Jackbauer
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,038
- 2,199
Nikiwa kama mwananchi natoa ombi halali kwa wabunge wetu ambao leo wanatarajiwa kuijadili bajeti ya wizara ya nishati na madini kuipinga bajeti hiyo.misingi ya kuipinga bajeti hii iko miwili na iko wazi kabisa.Mosi;suala zima la nishati ya umeme limebakia kuwa kero toka waziri huyu ashike wizara hii.wizara inatuhadaa kwa kuingiza mtambo wa Mw 34 siku moja kabla ya bajeti ili tuone wanafanya effort??!Pili;kuhusu nchi yetu kushindwa kunufaika na madini yanayovunwa kila kukicha badala yake tunaumizwa na uchafuzi wa mazingira pamoja na mauaji ya raia.Kama kwa miaka yote zaidi ya minne tunapitisha bajeti na kusisitiza mambo haya haya bila kufanyiwa kazi(wabunge mna uthibitisho) sioni sababu ya kupitisha bajeti hii,badala yake tumuwajibishe kwa kumtaka ajiuzulu.Nawasilisha.