHD yao ya ulaya na kwingineko! jamani ndo maana nchi hii kila mtu anataka kuwa mwanasiasa yaani watu wanavunja heshima zao ili wajipendekeze kwa wenye madaraka,... hiii nchi usanii mtupu haina proffessionalism kabisaaaaaa! AIBU AIBU AIBU :tonguez:
 
ANGALIA 'TRUE SCENARIO' ya Drama kati ya REDET, SINOVET na mikono michafu ya hao WaChakaChuaji-Maisha yetu -CCM!
Tatizo sio Usomi, ni utumwa wa fikra na kujikomba pasipo mental independence. Akina Dokta Bana washauri wa Kikwete kwa muda mrefu..kamwe hawakukosea, na baadaya Repoti, wanapigiana simu na JK na akina Kinana na Makamba na dole juu, ..eti "tumewamaliza"..halafu wanasemezana.....na pia wanaambizana "..tafuata na wale Jamaa Wakenya, Sinoveti tuwaamuru nao wabadili ripoti yao waiwasilishe kuwa mie JK nipo juu mapema la sivyo wajiandae kuondoka zao ktk ardhi hii wawahi Nairobi kabla ya Jumanne...." Sinovet wakakurupuka wakawahi ku-edit reports, jamaa wamewasimamia mgongoni...wakascreatch historical samples wakazi-blend na kufix wakasahau ku-edit maeneo mengine kama Pg 11 inasomeka JK anayo 70% (hii ikimaanisha ni ya utafiti mwingine kabisa, labda ule wake dhidi ya mawaziri wake), na ndio maana hata Sinovet walipowasilisha, walikuwa wanatetemeka, kila mtu kavaa kivyake, anaangalia kimang'amung'amu...yule dada ndio hata kimawazo hakuwa nao kabisaaaa...roho ilikuwa zake Kenyaaa....hadi anashtukashtuka, anarudi Tanzania....! NDIYO HALI HALISI KUUDHULUMU UTAIFA NA HAKI ZA WATANZANIA...!'
Ole wao! WASHINDWE KAMA PHARAOH na jeshi lake chafu lilivyoliwa na ulimi wa maji ya bahari wa Mwenyezi Mungu ktk Bahari ya Sham, ndivyo wataangamizwa watu hawa. Sio SINOVET, sio REDET, sio CCM, wote hawa Fimbo ya mteule wa ukombozi MUSA wa Tanzania (Dr W.P. Slaa) itawapitisha Waana wa Israel ktk Bahari Kavu, ila Pharaoh na Jeshi lake Chafu, ovu, na vibaraka wao wawafuatapo Watanzania kuwadhulumu wataangamizwa ktk Maji ya Bahari....
KURA ZOTE KWA DR SLAA aivushe Tanzania na kuiokoa mikononi mwa WAOVU hawa! Sinovet watikimbia nchi kwa woga baada ya Oktoba 31 Slaa atapopita katikati yao, REDET na CCM YAO.
MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU BARIKI UKOMBOZI WETU UNAOKUJA KWA KURA TUTAZOPIGA!
 
Kama viongozi wanachakachua , wengine wafanyeje, kwani dr.bana hataki kumfuta mkandara. Kupewa cheo. Nyerere alisema umasini wa akili ni umasikini mbaya kuliko wote. Wasomi wamezidi kuendekeza njaa. Watapika mpaka matokeo ya mitihani sasa.
 
Kitu ambacho kinajitokeza tena na tena kwenye mijadala ya hizi opinion polls ni kwamba Watanzania wengi hatujui hizi tafiti zinafanywa vipi. Hatujui sample inakusanywa vipi na wengine wana question ukubwa wa sample.

Kwa mfano watu wengi na safari zote wanashangaa kwanini watu 2000 tu kati ya watu milioni 40? Hii ni ishara tosha kwamba elimu yetu haikidhi haja ya kutoa wasomi hasa wale waliomaliza chuo kikuu ambao wanaweza kufanya tafiti japo ndogo. Maana kama mtu huyo ana question mambo hata ambayo ni basic kwenye tafiti kama hizo ni kwamba sio ajabu hata statistics na probability hajawahi kukutana nayo maishani.

Tunaweza ku question bias kwenye utafiti lakini ukubwa wa sample ni issue ndogo sana.

Haina maana kwasababu opinion poll hiyo imehusisha watu 2000 basi walihojiwa 2000. Inawezekana hata wakahoji watu 20,000 ila baada ya hapo ndipo wanaanza kuchunja ili kupata watu wanaofit vyema kwenye criteria walizojiwekea. Ndio maana wahusika wanatakiwa wasiwe na upendeleo vinginevyo opinion poll inakuwa haina maana.

Kama ni kuwabana REDET au Synovate basi iwe kwenye suala la je hawako biased? Njia walizotumia kufanya utafiti wao ndio zinatumika duniani kote. USA yenye watu 300m kikawaida wanatumia sample mpaka za watu 800 kuwakilisha jamii.

Ni gharama sana kufanya utafiti wa maelfu ya watu wakati faida inayoongezeka ni ndogo sana. Kwa mfano ukihusisha watu 2000 unaweza kuta makosa kwenye utafiti wako ni 5% lakini ukihusisha 20,000 makosa yakawa 4%. Tofauti ya asilimia moja haiendani na cost kubwa ya kufanya utafiti wa watu wengi na ndio maana watafiti wengi wanatumia namba ndogo.

Hiyo ni opinion poll na opinion poll iliyo sahihi ni hapo tarehe 31/10/2010, hakuna haja ya kutoana ngeu kubishana juu ya hili wakati baada ya wiki mbili tutajua ukweli.

Nikiongeza nitaaribu.
 
  • Jakaya Mrisho Kikwete (CCM)

    2,011 21.90%
  • Willibrod Slaa (CHADEMA)

    6,304 68.66%
  • Ibrahim Lipumba (CUF)

    262 2.85%
  • Hashim Rungwe (NCCR-Mageuzi)

    484 5.27%
  • Mutamwega Mugahywa (TLP)

    121 1.32%
  • Ata hii CCM hawaikubali
Watakubali wapi kama si ya REDET na Synovate?
 
huyu mchkachuaji ame-specialise kwenye nguine au statistics, maana inawezekana hajui jinsi ya ku-collect data na kuzifanyia kazi
 
Du. nimeshangazwa na ujasiri wa mtangazaji, alikuwa anamuuliza maswali magumu na jamaa alionekana wazi kubabaika. hakuwa na majibu ya kueleweka. nadhani jamaa alikwenda studio akijua atahojiwa na marine hassana yule anayejipendekeza kwa mafisadi. Du kakutana na kichwa jamaa ni pande la mtu lakini alikuwa mdogo kama joti. kudadek

...Na mimi ndio nilivyoona. Kwa hakika kipindi kilipoanza nilitaka kuondoka kwa kuelewa kuwa ni wale walee na watapeana maswali ya kishkaji kuhalalisha matokeo. Kwa TBC ilivyo, mtangazaji wa leo kweli alikuwa jasiri. Nina wasiwasi kama atapewa tena kipindi!

 
hao wote ni wahuni hawajaenda nje ya dar es salaam, wmefanyia mtaa wa Lumumba chini ya usimamizi wa Makamba na Kinana. I bet you hata std seven leavers wasingeweza kuwahoji watu 2500 tu kati ya watu zaidi ya milioni 16 wanaotazamiwa kupiga kura

Watu 2000 wanatosha kabisa kufanya Statistical Inference labda useme hizo data hazikuwa random.
 
Back
Top Bottom